· Februari, 2010

Habari kuhusu Amerika Kusini kutoka Februari, 2010

Chile: Tetemeko Kubwa la Ardhi lenye Ukubwa wa 8.8 Laikumba Chile

  28 Februari 2010

Saa 9:34 usiku kwa saa za Chile, tetemeko la ardhi lenye ukubwa wa 8.8 liliukumba mwambao wa eneo la Maule nchini Chile. Tetemeko hilo liliutetemesha mji mkuu wa Santiago uliopo Kilomita 325 kutoka katika kiini cha tetemeko hilo. Uharibifu mkubwa umeripotiwa nchin nzima, na idadi ya waliofariki inazidi kwenda juu.

Haiti: Pesa Zinazotumwa na Ndugu na Jamaa Zasaidia Kabla ya Misaada Rasmi

  3 Februari 2010

Huku simu zikiwa zinaanza kufanya kazi tena nchini Haiti, pesa zinazotumwa na ndugu walio nje ya nchi “kwa waya” zinaanza kuwasili tena, na kusaidia ujenzi hata kule ambako mashirika ya kimataifa bado hayajafika. Pesa zinazotumwa na wanafamilia wanaoishi nje ya nchi, kwa uchache, zilikuwa kama asilimia thelathini ya Mapato ya Taifa ya Haiti kabla ya tetemeko la ardhi la Januari 12.