Habari kuhusu Venezuela kutoka Februari, 2014
Orodha ya Waliouawa Katika Maandamano ya Venezuela Yapatikana kwa Lugha Tano
Katika blogu ya Panfleto Negro [es], John Manuel Silva na Emiliana Duarte wanafuatilia orodha ya vifo vilivyotokea kufuatia maandamano yanayoendelea nchini Venezuela. Orodha hiyo -ambayo awali ilikuwa kwa lugha ya Kihispania-imetafsiriwa kwenda lugha ya Kiingereza, Kijerumani, Kiitaliano/a> na Kifaransa.
Caribian: Namna Vyombo vya Habari Vinavyoathiri Mitazamo
Venezuela na Haiti zimekuwa zikikabiliwa na maandamano ya kupinga serikali. Hata hivyo, ukuzaji wa mgogoro wa Venezuela unaofanywa na vyombo vya habari vya kimataifa na ukimya wake kwa mgogoro wa Haiti, unaibua maswali muhimu kuhusu kuyumba kwa Marekani katika kuimaisha tunu ya haki za binadamu na demokrasia. Kevin Edmonds anatoa...
Wavenezuela Waishio Mexico Wawambia Waandamanaji: “Hamko Pekeyenu”
Hali ya mambo nchini Venezuela yaendelea kuzorota, huku pakiwa na maandamano na mikusanyiko nchi nzima ayalisababisha vifo vya watu kumi na mamia kujeruhiwa mpaka sasa. Wavenezuela duniani kote wanaopinga serikali yao wameandaa mikusanyiko ya amani kupaza sauti zao na kuzifanya serikali za nchi wanazoishi kuelewa mwenendo wa mambo. Mexico haija...
Majadiliano ya GV: Maandamano ya Venezuela
Maandamano ya Venezuela yanahusu nini? Vyombo vya habari za kiraia vina wajibu upi? Tunazungumza na mwandishi wa Global Voices Marianne Díaz kuhusu hali ya mambo inavyoendelea nchini humo hivi sasa.
Maandamano ya Venezuela: ‘Vyombo vya Habari vya Kimataifa: Ingilieni Kati!’
Mpendwa Mhariri wa Kimataifa: Sikiliza na uelewe. Hali ya mambo imebadilika nchini Venezuela usiku wa kuamkia leo. Kile kilichokuwa kinaonekana kuwa hali ya kutokuelewana iliyokuwepo kwa miaka sasa imebadilika ghafla. Kile tulichokishuhudia asubuhi hii si habari ya Venezuela uliyodhani unaielewa. Kwenye blogu ya Caracas Chronicles Francisco Toro anashutumu kutokuwepo kwa vyombo...
Kiongozi wa Upinzani Nchini Venezuela Leopoldo López Ajisalimisha Serikalini
Kiongozi wa Upinzani nchini Venezuela Leopoldo López amejisalimisha mwenyewe kwa Vikosi vya Polisi, kama alivyokuwa ametangaza angefanya kwenye video [es] hiyo hapo juu. López, kiongozi wa chama cha Voluntad Popular, alitakiwa kujisalimisha kwa agizo la mahakama jijini Caracas kwa kutuhumiwa kuhusika na makosa ya jinai yanayohusiana na maandamano yanayoendelea nchini...
PICHA: Wavenezuela Waishio Ng'ambo Waungana na Waandamanaji
Wavenezuela wnaoishi nje ya nchi hiyo wameandaa maandamano kuunga mkono maandamano yanayoendelea nchini mwao. Picha zinasambazwa kwenye mitandao ya kijamii kwa alama za #iamyourvoicevenezuela #SOSVenezuela na #PrayForVenezuela, chache kwa kuzitaja.
Mrembo wa Venezuela Auawa kwa Risasi Wakati Akiandamana
Genesis Carmona ameuawa kwa risasi iliyomjeruhi kichwani. Amekuwa mwathirika wa maandamano yanayoendelea nchini Venezuela.
PICHA: Maandamano Yanaendelea Kote Nchini Venezuela
Maandamano yanaendelea katika majiji kadhaa kote nchini Venezuela. Mitandao ya kijamii, hususani twita, imekuwa ikifurika na picha zinazoonyesha yanayoendelea katika kila mkoa.