Repoti ya Unesco inaonesha ‘udhibiti wa hali juu’ wa vyombo vikuu vya habari nchini Singapore huku ikizitambua blogu na tovuti za vyombo vyauanahabari mpya kuwa vinatoa “mazungumzo makini mbadala juu ya masuala muhimu ya kisiasa na jamii kama vile siasa za ndani ya nchi, haki za mashoga na wazee.”
Habari mpya Kuhusu Singapore
4 Mei 2013
Maelfu ya Wafanyakazi Waandamana Barani Asia
Global Voices inayapitia kwa haraka maandamano ya Siku ya Wafanyakazi Mei Mosi kwenye nchi za Cambodia, Filipino, Indonesia na Singapore. Mikutano, ambayo iliandaliwa kudai haki za wafanyakazi na makundi mengine ya utetezi, yalifanyika kwa amani katika bara lote la Asia ya Kusini Mshariki.
27 Oktoba 2012
‘Mazungumzo ya Kitaifa’ Nchini Singapore Yatafanikiwa?
Katika juhudi za kupangilia mustakabali wa Singapore, serikali imezindua “mazungumzo ya kitaifa” yatakayodumu kwa mwaka mmoja ili kukusanya maoni ya watu. Baadhi ya wananchi wameupokea mpango huo kwa mikono miwili lakini pia wapo wengine wanaoupinga wakiuona kama mbinu tu ya kujiweka karibu na wananchi.
16 Januari 2012
Singapore: Maoni ya Waziri Yasababisha Tafrani Mtandaoni
Fahamu kwa nini sentensi hii “Nilipofanya uamuzi…” imezua tafrani mtandaoni nchini Singapore inayotokana na kauli iliyotolewa na waziri mwandamizi wa nchi hiyo. Hiyo ni kufuatia uamuzi wa serikali kupunguza mishahara ya wanasiasa ambao ni kati ya watu wanaolipwa zaidi duniani.
12 Mei 2011
Singapore: Wanablogu Waikosoa Ilani ya PAP
Chama kinachotawala Singapore, People’s Action Party (PAP), kilitoa ilani yake ya uchaguzi tarehe 17 aprili, 2011, ambayo mara moja ilikosolewa na wanablogu wengi kwa “kutokuwa wazi”. PAP tayari kimekuwa madarakani kwa miongo mitano. Uchaguzi mkuu nchini humo umefanyika tarehe 7 Mei.
5 Agosti 2010
Udhibiti Nchini Singapore
Singapore imesababisha kelele kubwa baada ya kupiga marufuku filamu ya aliyewahi kuwa mfungwa wa kisiasa na kumkamata mtunzi Mwingereza wa kitabu kilichoandiaka kuhusu adhabu ya kifo nchini humo. Wanablogu wanajadili.
23 Disemba 2009
Singapore: Kampeni ya “Kataa Ubakaji”
Nchini Singapore, mara nyingi kumbaka mke wako hakuchukuliwi kama tendo la kubaka. Waandaji wa kampeni ya “Kataa Ubakaji” wanataka kukomesha sheria inayokinga ubakaji ndani ya ndoa kwa kuzindua kampeni ya kukusanya saini ambazo zitawasilishwa kwa watunga sera. Wengi wa raia wa mtandaoni wanaiunga mkono kampeni hii.
25 Novemba 2009
Afya Duniani: Siku ya Vyoo Duniani Yatoa Harufu
Ingawa inaweza kusikika kama masihara, Siku ya Vyoo Duniani inatilia maanani kwenye suala ambalo si la mzaha linalowakwaza karibu nusu ya watu wote duniani – ukosefu wa vyoo na mfumo wa usafi.




























Kiungo cha RSS kwa Singapore 






mambo vipi wanablog muko powa wote.kama mumenisoma nijibuni.
Asante. Nimepita hapa natafuta japan na china wamemalizaje ugomvi wao kuhusu visiwa,pia chanzo cha ugomvi...