Habari kuhusu Palestina
Ni Sikukuu ya Kuzaliwa Kristo (Noeli) Mjini Betlehemu
Ni sikukuu ya kuzaliwa Kristo mjini Betlehemu, katika ukanda wa Magharibi, Palestina, mahali alipozaliwa Yesu Kristo. Ni namna gani nzuri ya kusherehekea tukio hili zaidi ya kuwashirikisha picha na maoni mbalimbali ya watumiaji wa mtandao wa intaneti kuhusiana na tukio hili linalosherehekewa na mabilioni ya watu duniani kote.
Uarabuni: Sera ya Romney kwa Mashariki ya Kati Yaibua Mjadala
Hotuba ya Mgombea urais wa Marekani kupitia chama cha Republican Bw. Mitt Romney iliyoelezea sera yake ya nje imeibua mjadala mzito miongoni mwa raia wa mtandaoni leo hasa wale watokao katika nchi za ki-Arabuni. Twiti zinazohoji sera ya mambo ya nje ya Marekani kwa Mashariki ya Kati ziliendelea wakati ambao Romney, anayepeperusha bendera ya chama cha Republican, alipozungumza katika Chuo cha Jeshi cha Virginia. Endapo atachaguliwa, Romney ameahidi kuwa na sera rafiki za mambo ya nje, tofauti na mwelekeo usiotabirika wa sera za Obama wakati huu ambapo mabadiliko ya kisiasa yanaendelea kulikumba eneo la Mashariki ya Kati.
Palestina: Maandamano Yalipuka Kupinga Ongezeko la Bei za Bidhaa na Ukosefu wa Ajira
Maandamano yanashika kasi katika mipaka ya Palestina, hasa katika miji mikuu katika Ukanda wa Magharibi. Waandamanaji wanalalamikia kupanda sana kwa gharama za maisha na ukosefu mkubwa wa ajira miongoni mwa vijana wa kipalestina.
Palestina: Makala Kuhusu Kifo cha Arafat yaibua maswali
Kituo cha habari cha Al Jazeera hivi karibuni kilionyesha makala iliyohusu kifo cha utata cha rais wa Palestina Yasser Arafat kilichotokea mjini Paris mnamo Novemba, 2004. Makala hayo yanadai kwamba kiongozi huyo hakufa kifo cha kawaida, ila aliwekewa sumu ya poloni, madai ambayo yanaibua maswali mengi.
Palestina: Gaza yashambuliwa, watu 12 wauwawa na wengine wengi kujeruhiwa
Usiku kucha wa tarehe 9 Machi na asubuhi ya Machi 10, ndege za kivita za Israel zilishambulia maeneo maalumu katika Ukanda wa Gaza, na kuua takribani watu 12 na kujeruhi wengine 20.
Dunia ya Uarabu: “Acheni Kulia Juu Sudani”
Kura ya maoni kwa ajili ya uhuru wa Sudani ya Kusini leo imeiweka nchi hiyo kwenye uangalizi wa karibu miongoni mwa watumiaji wa twita wa Kiarabu. Kuanzia Saudi Arabia mpaka Palestina, watumiaji Twita wa Kiarabu wanajadiliana kuhusu mshikamano, kugawanyika na rasili mali za Sudani.
Mashariki ya Kati: Mawasiliano ya Siri Ambayo Sio Siri ya Ubalozi wa Marekani
Wakati vyombo vya habari vikuu Uarabuni vimeyapokea kwa bega baridi mawasiliano ya siri ya Balozi za Kimarekani, wanablogu na watumiaji wa Twita kutoka Mashariki ya Kati walipata habari zinazohitajika sana kwa uchambuzi.
Mashindano ya Video: Intaneti Kama Chombo cha Kueneza Amani
Mfumo wa Intaneti umependekezwa kwa ajili ya kupata Tuzo ya Amani ya Nobel kwa mwaka 2010. Kama sehemu ya mjadala unaoendelea kuhusu mchango wa Intaneti katika jamii nzima ya binadamu , Condé Nast na Google Ireland wameungana na kuandaa mashindano haya ya video na mshindi atapata fursa ya kusafiri na pia video yao kuoneshwa kupitia MTV ya Italia.
Palestina: Mateso ya Kuwa Uhamishoni
Wakimbizi wa Kipalestina ni miongoni mwa watu ambao wamejikuta wakikimbilia uhamishoni ulimwenguni kote, Umoja wa Mataifa unatoa msaada kwa jumla ya wakimbizi waliosajiliwa wapatao milioni 4.7 katika ukanda unaokaliwa kwa nguvu huko Palestina, Jordan, Lebanoni na Syria. Mamilioni ya wakimbizi wa Kipalestina na wale walioteguliwa kutoka kwenye makazi yao wanaishi sehemu mbalimbali duniani. However, their Hata hivyo, watu hawa daima mioyo yao ipo nyumbani kwao, au kwa wazazi au mababu na mabibi zao waliobaki nyuma. Wanablogu wawili wa huko Gaza wameandika kuhusu mateso ya kuwa uhamishoni.
Palestina/Gaza: Matayarisho ya Maandamano ya Uhuru Gaza
Ni kama wiki moja hivi mpaka Maandamano ya Uhuru Gaza yatakapoanza. Lengo lake ni kuonyesha mshikamano na Wapalestina na kuongeza ufahamu kuhusu vikwazo vinavyoizingira Gaza. Katharine Ganly anatazama baadhi ya matukio yaliyotokea katika maandalizi ya maandamano hayo.