Habari kuhusu Israel
Palestina: Gaza yashambuliwa, watu 12 wauwawa na wengine wengi kujeruhiwa
Usiku kucha wa tarehe 9 Machi na asubuhi ya Machi 10, ndege za kivita za Israel zilishambulia maeneo maalumu katika Ukanda wa Gaza, na kuua takribani watu 12 na kujeruhi wengine 20.
Mashariki ya Kati: Mawasiliano ya Siri Ambayo Sio Siri ya Ubalozi wa Marekani
Wakati vyombo vya habari vikuu Uarabuni vimeyapokea kwa bega baridi mawasiliano ya siri ya Balozi za Kimarekani, wanablogu na watumiaji wa Twita kutoka Mashariki ya Kati walipata habari zinazohitajika sana kwa uchambuzi.
Mashindano ya Video: Intaneti Kama Chombo cha Kueneza Amani
Mfumo wa Intaneti umependekezwa kwa ajili ya kupata Tuzo ya Amani ya Nobel kwa mwaka 2010. Kama sehemu ya mjadala unaoendelea kuhusu mchango wa Intaneti katika jamii nzima ya binadamu , Condé Nast na Google Ireland wameungana na kuandaa mashindano haya ya video na mshindi atapata fursa ya kusafiri na pia video yao kuoneshwa kupitia MTV ya Italia.
Palestina/Gaza: Matayarisho ya Maandamano ya Uhuru Gaza
Ni kama wiki moja hivi mpaka Maandamano ya Uhuru Gaza yatakapoanza. Lengo lake ni kuonyesha mshikamano na Wapalestina na kuongeza ufahamu kuhusu vikwazo vinavyoizingira Gaza. Katharine Ganly anatazama baadhi ya matukio yaliyotokea katika maandalizi ya maandamano hayo.
Israel: Kublogu Kwa Ajili Ya Mazingira Nchini Jordan
“Wanamazingira na Waandishi kutoka Palestina, Jordan na Israel watakutana huko Madaba, Jordan mwezi huu kwa ajili ya warsha ya siku 2: “Kublogu kwa Ajili ya Mazingira” tarehe 20-21 Desemba,” anaandika Muisrael Green Prophet, kwenye Mideast Youth.
Vijana wa Kiyahudi na Kipalestina Watumia Video Kuuelewa Mgogoro
Mashirika mawili tofauti nchini Israel na katika Majimbo ya Palestina yanatumia zana za video ili kuwasaidia vijana wa Kiarabu na Kiyahudi kuuelewa mgogoro na kujenga daraja kati yao.
Palestina: IDF Yachoma Moto Magari Ya Wapalestina
Kwenye Do Unto Others, Samuel Nichols anaandika kuwa doria ya jeshi la Israel imeanza kuchoma moto magari ambayo yanakamatwa yakijaribu kuvuka mpaka kutoka Ukanda wa Magharibikuingia Israel. Ametundika video hapa.
Mashariki ya Kati: Vikwazo kama Silaha ya Kisiasa
Watu wengi wa Mashariki ya Kati wamesusia bidhaa za Israeli na Marekani kama jibu la mashambulizi ya Israeli huko Gaza. Tarek Amr anapitia yale wanablogu wanayosema kuhusu suala hili.
Kivu Mpaka Gaza: Namna Vyombo Vya Habari Vinavyochagua Vipaumbele
Mdahalo unaodadisi ni kwa nini vita katika Mashariki ya Kongo vinapewa kipaumbele kidogo ikilinganishwa na migogoro inayotokea Mashariki ya kati. Mwandishi wa habari wa Rue89 anauliza, "ikiwa kifo cha Muisraeli mmoja ni sawa na vifo kadhaa vya Wapalestina, ni maiti ngapi za watu wa Kongo zitakazowekwa kwenye mnara wa mazishi huko Gaza?" Wanablogu wa pande zote mbili wanalichambua swala hilo.
Serikali Ya Irani Yautumia Mgogoro Wa Gaza Kukandamiza
Wakati wanablogu kadhaa wa Kiirani (pamoja na wale wa-Kiislamu) waliongeza makala zao na jitihada nyingine za kidijitali, kama vile "Google bomb" kulaani uvamizi wa Israeli katika ukanda wa Gaza, wanablogu wengine wanasema kwamba serikali ya Irani inatumia 'mwanya wa mgogoro wa Gaza' kukandamiza vyombo vya habari na jumuiya za kiraia ndani ya nchi hiyo.