<?xml version="1.0" encoding="UTF-8"?>
<rss version="2.0"
	xmlns:content="http://purl.org/rss/1.0/modules/content/"
	xmlns:wfw="http://wellformedweb.org/CommentAPI/"
	xmlns:dc="http://purl.org/dc/elements/1.1/"
	xmlns:atom="http://www.w3.org/2005/Atom"
	xmlns:sy="http://purl.org/rss/1.0/modules/syndication/"
	xmlns:slash="http://purl.org/rss/1.0/modules/slash/"
	>

<channel>
	<title>Global Voices in Swahili &#187; Morocco</title>
	<atom:link href="http://sw.globalvoicesonline.org/category/world/middle-east-north-africa/morocco/feed/" rel="self" type="application/rss+xml" />
	<link>http://sw.globalvoicesonline.org</link>
	<description>Dunia inaongea, je unasikiliza?</description>
	<lastBuildDate>Wed, 02 Dec 2009 12:35:07 +0000</lastBuildDate>
	<generator>http://wordpress.org/?v=2.8.4</generator>
	<language>en</language>
	<sy:updatePeriod>hourly</sy:updatePeriod>
	<sy:updateFrequency>1</sy:updateFrequency>
			<item>
		<title>MENA: Maoni Wakati Wa Kuapishwa Obama</title>
		<link>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/01/mena-maoni-wakati-wa-kuapishwa-obama/</link>
		<comments>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/01/mena-maoni-wakati-wa-kuapishwa-obama/#comments</comments>
		<pubDate>Mon, 26 Jan 2009 11:51:07 +0000</pubDate>
		<dc:creator>j nambiza tungaraza</dc:creator>
				<category><![CDATA[Americas]]></category>
		<category><![CDATA[Governance]]></category>
		<category><![CDATA[International Relations]]></category>
		<category><![CDATA[Middle East & North Africa]]></category>
		<category><![CDATA[Morocco]]></category>
		<category><![CDATA[Politics]]></category>
		<category><![CDATA[Syria]]></category>
		<category><![CDATA[U.S.A.]]></category>
		<category><![CDATA[United Arab Emirates]]></category>
		<category><![CDATA[War & Conflict]]></category>
		<category><![CDATA[Weblog]]></category>

		<guid isPermaLink="false">http://sw.globalvoicesonline.org/?p=49</guid>
		<description><![CDATA[Ilichapwa kwanza naJillian York  &#183; Imetafsiriwa na j nambiza tungaraza &#183;  Angalia ujumbe mama 
Tukio la kihistoria limetokea Marekani leo wakati Barack Obama alipoapishwa kuwa rais wa 44. Wakati kuungwa mkono kwa Obama kati ya Waarabu kumekuwa kukipungua katika miezi michache iliyopita kufuatia uteuzi wake wa baraza la mawaziri na ukimya wake kuhusu [...]]]></description>
			<content:encoded><![CDATA[<em>Ilichapwa kwanza na<a href="http://globalvoicesonline.org/author/jillian-york/">Jillian York</a>  &middot; Imetafsiriwa na <a href='http://sw.globalvoicesonline.org/author/j-nambiza-tungaraza/'>j nambiza tungaraza</a> &middot;  <a href='http://globalvoicesonline.org/2009/01/20/mena-reactions-to-obamas-inauguration/'>Angalia ujumbe mama</a></em> 
<br /><p>Tukio la kihistoria limetokea Marekani leo wakati Barack Obama <a href="http://www.irishtimes.com/newspaper/breaking/2009/0120/breaking8.html?via=mr">alipoapishwa kuwa rais </a>wa 44. Wakati kuungwa mkono kwa Obama kati ya Waarabu kumekuwa kukipungua katika miezi michache iliyopita kufuatia uteuzi wake wa baraza la mawaziri na ukimya wake kuhusu mashambulio ya Israeli huko Gaza, wanablogu wa Mashariki ya Kati na Afrika ya Kaskazini wanayo mengi ya kusema.</p>
<p>Bloga <em>A Syrian in London </em>anaorodhesha matukio ya wiki chache zilizopita wakati wa mashambulizi ya Israeli, halafu <a href="http://sy-in-london.blogspot.com/2009/01/yet-another-day.html">anaeleza</a>:</p>
<blockquote><p>Hapajatokea mwingine tangu Kennedy, na wengine wanasema hakuna rais mwingine wa Marekani aliyewahi kuwa na mvuto pamoja na matumaini makubwa, kutoka duniani kote, kwenye mabega yake. Katika hotuba yake ya kuapishwa, Rais obama alisema:</p>
<p>&#8220;tumechagua matumaini dhidi ya hofu, umoja wa nia dhidi ya migogoro na kutoelewana&#8221;</p>
<p>&#8220;tumetoa tamko la kumaliza manung&#39;uniko yasiyo na maana na ahadi za uongo, visingizio na imani zilizopitwa na wakati, ambazo kwa muda mrefu zimekuwa zikinyonga siasa yetu.&#8221;</p>
<p>&#8220;Katika kutilia mkazo ukuu wa taifa letu, tunaelewa kwamba ukuu si haki yetu ya kupewa hivi hivi tu. Ni lazima tuupiganie.&#8221;</p>
<p>&#8221; chaguo ama la usalama wetu au maadili yetu, ni la uongo na tunalikataa&#8221; </p>
<p>&#8220;Je tunathubutu kuomboleza wafu?</p>
<p>&#8220;Je tunaweza kuwa na matumaini kwa wale wanaoishi?</p></blockquote>
<p>Bloga Jar of Justice aliyeko Dubai, <a href="http://blog.jarofjuice.com/2009/01/obama-speech-lacking/">anadhani kwamba hotuba ya Obama ilikuwa na mapungufu</a>:</p>
<blockquote><p>Pamoja na kufikiri kwamba hotuba ya Obama ilikuwa nzuri - hakusita pale aliposema &#8216;Waislamu&#8221; lakini alijitahidi sana kuonekana mkweli pale &#8220;alipomshukuru&#8221; <a href="http://en.wikipedia.org/wiki/George_W._Bush">yule mpumbavu ambaye hatutamzungumzia tena baada ya leo</a> - nafikiri kulikuwa na jambo muhimu lililokosekana kwenye htukio hili…</p>
<p>… lakini ninahisi kuwa Obama hatajishusha na kumhusisha yule mjinga zaidi ya ishara tu ya kidplomasia kwenye hotuba yake.</p></blockquote>
<p>Bloga wa Kimoroko <em>Laila Lalami</em>, ambaye ni mkazi wa marekani ambye anakiri kumpigia kura Obama, <a href="http://lailalalami.com/2009/mr-44/">kidogo ana matumaini zaidi </a>na kuridhika kuwa siku ya Obama imewadia:</p>
<blockquote><p>Nimeridhika kwamba siku ya Obama imewadia. </p>
<p>Miaka minane iliyopita, nilimpigia kura Ralph Nader kwa sababu nilifikiri kuwa hapakuwa na tofauti kubwa kati ya vyama vya Democrat an Republicanm kwenye masuala muhimu. Lakini baada ya upuuzi uliotokea Florida, maamuzi ya Mahakama ya Rufaa, na urais dhaifu uliofuatia, nilijifunza somo moja: Si kweli kuwa wanasiasa wote wako sawa. Kuna wengine ambao hawana vipaji, hawaguswi na busara zilizo wazi, ambao hawana huruma kiasi kwamba wanaifanya ofisi ya rais kuwa ni kitu cha mzaha. Nadhani hivi sasa situmaini kama kutakuwa na tofauti kubwa katika sera za serikali, hata hivyo bado ninajawa na shauku kwenye haya mabadiliko, kwa Barack obama, na kwa kuondoka kwa George W. Bush.</p></blockquote>
<p>Washabiki wa Kimoroko wa Obama <a href="http://www.obamatospeakinmorocco.com/">bado wanaendelea kupiga kampeni</a> ya kumtaka rais Obama atoe hotuba yake ya kwanza nje ya nchi nchini Moroko.</p>
]]></content:encoded>
			<wfw:commentRss>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/01/mena-maoni-wakati-wa-kuapishwa-obama/feed/</wfw:commentRss>
		<slash:comments>0</slash:comments>
		</item>
		<item>
		<title>Arabeyes: Rais wa Mauritania Aliyepinduliwa Katika mapinduzi ya Kijeshi</title>
		<link>http://sw.globalvoicesonline.org/2008/08/arabeyes-rais-wa-mauritania-aliyepinduliwa-katika-mapinduzi-ya-kijeshi/</link>
		<comments>http://sw.globalvoicesonline.org/2008/08/arabeyes-rais-wa-mauritania-aliyepinduliwa-katika-mapinduzi-ya-kijeshi/#comments</comments>
		<pubDate>Sun, 17 Aug 2008 23:10:33 +0000</pubDate>
		<dc:creator>charahani</dc:creator>
				<category><![CDATA[Algeria]]></category>
		<category><![CDATA[Arabic]]></category>
		<category><![CDATA[Breaking News]]></category>
		<category><![CDATA[Egypt]]></category>
		<category><![CDATA[English]]></category>
		<category><![CDATA[French]]></category>
		<category><![CDATA[Governance]]></category>
		<category><![CDATA[Iraq]]></category>
		<category><![CDATA[Mauritania]]></category>
		<category><![CDATA[Morocco]]></category>
		<category><![CDATA[Politics]]></category>
		<category><![CDATA[War & Conflict]]></category>
		<category><![CDATA[Western Sahara]]></category>

		<guid isPermaLink="false">http://sw.globalvoicesonline.org/?p=10</guid>
		<description><![CDATA[ &#183; Imetafsiriwa na charahani &#183;  Angalia ujumbe mama 

MAKAMANDA wa jeshi wamemuondoa madarakani Rais Sidi Ould Cheikh Abdallahi, rais wa kwanza kuchaguliwa katika uchaguzi huru katika miongo miwili, katika mapinduzi ya kijeshi yaliyofanywa Jumatano iliyopita baada ya mtafaruku wa kisiasa uliotokana na rais huyo kuwatimua kazi majenerali wanne wa ngazi za juu wa [...]]]></description>
			<content:encoded><![CDATA[<em> &middot; Imetafsiriwa na <a href='http://sw.globalvoicesonline.org/author/charahani/'>charahani</a> &middot;  <a href='http://globalvoicesonline.org/2008/08/06/arabeyes-mauritanian-president-ousted-in-military-coup-detat/'>Angalia ujumbe mama</a></em> 
<br /><p><img src='http://globalvoicesonline.org/wp-content/uploads/2008/08/457px-sidi_mohamed_ould_cheikh_abdallahi2.jpg' alt='' class='alignright' /><br />
MAKAMANDA wa jeshi <a href="http://www.abc.net.au/news/stories/2008/08/07/2326564.htm">wamemuondoa</a> madarakani <a href="http://www.answers.com/President%20Sidi%20Ould%20Cheikh%20Abdallahi">Rais Sidi Ould Cheikh Abdallahi</a>, rais <a href="http://www.answers.com/Mauritania">wa kwanza kuchaguliwa katika uchaguzi huru katika miongo miwili</a>, katika mapinduzi ya kijeshi yaliyofanywa Jumatano iliyopita baada ya mtafaruku wa kisiasa uliotokana na rais huyo kuwatimua kazi majenerali wanne wa ngazi za juu wa jeshi.  Makamanda wa jeshi walitangaza kuundwa kwa Baraza jipya la taifa na kiongozi wake, <a href="http://en.wikipedia.org/wiki/Mohamed_Ould_Abdel_Aziz">Jenerali Mohamed Ould Abdel Aziz </a>(mmoja kati ya majenerali wanne wa jeshi waliotimuliwa), kwenye radio na vituo vya televisheni vya serikali. Jenerali Abdel Aziz ni miongoni mwa walioshiriki <a href="http://en.wikipedia.org/wiki/2005_Mauritanian_coup_d%27%C3%A9tat">mapinduzi ya kijeshi nchini Mauritania mwaka 2005</a>.</p>
<p>Bloga kutoka Algeria <em>The Moor next Door</em> amekuwa <a href="http://themoornextdoor.wordpress.com/2008/08/06/the-president-will-not-be-taking-calls-today/">akiblogu</a> <a href="http://themoornextdoor.wordpress.com/2008/08/06/china-and-mauritania/">habari</a> <a href="http://themoornextdoor.wordpress.com/2008/08/06/coup-snapshots/">hii</a> <a href="http://themoornextdoor.wordpress.com/2008/08/06/developing-story/">kwa kina</a> <a href="http://themoornextdoor.wordpress.com/2008/08/06/summer-time-coups/">anaripoti</a>:</p>
<blockquote><p>Ninapozungumza na Wa-Mauritania wanaojua, baadhi yao walihisi kutokea kwa mapinduzi wakati wa kiangazi kama ilivyotokea, wakati wa kipupwe au isingeweza kutokea kabisa. Hisia zangu mara zote zilikuwa zikinielekeza kwamba mapinduzi haya yangefanyika majira ya kiangazi (Sijawahi kuandika bayana juu ya hili, lakini nimelielezea hili katika majadiliano na sikutaka kuchangia lolote kuhusiana na sakata hili. (1) kwa sababu Western Sahara Info. taarifa za kutoka Sahara Magharibi zilielezea kinaganaga na hakukuwa na haja ya kushindana ikiwa wewe ni mmoja wa mabloga wawili au watatu  unakuwa miongonimwa  wanaofuatilia sakata hili kwa karibu sana. (2) nilitaka kuhakikisha kwamba kama &#8216;ningetabiri&#39; jambo hili nisingekosea; Ningeweza kutabiri kuwa &#8216;Mwishoni mwa miezi ya Mei, Juni, Julai na Agosti Serikali ya Rais Sidi, isingelikuwapo tena&#39; na ningekuwa nimekosea; mimi si mtabiri wa hali ya hewa, na (3)  sijawahi kukutana na raia wa Mmauritania ambaye lolote jema la kumzungumza kuhusu Sidi, ukiachilia mbali uzuri wa wajihi wake.) Mojawapo ya mashinikizo yaliyomfanya Rais Sidi afanye alivyofanya ni kuwapo tishio la kuundwa tume huru ya kuchunguza mapesa ya mfuko wa maendeleo wa mkewe, tume ambayo ingemuweka hata yeye mwenyewe pabaya zaidi. Tume hiyo pia ingeufanya utawala wa Rais Sidi kituko kutokana na matumizi mabaya ya fedha za umma. Kwa mfano, nimeambiwa kuwa, safari zake za ndege za nje ziliigharimu serikali zaidi ya dola za Marekani mbili bilioni, kwa kukodisha ndege za kifahari yeye na familia yake na ujumbe wake pamoja na anasa zingine zisizokuwa za lazima. Kwa hakika alikuwa katika wakati mgumu: Ama angelazimika kujiuzulu (kwa mujibu wa Olmert) katika aibu kubwa au angelazimika kuvunja bunge na hivyo kuunda serikali yake upya, hali ambayo ingempeleka katika mapinduzi kama haya tuliyoyoyashuhudia, ambayo angalau imeficha aibu yake kisiasa. Alibanwa pande zote na alikuwa hana pa kutokea zaidi ya kukumbana na hatima yake.</p></blockquote>
<p><em>Western Sahara Info</em> amekuwa akiblogu mgogoro huu tokea ulipoanza, na leo <a href="http://w-sahara.blogspot.com/2008/08/military-coup-in-mauritania.html">ametuletea</a> habari za mapinduzi hayo ya kijeshi kama zinavyotokea dakika kwa dakika, pamoja na muhtasari wa unyambuzi: </p>
<blockquote><p>Uchambuzi wa harakaharaka, ambao naweza kuujutia: balaa kwa demokrasia ya Mauritania, kwa upande mmoja, (demokrasia) ambayo haikuwa na nafasi, lakini muhimu zaidi ni kuwa (mapinduzi haya) yamerudisha nyuma nafasi iliyokuwepo kwa maendeleo ya kisiasa. Ingawa, Rais Abdellahi na washirika wake si malaika, lakini Majenerali Ghazouani na Abdelaziz wanawakilisha kundi baya la kinyonyaji katika utawala wa Mauritania, kwa kukataa kuruhusu utawala wa kiraia kutulia madarakani kwa kuwatishia kung&#39;oa kabisa utawala wa kiraia hatimaye. Kama mapinduzi ya mwisho ya kijeshi yaliyotokea Agosti 2005, yangalieleweka na Jumuiya ya Kimataifa baada ya kung&#39;olewa kwa Rais Ould Tayaa, na hatimaye kupelekea mabadiliko makubwa, mapinduzi haya ya juzi yalikuwa tofauti saana. Kilichotokea mwaka 2005 ilikuwa kwamba madikteta wa kijeshi walioegemea katika ukabila waling&#39;atuliwa na nafasi ilijitokeza ikasimika badala yake utawala wa kiraia uliokuwa na muundo wa nusu-mabavu ambao uliruhusu desturi nyingi za kidemokrasia kwa muda mwingi zaidi, (utawala huo) ulishughulikia zaidi muwafaka wa kitaifa, urejeshwaji wa wakimbizi na maendeleo ya kiuchumi; ingawa siyo hema, lakini ilikuwa bora. Mabadiliko haya hivi sasa yanageuzwa. Wapinduaji - japokuwa wengine ni miongoni mwa wale waliofanya mwaka 2005 - - ni lazima walaumiwe na matokeo ya mapinduzi yabatilishwe kama inawezekana; Mauritania ilikuwa na fursa ya pekee kuweza kuvunja mzunguko huu usiokwisha, na sasa (fursa hiyo ya pekee) inaponyoka.</p></blockquote>
<p>Blogu ya <em>Roads To Iraq</em>, katikaujumbe wenye kichwa cha habari &#8220;Wamarekani walipanga mapinduzi nchini Mauritania,&#8221; <a href="http://www.roadstoiraq.com/2008/08/06/american-orchestrated-coup-in-mauritania/">inaripoti</a> habari hiyo vile vile: </p>
<blockquote><p>Mambo yanabadilika kwa kasi sana nchini Mauritania, imeanza na mapinduzi asubuhi hii, kwa kutoa &#8220;taarifa nambari moja&#8221; katika kituo cha televisheni cha Mauritania, Mkuu wa kituo hicho cha televisheni<br />
alibadilishwa sababu alikataa kushirikiana na mkuu wa jeshi aliyeandaa mapinduzi na kumtangaza mtawala mpya wa kijeshi.</p></blockquote>
<p>Huko Misri, <em>Bella</em> [Ar]<a href="http://afkaar-bella.blogspot.com/2008/08/blog-post.html">anasema</a> kilichotokea Mauritania kimedhihirisha kuwa Waarabu hawakupangwa kwa demokrasia.</p>
<blockquote><p>Inaonekana demokrasia haikuumbwa kwa watu kama sisi - ambao hatuwezi kupumua nje ya tawala za kijeshi.</p></blockquote>
<p>Baada ya kutupa historia fupi ya demokrasia changa ya Mauritania <em>Bella</em> anaandika: </p>
<blockquote><p>Kwa njia hii, Mauritania, ambayo ilikuwa ianze kuvuna matunda ya demokrasia katika msukumo wa kiasisi ambao eneo lote la mataifa ya jirani yalikuwa yanaungalia kwa shauku, mambo yamerejea kule yalikotoka kiasili, na wanajeshi wakaingilia kati na mapinduzi kutokea.</p></blockquote>
<p>Bloga wa Kuwaiti <em>Wild Il Deera</em> <a href="http://wildildeera.blogspot.com/2008/08/blog-post_06.html">anahoji maswali machache </a>kuhusiana na mapinduzi haya. Anauliza:</p>
<blockquote><p>Jumuiya ya Kiarabu ina msimamo gani kuhusu viongozi wa mapinduzi haya?<br />
Hivi huyu kiongozi wa Mauritania hakuchaguliwa na watu wake?<br />
Hivi inawezekanaje kundi la kisiasa, kama Jumuiya ya Kiarabu, ambayo inataka kuheshimiwa katika jamii ya Kiarabu na katika ulingo wa kimataifa ikaruhusu mapinduzi kama haya kufanyika katika moja ya mataifa wanachama wake?</p></blockquote>
<p>Bloga maarufu nchini Morocco Larbi [Fr] alipachika kiungo cha makala ya ya habari, <a href="http://www.larbi.org/post/2008/08/Mauritanie%3A-Coup-d-Etat-en-cours">kisemacho</a>: </p>
<blockquote><p>Unaweza kusema: Afrika ni bara lililolaaniwa!</p></blockquote>
<p>Habari yake hiyo imepata maoni mengi. <em>Citoyen</em> anatoa maoni kwamba:</p>
<blockquote><p>Ni kweli mapinduzi hayatabiriki Afrika… Nashangaa, ingawa, kama kwa mara nyingine tena, Mashirika ya Moroko yamekatizwa kama yalivyokuwa mwezi Ogasti 2005? </p></blockquote>
<p>Mwishoni KABOBfest, ambaye huwa anaingiza vichekesho katika kila hali, <a href="http://www.kabobfest.com/2008/08/kickin-it-old-skool.html">anatoa maoni</a> yenye mzaha: </p>
<blockquote><p>Wakati utamaduni wa mapinduzi katika mataifa mengi ni utamaduni uliopitwa na wakati (kama vile Syria hakujapata kutokea mapinduzi kwa miongo kadhaa sasa) Baadhi ya mataifa yanapendelea mitindo ya kizamani,  rejea pale ambapo ianonekana palikuwa na mapinduzi kama juma moja lililopita sehemu fulani hapa duniani. Wakati Mauritania siyo Fiji, wanadumisha utamaduni usio na maana wa mapinduzi katika dunia ya Waarabu.</p></blockquote>
<p>Blogu ya Arabdemocracy pia anayo <a href="http://www.arabdemocracy.com/2008/08/mauritaniaobituary-for-young-democracy.html">taarifa ya maombolezo</a> ya iliyokuwa demokrasia changa.</p>
<p><em>Picha ya hapo juu ni ya Sidi Mohamed Ould Cheikh Abdallahi iliyopigwa na <a href="http://www.agenciabrasil.gov.br/media/imagens/2007/09/27/1254MCMauritania1.jpg/view">Marcello Casal Jr./Abr</a> (Septemba 2007)</em></p>
]]></content:encoded>
			<wfw:commentRss>http://sw.globalvoicesonline.org/2008/08/arabeyes-rais-wa-mauritania-aliyepinduliwa-katika-mapinduzi-ya-kijeshi/feed/</wfw:commentRss>
		<slash:comments>0</slash:comments>
		</item>
	</channel>
</rss>
