· Julai, 2012

Habari kuhusu Amerika Kusini kutoka Julai, 2012

Paraguai: Kutoka Kutumikishwa Hadi Kuwa Kiongozi Mzawa.

Sauti Chipukizi  21 Julai 2012

Kutana na Margarita Mbywangi, ambaye katika umri wa miaka mitano, alichukuliwa kutoka kwa wazazi wake na kuuzwa mara kadhaa na kulazimishwa kufanya kazi za nyumbani. Tangu wakati huo amekuwa kiongozi muhimu wa kabila la Aché na hata kuwa Waziri katika nchi yake. Mbywangi sasa anasimulia maisha yake binafsi kupitia Mradi wa Rising Voices.

Wananchi wa Mexico Wanamchagua Rais Mpya

  12 Julai 2012

Mnamo tarehe 1 Julai, Wa-Mexico walipiga kura kumchagua rais wao mpya. Punde tu kura zilipoanza kupigwa, watumiaji wa mtandao wa intaneti walianza kutoa mawazo na uzoefu wao. Walipanga pia namna tovuti na alama ishara za mtandao wa twita zitakavyotumika kukusanya taarifa juu ya udanganyifu na nyendo zilizo kinyume cha sheria wakati wa uchaguzi huo.

Cuba: Maandamano yafanyika Mara Mbili, Wengi Wakamatwa

  7 Julai 2012

Kikundi cha wanawake kijiitacho ‘wanawake wavaliao mavazi meupe’ (Ladies in White) kwa mara nyingine wametawala fikra za wanablogu wa Cuba waishio nje ya nchi. Maandamano ya amani ya kikundi hicho ambacho ni moja wapo ya vyombo vya upinzani vinavyoheshimika zaidi katika visiwa hivyo –pamoja na kukamatwa kwao mara kwa mara na vyombo vya dola –yanaendelea kuvuta hisia za watu. Mapambano ya hivi karibuni yalitokea mwishoni mwa juma lililopita wakati wanachama wa kikundi hicho walipojaribu kufanya maandamano mara mbili mjini Havana.