Habari kuhusu Amerika Kusini kutoka Februari, 2010
Chile: Tetemeko Kubwa la Ardhi lenye Ukubwa wa 8.8 Laikumba Chile
Saa 9:34 usiku kwa saa za Chile, tetemeko la ardhi lenye ukubwa wa 8.8 liliukumba mwambao wa eneo la Maule nchini Chile. Tetemeko hilo liliutetemesha mji mkuu wa Santiago uliopo Kilomita 325 kutoka katika kiini cha tetemeko hilo. Uharibifu mkubwa umeripotiwa nchin nzima, na idadi ya waliofariki inazidi kwenda juu.
China: Yatishiwa na Zuio la Mtandao Lililofanywa na Marekani
Maoni kutoka kwa watengeneza programu wa Kichina kuhusu uamuzi wa SourceForge.net wa kufuata sheria za Marekani na kuzuia watumiaji kutoka nchi kadhaa yanajumisha mapendekezo ya jinsi ya kuuzunguka uamuzi huo wa marekani kwenye wavuti wa dunia.
Costa Rica: Video za Mtandaoni Zaongeza Vichekesho Katika Uchaguzi wa Rais
Uchaguzi wa Rais wa Costa Rica unafanyika Jumapili hii na kwa kupitia video, wananchi wengi wa Costa Rica wanatoa hisia zao kuhusu wagombea na mustakabali wa nchi yao kupitia vichekesho na utani.
Haiti: Pesa Zinazotumwa na Ndugu na Jamaa Zasaidia Kabla ya Misaada Rasmi
Huku simu zikiwa zinaanza kufanya kazi tena nchini Haiti, pesa zinazotumwa na ndugu walio nje ya nchi “kwa waya” zinaanza kuwasili tena, na kusaidia ujenzi hata kule ambako mashirika ya kimataifa bado hayajafika. Pesa zinazotumwa na wanafamilia wanaoishi nje ya nchi, kwa uchache, zilikuwa kama asilimia thelathini ya Mapato ya Taifa ya Haiti kabla ya tetemeko la ardhi la Januari 12.