Habari kuhusu Mashariki ya Kati na Afrika Kaskazini kutoka Februari, 2010
Lebanon: wanablogu washinikiza jarida la Daily Star kubadilika
Wanablogu wa Lebanon wanapiga kampeni ya kwenye mtandao ili kulishinikiza gazeti pekee la kwenye wavuti kurekebisha tovuti yake. Mwanablogu mmoja amefanya jitihada kubuni tovuti ya kuiga - ambayo wenzake wanatumaini itahimiza mabadiliko katika gazeti la Daily Star, na kuibadili 'boti moshi ya Kirusi ya miaka ya 1920' kuwa meli ya karne ya 21 ya abiria.
Ethiopia: Wanablogu walitetea Shirika la Ndege la Ethiopia baada ya ajali ya ndege
Wanablogu waishio Ethiopia wameharakia kuitetea rekodi ya usalama wa safari za ndege za nchi hiyo siku ya Jumatatu baada ya ndege moja kuanguka karibu na Beirut, ikihofiwa kupoteza maisha ya watu wote 90 waliokuwepo.
Misri: Mwanablogu apoteza kazi kwa kufichua ukweli kuhusu habari ya bikra za bandia
Mwanablogu ambaye pia ni mwanahabari wa Kimisri Amira Al Tahawi amefukuzwa kazi kwa kufichua ukweli kuhusu habari ya uongo juu ya bikra za bandia zinazotengenezwa China katika makala alioyoichapa kwenye yake, ndivyo wanavyodai wanablogu. Yafuatayo ni baadhi ya maoni kutoka kwenye ulimwengu wa blogu za Kimisri kuhusu kisa hicho.
China: Yatishiwa na Zuio la Mtandao Lililofanywa na Marekani
Maoni kutoka kwa watengeneza programu wa Kichina kuhusu uamuzi wa SourceForge.net wa kufuata sheria za Marekani na kuzuia watumiaji kutoka nchi kadhaa yanajumisha mapendekezo ya jinsi ya kuuzunguka uamuzi huo wa marekani kwenye wavuti wa dunia.
Syria: Matembezi Kwenye Uwanja wa Blogu
Juma hili, bila utaratibu maalum, Yazan Badran anafanya matembezi kwenye blogu mbalimbali, na mada anuai katika mchanganyiko wa tofauti kidogo na masoko holela ya Aleppo.
Misri: Sisi Ni Washindi
Timu ya kandanda ya Misri iliifunga Ghana katika fainali ya Kombe la Mataifa ya Afrika, na ikapata ushindi wake kwa mara ya tatu mfululizo. Huu pia ni ushindi wa saba tangu kuanzishwa kwa mashindano hayo kwenye miaka ya hamsini. Wanablogu wanaungana na wananchi wa nchi hiyo kusherehekea mafanikio hayo.