<?xml version="1.0" encoding="UTF-8"?>
<rss version="2.0"
	xmlns:content="http://purl.org/rss/1.0/modules/content/"
	xmlns:wfw="http://wellformedweb.org/CommentAPI/"
	xmlns:dc="http://purl.org/dc/elements/1.1/"
	xmlns:atom="http://www.w3.org/2005/Atom"
	xmlns:sy="http://purl.org/rss/1.0/modules/syndication/"
	xmlns:slash="http://purl.org/rss/1.0/modules/slash/"
	>

<channel>
	<title>Global Voices in Swahili &#187; Iraq</title>
	<atom:link href="http://sw.globalvoicesonline.org/category/world/middle-east-north-africa/iraq/feed/" rel="self" type="application/rss+xml" />
	<link>http://sw.globalvoicesonline.org</link>
	<description>Dunia inaongea, je unasikiliza?</description>
	<lastBuildDate>Wed, 02 Dec 2009 12:35:07 +0000</lastBuildDate>
	<generator>http://wordpress.org/?v=2.8.4</generator>
	<language>en</language>
	<sy:updatePeriod>hourly</sy:updatePeriod>
	<sy:updateFrequency>1</sy:updateFrequency>
			<item>
		<title>Iraki:OBAMAAAAA!!! Huraaah Oyee!!</title>
		<link>http://sw.globalvoicesonline.org/2008/11/irakiobamaaaaa-huraaah-oyee/</link>
		<comments>http://sw.globalvoicesonline.org/2008/11/irakiobamaaaaa-huraaah-oyee/#comments</comments>
		<pubDate>Sun, 09 Nov 2008 05:52:33 +0000</pubDate>
		<dc:creator>Egidio Ndabagoye</dc:creator>
				<category><![CDATA[English]]></category>
		<category><![CDATA[Ethnicity]]></category>
		<category><![CDATA[Feature]]></category>
		<category><![CDATA[Governance]]></category>
		<category><![CDATA[International Relations]]></category>
		<category><![CDATA[Iraq]]></category>
		<category><![CDATA[Middle East & North Africa]]></category>
		<category><![CDATA[Politics]]></category>
		<category><![CDATA[U.S.A.]]></category>
		<category><![CDATA[War & Conflict]]></category>
		<category><![CDATA[Weblog]]></category>

		<guid isPermaLink="false">http://sw.globalvoicesonline.org/?p=37</guid>
		<description><![CDATA[Hivyo ndivyo asemavyo <em>Neurotic Iraqi Wife</em>. Kwa ujumla blogu nyingi za Iraki zimemchukulia vyema rais mteule Obama, lakini sio wanablogu wote waliofurahia. Salam Adil anaorodhesha maoni baada ya Uchaguzi wa rais huko Marekani. ]]></description>
			<content:encoded><![CDATA[<em>Ilichapwa kwanza na<a href="http://globalvoicesonline.org/author/salam-adil/">Salam Adil</a>  &middot; Imetafsiriwa na <a href='http://sw.globalvoicesonline.org/author/egidio-ndabagoye/'>Egidio Ndabagoye</a> &middot;  <a href='http://globalvoicesonline.org/2008/11/05/iraq-obamaaaaaaa-woooohooooo-wow/'>Angalia ujumbe mama</a></em> 
<br /><p>Hivyo ndivyo asemavyo <em>Neurotic Iraqi Wife</em>. Kwa ujumla blogu nyingi za Iraki zimemchukulia vyema rais mteule Obama, lakini sio wanablogu wote waliofurahia. </p>
<p><em>Layla Anwar</em> <a href="http://arabwomanblues.blogspot.com/2008/11/so-obama-booma-won.html">anabashiri jambo baya </a>kwa Iraki wakati wa uraisi wa Obama:</p>
<blockquote><p>Kwa hiyo Obama, booma[Booma ni bundi lakini katika lugha mojawapo ya Kiiraki neno hilo linamaanisha mtu mjinga ]…</p>
<p>Makamu wa raisi wa booma si mwingine zaidi ya J.Biden. J.Biden, Mzayonisti, muungaji mkono ngangari wa kuigawa Iraki katika majimbo matatu. Si ajabu Maliki na washirika wake wanamuunga mkono booma ubavuni na Irani….Nina furaha kwamba muovu, mwanaharamu Bush anaondoka. Sina shaka kwa hili. Lakini sitawapongeza kwa raisi wenu wa 44. Atakacho fanya ni kumalizia yale mazayonisti wenzake waliyoyaanza- Kuigawanya nchi yangu. </p>
<p>Ishieni jahanamu nyote pamoja na maraisi wenu</p></blockquote>
<p>Kusema kwamba <em>Neurotic Wife</em> <a href="http://neurotic-iraqi-wife.blogspot.com/2008/11/obama-era.html">anafurahishwa na uchaguzi wa Marekani</a> ni sawa kupunguza makali ya matamshi yake. Anaandika:</p>
<blockquote><p>Mabadiliko, mabadiliko, mabadiliko. Mabadiliko yako njiani. Mabadiliko kwa utawala wa kidhalimu wa Bush. Utawala wa Bush uliodanganya,uliolaghai, uliodhulumu dunia, na zaidi ya yote uliowadhulumu Wairaki&#8230; Kwangu mimi, hili si jambo linalohusu historia tu, hii inahusu mtu aliyeweza kuwashusha watu walioivunja nchi yangu. Ni konde kubwa kwa kila mtu alieangamiza Wairaki. Na kwangu mimi ni ushindi wa kutosha.</p>
<p>Nitapenda tu kumwambia Bwana Obama, usituangushe. Umetoka mbali, na kama Muiraki ninakutegemea. Usiziruhusu siasa chafu kukuvunjia ahadi zako… Nimejifunza mambo kadhaa katika maisha yangu, nayo ni katu kamwe usitegemee sana mambo kutoka kwa watu, lakini kwa hili nina matumaini. Nategemea mambo mengi toka kwa Obama. Na la kuangushwa SI mojawapo. Kwa wale wafuasi wenye siasa kali wa mlengo wa kulia, na kwenu nyote ambao hamtaki kukubali kuelewa Mmarekani mweusi anaweza kuwa raisi wenu, bahati mbaya. Ishi nalo…</p>
<p>Ni anga ya kupendeza leo. Anga ya KIBULUU. Mwanzo wa zama mpya. Zama za Obama… </p></blockquote>
<p>Na <em>Fatima</em> Mmarekani mwenye asili ya Iraki <a href="http://thoughtsfrombaghdad.blogspot.com/2008/11/now-for-some-deeper-thought.html">hatimaye anajivunia</a>. Anatanabaisha:</p>
<blockquote><p>Kwangu mimi, najivunia Marekani sasa hivi. Najivunia kwa kuyashinda mengi, kwa kutuonyesha yale ambayo inweza kuyafanya.<br />
Na kwangu mimi, nina matumaini kuwa Obama hatatuangusha. Nina matumaini ataliongoza taifa hili kufikia misingi ya sheria na usawa kwa wote, na kwamba atakaa mbali na vitendo vya kibabe, popote itakapokuwa. Natumaini hatakuwa mmoja wa wale maraisi.<br />
Na mwisho nampongeza John McCain kwa kazi yake na hotuba yake usiku wa jana. Ilikuwa ya kuiungwana, ninatumaini atapumzika baada ya miaka mingi ya utumishi. </p>
<p>GOOOBAMA! Idumu Haki, Usawa na haya yote mazuri katika katika hii dunia </p></blockquote>
<p><strong>Na mwisho</strong></p>
<p>Namalizia na ujumbe huu wa pongezi kutoka kwa Wairaki kwenda kwa wamarekani</p>
<p><a href="http://iraqimojo.blogspot.com/2008/11/guess-whos-coming-to-dinner.html"><em>Iraqi Mojo:</em></a></p>
<blockquote><p>Wamarekani wamechagua Muamerika mwenye asili ya Kiafrika aitwaye Barack Hussein Obama kuwa raisi wao. Mungu ibariki Marekani! </p></blockquote>
<p><a href="http://washingtonbureau.typepad.com/iraq/2008/11/obama.html"><em>Sahar:</em></a></p>
<blockquote><p>Nina furaha kwa Iraki? Sijui. Sijui nini kitatokea na ninaogopa.</p>
<p>Je ataondoa majeshi?<br />
Je atajali vilivyo na kufikia makubaliano mazuri - yaliyo sawa kwa watu wa Iraki?</p>
<p>Lakini pamoja na mashaka yangu yote, naionea raha Marekani - Mmetoka mbali. Mmlikuwa na ujasiri, na nia ya kumchagua mtu wa mabadiliko. Na kwa moyo wangu wote natumaini ataiweka marekani katika njia ya kupona.</p>
<p>Kuiona Marekani upya katika misingi ya uhuru na demokrasia, nguvu pole ambayo inapoza badala ya kuumiza, inaunganisha badala ya kugawanya - punde inshalla.<br />
Napenda kuwapongeza nyote. </p></blockquote>
<p><a href="http://iraqpundit.blogspot.com/2008/11/congratulations-to-obama.html"><em>Iraq Pundit:</em></a></p>
<blockquote><p>Kwa miaka kadhaa mara kwa mara nimejikuta nawatetea Wamarekani wanapokosolewa na wapinzani wao kama vile Wafaransa na Waarabu,ambao wanadai kuwa watu wa Marekani ni mazuzu wabaguzi hayawani. Nimejaribu kuongea na wakosoaji hao, lakini sikufika popote. Pengine kuchaguliwa kwa Baraka Obama kama raisi wa Marekani kutawafumbua jinsi gani walikosea… Ni wale tu wasio na mioyo ambao hawakusisimuka jana usiku wakati Obama alipotangazwa mshindi wa kiti cha urais… Kwa hiyo hongera kwa Barack Obama. Asitokee mtu na kusema hii sio nchi ya kustaajabisha.</p></blockquote>
<p>Na kutoka Baghdad, <a href="http://iraqi-roses.blogspot.com/2008/11/d-up-r-down.html"><em>Marshmallow26</em></a>:</p>
<blockquote><p>Hongereni wapendwa Wamarekani katika uchaguzi na kwa raisi mpya. Haijalishi matokeo yalivyokuja mna matumaini nasi tunatumaini raisi mpya ataleta mustakabali wenye mwangaza kwa Marekani na kwa Iraki.<br />
Zaidi ya Wamarekani milioni 130 wamepiga kura. Hii ni idadi kubwa.<br />
Kitu nilichokipenda kwa wamarekani ni kuwa hawakulipa kipaumbele suala la rangi katika kupiga kura, wengi wa watu weupe walimpigia kura Obama ambae ana nasaba ya Kiafrika, kwa sababu hawaamini katika rangi au dini lakini kanuni za nchi na watu wake…</p>
<p>kwa mara nyingine tena Mabrook :)</p></blockquote>
]]></content:encoded>
			<wfw:commentRss>http://sw.globalvoicesonline.org/2008/11/irakiobamaaaaa-huraaah-oyee/feed/</wfw:commentRss>
		<slash:comments>0</slash:comments>
		</item>
		<item>
		<title>Macho ya Kimataifa kwenye Uchaguzi wa Marekani</title>
		<link>http://sw.globalvoicesonline.org/2008/10/macho-ya-kimataifa-kwenye-uchaguzi-wa-marekani/</link>
		<comments>http://sw.globalvoicesonline.org/2008/10/macho-ya-kimataifa-kwenye-uchaguzi-wa-marekani/#comments</comments>
		<pubDate>Wed, 15 Oct 2008 13:09:23 +0000</pubDate>
		<dc:creator>Deogratias Simba</dc:creator>
				<category><![CDATA[Americas]]></category>
		<category><![CDATA[Arabic]]></category>
		<category><![CDATA[Canada]]></category>
		<category><![CDATA[China]]></category>
		<category><![CDATA[East Asia]]></category>
		<category><![CDATA[Elections]]></category>
		<category><![CDATA[English]]></category>
		<category><![CDATA[France]]></category>
		<category><![CDATA[General]]></category>
		<category><![CDATA[German]]></category>
		<category><![CDATA[Germany]]></category>
		<category><![CDATA[Governance]]></category>
		<category><![CDATA[Hindi]]></category>
		<category><![CDATA[International Relations]]></category>
		<category><![CDATA[Iran]]></category>
		<category><![CDATA[Iraq]]></category>
		<category><![CDATA[Israel]]></category>
		<category><![CDATA[LANGUAGES]]></category>
		<category><![CDATA[Law]]></category>
		<category><![CDATA[Middle East & North Africa]]></category>
		<category><![CDATA[Politics]]></category>
		<category><![CDATA[South Africa]]></category>
		<category><![CDATA[Sub-Saharan Africa]]></category>
		<category><![CDATA[Tanzania]]></category>
		<category><![CDATA[Travel]]></category>
		<category><![CDATA[U.S.A.]]></category>
		<category><![CDATA[United Kingdom]]></category>
		<category><![CDATA[Video]]></category>
		<category><![CDATA[War & Conflict]]></category>
		<category><![CDATA[Weblog]]></category>
		<category><![CDATA[Western Europe]]></category>

		<guid isPermaLink="false">http://sw.globalvoicesonline.org/?p=32</guid>
		<description><![CDATA[Kadiri uchaguzi wa Marekani unavyokaribia, ndivyo kadiri macho ya kimataifa yanavyozidi kuelekezwa katika sera za nje za taifa hilo na wagombea wake wakuu. Kazimiradi kama vile ile ya Collective Journalism inayofanywa na Current TV (Uandishi wa Habari wa Umma wa Current TV) na Global Voices' Voices Without Votes (Mradi wa Global Voices - Sauti Zisizo na Kura) zimechukua jukumu la kukusanya taarifa na kuzipa mtazamo wa kimataifa katika masuala ya ndani ya sehemu fulani tu ulimwenguni.]]></description>
			<content:encoded><![CDATA[<em>Ilichapwa kwanza na<a href="http://globalvoicesonline.org/author/juliana-rincon-parra/">Juliana Rincón Parra</a>  &middot; Imetafsiriwa na <a href='http://sw.globalvoicesonline.org/author/simbadeo/'>Deogratias Simba</a> &middot;  <a href='http://globalvoicesonline.org/2008/10/08/international-eye-on-the-us-elections/'>Angalia ujumbe mama</a></em> 
<br /><p>Kadiri uchaguzi wa Marekani unavyokaribia, ndivyo kadiri macho ya kimataifa yanavyozidi kuelekezwa katika sera za nje za taifa hilo na wagombea wakuu. Kazimiradi kama vile ile ya <a href="http://current.com/people/CJCollectiveWorks">Collective Journalism </a>inayofanywa na Current TV (Uandishi wa Habari wa Umma wa Current TV) na Global Voices&#39; <a href="http://voiceswithoutvotes.org/"><em>Voices Without Votes</em></a> (Mradi wa Global Voices - Sauti Zisizo na Kura) zimechukua jukumu la kukusanya taarifa na kuzipa mtazamo wa kimataifa katika masuala ya ndani ya sehemu fulani tu ulimwenguni.</p>
<p>Programu ya <a href="http://current.com/topics/511_collective_journalism">Collective Journalism </a>inayorushwa na Current TV imeanzisha mfululizo wa ripoti za video zinaoonyesha maoni ya watu wengine ulimwenguni kuhusu Marekani. Katika programu ya <a href="http://current.com/items/89378240_the_view_from_over_there">The View from Over There </a>(Mtazamo Kutoka Kwingineko) watu kutoka mataifa mbalimbali wanatoa maoni yao kuhusu sera ya nje, vita vya Iraki, hali tete juu ya Irani na kumtaja ni nani wangependa awe rais anayefuata wa Marekani. Mahojiano hayo ya video mara nyingine huwa katika lugha mbalimbali, lakini hewekewa tafsiri zake katika Kiingereza. </p>
<p><object classid="clsid:D27CDB6E-AE6D-11cf-96B8-444553540000" width="400" height="400"><param name="movie" value="http://current.com/e/89378240/en_US"></param><param name="wmode" value="transparent"></param><param name="allowfullscreen" value="true"></param><param name="allowscriptaccess" value="always"></param><embed src="http://current.com/e/89378240/en_US" type="application/x-shockwave-flash"  width="400" height="400" wmode="transparent" allowfullscreen="true" allowscriptaccess="always"></embed></object></p>
<p>Video hii pia inatumia vipande vya video vinavyoonyesha <a href="http://current.com/topics/32967338_election_2008">Uchaguzi wa Marekani 2008</a>, lakini hasa vile vinavyokazia mtazamo wa kigeni. Hili ni jambo moja ambalo Global Voices na Shirika la Reuters wamekuwa wakifanya kwa kitambo fulani kupitia programu ya <a href="http://voiceswithoutvotes.org/">Voices Without Votes</a>: kwa kukusanya maoni kutoka pande zote za ulimwengu juu ya uchaguzi wa Marekani. Kama kuna taarifa ungependa kutuma kwenye programu hii, unaweza kufanya hivyo <a href="http://voiceswithoutvotes.org/submit/">hapa</a>. </p>
<p>Programu ifuatayo ya Collective Journalism inayotolewa na Current TV katika kazi zake itakuwa ni mtazamo wa dunia nzima juu ya sera za Marekani za uhamiaji.</p>
]]></content:encoded>
			<wfw:commentRss>http://sw.globalvoicesonline.org/2008/10/macho-ya-kimataifa-kwenye-uchaguzi-wa-marekani/feed/</wfw:commentRss>
		<slash:comments>0</slash:comments>
		</item>
		<item>
		<title>Arabeyes: Rais wa Mauritania Aliyepinduliwa Katika mapinduzi ya Kijeshi</title>
		<link>http://sw.globalvoicesonline.org/2008/08/arabeyes-rais-wa-mauritania-aliyepinduliwa-katika-mapinduzi-ya-kijeshi/</link>
		<comments>http://sw.globalvoicesonline.org/2008/08/arabeyes-rais-wa-mauritania-aliyepinduliwa-katika-mapinduzi-ya-kijeshi/#comments</comments>
		<pubDate>Sun, 17 Aug 2008 23:10:33 +0000</pubDate>
		<dc:creator>charahani</dc:creator>
				<category><![CDATA[Algeria]]></category>
		<category><![CDATA[Arabic]]></category>
		<category><![CDATA[Breaking News]]></category>
		<category><![CDATA[Egypt]]></category>
		<category><![CDATA[English]]></category>
		<category><![CDATA[French]]></category>
		<category><![CDATA[Governance]]></category>
		<category><![CDATA[Iraq]]></category>
		<category><![CDATA[Mauritania]]></category>
		<category><![CDATA[Morocco]]></category>
		<category><![CDATA[Politics]]></category>
		<category><![CDATA[War & Conflict]]></category>
		<category><![CDATA[Western Sahara]]></category>

		<guid isPermaLink="false">http://sw.globalvoicesonline.org/?p=10</guid>
		<description><![CDATA[ &#183; Imetafsiriwa na charahani &#183;  Angalia ujumbe mama 

MAKAMANDA wa jeshi wamemuondoa madarakani Rais Sidi Ould Cheikh Abdallahi, rais wa kwanza kuchaguliwa katika uchaguzi huru katika miongo miwili, katika mapinduzi ya kijeshi yaliyofanywa Jumatano iliyopita baada ya mtafaruku wa kisiasa uliotokana na rais huyo kuwatimua kazi majenerali wanne wa ngazi za juu wa [...]]]></description>
			<content:encoded><![CDATA[<em> &middot; Imetafsiriwa na <a href='http://sw.globalvoicesonline.org/author/charahani/'>charahani</a> &middot;  <a href='http://globalvoicesonline.org/2008/08/06/arabeyes-mauritanian-president-ousted-in-military-coup-detat/'>Angalia ujumbe mama</a></em> 
<br /><p><img src='http://globalvoicesonline.org/wp-content/uploads/2008/08/457px-sidi_mohamed_ould_cheikh_abdallahi2.jpg' alt='' class='alignright' /><br />
MAKAMANDA wa jeshi <a href="http://www.abc.net.au/news/stories/2008/08/07/2326564.htm">wamemuondoa</a> madarakani <a href="http://www.answers.com/President%20Sidi%20Ould%20Cheikh%20Abdallahi">Rais Sidi Ould Cheikh Abdallahi</a>, rais <a href="http://www.answers.com/Mauritania">wa kwanza kuchaguliwa katika uchaguzi huru katika miongo miwili</a>, katika mapinduzi ya kijeshi yaliyofanywa Jumatano iliyopita baada ya mtafaruku wa kisiasa uliotokana na rais huyo kuwatimua kazi majenerali wanne wa ngazi za juu wa jeshi.  Makamanda wa jeshi walitangaza kuundwa kwa Baraza jipya la taifa na kiongozi wake, <a href="http://en.wikipedia.org/wiki/Mohamed_Ould_Abdel_Aziz">Jenerali Mohamed Ould Abdel Aziz </a>(mmoja kati ya majenerali wanne wa jeshi waliotimuliwa), kwenye radio na vituo vya televisheni vya serikali. Jenerali Abdel Aziz ni miongoni mwa walioshiriki <a href="http://en.wikipedia.org/wiki/2005_Mauritanian_coup_d%27%C3%A9tat">mapinduzi ya kijeshi nchini Mauritania mwaka 2005</a>.</p>
<p>Bloga kutoka Algeria <em>The Moor next Door</em> amekuwa <a href="http://themoornextdoor.wordpress.com/2008/08/06/the-president-will-not-be-taking-calls-today/">akiblogu</a> <a href="http://themoornextdoor.wordpress.com/2008/08/06/china-and-mauritania/">habari</a> <a href="http://themoornextdoor.wordpress.com/2008/08/06/coup-snapshots/">hii</a> <a href="http://themoornextdoor.wordpress.com/2008/08/06/developing-story/">kwa kina</a> <a href="http://themoornextdoor.wordpress.com/2008/08/06/summer-time-coups/">anaripoti</a>:</p>
<blockquote><p>Ninapozungumza na Wa-Mauritania wanaojua, baadhi yao walihisi kutokea kwa mapinduzi wakati wa kiangazi kama ilivyotokea, wakati wa kipupwe au isingeweza kutokea kabisa. Hisia zangu mara zote zilikuwa zikinielekeza kwamba mapinduzi haya yangefanyika majira ya kiangazi (Sijawahi kuandika bayana juu ya hili, lakini nimelielezea hili katika majadiliano na sikutaka kuchangia lolote kuhusiana na sakata hili. (1) kwa sababu Western Sahara Info. taarifa za kutoka Sahara Magharibi zilielezea kinaganaga na hakukuwa na haja ya kushindana ikiwa wewe ni mmoja wa mabloga wawili au watatu  unakuwa miongonimwa  wanaofuatilia sakata hili kwa karibu sana. (2) nilitaka kuhakikisha kwamba kama &#8216;ningetabiri&#39; jambo hili nisingekosea; Ningeweza kutabiri kuwa &#8216;Mwishoni mwa miezi ya Mei, Juni, Julai na Agosti Serikali ya Rais Sidi, isingelikuwapo tena&#39; na ningekuwa nimekosea; mimi si mtabiri wa hali ya hewa, na (3)  sijawahi kukutana na raia wa Mmauritania ambaye lolote jema la kumzungumza kuhusu Sidi, ukiachilia mbali uzuri wa wajihi wake.) Mojawapo ya mashinikizo yaliyomfanya Rais Sidi afanye alivyofanya ni kuwapo tishio la kuundwa tume huru ya kuchunguza mapesa ya mfuko wa maendeleo wa mkewe, tume ambayo ingemuweka hata yeye mwenyewe pabaya zaidi. Tume hiyo pia ingeufanya utawala wa Rais Sidi kituko kutokana na matumizi mabaya ya fedha za umma. Kwa mfano, nimeambiwa kuwa, safari zake za ndege za nje ziliigharimu serikali zaidi ya dola za Marekani mbili bilioni, kwa kukodisha ndege za kifahari yeye na familia yake na ujumbe wake pamoja na anasa zingine zisizokuwa za lazima. Kwa hakika alikuwa katika wakati mgumu: Ama angelazimika kujiuzulu (kwa mujibu wa Olmert) katika aibu kubwa au angelazimika kuvunja bunge na hivyo kuunda serikali yake upya, hali ambayo ingempeleka katika mapinduzi kama haya tuliyoyoyashuhudia, ambayo angalau imeficha aibu yake kisiasa. Alibanwa pande zote na alikuwa hana pa kutokea zaidi ya kukumbana na hatima yake.</p></blockquote>
<p><em>Western Sahara Info</em> amekuwa akiblogu mgogoro huu tokea ulipoanza, na leo <a href="http://w-sahara.blogspot.com/2008/08/military-coup-in-mauritania.html">ametuletea</a> habari za mapinduzi hayo ya kijeshi kama zinavyotokea dakika kwa dakika, pamoja na muhtasari wa unyambuzi: </p>
<blockquote><p>Uchambuzi wa harakaharaka, ambao naweza kuujutia: balaa kwa demokrasia ya Mauritania, kwa upande mmoja, (demokrasia) ambayo haikuwa na nafasi, lakini muhimu zaidi ni kuwa (mapinduzi haya) yamerudisha nyuma nafasi iliyokuwepo kwa maendeleo ya kisiasa. Ingawa, Rais Abdellahi na washirika wake si malaika, lakini Majenerali Ghazouani na Abdelaziz wanawakilisha kundi baya la kinyonyaji katika utawala wa Mauritania, kwa kukataa kuruhusu utawala wa kiraia kutulia madarakani kwa kuwatishia kung&#39;oa kabisa utawala wa kiraia hatimaye. Kama mapinduzi ya mwisho ya kijeshi yaliyotokea Agosti 2005, yangalieleweka na Jumuiya ya Kimataifa baada ya kung&#39;olewa kwa Rais Ould Tayaa, na hatimaye kupelekea mabadiliko makubwa, mapinduzi haya ya juzi yalikuwa tofauti saana. Kilichotokea mwaka 2005 ilikuwa kwamba madikteta wa kijeshi walioegemea katika ukabila waling&#39;atuliwa na nafasi ilijitokeza ikasimika badala yake utawala wa kiraia uliokuwa na muundo wa nusu-mabavu ambao uliruhusu desturi nyingi za kidemokrasia kwa muda mwingi zaidi, (utawala huo) ulishughulikia zaidi muwafaka wa kitaifa, urejeshwaji wa wakimbizi na maendeleo ya kiuchumi; ingawa siyo hema, lakini ilikuwa bora. Mabadiliko haya hivi sasa yanageuzwa. Wapinduaji - japokuwa wengine ni miongoni mwa wale waliofanya mwaka 2005 - - ni lazima walaumiwe na matokeo ya mapinduzi yabatilishwe kama inawezekana; Mauritania ilikuwa na fursa ya pekee kuweza kuvunja mzunguko huu usiokwisha, na sasa (fursa hiyo ya pekee) inaponyoka.</p></blockquote>
<p>Blogu ya <em>Roads To Iraq</em>, katikaujumbe wenye kichwa cha habari &#8220;Wamarekani walipanga mapinduzi nchini Mauritania,&#8221; <a href="http://www.roadstoiraq.com/2008/08/06/american-orchestrated-coup-in-mauritania/">inaripoti</a> habari hiyo vile vile: </p>
<blockquote><p>Mambo yanabadilika kwa kasi sana nchini Mauritania, imeanza na mapinduzi asubuhi hii, kwa kutoa &#8220;taarifa nambari moja&#8221; katika kituo cha televisheni cha Mauritania, Mkuu wa kituo hicho cha televisheni<br />
alibadilishwa sababu alikataa kushirikiana na mkuu wa jeshi aliyeandaa mapinduzi na kumtangaza mtawala mpya wa kijeshi.</p></blockquote>
<p>Huko Misri, <em>Bella</em> [Ar]<a href="http://afkaar-bella.blogspot.com/2008/08/blog-post.html">anasema</a> kilichotokea Mauritania kimedhihirisha kuwa Waarabu hawakupangwa kwa demokrasia.</p>
<blockquote><p>Inaonekana demokrasia haikuumbwa kwa watu kama sisi - ambao hatuwezi kupumua nje ya tawala za kijeshi.</p></blockquote>
<p>Baada ya kutupa historia fupi ya demokrasia changa ya Mauritania <em>Bella</em> anaandika: </p>
<blockquote><p>Kwa njia hii, Mauritania, ambayo ilikuwa ianze kuvuna matunda ya demokrasia katika msukumo wa kiasisi ambao eneo lote la mataifa ya jirani yalikuwa yanaungalia kwa shauku, mambo yamerejea kule yalikotoka kiasili, na wanajeshi wakaingilia kati na mapinduzi kutokea.</p></blockquote>
<p>Bloga wa Kuwaiti <em>Wild Il Deera</em> <a href="http://wildildeera.blogspot.com/2008/08/blog-post_06.html">anahoji maswali machache </a>kuhusiana na mapinduzi haya. Anauliza:</p>
<blockquote><p>Jumuiya ya Kiarabu ina msimamo gani kuhusu viongozi wa mapinduzi haya?<br />
Hivi huyu kiongozi wa Mauritania hakuchaguliwa na watu wake?<br />
Hivi inawezekanaje kundi la kisiasa, kama Jumuiya ya Kiarabu, ambayo inataka kuheshimiwa katika jamii ya Kiarabu na katika ulingo wa kimataifa ikaruhusu mapinduzi kama haya kufanyika katika moja ya mataifa wanachama wake?</p></blockquote>
<p>Bloga maarufu nchini Morocco Larbi [Fr] alipachika kiungo cha makala ya ya habari, <a href="http://www.larbi.org/post/2008/08/Mauritanie%3A-Coup-d-Etat-en-cours">kisemacho</a>: </p>
<blockquote><p>Unaweza kusema: Afrika ni bara lililolaaniwa!</p></blockquote>
<p>Habari yake hiyo imepata maoni mengi. <em>Citoyen</em> anatoa maoni kwamba:</p>
<blockquote><p>Ni kweli mapinduzi hayatabiriki Afrika… Nashangaa, ingawa, kama kwa mara nyingine tena, Mashirika ya Moroko yamekatizwa kama yalivyokuwa mwezi Ogasti 2005? </p></blockquote>
<p>Mwishoni KABOBfest, ambaye huwa anaingiza vichekesho katika kila hali, <a href="http://www.kabobfest.com/2008/08/kickin-it-old-skool.html">anatoa maoni</a> yenye mzaha: </p>
<blockquote><p>Wakati utamaduni wa mapinduzi katika mataifa mengi ni utamaduni uliopitwa na wakati (kama vile Syria hakujapata kutokea mapinduzi kwa miongo kadhaa sasa) Baadhi ya mataifa yanapendelea mitindo ya kizamani,  rejea pale ambapo ianonekana palikuwa na mapinduzi kama juma moja lililopita sehemu fulani hapa duniani. Wakati Mauritania siyo Fiji, wanadumisha utamaduni usio na maana wa mapinduzi katika dunia ya Waarabu.</p></blockquote>
<p>Blogu ya Arabdemocracy pia anayo <a href="http://www.arabdemocracy.com/2008/08/mauritaniaobituary-for-young-democracy.html">taarifa ya maombolezo</a> ya iliyokuwa demokrasia changa.</p>
<p><em>Picha ya hapo juu ni ya Sidi Mohamed Ould Cheikh Abdallahi iliyopigwa na <a href="http://www.agenciabrasil.gov.br/media/imagens/2007/09/27/1254MCMauritania1.jpg/view">Marcello Casal Jr./Abr</a> (Septemba 2007)</em></p>
]]></content:encoded>
			<wfw:commentRss>http://sw.globalvoicesonline.org/2008/08/arabeyes-rais-wa-mauritania-aliyepinduliwa-katika-mapinduzi-ya-kijeshi/feed/</wfw:commentRss>
		<slash:comments>0</slash:comments>
		</item>
	</channel>
</rss>
