GlobalVoices katika

Egypt

Kumbukumbu za nchi · 32 jumbe


Habari mpya Kuhusu Egypt

2 Machi 2013

Wa-Mauritania Wapinga Udhalilishaji wa Viwanja vya Tahrir Square

صورة من الوقفة نشرها حساب موريتانيا اليوم على فيسبوك

Mwandamanaji akisema “Tunapinga Udhalilishaji” picha ya Jarida la “Mauritania Today” kwenye mtandao wa Facebook.


Siku ya Jumanne Februari 12, 2013, kikundi cha wanaharakati wa ki-Mauritania kiliandaa [ar] maandamano mbele ya Ubalozi wa Misri jijini Nouakchott, mji mkuu wa Mauritania, kupinga udhalilishaji wa kijinsia na ubakaji ambao wanawake wa ki-Misri wamekuwa wakikumbana nao kwenye viwanja vya Tahrir jijini Cairo.

Tukio hilo la maandamano liliratibiwa na “Etkelmi” (Sema kwa kiarabu) [ar - fr], Asasi Isiyo ya Kiserikali inayopambana na ubakaji nchini Mauritania. Mekfoula Brahim anawapa heshima wale wote walioshiriki maandamano hayo [ar]:

شكرا لكم يا مواطنو ا العالم على وقفتكم امام السفارة المصرية فى انواكشوط لدعم نساء مصر اللائى يمارسن حقهن فى التظاهر السلمى فى مصر وعلينا جميعا القيام بوقفة اخرى احتجاجا على دعم الارهاب علنا من طرف الكثيرين والتأصيل له فى ثقافتنا المنفتحة

Asante sana wananchi wote duniani kote kwa kuandamana mbele ya Ubalozi wa Misri jijini Nouakchott kuwaunga mkono wanawake wa Misri wanaotumia haki yao ya kuandamana kwa amani nchini Misri. Tuanze kuandaa mandamano mengine kuwapinga wale (wengi) wanaounga mkono ugaidi na wale wanaojaribu kuuchukua utamaduni wentu wa uwazi.

27 Oktoba 2012

Misri: Ushauri kwa Waandamanaji wa Kuwait

Soma makala hii.

Wakati watu wa Kuwait walipoanzisha maandamano makubwa ambayo hayakuwahi kutokea ya kuonesha waziwazi kutokukubaliana na mabadiliko ya sheria ya uchaguzi yaliyopitishwa chini ya mtawala wa kurithi kufuatia kuvunjwa kwa bunge, watu wa Misri wametumia muda wao mwingi katika Twita wakitoa ushauri kwa watu wa Kuwait kuhusiana na yapi ya kufanya na yapi ya kutokufanya.

7 Julai 2012

Misri: Mubarak Afariki Dunia kwa Mara Nyingine

Rais wa zamani wa Misri Hosni Mubarak amewahi kufa angalau mara moja kwa kila baada ya majuma machache tangu kuanza kwa mapinduzi ya Misri, yaliyouangusha utawala wake uliodumu kwa miaka 32. Watumiaji wa mtandao wanaitikia tetesi za hivi karibuni kuhusu afya yake.

24 Juni 2012

Sudani: Watumia Mtandao Wathibitisha Tetesi za Kukatwa kwa Intaneti

Raia wa kwenye mtandao wanaifuatilia kwa karibu Sudani, kufuatia tetesi kuwa serikali ya Sudani inadhamiria kuukata mtandao wa intaneti - hatua inayokumbushia jaribio la Misri kuwanyamazisha wanaharakati na kuthibiti mapinduzi ya Januari 25 pale ilipoondoa uwezekano wa watu kuwasiliana kwa mtandao wa intanenti mnamo Januari 27.

12 Juni 2012

Misri: Maandamano ya Kukomesha Udhalilishaji wa Kijinsia Yavamiwa

Soma makala hii.

Maandamano kudai kukomeshwa kwa udhalilishaji wa kijinsia yaligeuka kuwa shubiri baada ya wanawake waliokuwa wanahusika nayo kuvamiwa na kundi la wanaume wenye hasira kwenye viwanja vya Tahrir leo(June 8, 2012). Watu walioshuhudia tukio hilo walielezea maoni yao kupitia twita.

16 Aprili 2012

Misri: Kundi la “Muslim Brotherhood” dhidi ya Baraza la Kijeshi – Waonyesha Sura Halisi?

Soma makala hii.

“Maandamano ya watu milioni ya kudai kung'olewa kwa baraza la Ganzouri" ndivyo kilivyosomeka kichwa cha habari cha gazeti rasmi la Freedom and Justice Party kufuatia matukio yaliouacha umma wa Wamisri wakiwa mdomo wazi. Je, nini kimetokea kiasi cha karibia "mvunjiko mbaya" kati ya Baraza la Kijeshi na chama cha kisiasa kilichokuwa karibu kutwaa madaraka, pande ambazo zilikuwa na uhusiano mzuri?

28 Aprili 2011

Misri: Basboussa kwa Urais!

Soma makala hii.

Mtangazaji habari wa zamani wa televisheni ya Misri na mwanaharakati Bothaina Kamel alitangaza kwenye twita kwamba ana mipango ya kugombea urais. Yafuatayo ni maoni ya kumuunga mkono na kupinga hiyo mipango yake .

4 Februari 2011

Photos jumbe
Misri: Picha Zinapoongea Zaidi Ya Maneno

Soma makala hii.

Kadri ya watu milioni tayari wapo kwenye viwanja vya (Ukombozi) vya Tahrir jijini Cairo wakiimba, na kumtaka Mubarak aondoke. Maandamano ya kumpinga Mubarak yamekuwa yakifanywa nchini misri kwa siku 11 mfululizo na siku ya leo imepewa jina la Ijumaa ya Kuondoka au Ijumaa ya Mwisho. Hapa kuna baadhi ya picha zilizotumwa kwa njia ya Twita na watu waliopo kwenye eneo hilo, zinazoonyesha umma unaoandamana kuelekea kwenye viwanja (vya Tahrir), wanavyopekuliwa kwa makini katika vituo vya ukaguzi vilivyowekwa ili kuwalinda waandamanaji wa amani mbali na wahuni waliolipwa na serikali.

2 Februari 2011

Misri: El Baradei – Rafiki au Adui wa Waandamanaji?

Soma makala hii.

Kiongozi wa upinzani nchini Misri Dr Mohamed El Baradei alifanya ziara fupi kwa maelfu ya waandamanaji wanaompinga Mubarak, walioweka kambi kwenye viwanja vya Tahrir jijini Cairo, dakika chache zilizopita. Maoni kutoka Twita yanafuata.

31 Januari 2011

Misri: Habari Za Maandamano Ya Upinzani Moja Kwa Moja Kwenye Facebook

Habari za maandamano ya upinzani ya Januari 25 ya vuguvugu la la Vijana wa Aprili 6 zinapatikana kwenye ukurasa huu wa Facebook (Ar). Taarifa zimeibuka leo kuwa Facebook ilikuwa imezuiliwa isipatikane nchini Misri.

Sehemu za Dunia

Nchi

Lugha