<?xml version="1.0" encoding="UTF-8"?>
<rss version="2.0"
	xmlns:content="http://purl.org/rss/1.0/modules/content/"
	xmlns:wfw="http://wellformedweb.org/CommentAPI/"
	xmlns:dc="http://purl.org/dc/elements/1.1/"
	xmlns:atom="http://www.w3.org/2005/Atom"
	xmlns:sy="http://purl.org/rss/1.0/modules/syndication/"
	xmlns:slash="http://purl.org/rss/1.0/modules/slash/"
	>

<channel>
	<title>Global Voices in Swahili &#187; Egypt</title>
	<atom:link href="http://sw.globalvoicesonline.org/category/world/middle-east-north-africa/egypt/feed/" rel="self" type="application/rss+xml" />
	<link>http://sw.globalvoicesonline.org</link>
	<description>Dunia inaongea, je unasikiliza?</description>
	<lastBuildDate>Wed, 02 Dec 2009 12:35:07 +0000</lastBuildDate>
	<generator>http://wordpress.org/?v=2.8.4</generator>
	<language>en</language>
	<sy:updatePeriod>hourly</sy:updatePeriod>
	<sy:updateFrequency>1</sy:updateFrequency>
			<item>
		<title>Misri na Aljeria: Pambano la Twita</title>
		<link>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/11/misri-na-aljeria-pambano-la-twita/</link>
		<comments>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/11/misri-na-aljeria-pambano-la-twita/#comments</comments>
		<pubDate>Mon, 16 Nov 2009 12:04:35 +0000</pubDate>
		<dc:creator>j nambiza tungaraza</dc:creator>
				<category><![CDATA[Algeria]]></category>
		<category><![CDATA[Egypt]]></category>
		<category><![CDATA[International Relations]]></category>
		<category><![CDATA[Media]]></category>
		<category><![CDATA[Middle East & North Africa]]></category>
		<category><![CDATA[Sport]]></category>
		<category><![CDATA[Weblog]]></category>

		<guid isPermaLink="false">http://sw.globalvoicesonline.org/?p=673</guid>
		<description><![CDATA[Katika sehemu nyingi duniani, hakuna linalounganisha zaidi – au wakati mwingine kutenganisha – zaidi ya pambano la mpira wa miguu. Washabiki wa Misri na Aljeria, katika ulimwengu wote wa Waarabu na zaidi, walilidhihirisha hilo Jumamosi hii wakati timu zao zilipokwenda sambamba wakati wa kuwania kuingia fainali za Kombe la Dunia huko Afrika Kusini. ]]></description>
			<content:encoded><![CDATA[<em>Ilichapwa kwanza na<a href="http://globalvoicesonline.org/author/jillian-york/">Jillian C. York</a>  &middot; Imetafsiriwa na <a href='http://sw.globalvoicesonline.org/author/j-nambiza-tungaraza/'>j nambiza tungaraza</a> &middot;  <a href='http://globalvoicesonline.org/2009/11/15/egypt-vs-algeria-the-twitter-match/'>Angalia ujumbe mama</a></em> 
<br /><p>Katika sehemu nyingi duniani, hakuna linalounganisha zaidi – au wakati mwingine kutenganisha – zaidi ya pambano la mpira wa miguu. Washabiki wa Misri na Aljeria, katika ulimwengu wote wa Waarabu na zaidi, walilidhihirisha hilo Jumamosi hii wakati timu zao zilipokwenda sambamba wakati wa kuwania kuingia fainali za Kombe la Dunia huko Afrika Kusini. Wakati vihoro vilipanda juu huko mjini Cairo, pia vilikuwa hai na katika hali nzuri kwenye uwanja yakini mtandaoni, pamoja na kwenye <a href="http://twitter.com/">Twita</a>, ambako watumiaji walitaarifu kuwa skrini zao zilijaa hisia za mpira. Mtumiaji wa Twita <em><a href="http://twitter.com/mbaa">mbaa</a></em> alituma picha ya skrini yake, ambayo ilifurika mazungumzo ya pambano hilo:</p>
<p><img alt="" src="http://globalvoicesonline.org/wp-content/uploads/2009/11/mbaa2.jpg" title="mbaa" class="aligncenter" width="535" height="410" /></p>
<p>Ujumbe wa twita kutoka kwa Mmisri <em><a href="http://twitter.com/embee">embee</a></em> <a href="http://twitter.com/embee/status/5718935256">ulionyesha</a> ushabiki uliokithiri wa baadhi ya washabiki:</p>
<p><img alt="" src="http://globalvoicesonline.org/wp-content/uploads/2009/11/embee-status-5718935256-300x113.PNG" title="embee-status-5718935256" class="aligncenter" width="300" height="113" /></p>
<p>Baadhi ya taarifa zinadai kuwa tiketi zote zimekwishauzwa hivi sasa! Wakati huo huo, Mmisri <em><a href="http://twitter.com/norayounis">NoraYounis</a></em> <a href="http://twitter.com/norayounis/status/5718108814">alielezea kutoamini</a> kwake katika nguvu ya kuunganisha ya mpira wa miguu kwa Wamisri:</p>
<p><img alt="" src="http://globalvoicesonline.org/wp-content/uploads/2009/11/NoraYounis-status-5718108814-300x152.PNG" title="NoraYounis-status-5718108814" class="aligncenter" width="300" height="152" /></p>
<p><a href="http://twitter.com/nohaatef/status/5718339271">Ujumbe wa twita</a> wa Mmisri <em><a href="http://twitter.com/nohaatef">NohaAtef</a></em>, kwa upande mwingine, ulionyesha vitu vinavyoweza kuinua mioyo katika mpira wa miguu:</p>
<p><img alt="" src="http://globalvoicesonline.org/wp-content/uploads/2009/11/NohaAtef-status-5718339271-300x151.PNG" title="NohaAtef-status-5718339271" class="aligncenter" width="300" height="151" /></p>
<p>Katika mifano mingi, mpira wa miguu ulichimbua ushindani wa kitaifa. Waaljeria na Wamisri walikwenda kichwa kwa kichwa kwenye twita wakati pambano likiendelea. Mmisri <em><a href="http://twitter.com/sandmonkey">Sandmonkey</a></em> <a href="http://twitter.com/sandmonkey/status/5714575409">aling’aka</a>: </p>
<p><img alt="" src="http://globalvoicesonline.org/wp-content/uploads/2009/11/Sandmonkey-status-5714575409-300x86.PNG" title="Sandmonkey-status-5714575409" class="aligncenter" width="300" height="86" /></p>
<p>Mualjeria-Mmarekani <em><a href="http://twitter.com/themoornextdoor">themoornextdoor</a></em> alijibu mapigo <a href="http://twitter.com/themoornextdoor/status/5715301341">akitania</a>:</p>
<p><img alt="" src="http://globalvoicesonline.org/wp-content/uploads/2009/11/themoornextdoor-status-5715301341-300x124.PNG" title="themoornextdoor-status-5715301341" class="aligncenter" width="300" height="124" /></p>
<p>Mwishowe, Mualjeria <em><a href="http://twitter.com/reemba">reemba</a></em> <a href="http://twitter.com/reemba/status/5717755317">alitukumbusha</a> kuwa mambo bado hayajaisha mpaka yaishe:</p>
<p><img alt="" src="http://globalvoicesonline.org/wp-content/uploads/2009/11/reemba-status-5717755317-300x147.PNG" title="reemba-status-5717755317" class="aligncenter" width="300" height="147" /></p>
]]></content:encoded>
			<wfw:commentRss>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/11/misri-na-aljeria-pambano-la-twita/feed/</wfw:commentRss>
		<slash:comments>0</slash:comments>
		</item>
		<item>
		<title>Misri: Haki ya Kijerumani kwa Marwa El Sherbini</title>
		<link>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/11/misri-haki-ya-kijerumani-kwa-marwa-el-sherbini/</link>
		<comments>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/11/misri-haki-ya-kijerumani-kwa-marwa-el-sherbini/#comments</comments>
		<pubDate>Mon, 16 Nov 2009 11:06:45 +0000</pubDate>
		<dc:creator>j nambiza tungaraza</dc:creator>
				<category><![CDATA[Arabic]]></category>
		<category><![CDATA[Breaking News]]></category>
		<category><![CDATA[Egypt]]></category>
		<category><![CDATA[English]]></category>
		<category><![CDATA[Ethnicity]]></category>
		<category><![CDATA[Germany]]></category>
		<category><![CDATA[International Relations]]></category>
		<category><![CDATA[Law]]></category>
		<category><![CDATA[Middle East & North Africa]]></category>
		<category><![CDATA[Politics]]></category>
		<category><![CDATA[Racism]]></category>
		<category><![CDATA[Weblog]]></category>

		<guid isPermaLink="false">http://sw.globalvoicesonline.org/?p=669</guid>
		<description><![CDATA[Muuaji wa Marwa El-Sherbini, mwanamke wa Kimisri ambaye alichomwa visu mpaka kufa na muhamiaji mwenye asili ya Urusi na Ujerumani, Alex Wiens,  ndani ya mahakama huko Ujerumani, amehukumiwa kifungo cha maisha, bila uwezekano wa kuachiwa mapema. Haki hatimaye imetolewa na muuaji anaadhibiwa, wanasema wanablogu wa Misri.]]></description>
			<content:encoded><![CDATA[<em>Ilichapwa kwanza na<a href="http://globalvoicesonline.org/author/tarek-amr/">Tarek Amr</a>  &middot; Imetafsiriwa na <a href='http://sw.globalvoicesonline.org/author/j-nambiza-tungaraza/'>j nambiza tungaraza</a> &middot;  <a href='http://globalvoicesonline.org/2009/11/15/egypt-german-justice-for-marwa-el-sherbini/'>Angalia ujumbe mama</a></em> 
<br /><p>Hatimaye, haki imetolewa katika <a href="http://globalvoicesonline.org/2009/07/06/egyptian-woman-killed-in-german-court-for-being-veiled/">shauri la Marwa El-Sherbini</a>, mwanamke wa Kimisri aliyeuwawa kwa kuchomwa visu na muhamiaji mwenye asili ya Urusi-na-Ujerumani ndani ya mahakama huko Ujerumani. Baada ya karibu miezi mine na nusu, Alex Wiens amehukumiwa kifungo cha maisha, bila ya matarajio ya kuachiwa mapema kabla ya kifungo kumalizika.</p>
<p><em>Bikya Misr</em> <a href="http://bikyamasr.com/?p=5678">ameandika kuhusu kesi hiyo</a>:</p>
<blockquote><p>Baada ya karibu miezi mine na nusu, mkasa wa Marwa el-Sherbini umefikia hitimisho la namna Fulani baada ya mahakama ya Ujerumani kumhukumu kifungo cha maisha bila uwezekano wa kuachiwa mapema mtu aliyemchoma visu “shahidi aliyevaa shela” mara 17 ndani ya mahakama mnamo mwezi Julai. Wamisri, Waarabu na kadhalika Wajerumani wameikaribisha hukumu hiyo na wanatumaini kuwa Ulaya na Mashariki ya Kati zitaanza kupona majeraha ya mauaji hayo na kusonga mbele “kuelekea mustakabali bora zaidi.”</p></blockquote>
<p><em>Hicham Maged </em><a href="http://blog.hichamaged.net/justice-and-stereotype/">ameandika jinsi alivyoridhika na hukumu, na kuwa ana imani na mfumo wa sheria wa Ujerumani</a>:</p>
<blockquote><p>Hakimu alikuwa anazitambua mbinu kadhaa za timu ya utetezi ya muuaji na hapa ninanukuu maneno kwa mujibu wa makala hii: “Aliua… si kutokana na hofu bali kutokana na kisasi. Kwa makusudi alitumia nia njema na udhaifu wake (marehemu). “Ninakubaliana na hili na usisahau kuwa alijaribu pia kumuua mume wake.<br />
Ninafarijika kuwa chumba cha mahakama ambamo usaliti huo ulitokea kimeoshwa kwa mikono na kimaadili kwa kutumia haki. Baada ya hayo, imani yangu kwa mfumo wa sheria wa Ujerumani haupaswi kuelezwa kwani kosa hili lilikuwa ni la kustusha kwetu sote na si kwa Wajerumani pekee. Kwa hivyo basi, ni leo hii Marwa na mwanawe ambaye alikuwa hajazaliwa wanaweza kupumzika kwa amani baada ya malipo kwa muuaji. </p></blockquote>
<p><em>Zeinobia</em> aliifurahia hukumu, naye pia <a href="http://egyptianchronicles.blogspot.com/2009/11/this-is-fair-rule-not-political-rule.html">aliandika kuwajibu wale ambao waliamini kuwa hukumu ile ilikuwa ni ya kisiasa, na kuwa mahakama ya Ujerumani ilitoa hukumu inayomnufaisha Marwa ili kuwaridhisha Wamisri na Waarabu</a>:</p>
<blockquote><p>Sasa nataka kusema jambo, baadhi ya wabaguzi “na si wachache duniani hivi sasa”, watasema kwamba uamuzi huu ni wa kisiasa; ambao mahakama ilibidi iuchukue ili kushinda mioyo na fikra za Waislamu duniani na kuokoa maslahi ya Ujerumani katika ulimwengu wa Kiislamu.<br />
Naam, kwa heshima yangu yote nilikwishasema hapo awali na nitasema tena; usimfikirie Marwa kama mwanamke wa Kiislamu; mfikirie kama mwanamke mjamzito na mama ambaye kwa yakini alichomwa visu mara 18 mbele ya mwanawe mdogo wa kiume. Aliua roho mbili, roho zisizo na hatia kwa sababu ya chuki isiyoona pamoja na ubaguzi. Anastahili kuwa jela kwa maisha yake yote yaliyobaki kwa kutoa maisha ya roho zisizo na hatia na kuota uhai wa mama kutoka kwa mwanawe.</p></blockquote>
<p><em>Aam Mina</em> kwa upande mwingine aliandika makala, ya <a href="http://voice-of-egypt.blogspot.com/2009/11/blog-post_12.html">kuwakebehi wale wanaoamini katika nadharia za njama na waliokuwa wakitarajia Wajerumani kufanya uamuzi utakaompendelea muuaji</a>:</p>
<blockquote><p>
مش عارف ليه من ساعة الجكم مش سامعين صوت الناس اللي فلقتنا وقت الحادث عن عنصرية الألمان و كرههم للعرب و المسلمين و عن إن القضية هتتظبط و الراجل هياخدله سنة أو سنتين و خلاص و انه الحل الوحيد هو الجهاد و محاربة الغرب الصهيوني الفاسد العلماني الكافر </p></blockquote>
<div class="translation">Sijui kwa nini, tangu kutangazwa kwa uamuzi, sijamsikia yeyote kati ya wale waliokuwa wakiongelea juu Wajerumani na jinsi walivyo wabaguzi, na kuwa wanawachukia Waarabu na Waislamu. Pia walidai kuwa mahakama ingetoa uamuzi uanompendelea muuaji na kuwa atafungwa kwa mwaka mmoja au miwili tu, na kuwa tumaini letu pekee ni kutangaza vita takatifu dhidi ya utawala usio na dini, uliooza, Wakizayonisti, na Wamagharibi makafiri.</div>
<p>Kisha aliandika kuhusu mafundisho mengi ambayo tunapaswa kujifunza kutokana na tukio hili:</p>
<blockquote><p>
دي بعض الدروس المستفادة من الغرب الكافر<br />
١- سرعة العدالة.. جريمة القتل تمت في يوليو ٢٠٠٩ يعني من حوالي ٤ شهور.. ماحتاجناش ٢٠ سنة دراسة للقضية زي ما بيحصل عندنا<br />
٢- عدالة الحكم.. تم تطبيق أقصي عقوبة علي المتهم و هي المؤبد (عقوبة الإعدام غير معمول بيها في القانون الألماني) من دون التمييز ما بين مسلم و مسيحي أو عربي و ألماني.. الكل سواسية أمام القانون </p></blockquote>
<div class="translation">Haya ni baadhi ya mafundisho tunayotakiwa kujifunza kutoka kwa makafiri wa Magharibi:<br />
1.	Toeni haki haraka: Mauaji yalitokea mwezi Julai 2009, yaani, takriban miezi 4 iliyopita, na haikuwachukua miaka 20 kulichambua shauri, kama ambavyo hufanyika hapa.<br />
2.	Haki yenyewe: Muuaji amepokea adhabu ya juu – adhabu ya kifo haimo kwenye sheria ya ujerumani – bila ya kubagua kati ya Muislamu, Mkiristu, Mwarabu au Mjerumani. Wote wako sawa mbele ya sheria. </div>
<p>Na mwisho, <em><a href="http://blog.hichamaged.net/justice-and-stereotype/">Hicham Maged</a></em> aliandika:</p>
<blockquote><p>Kilichotokea kwa Marwa kiwe ni mbiu ya ‘kuamsha’ ambayo itawafanya watu wafanye kazi ili kufanikisha, kwa kukosoa vitendo vilivyozidi mipaka ambavyo vinafanywa dhidi ya watu kutokana na imani zao au rangi na kuelewa tofauti zetu na hii inamaanisha kuzizima imani potofu kutoka kwa yeyote dhidi ya yeyote.</p></blockquote>
]]></content:encoded>
			<wfw:commentRss>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/11/misri-haki-ya-kijerumani-kwa-marwa-el-sherbini/feed/</wfw:commentRss>
		<slash:comments>0</slash:comments>
		</item>
		<item>
		<title>Algeria-Misri: Ugomvi Juu ya pambano la Mpira kwenye Mtandao</title>
		<link>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/11/algeria-misri-ugomvi-juu-ya-pambano-la-mpira-kwenye-mtandao/</link>
		<comments>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/11/algeria-misri-ugomvi-juu-ya-pambano-la-mpira-kwenye-mtandao/#comments</comments>
		<pubDate>Sun, 15 Nov 2009 10:52:06 +0000</pubDate>
		<dc:creator>j nambiza tungaraza</dc:creator>
				<category><![CDATA[Algeria]]></category>
		<category><![CDATA[Arabic]]></category>
		<category><![CDATA[Egypt]]></category>
		<category><![CDATA[English]]></category>
		<category><![CDATA[French]]></category>
		<category><![CDATA[Middle East & North Africa]]></category>
		<category><![CDATA[Photos]]></category>
		<category><![CDATA[Sport]]></category>
		<category><![CDATA[Video]]></category>
		<category><![CDATA[Weblog]]></category>

		<guid isPermaLink="false">http://sw.globalvoicesonline.org/?p=659</guid>
		<description><![CDATA[Hali tete kati ya mashabiki wa mpira wa miguu wa Misri na Algeria inazidi kukua kabla ya pambano litakalofanyika mjini Cairo tarehe 14 Novemba. Mchuano huo utaamua ipi kati ya timu hizo zitafaulu kwenda kwenye Kombe la Dunia la FIFA Afrika ya kusini mwaka ujao. Misri inahitaji japo ushindi wa magoli mawili ili kulazimisha mchezo wa kukata shauri katika uwanja wa nchi nyingine ambapo Algeria, ambayo imeshindwa kufaulu kwenda kombe la dunia tangu 1986, itapambana ili kutunza nafasi yake ya sasa ya kuongoza katika kundi la wanaogombania nafasi ya kufaulu. Wakati wa kuelekea pambano la Jumamosi, mashabiki washindani wamekuwa wakijiandaa nje ya mtandao wa intaneti, kadhalika katika malumbano makali ya mtandaoni, ambayo yamekua na kugeuka “vita-vya-mikwara-kwenye-mtandao” ]]></description>
			<content:encoded><![CDATA[<em>Ilichapwa kwanza na<a href="http://globalvoicesonline.org/author/hisham/">Hisham</a>  &middot; Imetafsiriwa na <a href='http://sw.globalvoicesonline.org/author/j-nambiza-tungaraza/'>j nambiza tungaraza</a> &middot;  <a href='http://globalvoicesonline.org/2009/11/12/algeria-egypt-online-feud-over-football-match/'>Angalia ujumbe mama</a></em> 
<br /><p>Hali tete kati ya mashabiki wa mpira wa miguu wa Misri na Algeria inazidi kukua kabla ya pambano litakalofanyika mjini Cairo tarehe 14 Novemba. Mchuano huo utaamua ipi kati ya timu hizo zitafaulu kwenda kwenye Kombe la Dunia la FIFA Afrika ya kusini mwaka ujao. Misri inahitaji japo ushindi wa magoli mawili ili kulazimisha mchezo wa kukata shauri katika uwanja wa nchi nyingine ambapo Algeria, ambayo imeshindwa kufaulu kwenda kombe la dunia tangu 1986, itapambana ili kutunza nafasi yake ya sasa ya kuongoza katika <a href="http://www.fifa.com/worldcup/preliminaries/africa/standings/group=252301/index.html">kundi la wanaogombania nafasi ya kufaulu</a>. Wakati wa kuelekea pambano la Jumamosi, mashabiki washindani wamekuwa wakijiandaa nje ya mtandao wa intaneti, kadhalika katika malumbano makali ya mtandaoni, ambayo yamekua na kugeuka “vita-vya-mikwara-kwenye-mtandao” </p>
<p>Mwanablogu wa Algeria <em><a href="http://adelife.wordpress.com/2009/11/10/football-avant-la-bataille-du-caire%E2%80%A6-une-guerre-pas-tres-nette/">Adel</a> </em>[Fr] anatoa muhtasari wa mlolongo wa matukio ambayo yamesababisha mzozo. Anaandika:</p>
<blockquote><p>Ce n’est pas sur le carré vert que le match a commencé à se jouer mais sur la toile. En attendant l’entrée des 22 joueurs sur la pelouse du fameux Cairo Stadium, la rencontre a débuté de manière assez peu banale entre les «Facebookeurs» (membres du réseau Facebook) algériens et égyptiens. Tout a commencé par de simples discussions dans les forums avant que cela ne prenne de l’ampleur. Voulant montrer leur savoir-faire dans la retouche d’image, les Egyptiens ont été les premiers à ouvrir les hostilités en publiant des photos «anti-algérien».</p>
<p>Les Egyptiens voulaient expliquer à travers un tel acte que leurs joueurs sont «très forts» et qu’ils sont en mesure d’écraser l’équipe nationale algérienne. Cela donna le top à une guerre d’un genre particulier. La guerre des images et des parodies.</p></blockquote>
<div class="translation">Inaelekea kuwa mechi imeshaanza mtandaoni, mbali na uwanja wa mpira. Kabla ya wachezaji 22 kuingia uwanja maarufu wa Cairo, pambano kali limeanza katik ya watumiaji wa Facebook wa Kialgeria na Kimisri. Yote yalianza na majadiliano ya kirafiki katika majukwaa ya mtandaoni, kabla ya mambo kuzidi kipimo. Wakitaka kuonyesha utaalamu wao wa kuhariri picha, Wamisri ndio walikuwa wa kwanza kuanzisha uhasama kwa kuchapisha picha “zinazoipinga Algeria”.</p>
<p>Wamisri walitaka kuonyesha kuwa wachezaji wao ndio “wenye nguvu” na kwamba wana uwezo wa kuiponda timu ya taifa ya Algeria. Hii ilitoa ishara ya kuanza vita ya namna ya pekee. Vita ya picha na utani. </p></div>
<p>Video, zilizoiga picha zilichokuliwa kutoka kwenye filamu maarufu za Hollywood, zilifurika kwenye YouTube, na kuweka ugomvi huu katika ngazi ya…..</p>
<p>Katika video inayofuata [Ar], iliyowekwa na <em><a href="http://www.youtube.com/user/hakemvoip">hakemvoip</a></em> [Fr], Mel Gibson ni <em>Rabah Wallace</em> (Katika filamu ya Braveheart), jemedari wa vita wa Kialgeria ambaye anajaribu kuhamasisha wapiganaji kabla ya vita inayotarajiwa:</p>
<p><object width="425" height="344"><param name="movie" value="http://www.youtube.com/v/yCtAQ_9XMAE&#038;color1=0xb1b1b1&#038;color2=0xcfcfcf&#038;hl=en&#038;feature=player_embedded&#038;fs=1"></param><param name="allowFullScreen" value="true"></param><param name="allowScriptAccess" value="always"></param><embed src="http://www.youtube.com/v/yCtAQ_9XMAE&#038;color1=0xb1b1b1&#038;color2=0xcfcfcf&#038;hl=en&#038;feature=player_embedded&#038;fs=1" type="application/x-shockwave-flash" allowfullscreen="true" allowScriptAccess="always" width="425" height="344"></embed></object></p>
<p>Katika video hii, Mmisri <em><a href="http://www.youtube.com/user/ulyesis">ulyesis</a></em> anawakaribisha mashabiki wa Algeria katika kile anachokiita “jehanam” ndani ya jiji la Cairo:</p>
<p><object width="425" height="344"><param name="movie" value="http://www.youtube.com/v/OZOgyioZxFs&#038;color1=0xb1b1b1&#038;color2=0xcfcfcf&#038;hl=en&#038;feature=player_embedded&#038;fs=1"></param><param name="allowFullScreen" value="true"></param><param name="allowScriptAccess" value="always"></param><embed src="http://www.youtube.com/v/OZOgyioZxFs&#038;color1=0xb1b1b1&#038;color2=0xcfcfcf&#038;hl=en&#038;feature=player_embedded&#038;fs=1" type="application/x-shockwave-flash" allowfullscreen="true" allowScriptAccess="always" width="425" height="344"></embed></object></p>
<p>Mwanablogu <em><a href="http://www.gemyhood.com/2009/11/blog-post_11.html">GEMYOoOD</a> </em>[Ar] katuma picha ya maelfu ya mashabiki wa Misri waliopanga foleni katika sehemu tofauti za Cairo, wakitarajia kupata tiketi kwa ajili ya mechi. <a href="http://www.gemyhood.com/2009/11/blog-post_11.html">Anachapisha</a> picha za mikusanyiko hiyo ya watu:</p>
<p><img alt="" src="http://globalvoicesonline.org/wp-content/uploads/2009/11/Egyptian-Fans-300x225.jpg" title="Egyptian Fans" class="aligncenter" width="300" height="225" /></p>
<p><img alt="" src="http://globalvoicesonline.org/wp-content/uploads/2009/11/Egyptian-Fans2-300x225.jpg" title="Egyptian Fans" class="aligncenter" width="300" height="225" /></p>
<p><em><a href="http://www.gemyhood.com/2009/11/blog-post_11.html">GEMYHOoOD</a></em> pia anatuma baadhi ya maoni ya watu wanaoshuhudia:</p>
<blockquote><p>انا خدت اجازة اليوم ونزلت من الصبح لنادي الصيد الساعة 8 الصبح وللاسف لقيت موت ناس وزحمة وطابور فيه حوالي 3000 واحد ودفع وشتيمة والناس كل شوية بتزيد ومش عارف اقف من الزق والعرق بجد مهزلة</p></blockquote>
<div class="translation">Nilichukua ruksa ya siku ili nije kwenye klabu saa 2 asubuhi [kununua tiketi]. Kwa masikitiko nilikuta kundi kubwa la watu na foleni kubwa ya kadri ya watu 3000, huku watu wakisukumana na kutukanana. Sikuweza kusogea. Nilikwama. Nikafikiri, hiini aibu.</div>
<p>Basi rasmi la timu ya mpira wa miguu ya Algeria, ambalo liliwasili mjini Cairo tarehe 12 Novemba, inadaiwa kuwa lilishambuliwa na mashabiki, kama video inayofuata, iliyotumwa katika YouTube na <em><a href="http://www.youtube.com/user/wmcvideotv">Vidéos Mouloudia Club d&#39;Oran</a></em>, inavoelekea kuonyesha:</p>
<p><object width="425" height="344"><param name="movie" value="http://www.youtube.com/v/XNbZqBTvWBw&#038;color1=0xb1b1b1&#038;color2=0xcfcfcf&#038;hl=en_US&#038;feature=player_embedded&#038;fs=1"></param><param name="allowFullScreen" value="true"></param><param name="allowScriptAccess" value="always"></param><embed src="http://www.youtube.com/v/XNbZqBTvWBw&#038;color1=0xb1b1b1&#038;color2=0xcfcfcf&#038;hl=en_US&#038;feature=player_embedded&#038;fs=1" type="application/x-shockwave-flash" allowfullscreen="true" allowScriptAccess="always" width="425" height="344"></embed></object></p>
<p>Baraza linalodhibiti mpira wa miguu duniani <a href="http://www.fifa.com/">FIFA</a>, lilihisi umuhimu wa kutoa onyo kwa vyama vya mpira wa miguu vya Algeria na Misri, likiwakumbusha wote kuwa “mashindano ya awali kwa ajili ya kombe la Dunia 2010 yamalizike kama yalivyoanza, katika moyo wa mchezo wenye haki ulio na ushirikiano unaohitajika kutoka kwa washiriki wote.”<br />
<img alt="" src="http://globalvoicesonline.org/wp-content/uploads/2009/11/One-People.jpg" title="One People, One Language One Goal" class="alignright" width="200" height="500" /><br />
Tovuti, <a href="http://www.algerieegypte.com/">Algerie Egypte Match</a> [Ar, Fr], inayoandika kuhusu tukio hili na kufuatilia kila namna ya habari inayohusiana na mechi, iliundwa na washabiki wa Algeria.</p>
<p>Katika hali hii ya ushindani mkali, baadhi ya watu wameunda <a href="http://www.facebook.com/group.php?v=wall&#038;gid=167702883826">kundi</a> kwenye tovuti ya mtandao wa kijamii Facebook, wakiomba hisia mbaya zaidi. <em>Laama Bouchema</em> katuma ujumbe katika ukuta wa kundi hilo unaosema:</p>
<blockquote><p>Pamoja na kukasirika kwangu kutokana na kilichoitokea timu ya Algeria, siihukumu nchi yote kwa kile alichofanya mpumbavu mmoja! Wanachokifanya mashabiki wenye hasira ni upumbavu! kwa ajili ya mungu si jambo kubwa ni nani atakeyeingia katika [kombe la dunia].</p></blockquote>
<p>Mwanablogu wa Kimisri <em><a href="http://www.lastoadri.com/2009/10/blog-post.html">Lasto Adri</a></em> [Ar] anaeleza kuchukizwa kwake na jinsi kile kilichopaswa kuwa tukio la michezo, kimeshushwa hadhi na kuwa pambano chafu. Anaandika:</p>
<blockquote><p>
مندهشة من التعصب وتدنى مستوى لغة الحوار بين مشجعى منتجب مصر ومنتخب الجزائر والظاهر بوضوح فى التعليقات على المواقع الإخبارية أو الرياضية… ومندهشة أكثر بتغذية هذه المأساه إعلاميا بتعليقات من بعض المذيعين (من كلا الجانبين)…<br />
المشجعون الجزائريون أخطؤوا فى المبارة السابقة.. لكن هل الرد يكون هكذا؟.. هل الرد يكون بطلب البعض تسميم اللعيبة ولا إقلاقهم فى منامهم ولا توليع الإستاد وقت الماتش من التشجيع؟..<br />
ونرفزتنى التعليقات على أغلب المواقع.. وإفتكرت لما الجزائر -بزعامة الرئيس الجزائري هواري بومدين- كانت أكتر دولة ساندت مصر فى حرب 1973، رغم فقرها الشديد..<br />
حزينة ان انتهاء علاقة مابين شعبين تكون بشقاق على كورة…</p></blockquote>
<div class="translation">Ninashangazwa na kiwango cha kutovumiliana na lugha chafu inayotumiwa na mashabiki wa timu za Algeria na Misri, ambayo inajitokeza katika maoni mengi kwenye tovuti za habari na michezo… pia ninashangazwa na jinsi ambayo baadhi ya watangazaji na wanahabari (kutoka pande zote), wanavyochochea dhahama hii kupitia maoni yao makali…<br />
Mashabiki wa Algeria hawakujiheshimu katika mchezo uliopita… lakini je jibu la Wamisri ni sahihi?..<br />
Je jibu linapaswa kuwa (kama baadhi walivyosema) kuwapa sumu wachezaji wa Algeria? Kuwaghasi na kuwanyima usingizi? Kuuchoma moto uwanja siku ya pambano?<br />
Nimeudhika na maoni yaliyo kwenye tovuti nyingi… Ninakumbuka wakati Algeria – ikiongozwa na Rais Houari Boumedienne – bila kujali umaskini wao uliokithiri, alikuja kuiunga mkono misri wakati wa vita ya mwaka 1973…</div>
]]></content:encoded>
			<wfw:commentRss>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/11/algeria-misri-ugomvi-juu-ya-pambano-la-mpira-kwenye-mtandao/feed/</wfw:commentRss>
		<slash:comments>0</slash:comments>
		</item>
		<item>
		<title>Misri: Mwanablogu wa Kiume Aagizia Bikra ya Bandia</title>
		<link>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/11/misri-mwanablogu-wa-kiume-aagizia-bikra-ya-bandia/</link>
		<comments>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/11/misri-mwanablogu-wa-kiume-aagizia-bikra-ya-bandia/#comments</comments>
		<pubDate>Fri, 06 Nov 2009 10:13:43 +0000</pubDate>
		<dc:creator>j nambiza tungaraza</dc:creator>
				<category><![CDATA[China]]></category>
		<category><![CDATA[Egypt]]></category>
		<category><![CDATA[English]]></category>
		<category><![CDATA[Entertainment]]></category>
		<category><![CDATA[Feature]]></category>
		<category><![CDATA[Gender]]></category>
		<category><![CDATA[Human Rights]]></category>
		<category><![CDATA[Ideas]]></category>
		<category><![CDATA[Middle East & North Africa]]></category>
		<category><![CDATA[Religion]]></category>
		<category><![CDATA[Weblog]]></category>

		<guid isPermaLink="false">http://sw.globalvoicesonline.org/?p=543</guid>
		<description><![CDATA[Mengi yalisemwa na kuandikwa juu ya zana ya kutengeneza bikra ya bandia - mpaka mwanablogu Mmisri wa kiume Mohamed Al Rahhal akanunua moja. Marwa Rakha anatuletea habari hiyo.]]></description>
			<content:encoded><![CDATA[<em>Ilichapwa kwanza na<a href="http://globalvoicesonline.org/author/marwa-rakha/">Marwa Rakha</a>  &middot; Imetafsiriwa na <a href='http://sw.globalvoicesonline.org/author/j-nambiza-tungaraza/'>j nambiza tungaraza</a> &middot;  <a href='http://globalvoicesonline.org/2009/10/29/egypt-egyptian-male-blogger-orders-artificial-hymen/'>Angalia ujumbe mama</a></em> 
<br /><p>Wakati <a href="http://www.rnw.nl/english">Redio ya Uholanzi</a> ilporusha hewani tafsiri ya Kiarabu kuhusu <em>Zana ya Kutengeneza Bikira ya Bandia</em>, pale <a href="http://www.youm7.com/News.asp?NewsID=136364">gazeti la Youm7</a> lilipotangaza kuwa bidhaa hiyo itaanza kupatikana kwenye soko la Misri, wabunge wahafidhina huko Misri walitaka <a href="http://www.huffingtonpost.com/2009/10/05/egypt-fake-hymen-kit-may-_n_309737.html">bidhaa hiyo izuiwe na muagizaji yeyote afukuzwe nchini au akatwe kichwa</a>, na habari hiyo <a href="http://globalvoicesonline.org/2009/10/08/will-egypt-import-chinese-hymens/">ilipozua kelele kwenye ulimwengu wa blogu wa Misri</a>, <a href="http://www.guardian.co.uk/commentisfree/2009/oct/28/artificial-hymen">Mohamed Al Rahhal</a> alinunua zana hiyo maalum ya kutengeneza bikira ya bandia.</p>
<p>Wakati alipokwenda kuchukua kifurushi chake ofisi ya posta:</p>
<blockquote><p>
Nilikuta kimeshafunguliwa na maafisa mbalimbali wa forodha na posta ambao, baada ya kukosa majibu, waliandika utambulisho wa bidhaa hiyo kama “yenye majimaji mekundu yasiyofahamika” – na walisubiri maelezo yangu.</p></blockquote>
<p><img alt="" src="http://globalvoicesonline.org/wp-content/uploads/2009/10/fakehymen.jpg" title="fakehymen" class="aligncenter" width="460" height="276" /></p>
<p>Aliwaeleza kuwa ni “vipodozi vya wacheza sinema” na kuichukua bidhaa ile nyumbani:</p>
<blockquote><p>Hiyo ndiyo “bikira”: kipande kilichokunjwa cha plastiki cha sentimeta 5&#215;7 – cha ute wa protini unaoitwa albumin, maelezo yalinisahihisha kwa haraka – kilichopakwa wino mwekundu kwenye upande mmoja. Kikiwekwa ukeni kabla ya kujamiiana, plastiki hiyo huganda kidogo, na hupasuka wakati wa tendo. Matone machache ya “damu” huchafua shuka, na kutunza “heshima” ya mwanamke, familia yake au jamii yake.</p>
<p>Kama fanya kazi au la siwezi kujibu. Kutokuwepo kabisa kwa maelezo ya kitaalamu kwenye bidhaa hiyo, pamoja na shutuma mtandaoni kuwa bidhaa hii inaweza kusababisha magonjwa, vilinifanya nisite kumpoatia mtu atakayejitolea kufanya jaribio.</p></blockquote>
<p><em>Mona El Tahawy</em> hakupendezwea na jinsi Wamisri <a href="http://www.monaeltahawy.com/blog/?p=188">walivyopamba moto na kuguswa</a> juu ya bikira bandia pamoja na matatizo yote Wamisri wanayoyakabili siku hizi – gharama za maisha zinazopanda, rais aliye madarakani kwa miaka 28 ambaye mwanawe anaelekea kumrithi, nk. – kelele zote za nini juu ya bikira, iwe ya kweli au ya bandia? </p>
<p>Karibuni kwenye unafiki na kujidanganya ambavyo kwa pamoja vinadunda katikati ya roho mitazamo ya kihafidhina ya kidini juu ya wanawake na uadilifu katika kufanya mapenzi. Na katika shauri la Misri, uhafidhina huo upokatika mizani sawa kote, kwa Waislamu na Wakristu.</p>
<p>Kama Muislamu, ninajua kuwa Qur’an inahubiri uadilifu katika kufanya mapenzi kwa wanaume na wanawake, lakini kushupaliwa huku kwa wanawake na wahafidhina kunamaanisha kuwa ni wanawake tu ambao wanatarajiwa kuzingatia makatazo juu ngono nje ya ndoa. Huku kushupaliwa kwa bikira kumekosa kina zaidi ya yote na kuna hali ya umauti zaidi.</p>
<p><em>Mohamed El Rahhal</em> anashutumu vikali:</p>
<blockquote><p>Unafiki ambao unaturuhusu kubagua dhidi ya asilimia 50 ya jamii wakati tunatoa kibali cha bure kwa nusu nyingine. Ninapinga kuwalazimisha wanawake kwenda umbali huo, mara nyingine kuhatarisha afya zao, ili kuruhusu kucheleweshwa kwa sheria ya kitaifa juu ya mahusiano ya kijinsia. </p>
<p>Uadilifu unatafsiriwa vibaya zaidi na maumbile. Na kama tunasubiri kipande kidogo cha plastiki kifafanue uadilifu, basi tumeshashindwa – na ni budi tutafute ufafanuzi mzuri zaidi.</p></blockquote>
]]></content:encoded>
			<wfw:commentRss>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/11/misri-mwanablogu-wa-kiume-aagizia-bikra-ya-bandia/feed/</wfw:commentRss>
		<slash:comments>0</slash:comments>
		</item>
		<item>
		<title>Misri: Watu 10 Wenye Ushawishi Zaidi Nchini</title>
		<link>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/11/misri-watu-10-wenye-ushawishi-zaidi-nchini/</link>
		<comments>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/11/misri-watu-10-wenye-ushawishi-zaidi-nchini/#comments</comments>
		<pubDate>Wed, 04 Nov 2009 10:42:30 +0000</pubDate>
		<dc:creator>Deogratias Simba</dc:creator>
				<category><![CDATA[Business]]></category>
		<category><![CDATA[Cyber-Activism]]></category>
		<category><![CDATA[Egypt]]></category>
		<category><![CDATA[Elections]]></category>
		<category><![CDATA[English]]></category>
		<category><![CDATA[Governance]]></category>
		<category><![CDATA[Middle East & North Africa]]></category>
		<category><![CDATA[Politics]]></category>
		<category><![CDATA[Weblog]]></category>

		<guid isPermaLink="false">http://sw.globalvoicesonline.org/?p=517</guid>
		<description><![CDATA[Mtoto wa Rais wa Misri, Hosni Mubarak, anayitwa Gamal Mubarak, -- na ambaye anatarajiwa kumrithi baba yake nafasi hiyo -- aliibuka kama mmoja wa washindi 100 wa TIME. Wanablogu wa Ki-Misri wana ya kueleza kuhusu jambo hili. ]]></description>
			<content:encoded><![CDATA[<em>Ilichapwa kwanza na<a href="http://globalvoicesonline.org/author/marwa-rakha/">Marwa Rakha</a>  &middot; Imetafsiriwa na <a href='http://sw.globalvoicesonline.org/author/simbadeo/'>Deogratias Simba</a> &middot;  <a href='http://globalvoicesonline.org/2009/10/29/egypt-the-top-10-most-influential-people/'>Angalia ujumbe mama</a></em> 
<br /><p>Mwanablogu <em>Ahmed Shokeir</em> aliendesha <a href="http://shokeir.blogspot.com/2009/10/2009.html">taftishi</a> ya kutafuta watu 10 wenye ushawishi zaidi nchini Misri baada ya <a href="http://shokeir.blogspot.com/2009/10/2009.html">kushangazwa </a>na matokeo ya <em><a href="http://globalvoicesonline.org/2009/08/16/egypt-gamal-mubarak-why-not/">Gamal Mubarak</a></em>, mtoto wa Rais Hosni Mubarak wa Misri - kama mmoja wa <a href="http://www.time.com/time/specials/packages/article/0,28804,1883644_1886141,00.html">washindi 100 wa mwisho wa mwaka 2009 wa TIME</a>.</p>
<p>Shokeir anaandika: </p>
<blockquote><p>
المفاجأة الحقيقة كانت في إسم الشخصية العربية التالية والتي تظهر في القائمة أيضا للمرة الأولى وتحتل المركز الثامن عشر بفارق بسيط عن الشيخ أحمد وتحصل على ثمانمائة وثلاثون ألف صوت بمتوسط 31 نقطة وهو جمال مبارك متقدماً على أسماء مثل بريتني سبيرز التي حلت في المركز الثلاثون وباراك أوباما في المركز السابع والثلاثون
</p></blockquote>
<div class="translation">Jambo la kushangaza sana lilikuwa kwamba Mwarabu wa pili mwenye ushawishi zaidi baada ya Shehe <a href="http://www.time.com/time/specials/packages/article/0,28804,1883644_1883653_1884132,00.html">Ahmed bin Zayed Al Nahyan</a>, ambaye ni mkurugenzi wa Abu Dhabi Investment Authority, aliyeshika nafasi ya 13 baada ya kupata kura 839,000. Kwa mara ya kwanza <a href="http://www.time.com/time/specials/packages/article/0,28804,1883644_1883653_1885482,00.html">jina la Gamal Mubarak</a> limejitokeza katika nafasi ya 18 ya orodha baada ya kupata kiasi cha kura 832,593. Gamal Mubarak alimshinda <a href="http://www.time.com/time/specials/packages/article/0,28804,1883644_1883653_1884106,00.html">Britney Spears</a> (aliyeshika nafasi ya 30) na <a href="http://www.time.com/time/specials/packages/article/0,28804,1883644_1883653_1883950,00.html">Barack Obama</a> (nafasi ya 37). </div>
<p><em>Zeinobia</em> <a href="http://egyptianchronicles.blogspot.com/2009/10/shokeirs-100-egyptian-2009.html">alikuja na orodha ya watu 10 wenye ushawishi zaidi nchini Misri</a> kwa mujibu wa taftishi ya Shokeir: </p>
<blockquote><p>Kwanza kabisa huwa hatuna aina hii ya ushindanishaji nchini Misri mara kwa mara, pili huna budi kutambua kwamba jambo hili liliendeshwa kwenye blogu ya nchini Misri, washiriki wanaweza kusemwa kwamba ilikuwa ni sampuli ndogo sana katika jamii ya Wa-Misri &#8220;Zaidi ya washiriki 120 kwenye blogu yake na <a href="http://www.facebook.com/event.php?eid=139748076249">zaidi ya washiriki 300 kwenye tukio katika face book</a>&#8221; na kwa hiyo baadhi ya watu huenda watasema kwamba sampuli haikuwa wakilishi vya kutosha, hata hivyo, kwa namna ya kushangaza kabisa, baadhi ya majibu yanawakilisha maoni ya Wa-Misri walio wengi. </p></blockquote>
<p>Akitunza kile kizuri ili kukitoa mwishoni kabisa, <em>Zeinobia</em> alianza na washindi bora 9: </p>
<blockquote><p>Katika nafasi ya 10 yenye pointi 168 yupo kocha wa timu ya taifa ya soka ya Misri Hassan Shahata.<br />
Katika nafasi ya 9 yenye pointi 181 ni mfanyabiashara Naguib Sawiris.<br />
Katika nafasi ya 8 yenye pointi 200 ni Rais Hosni Mubarak. &#8220;kura 26&#8243;<br />
Katika nafasi ya 7 yenye pointi 200 ni mwandishi wa habari Ibrahim Eissa. &#8220;Kura 46&#8243;<br />
Katika nafasi ya 6 yenye pointi 202 ni mfanyabiashara Ahmed Ezz.<br />
Katika nafasi ya 5 yenye pointi 215 ni mwanasayansi Ahmed Zowail.<br />
Katika nafasi ya 4 yenye pointi 262 ni mwendesha kipindi cha TV Mona El-Shazely.<br />
Katika nafasi ya 3 yenye pointi 325 ni mcheza soka Mohamed Abu-Tarika.<br />
Katika nafasi ya 2 yenye pointi 364 ni Gamal Mubarak.</p></blockquote>
<p>Sasa kuhusu mtu mwenye ushawishi zaidi nchini Misri, </p>
<blockquote><p>Na kwa mshangao wangu mkubwa:</p>
<p>Katika nafasi ya 1 yenye pointi 496 ni Mhubiri wa dini ya Kiislamu kwenye TV Amr Khalid.<br />
Hakuna shaka kwamba hao wengine tisa ukitoa Ahmed Zoweil wamekuwa na nafasi ya pekee katika maisha yetu katika mwaka 2009,lakini Amr Khalid!!??</p></blockquote>
<p>Zeinobia anatambua kwamba: </p>
<blockquote><p>Taftishi hii ilikuja katika kilele cha matukio ya Khalid hasa kwa umaarufu wake kutokana na vipindi vyake vya TV vya wakati wa Ramadhani, hivyo hicho kilichangia sana matokeo hayo na bila shaka nafasi ya dini katika maisha yetu. </p></blockquote>
<p>Hata hivyo, bado anajiuliza kama kweli alistahili kushika nafsi ya kwanza kwenye orodha hiyo.</p>
]]></content:encoded>
			<wfw:commentRss>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/11/misri-watu-10-wenye-ushawishi-zaidi-nchini/feed/</wfw:commentRss>
		<slash:comments>0</slash:comments>
		</item>
		<item>
		<title>Misri: Watawala Wa Kiimla na Wake Zao</title>
		<link>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/10/misri-watawala-wa-kiimla-na-wake-zao/</link>
		<comments>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/10/misri-watawala-wa-kiimla-na-wake-zao/#comments</comments>
		<pubDate>Mon, 26 Oct 2009 12:28:35 +0000</pubDate>
		<dc:creator>j nambiza tungaraza</dc:creator>
				<category><![CDATA[Cameroon]]></category>
		<category><![CDATA[Egypt]]></category>
		<category><![CDATA[English]]></category>
		<category><![CDATA[Humor]]></category>
		<category><![CDATA[Middle East & North Africa]]></category>
		<category><![CDATA[Roundups]]></category>

		<guid isPermaLink="false">http://sw.globalvoicesonline.org/?p=475</guid>
		<description><![CDATA[Ilichapwa kwanza naAmira Al Hussaini  &#183; Imetafsiriwa na j nambiza tungaraza &#183;  Angalia ujumbe mama 
Baada ya kuziangalia picha za mke wa Rais wa Cameroon, Mmisri Zeinobia anasema: “Sijui ni ni kiasi gani cha pesa alichotumia kwa ajili ya nywele zake na muonekano wake lakini ninafahamu kuwa watu wa Camerron wanazihitaji zaidi hizo [...]]]></description>
			<content:encoded><![CDATA[<em>Ilichapwa kwanza na<a href="http://globalvoicesonline.org/author/amira-al-hussaini/">Amira Al Hussaini</a>  &middot; Imetafsiriwa na <a href='http://sw.globalvoicesonline.org/author/j-nambiza-tungaraza/'>j nambiza tungaraza</a> &middot;  <a href='http://globalvoicesonline.org/2009/10/22/egypt-dictators-and-their-wives/'>Angalia ujumbe mama</a></em> 
<br /><p>Baada ya kuziangalia picha za mke wa Rais wa Cameroon, Mmisri <em><a href="http://egyptianchronicles.blogspot.com/2009/10/first-lady-from-third-world.html">Zeinobia</a></em> anasema: “Sijui ni ni kiasi gani cha pesa alichotumia kwa ajili ya nywele zake na muonekano wake lakini ninafahamu kuwa watu wa Camerron wanazihitaji zaidi hizo pesa.”</p>
]]></content:encoded>
			<wfw:commentRss>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/10/misri-watawala-wa-kiimla-na-wake-zao/feed/</wfw:commentRss>
		<slash:comments>0</slash:comments>
		</item>
		<item>
		<title>Nchi za Kiarabu: Homa ya Mafua ya Nguruwe Yaendelea</title>
		<link>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/07/nchi-za-kiarabu-homa-ya-mafua-ya-nguruwe-yaendelea/</link>
		<comments>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/07/nchi-za-kiarabu-homa-ya-mafua-ya-nguruwe-yaendelea/#comments</comments>
		<pubDate>Fri, 24 Jul 2009 14:17:11 +0000</pubDate>
		<dc:creator>Christian Bwaya</dc:creator>
				<category><![CDATA[Bahrain]]></category>
		<category><![CDATA[Egypt]]></category>
		<category><![CDATA[English]]></category>
		<category><![CDATA[General]]></category>
		<category><![CDATA[Health]]></category>
		<category><![CDATA[Media]]></category>
		<category><![CDATA[Middle East & North Africa]]></category>
		<category><![CDATA[Religion]]></category>
		<category><![CDATA[Saudi Arabia]]></category>
		<category><![CDATA[Syria]]></category>
		<category><![CDATA[Travel]]></category>
		<category><![CDATA[Weblog]]></category>

		<guid isPermaLink="false">http://sw.globalvoicesonline.org/?p=241</guid>
		<description><![CDATA[Homa ya mafua ya nguruwe au H1N1 bado inatawala vichwa vya habari vya magazeti katika nchi za Kiarabu kwani wagonjwa wapya wanaendelea kugunduliwa na mamlaka za afya na kutangazwa katika vyombo vya habari kila siku. Huu ni muhtasari wa yale wanayoongea wanablogu huko Bahrain, Jordan, Misri na Syria.]]></description>
			<content:encoded><![CDATA[<em>Ilichapwa kwanza na<a href="http://globalvoicesonline.org/author/amira-al-hussaini/">Amira Al Hussaini</a>  &middot; Imetafsiriwa na <a href='http://sw.globalvoicesonline.org/author/bwaya/'>Christian Bwaya</a> &middot;  <a href='http://globalvoicesonline.org/2009/07/09/arab-world-swine-flu-fever-continues/'>Angalia ujumbe mama</a></em> 
<br /><p>Homa ya mafua ya nguruwe au H1N1 bado inatawala vichwa vya habari vya magazeti katika nchi za Kiarabu kwani wagonjwa wapya wanaendelea kugunduliwa na mamlaka za afya na kutangazwa katika vyombo vya habari kila siku.</p>
<p>Huko Bahraini, <em><a href="http://sillybahrainigirl.blogspot.com/2009/07/coming-home-to-sick-place.html">Silly Bahraini Girl </a></em>(ambaye ni mimi) amerudi nyumbani na kushangazwa na kile alichokiona katika kiwanja cha ndege cha nchini mwake:</p>
<blockquote><p>Ukweli wa jinsi sehemu hii ilivyogeuka na kuwa ya kiwendawazimu unakupiga usoni sekunde ile unapotua kwenye kiwanja cha ndege cha kimataifa na kuona wafanyakazi wa ardhini wamevaa vitambaa vya kitabibu kufunika pua, kuanzia wahudumu mpaka maofisa wa uhamiaji.<br />
“Mna tatizo gani?” Ninawauliza. “Kuna maambukizi Bahraini?” Niliendelea kuuliza […] hali ilionekana kuwa ngumu na kiwango cha wendawazimu wa mafua haya ya nguruwe kilikuwa juu kuliko niliyokutana nao kokote nilikosafiri tangu matatizo haya ya nguruwe yalipoikamata dunia. Kwanini hapakuwepo hata mtu mmoja aliyevaa matambara haya kwenye viwanja vya San Fransisco, Chicago, Toronto na Heathrow ambako nilisafiri<br />
katika majuma machache yaliyopita?</p></blockquote>
<p>Bado tukiwa Bahraini, <em><a href="http://suhailalgosaibi.com/2009/07/09/the-shocking-truth-about-swine-flue/">Sohail Al Gosaibi</a></em> ananusa njama kwenye hewa, anaona kwamba kukuza sana madhara ya mafua ya nguruwe kunayanufaisha mashirika ya habari, watangaza biashara na viwanda vya madawa. Mwanablogu wa Kisaudia anaandika:</p>
<blockquote><p>Vyombo vya habari siku zote hukuza hali ya mambo, kumbuka kwamba hofu huuza. Na magazeti na idhaa za habari ni lazima viuze nafasi za matangazo na muda wa kurusha matangazo hewani ili kutengeneza fedha, na kwa kadiri habari inavyokuwa inatishia na kuogopesha ndivyo wanavyopata watazamaji na wasomaji wengi zaidi, ambavyo huongeza watangaza biashara, na faida zaidi.</p></blockquote>
<p><em>Al Gosaibi </em>ananukuu makala aliyoisoma na kuhitimisha:</p>
<blockquote><p>Kwa mujibu wa makala, Serikali za Marekani na Uingereza zina hifadhi ya madawa ya Tamifluiflu yenye thamani ya mabilioni ya dola ambazo lazima wazitumie ndani ya miezi michache ijayo, vinginevyo yatapita muda wake. Inafurahisha, eeh?</p></blockquote>
<p>Na akizungumzia nadharia, mwanablogu wa <em><a href="http://jordanreformwatch.wordpress.com/2009/06/30/stupid-watch/">Jordan Reform Watch</a> </em>pia anacho cha kusema na kuandika:</p>
<blockquote><p>Ahhh..mafua ya nguruwe pamoja na nadharia zote za njama zinazoambatana nayo… “mwanasayansi” wa Kijordani bingwa wa magonjwa anadai kuwa Maka na Madina ziko mbali na ugonjwa huo, kwa hiyo hakuna haja ya kuzungumzia uwezekano wa mlipuko ambao unaweza kutokea kutokana na mamilioni ya mahujaji kuwa karibu karibu wakati wa hija…</p>
<p>Uweni nguruwe…Nendeni kwenye Hija…na mtakuwa mbali na ugonjwa…</p></blockquote>
<p>Mwanablogu wa Kimisri <em><a href="http://egyptianchronicles.blogspot.com/2009/07/h1n1-follow-up-5-more-cases.html">Zeinobia</a></em>, anayeblogu kupitia blogu ya<em> Egyptian Chronicles</em>, kadhalika anaguswa na jinsi ugonjwa utakavyosambaa wakati wa Haji [Msimu wa Hija ya Waislamu Maka kila mwaka], ambapo mamilioni ya mahujaji kutoka sehemu mbalimbali duniani hukusanyika Maka ili kutimiza nguzo hiyo. Anaandika:</p>
<blockquote><p>majadiliano kuhusu mustakabali wa Hija na Omra [hija ndogo] mwaka huu bado ni suala linaloendelea. Waziri wa Afya anataka kuifuta Omra wakati Waziri wa Utalii anapinga kufutwa huko, sihitaji kuzungumzia kuhiji.<br />
Ni kweli majadiliano ni makali miongoni mwa mashehe wa dini wenyewe. Saudia Arabia inaelewa changamoto iliyonayo tayari na imeamua kushughulikia hali hiyo kwa kadiri inavyoweza katika Omra na hija, inashauri kuwa mahujaji wajawazito, wazee na watoto waepuke kuhiji mwaka huu, Ninauheshimu uamuzi huu.<br />
Pia ninalo pendekezo zuri zaidi. Katika mnazingira kama haya<br />
kwa nini tusiwaruhusu tu wale mahujaji wa kwanza wake kwa waume kuhudhuria Omra na Hija.</p></blockquote>
<p>Kituo chetu cha mwisho ni Syria, ambapo mwanablogu <em><a href="http://yaser1978.wordpress.com/2009/07/04/%D8%A5%D8%B9%D9%84%D8%A7%D9%86-%D8%A3%D9%88%D9%84-%D8%AD%D8%A7%D9%84%D8%A9-%D8%A7%D8%B5%D8%A7%D8%A8%D8%A9-%D8%A8%D8%A5%D9%86%D9%81%D9%84%D9%88%D9%86%D8%B2%D8%A7-%D8%A7%D9%84%D8%AE%D9%86%D8%A7%D8%B2/">Yaser Arwani</a></em> [ar] anatuunganisha na habari inayosema kwamba mgonjwa wa kwanza wa mafua wa nguruwe kuripotiwa Syria ilitaarifiwa na daktari wa Ki-Syria, anayefanya kazi Australia na alikuwa akiitembelea nchi yake. Daktari huyu wa kike alisafiri kwenda Syria kupitia Uwanja wa Kimataifa wa Dubai na ugonjwa haukuwa umegunduliwa mpaka siku chache baada ya kuwasili kwake.</p>
]]></content:encoded>
			<wfw:commentRss>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/07/nchi-za-kiarabu-homa-ya-mafua-ya-nguruwe-yaendelea/feed/</wfw:commentRss>
		<slash:comments>1</slash:comments>
		</item>
		<item>
		<title>Tajiri Wa Kimisri Ahukumiwa Kifo</title>
		<link>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/05/tajiri-wa-kimisri-ahukumiwa-kifo/</link>
		<comments>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/05/tajiri-wa-kimisri-ahukumiwa-kifo/#comments</comments>
		<pubDate>Wed, 27 May 2009 13:56:23 +0000</pubDate>
		<dc:creator>j nambiza tungaraza</dc:creator>
				<category><![CDATA[Arabic]]></category>
		<category><![CDATA[Breaking News]]></category>
		<category><![CDATA[Economics]]></category>
		<category><![CDATA[Egypt]]></category>
		<category><![CDATA[English]]></category>
		<category><![CDATA[Law]]></category>
		<category><![CDATA[Lebanon]]></category>
		<category><![CDATA[Middle East & North Africa]]></category>
		<category><![CDATA[Politics]]></category>
		<category><![CDATA[Weblog]]></category>

		<guid isPermaLink="false">http://sw.globalvoicesonline.org/?p=164</guid>
		<description><![CDATA[Wamisri walishuhudia hukumu isiyotarajiwa katika historia ya vyombo vya sheria nchini humo: Bilionea Hesham Talaat Moustafa, pamoja na mamluki wake (mpiga risasi wa kukodi) Mohsen El Sokari wamehukumiwa adhabu ya kifo kutokana na kuhusika kwao katika mauaji ya mwimbaji wa Kilebanoni Suzanne Tameem. Mauaji hayo ya kinyama yalitokea huko Dubai, UAE, na hukumu iliyotolewa Alhamisi imesababisha mshtuko na mshangao wakati wanablogu walipojaribu kukubaliana na yaliyotukia.]]></description>
			<content:encoded><![CDATA[<em>Ilichapwa kwanza na<a href="http://globalvoicesonline.org/author/nermeen-edress/">Nermeen Edrees</a>  &middot; Imetafsiriwa na <a href='http://sw.globalvoicesonline.org/author/j-nambiza-tungaraza/'>j nambiza tungaraza</a> &middot;  <a href='http://globalvoicesonline.org/2009/05/23/egyptian-tycoon-sentenced-to-death/'>Angalia ujumbe mama</a></em> 
<br /><p>Wamisri walishuhudia hukumu isiyotarajiwa katika historia ya vyombo vya sheria nchini humo: Bilionea <a href="http://en.wikipedia.org/wiki/Hisham_Talaat_Moustafa">Hesham Talaat Moustafa</a>, pamoja na mamluki wake (mpiga risasi wa kukodi) Mohsen El Sokari <a href="http://www.time.com/time/world/article/0,8599,1900311,00.html">wamehukumiwa</a> adhabu ya kifo kutokana na kuhusika kwao katika mauaji ya mwimbaji wa Kilebanoni <a href="http://en.wikipedia.org/wiki/Suzanne_Tamim">Suzanne Tameem</a>. Mauaji hayo ya kinyama yalitokea huko Dubai, UAE, na hukumu iliyotolewa Alhamisi imesababisha mshtuko na mshangao wakati wanablogu walipojaribu kukubaliana na yaliyotukia.</p>
<p>Mwanablogu anayeandika sana wa Kimisri, <em><a href="http://egyptianchronicles.blogspot.com/2009/05/after-verdict.html">Zeinobia</a> </em>alitangaza habari:</p>
<blockquote><p>Mnamo tarehe 21 Mei, Hakimu Muhammadi Qunsuwa alitangaza kuwa kesi hiyo itapelekwa kwa Mufti Mkuu Ali Gomaa, Kiongozi wa juu zaidi wa Kidini nchini humo, ambaye angetoa hukumu ya kifo kwa Moustafa siku ya tarehe 25 Juni.</p></blockquote>
<p>Kama ilivyomstaajabisha kila mmoja, hukumu hiyo pia ilimuacha mshtakiwa akiwa na mshangao. <a href="http://">Mwanahabari <em>Ahmed El Desouky</em></a> alikuwa ni mmojawapo wa watu wa kwanza kuandika maoni ya watu mahakamani kwa ajili ya jamii ya Wamisri katika mtandao wa intaneti, alisema:</p>
<blockquote><p>Kulikuwa na ulalamishi mahakamani baada ya sentesi kusomwa na wale waliohusika walionyesha hasira kali na mshangao wakieleza kuwa hukumu ile ilikuwa ni kali kupita kiasi. Maoni yalitofautiana nje ya jumba la mahakama, ambapo watu wengi waliiona ile adhabu ni stahiki kwa mtu ambaye aliyatumia mamlaka, ushawishi na pesa zake  vibaya, akifikiri kwamba alikuwa yuko juu ya sheria.</p></blockquote>
<p>Maoni yalikuwa yakipishana, kati ya kukubali na kuiunga mkono ile hukumu na huruma pamoja na huzuni. Katika makala yake, <a href="http://catofdesert.blogspot.com/2009/05/blog-post_21.html"><em>Desert Cat</em></a> alishangazwa na ukweli kwamba Moustafa na El Sokary walipewa hukumu inayofanana:</p>
<blockquote><p>Kwa masikitiko hukumu imetolewa leo kinyume na vile kila mmoja alivyokuwa akitarajia na kesi hiyo hivi sasa inapelekwa kwa Mufti Mkuu. Baada ya kusomwa kwa hukumu, mushkeli ulizuka mahakamani, huku wanafamilia wa Mohsen na Hesham wakipiga mayowe kadhalika wafanyakazi wa kundi la Talaat Moustafa, ambao hawakuamini kile walichokisikia. Wakati huo huo Hesham na Mohsen walikuwa kimya kabisa. Binafsi, sikuamini kwa sababu kosa la Hisham lilikuwa ni kuchochea mauaji wakati Mohsen ndiye aliyeua. Iweje adhabu zao ziwe sawasawa?</p></blockquote>
<p><em>Ahmed Shokeir</em> alijibu swali hilo katika sehemu ya maoni ya ujumbe ule kwa kusema:</p>
<blockquote><p>Katika sheria nyingi, adhabu ya wale waliotoa wazo la jinai ni sawasawa na ile ya watekelezaji. Katika baadhi ya sheria, adhabu huwa kali zaidi kwa mchochezi kuliko kwa mtekelezaji.</p></blockquote>
<p>Wanaomuunga mkono mfanyabiashara huyu tajiri wa majengo nchini Misri kwenye huduma ya <em>Facebook</em>, waliijibu hukumu ile kwa kuanzisha kundi la <a href="http://www.facebook.com/pages/Free-Hisham-Talaat-Mostafa/36546446359#/album.php?aid=58513&#038;id=36546446359&#038;comments"><em>“Muachieni Heshaam Talaat Moustafa</em></a>.”</p>
<p><em>Ashraf Elmanwaty</em> alisema:</p>
<p>Bado nina matumaini kuwa HTM ataachiwa huru… Hii ni hukumu iliyovuka mipaka</p>
<p>Wakati <em>Miral El Ramlawy</em> aliandika:</p>
<blockquote><p>Asilimia 90 ya Wamisri hawaamini kuwa alifanya na mahakama inapaswa kuwaeleza Wamisri msingi wa hukumu hii!!! Simu ambazo hazionyeshi ujumbe ulio wazi siyo USHAHIDI… tunasubiri ufafanuzi!</p></blockquote>
<p>Baada ya mshtuko, uchambuzi ulianza kuchukua nafasi. <a href="http://egyptianchronicles.blogspot.com/2009/05/after-verdict.html"><em>Zeinobia</em> </a>alifafanua:</p>
<blockquote><p>Ikiwa Hakimu anasema kuwa mafaili ya mkosefu yatapelekwa kwa Mufti Mkuu kwa ajili ya ushauri inamaanisha katika mazingira mengi kwamba mkosefu atakutana na adhabu ya kifo. Adhabu ya kifo inahitaji maoni ya Mufti Mkuu ili kuiunga mkono kutokana na mtazamo wa kidini, mtazamo wa Sharia ili kuitimiza hukumu. Siyo kila siku watu hutoa adhabu ya kifo kwa yeyote.<br />
	Katika kesi nyingi, kama siyo zote Mufti Mkuu hukubali na kuunga mkono hukumu ya hakimu.</p></blockquote>
<p>Na anaendelea:</p>
<blockquote><p>	Pili katika kesi ya Hisham na Sokary, hakimu atatangaza hukumu ya mwisho tarehe 25 Juni 2009, karibu mwezi mmoja na siku 5, naamini ni muda mrefu kusubiri adhabu ya kifo.<br />
	Tatu, wakati ambapo hakimu atatangaza hukumu ya mwisho, mawakili wa mtuhumiwa watakuwa na haki ya kukata rufaa.</p></blockquote>
<p>Kwa hiyo panaweza kuwa na duru la pili, jambo ambalo tutalifahamu siku ya tarehe 25 Juni.</p>
<p>Wakati huo huo, kuna maswali na mashaka juu ya biashara ya majengo ya Hisham. Blogu ya <a href="http://mideasti.blogspot.com/2009/05/talaat-mustafa-group-investors-neednt.html"><em>Middle East Intitute</em> inaripot</a>i:</p>
<blockquote><p>Kundi la Talaat Mustafa (TMG), ubia mkubwa wa biashara ya majengo ambao Mustafa alitengeneza mabilioni, hautaki wadau wahofu kwa sababu tu mwenye kampuni amehukumiwa adhabu ya kifo. <a href="http://www.thedailynewsegypt.com/article.aspx?ArticleID=21880">Kundi la TMG limewahakikishia wawekezaj</a>i:<br />
Sawaftah alisema kwamba muundo wa kiufanisi wa TMG utakinga athari zitakazotokana na ‘kutokuwepo kwa mtu mmoja’. </p></blockquote>
]]></content:encoded>
			<wfw:commentRss>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/05/tajiri-wa-kimisri-ahukumiwa-kifo/feed/</wfw:commentRss>
		<slash:comments>0</slash:comments>
		</item>
		<item>
		<title>Misri: Wanablogu Wafuatilia Milipuko ya Mabomu Mjini Kairo</title>
		<link>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/02/misri-wanablogu-wafuatilia-milipuko-ya-mabomu-mjini-kairo/</link>
		<comments>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/02/misri-wanablogu-wafuatilia-milipuko-ya-mabomu-mjini-kairo/#comments</comments>
		<pubDate>Thu, 26 Feb 2009 03:46:44 +0000</pubDate>
		<dc:creator>j nambiza tungaraza</dc:creator>
				<category><![CDATA[Breaking News]]></category>
		<category><![CDATA[Disaster]]></category>
		<category><![CDATA[Egypt]]></category>
		<category><![CDATA[English]]></category>
		<category><![CDATA[Feature]]></category>
		<category><![CDATA[France]]></category>
		<category><![CDATA[Middle East & North Africa]]></category>
		<category><![CDATA[Politics]]></category>
		<category><![CDATA[Travel]]></category>
		<category><![CDATA[U.S.A.]]></category>
		<category><![CDATA[Weblog]]></category>

		<guid isPermaLink="false">http://sw.globalvoicesonline.org/?p=76</guid>
		<description><![CDATA[Mtalii wa Kifaransa ameuwawa na watu wapatao 20 wamejeruhiwa wakati bomu lilipolipuka nje ya msikiti wa Al Hussein uliopo katika eneo la utalii la Khan Al Khalili mjini Kairo. Na wakati dunia ilipokuwa inaanza kufahamu ni kipi kilichokuwa kinatokea, wanablogu wa Misri waliingia kazini haraka, wakipashana habari za yanayotukia, taarifa, uchambuzi na hofu zao.]]></description>
			<content:encoded><![CDATA[<em>Ilichapwa kwanza na<a href="http://globalvoicesonline.org/author/lasto-adri/">Lasto Adri</a>  &middot; Imetafsiriwa na <a href='http://sw.globalvoicesonline.org/author/j-nambiza-tungaraza/'>j nambiza tungaraza</a> &middot;  <a href='http://globalvoicesonline.org/2009/02/22/egypt-bloggers-react-to-cairo-bombings/'>Angalia ujumbe mama</a></em> 
<br /><p></a>Mtalii wa Kifaransa <a href="http://english.aljazeera.net/news/middleeast/2009/02/2009222175234931911.html">ameuwawa</a> na watu wapatao 20 wamejeruhiwa wakati bomu lilipolipuka nje ya <a href="http://www.answers.com/Al%20Hussein%20Mosque">msikiti wa Al Hussein</a> uliopo katika eneo la utalii la <a href="http://www.answers.com/Khan%20Al%20Khalili">Khan Al Khalili</a> mjini Kairo mapema leo.</p>
<p>Na wakati dunia ilipokuwa inaanza kufahamu ni kipi kilichokuwa kinatokea, wanablogu wa Misri waliingia kazini haraka, wakipashana habari za yanayotukia, taarifa, uchambuzi na hofu zao.</p>
<p>Yote yalianza wakati <a href="http://twitter.com/Zeinobia/status/1237624709"><em>Zenobia</em></a> alipotundika ujumbe katika ukurasa wa Twita akiripoti kuwa “Kumetokea mlipuko wa aina fulani kwenye mgahawa uliopo Al Azhar.” Dakika chache baadaye <a href="http://twitter.com/3arabawy/status/1237645532"><em>Arabawy</em></a> alifuatia na ujumbe mwingine uliothibitisha: “Mlipuko katika mtaa wa el-mashhad el-Husseini mjini Kairo.”</p>
<p><img alt="" src="http://globalvoicesonline.org/wp-content/uploads/2009/02/moftasa-300x131.png" class="aligncenter" width="300" height="131" /></p>
<p><a href="http://twitter.com/moftasa/status/1237694368"><em>Moftasa</em></a> ndiye alikuwa wa kwanza kuuhisi uhusiano wa milipuko na sheria mpya ya kuzuia-ugaidi, ambayo itajadiliwa katika siku chache zijazo kwenye bunge la Misri. Rasimu ya sheria hiyo imekumbana na vipingamizi vikubwa.</p>
<p>Hakuna lililothibitishwa mpaka sasa, na uvumi unaenea; hata hivyo, <em>Zeinobia </em>alijaribu <a href="http://egyptianchronicles.blogspot.com/2009/02/breaking-news-blast-in-al-hussein.html">kukusanya habari kama zinavyotokea kutoka vyanzo tofauti vya magazeti na idhaa za televisheni </a>katika muhtasari. </p>
<p>Mwanablogu <a href="http://arabist.net/archives/2009/02/22/report-explosion-in-cairo/"><em>Arabist</em></a>, ambaye alikuwa Karibu na eneo na kuusikia mlipuko huo yeye mwenyewe, aliandika:</p>
<blockquote><p>Nimesikia taarifa za mabomu yanayolipuka katika mji mkongwe wa Kairo Karibu na Khan al-Khalili, sehemu maarufu kwa watalii. Nitawapasha kadri habari zitakapopatikana.</p>
<p>Habari mpya: Al Jazeera inaripoti <del datetime="2009-02-26T03:13:58+00:00">vifo 11, Wamisri watatu, Wajerumani watatu, Mfaransa mmoja,</del> 16 wamejeruhiwa, Mfaransa mmoja amefariki, haya na mengineyo bado hayajathibitishwa.</p>
<p>Habari mpya 2: Tayari wanaharakati wanasema kuwa tukio hili limetukia Karibu sana na mwezi ujao ambapo Sheria ya Dharura itajadiliwa Bungeni…</p>
<p>Habari mpya 3: Wanne wamefariki (Wajerumani na Wafaransa) 12 wamejeruhiwa, wa mataifa mbalimbali.</p></blockquote>
<p>Halafu <a href="http://twitter.com/moftasa/status/1237863455"><em>moftasa</em></a> alibandika kiungo cha picha kutoka kwenye eneo la mlipuko kwenye Twita.</p>
<p>Wakati <a href="http://egypt4.wordpress.com/"><em>Msfour</em></a>, mfanyakazi wa Kimarekani anayeishi Kairo, <a href="http://twitter.com/msfour/status/1237956556">alikuwa wa kwanza kuwataka wanablogu wanaotumia Twita</a> kutumia kielelezo cha <a href="http://search.twitter.com/search?q=%23cairobomb">#cairobomb</a>, <em>Arabawy</em> ndiye <a href="http://twitter.com/3arabawy/status/1237819035">alikuwa wa kwanza kuwataka wanablogu watumie kielelezo jumuishi cha delicious</a>: <em>El-HusseinExplosion</em> ili kukusanya viunganishi vyote chini ya <a href="http://delicious.com/tag/El-HusseinExplosion">anwani pepe moja</a>.</p>
<p>Wanablogu <a href="http://www.gaberism.net/2009/02/22/explosion-in-cairo/"><em>Yassary Masry </em></a>[Ar], <a href="http://carlincairo.blogspot.com/2009/02/explosion-at-khan.html"><em>Carl</em>, <a href="http://egypt4.wordpress.com/2009/02/22/we-are-fine/"><em>Msfour</em></a>, <a href="http://egytimes.org/2009/02/fuck-terrorism/"><em>Maree</em></a>, <a href="http://arabicsource.wordpress.com/2009/02/22/blast-in-cairo/"><em>Rob</em></a>, <a href="http://www.sandmonkey.org/2009/02/22/terrorist-attack-in-cairo/"><em>SandMonkey</em></a> pamoja na <a href="http://www.greywoolknickers.net/?p=178"><em>Grey wool Knickers </em></a>walikuwa ni miongoni mwa wanablogu wa kwanza kuandika kuhusu tukio hilo, ama kuwafariji marafiki na familia au kujadili uhusiano wa milipuko ya mabomu na sheria ya kuzuia ugaidi. <a href="http://www.greywoolknickers.net/?p=178"><em>Grey wool Knickers </em></a>aliandika ujumbe mfupi unaohusianisha matukio ya mwisho yaliyotokea Misri, akijaribu kuyaunganisha na milipuko ya hivi karibuni: </p>
<blockquote><p>Kama <a href="http://moftasa.jaiku.com/presence/54233060">watu</a> <a href="http://arabist.net/arabawy/2009/02/22/explosion-in-al-azhar-area/">kadhaa</a> wanavyoona, matukio haya yametokea katika wakati wa kushuku, tukizingatia kwamba <a href="http://www.fidh.org/spip.php?article1397">Sheria ya Dharura</a> (iliyokuwepo tangu mwaka 1967 wakati wa vita vya Waarabu-na-Waisraeli, vilivyositishwea kwa muda wakati wa utawala wa Rais Sadat) ilitaka kuanzishwa tena. Serikali ya Rais Mubarak <a href="http://www.arabicnews.com/ansub/Daily/Day/050818/2005081819.html">imekuwa ikiahidi kwa miaka mingi</a> kuanzisha sheria ya kuzuia ugaidi ambayo ingechukua nafasi ya sheria za kijeshi, ambayo ingewapa raia angalau kinga kidogo kwenye katiba ya Misri.  Utawala wa sasa unao uwezo wa kurejesha Sheria ya Dharura na kutenda inavyotaka, kama wasomaji watakavyogundua katika <a href="http://www.greywoolknickers.net/?p=143">kutekwa kwa Philip Rizk</a> na <a href="http://prisonersforgaza.wordpress.com/">Diaa Gad</a>, kati yaw engine wengi. Huku kukiwa na matarajio ya mabadiliko katika serikali za Marekani na Israeli – pamoja na makundi ya upinzani yenye sauti na yaliyo mitandao ya ndani na ile inayovuka mipaka na kuingia Gaza – inaonekana kuwa utawala unaozeeka wa Mubarak unaanza kuingiwa na kihoro na kujikuta una machaguo machache ya kuendeleza mshiko wake madarakani isipokuwa kwa kutumia <a href="http://en.wikipedia.org/wiki/Strategy_of_tension">mikakati ya kuongeza hali ya vuguvugu</a>. Nafikiri <a href="http://globalvoicesonline.org/2009/02/22/2009/02/19/egypt-ayman-nour-released/">kuachiwa kwa mfungwa wa kisiasa Ayman Nour hivi karibuni </a>kunaweza kuwa ni ushahidi wa mchechetu unaozikumba ngazi za juu za utawala huu wa kiimla. Ili kupata habari kama zinavyotukia, angalia <a href="http://delicious.com/tag/El-HusseinExplosion">ukurasa huu wa delicious</a>.</p></blockquote>
<p>Mpaka wakati makala hii ilipokuwa ikiandikwa imethibitishwa kwamba msichana wa Kifaransa mwenye umri wa miaka 21 ameuwawa, na watu wengine wapatao 20 wa mataifa mbalimbali wamejeruhiwa. Hata hivyo, bado ni mapema mno kurukia hitimisho la ni nani aliyehusika na milipuko.</p>
<p>Picha zinaweza kupatikana katika <a href="http://yalally.blogspot.com/2009/02/blog-post_22.html">blogu ya AbdelFatah</a> na wasomaji wanaweza kuwafuatilia wanablogu wa Misri kwenye twita <a href="http://search.twitter.com/search?q=%23cairobomb">hapa</a>.</p>
]]></content:encoded>
			<wfw:commentRss>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/02/misri-wanablogu-wafuatilia-milipuko-ya-mabomu-mjini-kairo/feed/</wfw:commentRss>
		<slash:comments>0</slash:comments>
		</item>
		<item>
		<title>Mashariki ya Kati: Vikwazo kama Silaha ya Kisiasa</title>
		<link>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/02/mashariki-ya-kati-vikwazo-kama-silaha-ya-kisiasa/</link>
		<comments>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/02/mashariki-ya-kati-vikwazo-kama-silaha-ya-kisiasa/#comments</comments>
		<pubDate>Mon, 02 Feb 2009 12:06:40 +0000</pubDate>
		<dc:creator>j nambiza tungaraza</dc:creator>
				<category><![CDATA[Arabic]]></category>
		<category><![CDATA[Business]]></category>
		<category><![CDATA[Cyber-Activism]]></category>
		<category><![CDATA[Economics]]></category>
		<category><![CDATA[Egypt]]></category>
		<category><![CDATA[English]]></category>
		<category><![CDATA[Feature]]></category>
		<category><![CDATA[International Relations]]></category>
		<category><![CDATA[Israel]]></category>
		<category><![CDATA[Jordan]]></category>
		<category><![CDATA[Middle East & North Africa]]></category>
		<category><![CDATA[Palestine]]></category>
		<category><![CDATA[Politics]]></category>
		<category><![CDATA[Saudi Arabia]]></category>
		<category><![CDATA[U.S.A.]]></category>
		<category><![CDATA[War & Conflict]]></category>
		<category><![CDATA[Weblog]]></category>

		<guid isPermaLink="false">http://sw.globalvoicesonline.org/?p=53</guid>
		<description><![CDATA[Watu wengi wa Mashariki ya Kati wamesusia bidhaa za Israeli na Marekani kama jibu la mashambulizi ya Israeli huko Gaza. Tarek Amr anapitia yale wanablogu wanayosema kuhusu suala hili.]]></description>
			<content:encoded><![CDATA[<em>Ilichapwa kwanza na<a href="http://globalvoicesonline.org/author/tarek-amr/">Tarek Amr</a>  &middot; Imetafsiriwa na <a href='http://sw.globalvoicesonline.org/author/j-nambiza-tungaraza/'>j nambiza tungaraza</a> &middot;  <a href='http://globalvoicesonline.org/2009/01/22/middle-east-boycott-as-a-political-weapon/'>Angalia ujumbe mama</a></em> 
<br /><p>Watu wengi Mashariki ya Kati wamesusia bidhaa za Israeli na Marekani kama jibu la mashambulizi ya Israeli huko Gaza.</p>
<p>Bloga anayejiita <a href="http://angryarab.blogspot.com/2009/01/to-samah-and-kirsten.html">Shirika la Habari la Kiarabu Lenye Hasira </a>anaandika:</p>
<blockquote><p>Katika nchi tano za Kiarabu kampeni mpya na nyeti iliyoratibiwa ili kususia bidhaa za Kimarekani imezinduliwa, na migahawa ya kahawa ya Starbucks ndio shabaha yake ya kwanza, ikifuatiwa kwenye orodha hiyo na maduka ya Nestlè, Coca-Cola, Johnson &#038; Johnson pamoja na Burger King.</p></blockquote>
<p>Miongoni mwa maduka yote yenye chapa ya Marekani, Starbucks ndio iliyokuwa inalengwa zaidi na kampeni hizo za kususia. Bloga <a href="http://egyptianchronicles.blogspot.com/2009/01/starbucks-in-beirut-is-closed-for-day.html">Zeinobia</a> wa Misri, anaandika:</p>
<blockquote><p>Starbucks, tawi maarufu la Starbucks mjini Beirut lilifungwa kwa siku moja kufuatia maandamano ya kulipinga. Kuna wito umetolewa na kuitikiwa katika ulimwengu wa Waarabu kususia bidhaa za Marekani hasa 84268245 bidhaa ambazo zinazohusishwa na Israeli kwa njia moja au nyingine.</p></blockquote>
<p>Halafu anaendelea:</p>
<blockquote><p>Umma wa Waarabu unaamini kwamba Starbucks ya Marekani hulipatia Jeshi la Israeli, IDF mchango wa mwaka kutokana na ukweli kwamba mwanzilishi wa Starbucks ni Myahudi, na nikitaka kuwa mkweli, ukweli huo hautoshi kufikia hitimisho kwamba kampuni hiyo hutoa michango kwa jeshi la Israeli, lakini habari kama hizi zinaufanya umma wa Waarabu kufikiri mara mbili.<br />
Uvumi wa Starbucks-Jeshi la Israeli ni uvumi wa siku nyingi hata kabla ya kufungua tawi lake nchini Misri, kampuni hiyo ilipingwa na ulimwengu wa Waarabu.<br />
Nakumbuka siku moja nilipokea barua pepe inayohusu nembo ya Starbucks na historia yake, ikisema kwamba nembo hiyo ni alama ya binti mfalme wa Kiebrania aliyewakomboa Wayahudi waliokuwa Babeli wakati wa zamani ilhali hilo ni jambo jingine kabisa.</p></blockquote>
<p>Kampeni hizo za kususia hazipo tu huko Uarabuni, kundi la wanablogu wa Kimarekani na Kipalestina <a href="http://www.kabobfest.com/2009/01/malaysia-boycotts-coke.html">KABOBfest</a> linaripoti jinsi watu huko Malaysia wanavyoshiriki katika kampeni hizo: </p>
<blockquote><p>Zaidi ya migahawa 2,000 inayomilikiwa na Waislamu nchini Malaysia imeondoa Coca-Cola kwenye orodha za vyakula katika jitihada za kuunga mkono migomo dhidi ya Israeli. Mashirika ya kizawa yanawashawishi wafanyakazi wa Coca-Cola, kadhalika na wale wa Starbucks na makampuni mengine, waziachee ajira zao.</p></blockquote>
<p>Kutokea Jordan, <a href="http://khobbeizeh.blogspot.com/2006/04/starsucks.html">Khobbeizeh</a> pia anaandika kuhusu ususiaji wa Starbucks:</p>
<blockquote><p>Howard Schultz ni Mzayonisti mwenye siasa kali zinzounga mkono jeshi la Israeli. Anawaunga mkono na mamia ya mamilioni kila mwaka kutoka katika kipato cha Starbucks, ni mmoja wa wadhamini wakubwa wa silaha.</p></blockquote>
<p>Kwa hakika, bidhaa za Israeli zimegomewa na watu wengi, haya ndiyo alioandika bloga <a href="http://bodyontheline.wordpress.com/2009/01/17/on-solidarity-not-forgetting-gaza/">Body on the Line </a>katika blogu yake:</p>
<blockquote><p>Wakulima wanasema kwamba mazao yao mengi yamezuiliwa kwenye maghala kutokana na kusitishwa kwa ununuzi, na kuna hofu ya kupungua kwa uuzwaji wa matunda kuelekea nchi kama vile Jordan, Uingereza na nchi za Skandinavia.<br />
&#8230;<br />
Ilan Eshel, mkurugenzi wa shirika la wakulima wa matunda nchini Israeli, alisema kuwa nchi za Kiskandinavia pia zimekuwa zikisitisha uagizaji.</p></blockquote>
<p>Bloga wa Kimarekani anayeishi Palestina, anaandika yale wasomi wa Uingereza wanayosema kuhusu mashambulizi ya Israeli huko Gaza:</p>
<blockquote><p>Wasomi wa Uingereza wameandika barua ya wazi, iliyochapwa  kwenye gazeti la Guardian, inayoitisha ususiaji, kuondoa vitega uchumi, na migomo:<br />
&#8220;Ni lazima tufanye tunaloweza ili kuizua Israeli kushinda vita hivi. Israeli ni lazima ikubali kuwa usalama wake unategemea haki na kuishi salama pamoja na majirani zake, na siyo kwa kutegemea matumizi maovu ya nguvu.<br />
&#8220;Tunaamini israeli lazima isitishe mara moja bila masharti mashambulizi yake huko gaza, isitishe ukaliaji wa mabavu kwenye Ukingo wa Magharibi, waache madai ya kumiliki au kuendesha himaya inayovuka mipaka yake ya 1967. Tuanitaka serikali ya Uingereza na watu wa Uingereza kuchukua hatua zote zinazowezekana za kuitaka Israeli ikubaliane na madai haya, kwa kuanza na programuya ususiaji, kuondoa vitega uchumi, na vikwazo.&#8221;<br />
Mjini London wanafunzi pia walichukua hatua ya mshikamano na Gaza katika chuo cha Uchumi cha London:</p>
<p>Zaidi ya wanafunzi 40 waliendela na kampeni yao ya kukaa chini katika Chuo Cha Uchumi cha London leo hii ili kupinga machafuko huko Gaza.</p></blockquote>
<p>Pia kuna asasi na tovuti ambazo zinalenga tu kusambaza habari juu ya kampeni kama <a href="http://www.pacbi.org/">hii</a>, <a href="http://www.bigcampaign.org/">hii</a> na <a href="http://www.bdsmovement.net/">hii</a>.</p>
<p>Lakini kwa upande mwingine, wengine, kama vile bloga <a href="http://xrdarabia.org/2009/01/13/saudis-boycotting-american-goods/">Crossroads Arabia </a>hawakutilia mkazo sana kwenye kususia bidhaa:</p>
<blockquote><p>Gazeti la Saudi liliripoti kwamba kususia bidhaa za Marekani ili kuwaunga mkono watu wa Gaza kumeanza kumea nchini Saudi Arabia. Kama ilivyowahi kutokea awali, ususiaji huu unaweza a) kupunguza hisia za kutokuwa na nguvu [za Waarabu] na b) kuumiza wamiliki wa Kiarabu pamoja na wafanyakazi wao, bila ya kuathiri uchumi wa Marekani, kinyume na vile anavyodai profesa wa Chuo Kikuu cha Abdulaziz.<br />
Hata hivyo, ni wazi kwamba dhana ya kususa inaungwa mkono na wengi.</p></blockquote>
<p>Kadhalika, bloga <a href="http://www.jewlicious.com/2006/04/starbucks-one-of-the-most-dangerous-zionist-terrorism-tools-in-the-world/">Jewlicious</a> ameandika makala kumjibu Khobbeizeh:</p>
<blockquote><p>Mimi si mshabiki wa Starbucks, au kahawa, lakini suala la Starbucks kuunga mkono Jeshi la Israeli kwa kiasi cha &#8220;mamia ya mamilioni kila mwaka&#8221; ni jambo ambalo ni vigumu kuaminika. Rafiki yangu Khobbeizeh, tukiweka pembeni ufundi wako wa kutumia Photoshop, wewe ni mbumbumbu.</p></blockquote>
]]></content:encoded>
			<wfw:commentRss>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/02/mashariki-ya-kati-vikwazo-kama-silaha-ya-kisiasa/feed/</wfw:commentRss>
		<slash:comments>0</slash:comments>
		</item>
	</channel>
</rss>
