Habari kuhusu Malaysia
Kupotea kwa Ndege ya MH370: Waziri Mkuu wa Australia Ajichanganya
Waziri Mkuu wa Australia Tony Abbott anazungumza kuhusu zoezi la utafutaji wa ndege ya shirika la ndege la Malaysia MH370.
Nukuu 8 za Kushangaza Zilizopata Kutolewa na Wanasiasa wa Malaysia
Balik Cina ni tovuti mpya ya habari inayokusanya nukuu za kuchekesha na za ajabu zinazotolewa na wanasiasa wa Malaysia.
Waziri Mkuu wa Zamani wa Malayasia Aitaka Boeing Kuwajibika kwa Ajali ya Ndege MH370
Waziri Mkuu wa zamani wa Malaysia Mahathir Mohamad ameitaka Boeing kuwajibika kufuatia tukio la kupotea kwa ndege ya Shirika la ndege la Malaysia yenye namba MH370. Hivi ndivyo alivyoandika kwenye blogu yake: Boeing ndiyo imetengeneza ndege hii. Boeing lazima waeleze inakuwaje njia zote za kuifuatilia mwenendo wa ndege hiyo ziweze...
Ndege ya Malaysia Haijulikani Ilipo Ikiwa na Abiria 239
Ndege MH370 kutoka Kuala Lumpur kuelekea Beijing ilipoteza mawasiliano na waongoza ndege, na mamlaka za kiserikali zimeshindwa kujua iliko ndege hiyo iliyokuwa na watu 239
Kuumaliza Umasikini Nchini Malaysia
Kikundi cha Saya Anak Bangsa Malaysia kinashinikiza kupitishwa kwa Sheria ya Ujumuishi wa Kijamii ili kutatua tatizo la umasikini nchini Malaysia: Maelekezo yatokayo juu kuja chini yanaonekana kutokufanya kazi pamoja na madai tofauti ya serikali. Ili misaada ifanye kazi kweli, basi iende kupunguza ‘maumivu binafsi ya mfukoni’ kwa sababu kila...
Ufuatiliaji wa Upendeleo Kwenye Vyombo vya Habari Nchini Malaysia
Tessa Houghton anashiriki matokeo ya utafiti ambao ulifuatilia upendeleo katika vyombo vya habari nchini Malaysia wakati wa Uchaguzi Mkuu wa 13 miezi michache iliyopita: Wananchi wa Malaysia ambao walitegemea Kiingereza na Bahasa magazeti ya Malaysia na/au televisheni kama chanzo cha vyombo vyao vya habari wakati wa kampeni ya GE13 hawakutolewa...
Vumbi la Uchafuzi wa Mazingira Larudi Nchini Indonesia
Vumbi linalosababishwa na uchafuzi wa mazingira ni tatizo la mara kwa mara katika eneo hilo linalosababishwa zaidi na matukio ya moto wa msituni nchini Indonesia.
Hali ya Uislamu Katika Asia ya Kusini
Murray Hunter wa Chuo Kikuu cha Malaysia Perlis anajadili hali ya jamii ya Kiislamu katika Asia ya Kusini pamoja na masuala yanayohusiana na kukua kwa Uislamu katika eneo hilo. Umaskini, kujua kusoma na kuandika, elimu, kuhamishwa, ukabaila, ukosefu wa ajira, ukandamizaji, na udhibiti ni mambo yanayowaonea Waislamu ndani ya ASEAN. Serikali pamoja na...
Kufilisika kwa Watu nchini Malaysia
iMoney.my wametengeneza mchoro unaoelezea takwimu za kufilisika nchini Malaysia. Wastani wa matukio 20,000 ya kufilisika yamerekodiwa mwaka 2012 hiyo na maana kwamba wa-Malaysia 53 wanafilisika kila siku.
Raia wa Myanmar Wachukizwa na Mashambulizi Dhidi ya Wahamiaji Wenzao Nchini Malasia.
Vurugu za kikabila nchini Mynmar inaonekana kusambaa hata katika nchi za jirani.. Baadhi ya wahamiaji wa Mynmar wa jamii ya budha wanaoishi nchini Malasia wiki chache zilizopita ambapo watu wengi wanaamini kuwa mashambulia hayo yanahusiana mvutano wa kimakabila na kidini unaoendelea nchini Myanmar. Mwitikio wa awali wa serikali ya Myanmar wa kukanusha matukio haya uliwakasirisha watumiaji wengi wa mtandao.