Habari kuhusu Mashariki ya Kati na Afrika Kaskazini kutoka Novemba, 2013
Mwanaharakati wa Misri Alaa Abd El Fattah Akamatwa — Tena
Mwanablogu mashuhuri na mwanaharakati Alaa Abd El Fattah alikamatwa jana jijini Cairo usiku wa Alhamisi. Wanaomwuunga mkono wanahisi amekamatwa kwa kutumia sheria mpya ya kuzuia maandamano.
Iran: Mwanablogu Aliyefungwa Jela Ahitaji Huduma ya Matibabu ya Haraka
Mwanablogu aliyefungwa jela,Hossein Ronaghi Maleki anahitaji huduma ya matibabu ya haraka. Alihukumiwa kifungo cha jela cha miaka 15. Laleh alitwiti Mwanaharakati aliyefungwa jela Hossein Ronaghi yuko katika hali mbaya ya afya, kuvimba figo -(moja haifanyi kazi), kibofu cha mkojo na ugonjwa wa kibofu #Iran #Iranelection — Lalehلاله (@Lalehsr) Novemba 25,...
Mkutano wa Global Voices Cairo, Misri
Mkutano mwingine wa Global Voices unapangwa kufanyika Novemba 16 jijini Cairo, Misri. Tafadhali shiriki na wanachama wetu wa Jumuiya ya GV kwa kusanyiko hili maalumu.
Udadisi wa Sami Anan
Mwanablogu wa Misri Zeinobia anatoa maoni yake machache kuhusu kuibuka tena kwa Sami Anan, Mnadhimu mkuu wa zamani wa Majeshi ya Misri. Je, ana mpango wa kugombea urais? Mwanahabari wa Sauti za Dunia Mtandaoni Victor Salama anasimulia zaidi.
Misri: “Morsi Hatarudi Madarakani”
Aliyekuwa rais wa Misri Mohamed Morsi hatarudi madarakani, anasema mwanablogu wa Misri Alya Gadi, kwenye mtandao wa Twita. Kuufanya ujumbe wake wazi, ametafsiri kwa lugha mbalimbali: مرسي لن يعود – Morsi is not coming back – Morsi no va a volver – Morsi ne reviendra pas – Morsi kommt nicht zurück...
Iran: Hukumu ya Jela ya Mwanablogu Yapunguzwa Hadi Miaka 17
“Haki kwa Hossein Derakhshan” blogu ilitangaza mnamo Oktoba 16, 2013 kwamba mamlaka ya Iran imepunguza kifungo cha jela cha mwanablogu wa Iran Hossein Derakhshan (pia anajulikana kama “Hoder”) hadi miaka 17 kutoka miaka 19.5 Derakhshan alikamatwa mnamo Novemba 1, 2008.
Wimbo wa Mahadhi ya Kufoka Upendwao na Vijana nchini Tunisia
Ukiwa umetazamwa zaidi ya mara milioni 3 kwenye mtandao wa YouTube, wimbo wa Houmani umegeuka kuwa wimbo wa taifa kwa vijana wa Tunisia. Afef Abrougui anaeleza kwa nini,
Misri katika Harakati za Kujitafutia Makazi
Ni wapi mtu hujisikia kuwa yupo nyumbani? mwanablogu wa Misri Tarek Shalaby atoa maoni yake: Baadhi ya watu wanasema kuwa nyumbani ni pale palipo na kitanda chake, wengine wanadai kuwa nyumbani ni pale unapoweza kupata mtandao huru wa intaneti. naweza kusema kuwa nyumbani ni pale ambapo mishahara yako imehamishiwa.
“Acheni Unyanyasaji wa ‘Wanachama wa Familia’ za Waandishi wa Habari wa Iran”
Kundi la raia wa mtandaoni wa Iran na wanaharakati waliandika barua ya wazi kwa rais wa Iran Hassan Rouhani na kumtaka kutumia mamlaka yake ya kukomesha unyanyasaji‘wanachama wa familia’ wa waandishi wa habari wa Iran. Zaidi ya watu 100, kutoka ndani na nje ya Iran, walitia saini barua hii ya...
Misri: Sabuni ya Ubikira?
Mwanaharakati wa Kimsiri Nelly Ali anashangaa: Wakati #Misri iko bize…Upuuzi kama huu uko kwenye makabati yetu ukiharibu maisha yetu "Sabuni ya Ubikira"#wanawake/a> pic.twitter.com/IXplFn2kY7 — Nelly Ali (@nellyali) November 1, 2013 Wakati #Misri iko bize…Upuuzi kama huu uko kwenye makabati yetu ukiharibu maisha yetu Sabuni ya Ubikira Akimjibu, anamwambia: @nellyali imekuwa...