Habari kuhusu Amerika Kusini kutoka Februari, 2014
Honduras Yazindua Kamusi ya Mtandaoni ya Lugha za Asili
Kamusi ya lugha za asili nchini Honduras ilisambazwa mtandaoni hivi karibuni[es]. Gazeti la Honduras liitwalo Tiempo [es] linaeleza kuwa kamusi hii “imejumuisha maneno yanayofanana katika lugha ya Kihispaniola, chortí, garífuna, isleño, miskito, pech, tawahka na tolupán, lugha ambazo ndizo zinazotengeneza urithi wa lugha wa nchi hiyo.” Kwa mfano, unapotafuta neno...
Orodha ya Waliouawa Katika Maandamano ya Venezuela Yapatikana kwa Lugha Tano
Katika blogu ya Panfleto Negro [es], John Manuel Silva na Emiliana Duarte wanafuatilia orodha ya vifo vilivyotokea kufuatia maandamano yanayoendelea nchini Venezuela. Orodha hiyo -ambayo awali ilikuwa kwa lugha ya Kihispania-imetafsiriwa kwenda lugha ya Kiingereza, Kijerumani, Kiitaliano/a> na Kifaransa.
Caribian: Namna Vyombo vya Habari Vinavyoathiri Mitazamo
Venezuela na Haiti zimekuwa zikikabiliwa na maandamano ya kupinga serikali. Hata hivyo, ukuzaji wa mgogoro wa Venezuela unaofanywa na vyombo vya habari vya kimataifa na ukimya wake kwa mgogoro wa Haiti, unaibua maswali muhimu kuhusu kuyumba kwa Marekani katika kuimaisha tunu ya haki za binadamu na demokrasia. Kevin Edmonds anatoa...
Wavenezuela Waishio Mexico Wawambia Waandamanaji: “Hamko Pekeyenu”
Hali ya mambo nchini Venezuela yaendelea kuzorota, huku pakiwa na maandamano na mikusanyiko nchi nzima ayalisababisha vifo vya watu kumi na mamia kujeruhiwa mpaka sasa. Wavenezuela duniani kote wanaopinga serikali yao wameandaa mikusanyiko ya amani kupaza sauti zao na kuzifanya serikali za nchi wanazoishi kuelewa mwenendo wa mambo. Mexico haija...
Majadiliano ya GV: Maandamano ya Venezuela
Maandamano ya Venezuela yanahusu nini? Vyombo vya habari za kiraia vina wajibu upi? Tunazungumza na mwandishi wa Global Voices Marianne Díaz kuhusu hali ya mambo inavyoendelea nchini humo hivi sasa.
Maandamano ya Venezuela: ‘Vyombo vya Habari vya Kimataifa: Ingilieni Kati!’
Mpendwa Mhariri wa Kimataifa: Sikiliza na uelewe. Hali ya mambo imebadilika nchini Venezuela usiku wa kuamkia leo. Kile kilichokuwa kinaonekana kuwa hali ya kutokuelewana iliyokuwepo kwa miaka sasa imebadilika ghafla. Kile tulichokishuhudia asubuhi hii si habari ya Venezuela uliyodhani unaielewa. Kwenye blogu ya Caracas Chronicles Francisco Toro anashutumu kutokuwepo kwa vyombo...
Kiongozi wa Upinzani Nchini Venezuela Leopoldo López Ajisalimisha Serikalini
Kiongozi wa Upinzani nchini Venezuela Leopoldo López amejisalimisha mwenyewe kwa Vikosi vya Polisi, kama alivyokuwa ametangaza angefanya kwenye video [es] hiyo hapo juu. López, kiongozi wa chama cha Voluntad Popular, alitakiwa kujisalimisha kwa agizo la mahakama jijini Caracas kwa kutuhumiwa kuhusika na makosa ya jinai yanayohusiana na maandamano yanayoendelea nchini...
PICHA: Wavenezuela Waishio Ng'ambo Waungana na Waandamanaji
Wavenezuela wnaoishi nje ya nchi hiyo wameandaa maandamano kuunga mkono maandamano yanayoendelea nchini mwao. Picha zinasambazwa kwenye mitandao ya kijamii kwa alama za #iamyourvoicevenezuela #SOSVenezuela na #PrayForVenezuela, chache kwa kuzitaja.
Mrembo wa Venezuela Auawa kwa Risasi Wakati Akiandamana
Genesis Carmona ameuawa kwa risasi iliyomjeruhi kichwani. Amekuwa mwathirika wa maandamano yanayoendelea nchini Venezuela.
VIDEO: Kuelekea Mfumo wa Haki na Jumuishi Nchini Chile
Katika video hiyo hapo juu iliyowekwa na Mfuko wa Jamii Wazi , Giorgio Jackson, kiongozi wa zamani wa wanafunzi na mbunge mpya kabisa nchini Chile, anajadili mfumo wa elimu nchini mwake na maanaa hasa ya kuwa “jamii wazi”. Trine Petersen anaandika: Mfumo wa haki na jumuishi unaoifanya elimu ipatikane kwa...