<?xml version="1.0" encoding="UTF-8"?>
<rss version="2.0"
	xmlns:content="http://purl.org/rss/1.0/modules/content/"
	xmlns:wfw="http://wellformedweb.org/CommentAPI/"
	xmlns:dc="http://purl.org/dc/elements/1.1/"
	xmlns:atom="http://www.w3.org/2005/Atom"
	xmlns:sy="http://purl.org/rss/1.0/modules/syndication/"
	xmlns:slash="http://purl.org/rss/1.0/modules/slash/"
	>

<channel>
	<title>Global Voices in Swahili &#187; Algeria</title>
	<atom:link href="http://sw.globalvoicesonline.org/category/world/middle-east-north-africa/algeria/feed/" rel="self" type="application/rss+xml" />
	<link>http://sw.globalvoicesonline.org</link>
	<description>Dunia inaongea, je unasikiliza?</description>
	<lastBuildDate>Wed, 02 Dec 2009 12:35:07 +0000</lastBuildDate>
	<generator>http://wordpress.org/?v=2.8.4</generator>
	<language>en</language>
	<sy:updatePeriod>hourly</sy:updatePeriod>
	<sy:updateFrequency>1</sy:updateFrequency>
			<item>
		<title>Misri na Aljeria: Pambano la Twita</title>
		<link>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/11/misri-na-aljeria-pambano-la-twita/</link>
		<comments>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/11/misri-na-aljeria-pambano-la-twita/#comments</comments>
		<pubDate>Mon, 16 Nov 2009 12:04:35 +0000</pubDate>
		<dc:creator>j nambiza tungaraza</dc:creator>
				<category><![CDATA[Algeria]]></category>
		<category><![CDATA[Egypt]]></category>
		<category><![CDATA[International Relations]]></category>
		<category><![CDATA[Media]]></category>
		<category><![CDATA[Middle East & North Africa]]></category>
		<category><![CDATA[Sport]]></category>
		<category><![CDATA[Weblog]]></category>

		<guid isPermaLink="false">http://sw.globalvoicesonline.org/?p=673</guid>
		<description><![CDATA[Katika sehemu nyingi duniani, hakuna linalounganisha zaidi – au wakati mwingine kutenganisha – zaidi ya pambano la mpira wa miguu. Washabiki wa Misri na Aljeria, katika ulimwengu wote wa Waarabu na zaidi, walilidhihirisha hilo Jumamosi hii wakati timu zao zilipokwenda sambamba wakati wa kuwania kuingia fainali za Kombe la Dunia huko Afrika Kusini. ]]></description>
			<content:encoded><![CDATA[<em>Ilichapwa kwanza na<a href="http://globalvoicesonline.org/author/jillian-york/">Jillian C. York</a>  &middot; Imetafsiriwa na <a href='http://sw.globalvoicesonline.org/author/j-nambiza-tungaraza/'>j nambiza tungaraza</a> &middot;  <a href='http://globalvoicesonline.org/2009/11/15/egypt-vs-algeria-the-twitter-match/'>Angalia ujumbe mama</a></em> 
<br /><p>Katika sehemu nyingi duniani, hakuna linalounganisha zaidi – au wakati mwingine kutenganisha – zaidi ya pambano la mpira wa miguu. Washabiki wa Misri na Aljeria, katika ulimwengu wote wa Waarabu na zaidi, walilidhihirisha hilo Jumamosi hii wakati timu zao zilipokwenda sambamba wakati wa kuwania kuingia fainali za Kombe la Dunia huko Afrika Kusini. Wakati vihoro vilipanda juu huko mjini Cairo, pia vilikuwa hai na katika hali nzuri kwenye uwanja yakini mtandaoni, pamoja na kwenye <a href="http://twitter.com/">Twita</a>, ambako watumiaji walitaarifu kuwa skrini zao zilijaa hisia za mpira. Mtumiaji wa Twita <em><a href="http://twitter.com/mbaa">mbaa</a></em> alituma picha ya skrini yake, ambayo ilifurika mazungumzo ya pambano hilo:</p>
<p><img alt="" src="http://globalvoicesonline.org/wp-content/uploads/2009/11/mbaa2.jpg" title="mbaa" class="aligncenter" width="535" height="410" /></p>
<p>Ujumbe wa twita kutoka kwa Mmisri <em><a href="http://twitter.com/embee">embee</a></em> <a href="http://twitter.com/embee/status/5718935256">ulionyesha</a> ushabiki uliokithiri wa baadhi ya washabiki:</p>
<p><img alt="" src="http://globalvoicesonline.org/wp-content/uploads/2009/11/embee-status-5718935256-300x113.PNG" title="embee-status-5718935256" class="aligncenter" width="300" height="113" /></p>
<p>Baadhi ya taarifa zinadai kuwa tiketi zote zimekwishauzwa hivi sasa! Wakati huo huo, Mmisri <em><a href="http://twitter.com/norayounis">NoraYounis</a></em> <a href="http://twitter.com/norayounis/status/5718108814">alielezea kutoamini</a> kwake katika nguvu ya kuunganisha ya mpira wa miguu kwa Wamisri:</p>
<p><img alt="" src="http://globalvoicesonline.org/wp-content/uploads/2009/11/NoraYounis-status-5718108814-300x152.PNG" title="NoraYounis-status-5718108814" class="aligncenter" width="300" height="152" /></p>
<p><a href="http://twitter.com/nohaatef/status/5718339271">Ujumbe wa twita</a> wa Mmisri <em><a href="http://twitter.com/nohaatef">NohaAtef</a></em>, kwa upande mwingine, ulionyesha vitu vinavyoweza kuinua mioyo katika mpira wa miguu:</p>
<p><img alt="" src="http://globalvoicesonline.org/wp-content/uploads/2009/11/NohaAtef-status-5718339271-300x151.PNG" title="NohaAtef-status-5718339271" class="aligncenter" width="300" height="151" /></p>
<p>Katika mifano mingi, mpira wa miguu ulichimbua ushindani wa kitaifa. Waaljeria na Wamisri walikwenda kichwa kwa kichwa kwenye twita wakati pambano likiendelea. Mmisri <em><a href="http://twitter.com/sandmonkey">Sandmonkey</a></em> <a href="http://twitter.com/sandmonkey/status/5714575409">aling’aka</a>: </p>
<p><img alt="" src="http://globalvoicesonline.org/wp-content/uploads/2009/11/Sandmonkey-status-5714575409-300x86.PNG" title="Sandmonkey-status-5714575409" class="aligncenter" width="300" height="86" /></p>
<p>Mualjeria-Mmarekani <em><a href="http://twitter.com/themoornextdoor">themoornextdoor</a></em> alijibu mapigo <a href="http://twitter.com/themoornextdoor/status/5715301341">akitania</a>:</p>
<p><img alt="" src="http://globalvoicesonline.org/wp-content/uploads/2009/11/themoornextdoor-status-5715301341-300x124.PNG" title="themoornextdoor-status-5715301341" class="aligncenter" width="300" height="124" /></p>
<p>Mwishowe, Mualjeria <em><a href="http://twitter.com/reemba">reemba</a></em> <a href="http://twitter.com/reemba/status/5717755317">alitukumbusha</a> kuwa mambo bado hayajaisha mpaka yaishe:</p>
<p><img alt="" src="http://globalvoicesonline.org/wp-content/uploads/2009/11/reemba-status-5717755317-300x147.PNG" title="reemba-status-5717755317" class="aligncenter" width="300" height="147" /></p>
]]></content:encoded>
			<wfw:commentRss>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/11/misri-na-aljeria-pambano-la-twita/feed/</wfw:commentRss>
		<slash:comments>0</slash:comments>
		</item>
		<item>
		<title>Algeria-Misri: Ugomvi Juu ya pambano la Mpira kwenye Mtandao</title>
		<link>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/11/algeria-misri-ugomvi-juu-ya-pambano-la-mpira-kwenye-mtandao/</link>
		<comments>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/11/algeria-misri-ugomvi-juu-ya-pambano-la-mpira-kwenye-mtandao/#comments</comments>
		<pubDate>Sun, 15 Nov 2009 10:52:06 +0000</pubDate>
		<dc:creator>j nambiza tungaraza</dc:creator>
				<category><![CDATA[Algeria]]></category>
		<category><![CDATA[Arabic]]></category>
		<category><![CDATA[Egypt]]></category>
		<category><![CDATA[English]]></category>
		<category><![CDATA[French]]></category>
		<category><![CDATA[Middle East & North Africa]]></category>
		<category><![CDATA[Photos]]></category>
		<category><![CDATA[Sport]]></category>
		<category><![CDATA[Video]]></category>
		<category><![CDATA[Weblog]]></category>

		<guid isPermaLink="false">http://sw.globalvoicesonline.org/?p=659</guid>
		<description><![CDATA[Hali tete kati ya mashabiki wa mpira wa miguu wa Misri na Algeria inazidi kukua kabla ya pambano litakalofanyika mjini Cairo tarehe 14 Novemba. Mchuano huo utaamua ipi kati ya timu hizo zitafaulu kwenda kwenye Kombe la Dunia la FIFA Afrika ya kusini mwaka ujao. Misri inahitaji japo ushindi wa magoli mawili ili kulazimisha mchezo wa kukata shauri katika uwanja wa nchi nyingine ambapo Algeria, ambayo imeshindwa kufaulu kwenda kombe la dunia tangu 1986, itapambana ili kutunza nafasi yake ya sasa ya kuongoza katika kundi la wanaogombania nafasi ya kufaulu. Wakati wa kuelekea pambano la Jumamosi, mashabiki washindani wamekuwa wakijiandaa nje ya mtandao wa intaneti, kadhalika katika malumbano makali ya mtandaoni, ambayo yamekua na kugeuka “vita-vya-mikwara-kwenye-mtandao” ]]></description>
			<content:encoded><![CDATA[<em>Ilichapwa kwanza na<a href="http://globalvoicesonline.org/author/hisham/">Hisham</a>  &middot; Imetafsiriwa na <a href='http://sw.globalvoicesonline.org/author/j-nambiza-tungaraza/'>j nambiza tungaraza</a> &middot;  <a href='http://globalvoicesonline.org/2009/11/12/algeria-egypt-online-feud-over-football-match/'>Angalia ujumbe mama</a></em> 
<br /><p>Hali tete kati ya mashabiki wa mpira wa miguu wa Misri na Algeria inazidi kukua kabla ya pambano litakalofanyika mjini Cairo tarehe 14 Novemba. Mchuano huo utaamua ipi kati ya timu hizo zitafaulu kwenda kwenye Kombe la Dunia la FIFA Afrika ya kusini mwaka ujao. Misri inahitaji japo ushindi wa magoli mawili ili kulazimisha mchezo wa kukata shauri katika uwanja wa nchi nyingine ambapo Algeria, ambayo imeshindwa kufaulu kwenda kombe la dunia tangu 1986, itapambana ili kutunza nafasi yake ya sasa ya kuongoza katika <a href="http://www.fifa.com/worldcup/preliminaries/africa/standings/group=252301/index.html">kundi la wanaogombania nafasi ya kufaulu</a>. Wakati wa kuelekea pambano la Jumamosi, mashabiki washindani wamekuwa wakijiandaa nje ya mtandao wa intaneti, kadhalika katika malumbano makali ya mtandaoni, ambayo yamekua na kugeuka “vita-vya-mikwara-kwenye-mtandao” </p>
<p>Mwanablogu wa Algeria <em><a href="http://adelife.wordpress.com/2009/11/10/football-avant-la-bataille-du-caire%E2%80%A6-une-guerre-pas-tres-nette/">Adel</a> </em>[Fr] anatoa muhtasari wa mlolongo wa matukio ambayo yamesababisha mzozo. Anaandika:</p>
<blockquote><p>Ce n’est pas sur le carré vert que le match a commencé à se jouer mais sur la toile. En attendant l’entrée des 22 joueurs sur la pelouse du fameux Cairo Stadium, la rencontre a débuté de manière assez peu banale entre les «Facebookeurs» (membres du réseau Facebook) algériens et égyptiens. Tout a commencé par de simples discussions dans les forums avant que cela ne prenne de l’ampleur. Voulant montrer leur savoir-faire dans la retouche d’image, les Egyptiens ont été les premiers à ouvrir les hostilités en publiant des photos «anti-algérien».</p>
<p>Les Egyptiens voulaient expliquer à travers un tel acte que leurs joueurs sont «très forts» et qu’ils sont en mesure d’écraser l’équipe nationale algérienne. Cela donna le top à une guerre d’un genre particulier. La guerre des images et des parodies.</p></blockquote>
<div class="translation">Inaelekea kuwa mechi imeshaanza mtandaoni, mbali na uwanja wa mpira. Kabla ya wachezaji 22 kuingia uwanja maarufu wa Cairo, pambano kali limeanza katik ya watumiaji wa Facebook wa Kialgeria na Kimisri. Yote yalianza na majadiliano ya kirafiki katika majukwaa ya mtandaoni, kabla ya mambo kuzidi kipimo. Wakitaka kuonyesha utaalamu wao wa kuhariri picha, Wamisri ndio walikuwa wa kwanza kuanzisha uhasama kwa kuchapisha picha “zinazoipinga Algeria”.</p>
<p>Wamisri walitaka kuonyesha kuwa wachezaji wao ndio “wenye nguvu” na kwamba wana uwezo wa kuiponda timu ya taifa ya Algeria. Hii ilitoa ishara ya kuanza vita ya namna ya pekee. Vita ya picha na utani. </p></div>
<p>Video, zilizoiga picha zilichokuliwa kutoka kwenye filamu maarufu za Hollywood, zilifurika kwenye YouTube, na kuweka ugomvi huu katika ngazi ya…..</p>
<p>Katika video inayofuata [Ar], iliyowekwa na <em><a href="http://www.youtube.com/user/hakemvoip">hakemvoip</a></em> [Fr], Mel Gibson ni <em>Rabah Wallace</em> (Katika filamu ya Braveheart), jemedari wa vita wa Kialgeria ambaye anajaribu kuhamasisha wapiganaji kabla ya vita inayotarajiwa:</p>
<p><object width="425" height="344"><param name="movie" value="http://www.youtube.com/v/yCtAQ_9XMAE&#038;color1=0xb1b1b1&#038;color2=0xcfcfcf&#038;hl=en&#038;feature=player_embedded&#038;fs=1"></param><param name="allowFullScreen" value="true"></param><param name="allowScriptAccess" value="always"></param><embed src="http://www.youtube.com/v/yCtAQ_9XMAE&#038;color1=0xb1b1b1&#038;color2=0xcfcfcf&#038;hl=en&#038;feature=player_embedded&#038;fs=1" type="application/x-shockwave-flash" allowfullscreen="true" allowScriptAccess="always" width="425" height="344"></embed></object></p>
<p>Katika video hii, Mmisri <em><a href="http://www.youtube.com/user/ulyesis">ulyesis</a></em> anawakaribisha mashabiki wa Algeria katika kile anachokiita “jehanam” ndani ya jiji la Cairo:</p>
<p><object width="425" height="344"><param name="movie" value="http://www.youtube.com/v/OZOgyioZxFs&#038;color1=0xb1b1b1&#038;color2=0xcfcfcf&#038;hl=en&#038;feature=player_embedded&#038;fs=1"></param><param name="allowFullScreen" value="true"></param><param name="allowScriptAccess" value="always"></param><embed src="http://www.youtube.com/v/OZOgyioZxFs&#038;color1=0xb1b1b1&#038;color2=0xcfcfcf&#038;hl=en&#038;feature=player_embedded&#038;fs=1" type="application/x-shockwave-flash" allowfullscreen="true" allowScriptAccess="always" width="425" height="344"></embed></object></p>
<p>Mwanablogu <em><a href="http://www.gemyhood.com/2009/11/blog-post_11.html">GEMYOoOD</a> </em>[Ar] katuma picha ya maelfu ya mashabiki wa Misri waliopanga foleni katika sehemu tofauti za Cairo, wakitarajia kupata tiketi kwa ajili ya mechi. <a href="http://www.gemyhood.com/2009/11/blog-post_11.html">Anachapisha</a> picha za mikusanyiko hiyo ya watu:</p>
<p><img alt="" src="http://globalvoicesonline.org/wp-content/uploads/2009/11/Egyptian-Fans-300x225.jpg" title="Egyptian Fans" class="aligncenter" width="300" height="225" /></p>
<p><img alt="" src="http://globalvoicesonline.org/wp-content/uploads/2009/11/Egyptian-Fans2-300x225.jpg" title="Egyptian Fans" class="aligncenter" width="300" height="225" /></p>
<p><em><a href="http://www.gemyhood.com/2009/11/blog-post_11.html">GEMYHOoOD</a></em> pia anatuma baadhi ya maoni ya watu wanaoshuhudia:</p>
<blockquote><p>انا خدت اجازة اليوم ونزلت من الصبح لنادي الصيد الساعة 8 الصبح وللاسف لقيت موت ناس وزحمة وطابور فيه حوالي 3000 واحد ودفع وشتيمة والناس كل شوية بتزيد ومش عارف اقف من الزق والعرق بجد مهزلة</p></blockquote>
<div class="translation">Nilichukua ruksa ya siku ili nije kwenye klabu saa 2 asubuhi [kununua tiketi]. Kwa masikitiko nilikuta kundi kubwa la watu na foleni kubwa ya kadri ya watu 3000, huku watu wakisukumana na kutukanana. Sikuweza kusogea. Nilikwama. Nikafikiri, hiini aibu.</div>
<p>Basi rasmi la timu ya mpira wa miguu ya Algeria, ambalo liliwasili mjini Cairo tarehe 12 Novemba, inadaiwa kuwa lilishambuliwa na mashabiki, kama video inayofuata, iliyotumwa katika YouTube na <em><a href="http://www.youtube.com/user/wmcvideotv">Vidéos Mouloudia Club d&#39;Oran</a></em>, inavoelekea kuonyesha:</p>
<p><object width="425" height="344"><param name="movie" value="http://www.youtube.com/v/XNbZqBTvWBw&#038;color1=0xb1b1b1&#038;color2=0xcfcfcf&#038;hl=en_US&#038;feature=player_embedded&#038;fs=1"></param><param name="allowFullScreen" value="true"></param><param name="allowScriptAccess" value="always"></param><embed src="http://www.youtube.com/v/XNbZqBTvWBw&#038;color1=0xb1b1b1&#038;color2=0xcfcfcf&#038;hl=en_US&#038;feature=player_embedded&#038;fs=1" type="application/x-shockwave-flash" allowfullscreen="true" allowScriptAccess="always" width="425" height="344"></embed></object></p>
<p>Baraza linalodhibiti mpira wa miguu duniani <a href="http://www.fifa.com/">FIFA</a>, lilihisi umuhimu wa kutoa onyo kwa vyama vya mpira wa miguu vya Algeria na Misri, likiwakumbusha wote kuwa “mashindano ya awali kwa ajili ya kombe la Dunia 2010 yamalizike kama yalivyoanza, katika moyo wa mchezo wenye haki ulio na ushirikiano unaohitajika kutoka kwa washiriki wote.”<br />
<img alt="" src="http://globalvoicesonline.org/wp-content/uploads/2009/11/One-People.jpg" title="One People, One Language One Goal" class="alignright" width="200" height="500" /><br />
Tovuti, <a href="http://www.algerieegypte.com/">Algerie Egypte Match</a> [Ar, Fr], inayoandika kuhusu tukio hili na kufuatilia kila namna ya habari inayohusiana na mechi, iliundwa na washabiki wa Algeria.</p>
<p>Katika hali hii ya ushindani mkali, baadhi ya watu wameunda <a href="http://www.facebook.com/group.php?v=wall&#038;gid=167702883826">kundi</a> kwenye tovuti ya mtandao wa kijamii Facebook, wakiomba hisia mbaya zaidi. <em>Laama Bouchema</em> katuma ujumbe katika ukuta wa kundi hilo unaosema:</p>
<blockquote><p>Pamoja na kukasirika kwangu kutokana na kilichoitokea timu ya Algeria, siihukumu nchi yote kwa kile alichofanya mpumbavu mmoja! Wanachokifanya mashabiki wenye hasira ni upumbavu! kwa ajili ya mungu si jambo kubwa ni nani atakeyeingia katika [kombe la dunia].</p></blockquote>
<p>Mwanablogu wa Kimisri <em><a href="http://www.lastoadri.com/2009/10/blog-post.html">Lasto Adri</a></em> [Ar] anaeleza kuchukizwa kwake na jinsi kile kilichopaswa kuwa tukio la michezo, kimeshushwa hadhi na kuwa pambano chafu. Anaandika:</p>
<blockquote><p>
مندهشة من التعصب وتدنى مستوى لغة الحوار بين مشجعى منتجب مصر ومنتخب الجزائر والظاهر بوضوح فى التعليقات على المواقع الإخبارية أو الرياضية… ومندهشة أكثر بتغذية هذه المأساه إعلاميا بتعليقات من بعض المذيعين (من كلا الجانبين)…<br />
المشجعون الجزائريون أخطؤوا فى المبارة السابقة.. لكن هل الرد يكون هكذا؟.. هل الرد يكون بطلب البعض تسميم اللعيبة ولا إقلاقهم فى منامهم ولا توليع الإستاد وقت الماتش من التشجيع؟..<br />
ونرفزتنى التعليقات على أغلب المواقع.. وإفتكرت لما الجزائر -بزعامة الرئيس الجزائري هواري بومدين- كانت أكتر دولة ساندت مصر فى حرب 1973، رغم فقرها الشديد..<br />
حزينة ان انتهاء علاقة مابين شعبين تكون بشقاق على كورة…</p></blockquote>
<div class="translation">Ninashangazwa na kiwango cha kutovumiliana na lugha chafu inayotumiwa na mashabiki wa timu za Algeria na Misri, ambayo inajitokeza katika maoni mengi kwenye tovuti za habari na michezo… pia ninashangazwa na jinsi ambayo baadhi ya watangazaji na wanahabari (kutoka pande zote), wanavyochochea dhahama hii kupitia maoni yao makali…<br />
Mashabiki wa Algeria hawakujiheshimu katika mchezo uliopita… lakini je jibu la Wamisri ni sahihi?..<br />
Je jibu linapaswa kuwa (kama baadhi walivyosema) kuwapa sumu wachezaji wa Algeria? Kuwaghasi na kuwanyima usingizi? Kuuchoma moto uwanja siku ya pambano?<br />
Nimeudhika na maoni yaliyo kwenye tovuti nyingi… Ninakumbuka wakati Algeria – ikiongozwa na Rais Houari Boumedienne – bila kujali umaskini wao uliokithiri, alikuja kuiunga mkono misri wakati wa vita ya mwaka 1973…</div>
]]></content:encoded>
			<wfw:commentRss>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/11/algeria-misri-ugomvi-juu-ya-pambano-la-mpira-kwenye-mtandao/feed/</wfw:commentRss>
		<slash:comments>0</slash:comments>
		</item>
		<item>
		<title>Arabeyes: Rais wa Mauritania Aliyepinduliwa Katika mapinduzi ya Kijeshi</title>
		<link>http://sw.globalvoicesonline.org/2008/08/arabeyes-rais-wa-mauritania-aliyepinduliwa-katika-mapinduzi-ya-kijeshi/</link>
		<comments>http://sw.globalvoicesonline.org/2008/08/arabeyes-rais-wa-mauritania-aliyepinduliwa-katika-mapinduzi-ya-kijeshi/#comments</comments>
		<pubDate>Sun, 17 Aug 2008 23:10:33 +0000</pubDate>
		<dc:creator>charahani</dc:creator>
				<category><![CDATA[Algeria]]></category>
		<category><![CDATA[Arabic]]></category>
		<category><![CDATA[Breaking News]]></category>
		<category><![CDATA[Egypt]]></category>
		<category><![CDATA[English]]></category>
		<category><![CDATA[French]]></category>
		<category><![CDATA[Governance]]></category>
		<category><![CDATA[Iraq]]></category>
		<category><![CDATA[Mauritania]]></category>
		<category><![CDATA[Morocco]]></category>
		<category><![CDATA[Politics]]></category>
		<category><![CDATA[War & Conflict]]></category>
		<category><![CDATA[Western Sahara]]></category>

		<guid isPermaLink="false">http://sw.globalvoicesonline.org/?p=10</guid>
		<description><![CDATA[ &#183; Imetafsiriwa na charahani &#183;  Angalia ujumbe mama 

MAKAMANDA wa jeshi wamemuondoa madarakani Rais Sidi Ould Cheikh Abdallahi, rais wa kwanza kuchaguliwa katika uchaguzi huru katika miongo miwili, katika mapinduzi ya kijeshi yaliyofanywa Jumatano iliyopita baada ya mtafaruku wa kisiasa uliotokana na rais huyo kuwatimua kazi majenerali wanne wa ngazi za juu wa [...]]]></description>
			<content:encoded><![CDATA[<em> &middot; Imetafsiriwa na <a href='http://sw.globalvoicesonline.org/author/charahani/'>charahani</a> &middot;  <a href='http://globalvoicesonline.org/2008/08/06/arabeyes-mauritanian-president-ousted-in-military-coup-detat/'>Angalia ujumbe mama</a></em> 
<br /><p><img src='http://globalvoicesonline.org/wp-content/uploads/2008/08/457px-sidi_mohamed_ould_cheikh_abdallahi2.jpg' alt='' class='alignright' /><br />
MAKAMANDA wa jeshi <a href="http://www.abc.net.au/news/stories/2008/08/07/2326564.htm">wamemuondoa</a> madarakani <a href="http://www.answers.com/President%20Sidi%20Ould%20Cheikh%20Abdallahi">Rais Sidi Ould Cheikh Abdallahi</a>, rais <a href="http://www.answers.com/Mauritania">wa kwanza kuchaguliwa katika uchaguzi huru katika miongo miwili</a>, katika mapinduzi ya kijeshi yaliyofanywa Jumatano iliyopita baada ya mtafaruku wa kisiasa uliotokana na rais huyo kuwatimua kazi majenerali wanne wa ngazi za juu wa jeshi.  Makamanda wa jeshi walitangaza kuundwa kwa Baraza jipya la taifa na kiongozi wake, <a href="http://en.wikipedia.org/wiki/Mohamed_Ould_Abdel_Aziz">Jenerali Mohamed Ould Abdel Aziz </a>(mmoja kati ya majenerali wanne wa jeshi waliotimuliwa), kwenye radio na vituo vya televisheni vya serikali. Jenerali Abdel Aziz ni miongoni mwa walioshiriki <a href="http://en.wikipedia.org/wiki/2005_Mauritanian_coup_d%27%C3%A9tat">mapinduzi ya kijeshi nchini Mauritania mwaka 2005</a>.</p>
<p>Bloga kutoka Algeria <em>The Moor next Door</em> amekuwa <a href="http://themoornextdoor.wordpress.com/2008/08/06/the-president-will-not-be-taking-calls-today/">akiblogu</a> <a href="http://themoornextdoor.wordpress.com/2008/08/06/china-and-mauritania/">habari</a> <a href="http://themoornextdoor.wordpress.com/2008/08/06/coup-snapshots/">hii</a> <a href="http://themoornextdoor.wordpress.com/2008/08/06/developing-story/">kwa kina</a> <a href="http://themoornextdoor.wordpress.com/2008/08/06/summer-time-coups/">anaripoti</a>:</p>
<blockquote><p>Ninapozungumza na Wa-Mauritania wanaojua, baadhi yao walihisi kutokea kwa mapinduzi wakati wa kiangazi kama ilivyotokea, wakati wa kipupwe au isingeweza kutokea kabisa. Hisia zangu mara zote zilikuwa zikinielekeza kwamba mapinduzi haya yangefanyika majira ya kiangazi (Sijawahi kuandika bayana juu ya hili, lakini nimelielezea hili katika majadiliano na sikutaka kuchangia lolote kuhusiana na sakata hili. (1) kwa sababu Western Sahara Info. taarifa za kutoka Sahara Magharibi zilielezea kinaganaga na hakukuwa na haja ya kushindana ikiwa wewe ni mmoja wa mabloga wawili au watatu  unakuwa miongonimwa  wanaofuatilia sakata hili kwa karibu sana. (2) nilitaka kuhakikisha kwamba kama &#8216;ningetabiri&#39; jambo hili nisingekosea; Ningeweza kutabiri kuwa &#8216;Mwishoni mwa miezi ya Mei, Juni, Julai na Agosti Serikali ya Rais Sidi, isingelikuwapo tena&#39; na ningekuwa nimekosea; mimi si mtabiri wa hali ya hewa, na (3)  sijawahi kukutana na raia wa Mmauritania ambaye lolote jema la kumzungumza kuhusu Sidi, ukiachilia mbali uzuri wa wajihi wake.) Mojawapo ya mashinikizo yaliyomfanya Rais Sidi afanye alivyofanya ni kuwapo tishio la kuundwa tume huru ya kuchunguza mapesa ya mfuko wa maendeleo wa mkewe, tume ambayo ingemuweka hata yeye mwenyewe pabaya zaidi. Tume hiyo pia ingeufanya utawala wa Rais Sidi kituko kutokana na matumizi mabaya ya fedha za umma. Kwa mfano, nimeambiwa kuwa, safari zake za ndege za nje ziliigharimu serikali zaidi ya dola za Marekani mbili bilioni, kwa kukodisha ndege za kifahari yeye na familia yake na ujumbe wake pamoja na anasa zingine zisizokuwa za lazima. Kwa hakika alikuwa katika wakati mgumu: Ama angelazimika kujiuzulu (kwa mujibu wa Olmert) katika aibu kubwa au angelazimika kuvunja bunge na hivyo kuunda serikali yake upya, hali ambayo ingempeleka katika mapinduzi kama haya tuliyoyoyashuhudia, ambayo angalau imeficha aibu yake kisiasa. Alibanwa pande zote na alikuwa hana pa kutokea zaidi ya kukumbana na hatima yake.</p></blockquote>
<p><em>Western Sahara Info</em> amekuwa akiblogu mgogoro huu tokea ulipoanza, na leo <a href="http://w-sahara.blogspot.com/2008/08/military-coup-in-mauritania.html">ametuletea</a> habari za mapinduzi hayo ya kijeshi kama zinavyotokea dakika kwa dakika, pamoja na muhtasari wa unyambuzi: </p>
<blockquote><p>Uchambuzi wa harakaharaka, ambao naweza kuujutia: balaa kwa demokrasia ya Mauritania, kwa upande mmoja, (demokrasia) ambayo haikuwa na nafasi, lakini muhimu zaidi ni kuwa (mapinduzi haya) yamerudisha nyuma nafasi iliyokuwepo kwa maendeleo ya kisiasa. Ingawa, Rais Abdellahi na washirika wake si malaika, lakini Majenerali Ghazouani na Abdelaziz wanawakilisha kundi baya la kinyonyaji katika utawala wa Mauritania, kwa kukataa kuruhusu utawala wa kiraia kutulia madarakani kwa kuwatishia kung&#39;oa kabisa utawala wa kiraia hatimaye. Kama mapinduzi ya mwisho ya kijeshi yaliyotokea Agosti 2005, yangalieleweka na Jumuiya ya Kimataifa baada ya kung&#39;olewa kwa Rais Ould Tayaa, na hatimaye kupelekea mabadiliko makubwa, mapinduzi haya ya juzi yalikuwa tofauti saana. Kilichotokea mwaka 2005 ilikuwa kwamba madikteta wa kijeshi walioegemea katika ukabila waling&#39;atuliwa na nafasi ilijitokeza ikasimika badala yake utawala wa kiraia uliokuwa na muundo wa nusu-mabavu ambao uliruhusu desturi nyingi za kidemokrasia kwa muda mwingi zaidi, (utawala huo) ulishughulikia zaidi muwafaka wa kitaifa, urejeshwaji wa wakimbizi na maendeleo ya kiuchumi; ingawa siyo hema, lakini ilikuwa bora. Mabadiliko haya hivi sasa yanageuzwa. Wapinduaji - japokuwa wengine ni miongoni mwa wale waliofanya mwaka 2005 - - ni lazima walaumiwe na matokeo ya mapinduzi yabatilishwe kama inawezekana; Mauritania ilikuwa na fursa ya pekee kuweza kuvunja mzunguko huu usiokwisha, na sasa (fursa hiyo ya pekee) inaponyoka.</p></blockquote>
<p>Blogu ya <em>Roads To Iraq</em>, katikaujumbe wenye kichwa cha habari &#8220;Wamarekani walipanga mapinduzi nchini Mauritania,&#8221; <a href="http://www.roadstoiraq.com/2008/08/06/american-orchestrated-coup-in-mauritania/">inaripoti</a> habari hiyo vile vile: </p>
<blockquote><p>Mambo yanabadilika kwa kasi sana nchini Mauritania, imeanza na mapinduzi asubuhi hii, kwa kutoa &#8220;taarifa nambari moja&#8221; katika kituo cha televisheni cha Mauritania, Mkuu wa kituo hicho cha televisheni<br />
alibadilishwa sababu alikataa kushirikiana na mkuu wa jeshi aliyeandaa mapinduzi na kumtangaza mtawala mpya wa kijeshi.</p></blockquote>
<p>Huko Misri, <em>Bella</em> [Ar]<a href="http://afkaar-bella.blogspot.com/2008/08/blog-post.html">anasema</a> kilichotokea Mauritania kimedhihirisha kuwa Waarabu hawakupangwa kwa demokrasia.</p>
<blockquote><p>Inaonekana demokrasia haikuumbwa kwa watu kama sisi - ambao hatuwezi kupumua nje ya tawala za kijeshi.</p></blockquote>
<p>Baada ya kutupa historia fupi ya demokrasia changa ya Mauritania <em>Bella</em> anaandika: </p>
<blockquote><p>Kwa njia hii, Mauritania, ambayo ilikuwa ianze kuvuna matunda ya demokrasia katika msukumo wa kiasisi ambao eneo lote la mataifa ya jirani yalikuwa yanaungalia kwa shauku, mambo yamerejea kule yalikotoka kiasili, na wanajeshi wakaingilia kati na mapinduzi kutokea.</p></blockquote>
<p>Bloga wa Kuwaiti <em>Wild Il Deera</em> <a href="http://wildildeera.blogspot.com/2008/08/blog-post_06.html">anahoji maswali machache </a>kuhusiana na mapinduzi haya. Anauliza:</p>
<blockquote><p>Jumuiya ya Kiarabu ina msimamo gani kuhusu viongozi wa mapinduzi haya?<br />
Hivi huyu kiongozi wa Mauritania hakuchaguliwa na watu wake?<br />
Hivi inawezekanaje kundi la kisiasa, kama Jumuiya ya Kiarabu, ambayo inataka kuheshimiwa katika jamii ya Kiarabu na katika ulingo wa kimataifa ikaruhusu mapinduzi kama haya kufanyika katika moja ya mataifa wanachama wake?</p></blockquote>
<p>Bloga maarufu nchini Morocco Larbi [Fr] alipachika kiungo cha makala ya ya habari, <a href="http://www.larbi.org/post/2008/08/Mauritanie%3A-Coup-d-Etat-en-cours">kisemacho</a>: </p>
<blockquote><p>Unaweza kusema: Afrika ni bara lililolaaniwa!</p></blockquote>
<p>Habari yake hiyo imepata maoni mengi. <em>Citoyen</em> anatoa maoni kwamba:</p>
<blockquote><p>Ni kweli mapinduzi hayatabiriki Afrika… Nashangaa, ingawa, kama kwa mara nyingine tena, Mashirika ya Moroko yamekatizwa kama yalivyokuwa mwezi Ogasti 2005? </p></blockquote>
<p>Mwishoni KABOBfest, ambaye huwa anaingiza vichekesho katika kila hali, <a href="http://www.kabobfest.com/2008/08/kickin-it-old-skool.html">anatoa maoni</a> yenye mzaha: </p>
<blockquote><p>Wakati utamaduni wa mapinduzi katika mataifa mengi ni utamaduni uliopitwa na wakati (kama vile Syria hakujapata kutokea mapinduzi kwa miongo kadhaa sasa) Baadhi ya mataifa yanapendelea mitindo ya kizamani,  rejea pale ambapo ianonekana palikuwa na mapinduzi kama juma moja lililopita sehemu fulani hapa duniani. Wakati Mauritania siyo Fiji, wanadumisha utamaduni usio na maana wa mapinduzi katika dunia ya Waarabu.</p></blockquote>
<p>Blogu ya Arabdemocracy pia anayo <a href="http://www.arabdemocracy.com/2008/08/mauritaniaobituary-for-young-democracy.html">taarifa ya maombolezo</a> ya iliyokuwa demokrasia changa.</p>
<p><em>Picha ya hapo juu ni ya Sidi Mohamed Ould Cheikh Abdallahi iliyopigwa na <a href="http://www.agenciabrasil.gov.br/media/imagens/2007/09/27/1254MCMauritania1.jpg/view">Marcello Casal Jr./Abr</a> (Septemba 2007)</em></p>
]]></content:encoded>
			<wfw:commentRss>http://sw.globalvoicesonline.org/2008/08/arabeyes-rais-wa-mauritania-aliyepinduliwa-katika-mapinduzi-ya-kijeshi/feed/</wfw:commentRss>
		<slash:comments>0</slash:comments>
		</item>
	</channel>
</rss>
