GlobalVoices katika

Middle East & North Africa

Kumbukumbu za sehemu · 143 jumbe


Habari mpya Kuhusu Middle East & North Africa

16 Aprili 2013

Uturuki: Polisi Watumia Mabomu ya Machozi Kuwatawanya AkinaMama Waandamanaji

Soma makala hii.

Wafungwa wa kisiasa wa Kikurdi wamefikia siku yao ya 55 ya mgomo wa kula. Kuna mamia ya wafungwa wa kisiasa walio kwenye mgomo wa kula nchini Uturuki, na hii imesababisha maandamano mshikamano katika bara la Ulaya, na hususani ndani ya Uturuki. Mapema jana [4 Novemba 2012], wanawake ambao ni mama wa baadhi ya wafungwa wa kisiasa walifanya maandamano ya kukaa, na walijikuta wakipambana na mabomu ya machozi, pamoja na kunyunyuziwa maji ya kuwasha. Wa- Kurdi duniani kote wanapinga kimya kinachotumika kushughulikia adha yao.

2 Machi 2013

Wa-Mauritania Wapinga Udhalilishaji wa Viwanja vya Tahrir Square

صورة من الوقفة نشرها حساب موريتانيا اليوم على فيسبوك

Mwandamanaji akisema “Tunapinga Udhalilishaji” picha ya Jarida la “Mauritania Today” kwenye mtandao wa Facebook.


Siku ya Jumanne Februari 12, 2013, kikundi cha wanaharakati wa ki-Mauritania kiliandaa [ar] maandamano mbele ya Ubalozi wa Misri jijini Nouakchott, mji mkuu wa Mauritania, kupinga udhalilishaji wa kijinsia na ubakaji ambao wanawake wa ki-Misri wamekuwa wakikumbana nao kwenye viwanja vya Tahrir jijini Cairo.

Tukio hilo la maandamano liliratibiwa na “Etkelmi” (Sema kwa kiarabu) [ar - fr], Asasi Isiyo ya Kiserikali inayopambana na ubakaji nchini Mauritania. Mekfoula Brahim anawapa heshima wale wote walioshiriki maandamano hayo [ar]:

شكرا لكم يا مواطنو ا العالم على وقفتكم امام السفارة المصرية فى انواكشوط لدعم نساء مصر اللائى يمارسن حقهن فى التظاهر السلمى فى مصر وعلينا جميعا القيام بوقفة اخرى احتجاجا على دعم الارهاب علنا من طرف الكثيرين والتأصيل له فى ثقافتنا المنفتحة

Asante sana wananchi wote duniani kote kwa kuandamana mbele ya Ubalozi wa Misri jijini Nouakchott kuwaunga mkono wanawake wa Misri wanaotumia haki yao ya kuandamana kwa amani nchini Misri. Tuanze kuandaa mandamano mengine kuwapinga wale (wengi) wanaounga mkono ugaidi na wale wanaojaribu kuuchukua utamaduni wentu wa uwazi.

28 Januari 2013

Mauritania:Ghadhabu Dhidi ya Kauli ya Balozi wa Marekani

Picha ya maandamano dhidi ya Ubalozi wa Marekani mjini Nouakchott – Iliwekwa kwenye ukurasa wa Facebook ya Vijana wa Kukusanya Nguvu ya Kidemokrasia

zaidi »

23 Januari 2013

Mwandishi wa Kike wa Yemeni Asumbuliwa kwa “Kutokuheshimu Dini”

Samia Al-Agbhari

Samia Al-Agbhari..mwandishi wa Yemeni anakabiliwa na mashambulizi ya kipropaganda. Picha iliwekwa kwenye mtandao wa Facebook na Afra Nasser

zaidi »

1 Januari 2013

Photos jumbe
Hakuna Usalama kwa Waandishi wa Kiraia Nchini Bahrain

Soma makala hii.

Baada ya video ya "kibao" cha polisi wa Bahrain kusambaa sana mtandaoni, Waziri wa Mambo ya Ndani alitoa tamko akiomba kuwa yeyote aliyepiga picha tukio hilo aliripoti haraka kwa mamlaka zinazohusika. Siku mbili baadae, na kinyume na kauli hiyo, watu wengi walishangazwa na kukamatwa kwa mpiga picha.

31 Disemba 2012

Video jumbe
Habari za Upotoshaji Kuhusu Afrika Katika Vyombo vya Habari vya Kimataifa

Soma makala hii.

 Kampeni ya kumkamata #Kony2012 ilibeba mambo yaliyorahisishwa mno kuhusu Afrika. Vyombo vya habari vya Afrika vyenyewe, hata hivyo, kwa sasa havina kinga dhidi ya ukosoaji wa aina hii. Hapa ni muhtasari wa watu maarufu, makosa na kutokuwepo umakini katika habari zinazopewa nafasi katika vyombo vya habari vya dunia kuhusu Afrika na katika vyombo vya habari vya Afrika vyenyewe

28 Disemba 2012

Assad atumia Ndege ya Kivita Kuwaua Raia Wake

Serikali ya Syria imefanya shambulizi kubwa la angani dhidi ya raia wa nchi hiyo -waliokuwa wamesimama kwenye foleni waisubiri mikate kwenye kiwanda cha kuokea miakte huko Halfaya, Hama. Inakadiriwa kwamba watu waliouawa katika shambulio hilo mjini humo ni kati ya 90 na 300, waasi wakisema kuwa watu hao walikuwa wamejitenga na vikosi vya Assad. Mtandaoni, wanaharakati wanashangazwa inakuwaje dunia inaendelea kutazama tu maisha ya watu wasio na hatia wakiuawa kwa mamia.

27 Disemba 2012

Walimu wa Mauritania Wavunja Ofisi ya Waziri wa Elimu

Soma makala hii.

Kundi la walimu wa sekondari lilivunja na kuingia kwenye ofisi ya Waziri wa Elimu katika maandamano ya kipinga kuhamishwa kiholela kwa walimu wapatao 120 baada ya kushiriki kwao mgomo uliofanyika mwaka jana.

25 Disemba 2012

Photos jumbe Video jumbe
Ni Sikukuu ya Kuzaliwa Kristo (Noeli) Mjini Betlehemu

Soma makala hii.

Ni sikukuu ya kuzaliwa Kristo mjini Betlehemu, katika ukanda wa Magharibi, Palestina, mahali alipozaliwa Yesu Kristo. Ni namna gani nzuri ya kusherehekea tukio hili zaidi ya kuwashirikisha picha na maoni mbalimbali ya watumiaji wa mtandao wa intaneti kuhusiana na tukio hili linalosherehekewa na mabilioni ya watu duniani kote.

27 Novemba 2012

Photos jumbe
Uharibifu Nchini Syria Katika Picha

Soma makala hii.

Wapiga picha wa Syria wanatumia mitandao ya kijamii kuweka taswira ya uharibifu katika maeneo mbalimbali na kwenye mitaa. Pamoja na ufinyu wa vitendea kazi vya utoaji wa habari, habari zinazotoka Syria zinaonesha hali ya kutisha ya uharibifu inayoikabili nchi ya Syria.

Sehemu za Dunia

Nchi

Lugha