· Februari, 2010

Habari kuhusu Mashariki ya Kati na Afrika Kaskazini kutoka Februari, 2010

Lebanon: wanablogu washinikiza jarida la Daily Star kubadilika

  27 Februari 2010

Wanablogu wa Lebanon wanapiga kampeni ya kwenye mtandao ili kulishinikiza gazeti pekee la kwenye wavuti kurekebisha tovuti yake. Mwanablogu mmoja amefanya jitihada kubuni tovuti ya kuiga - ambayo wenzake wanatumaini itahimiza mabadiliko katika gazeti la Daily Star, na kuibadili 'boti moshi ya Kirusi ya miaka ya 1920' kuwa meli ya karne ya 21 ya abiria.

Syria: Matembezi Kwenye Uwanja wa Blogu

  14 Februari 2010

Juma hili, bila utaratibu maalum, Yazan Badran anafanya matembezi kwenye blogu mbalimbali, na mada anuai katika mchanganyiko wa tofauti kidogo na masoko holela ya Aleppo.

Misri: Sisi Ni Washindi

  14 Februari 2010

Timu ya kandanda ya Misri iliifunga Ghana katika fainali ya Kombe la Mataifa ya Afrika, na ikapata ushindi wake kwa mara ya tatu mfululizo. Huu pia ni ushindi wa saba tangu kuanzishwa kwa mashindano hayo kwenye miaka ya hamsini. Wanablogu wanaungana na wananchi wa nchi hiyo kusherehekea mafanikio hayo.