Habari kuhusu Asia Mashariki kutoka Oktoba, 2013
Vyuo Vikuu Vingi Mno Nchini Singapore?
Limpeh anabaini ongezeko kubwa la taasisi za eleimu ya juu nchini Singapore. Je, hizo ni habari njema au mbaya kwa nchi ya Singapore? …kupanuka huku [kwa elimu ya juu] kumekuwa na matokeo mabaya kwa soko? Kwa hiyo wakati kupanuka huku kunaweza kuwa kumeongeza ajira kwa baadhi ya baadhi ya watu...
Wali Unaonata Haufai kwa Watoto, Akina Mama Waambiwa
@LaotianMama anawakumbusha akina mama wa Lao kutokuwalisha watoto wenye njaa wali unaonata ambao ni chakula cha asili kwao. Wali unaonata kwa watoto wachanga ni sawa na punje za wali katika utamaduni wa ki-Magharibi. Wazo ni lile lile kuwa kuwapa watoto wachanga chakula kigumu kutawashibisha. Kwa hiyo, kuwaanzishia watoto wachanga chakula...
Masuala Matano ambayo Raia wa Brunei Wanahitaji Kuyajadili
Teah Abdullah anaorodhesha masuala matano ambayo raia wa Brunei citizens wanahitaji kuyajadili: Kuimarisha lugha halisi, ngono baina ya ndugu wa damu, maisha ya anasa, ulaji unaozidi kiwango wa “baga” [aina ya mandazi yenye nyama], utegemezi uliopitiliza kwa serikali. Anafafanua kwenye suala la mwisho: …serikali ni sehemu muhimu katika maisha yetu...
Hong Kong: Video Inayosambazwa Mtandoni Yamwonyesha Jamaa Akipigwa Makofi Mara 14 na Rafiki Yake wa Kike
Kama inavyoelezwa na Tom Grundy, mpita njia aliwaita polisi na mwanamke huyo aliwekwa chini ya ulinzi kwa kumpiga vibao rafiki yake wa kiume aliyekuwa amepiga magoti mbele yake akimwomba msamaha kwa kumleta mwanamke mwingine nyumbani.
Hong Kong: Pinga Biashara ya Pembe za Ndovu
Muungano wa watu binafsi na Asasi Zisizo za Serikali zinazoguswa na tatizo la ujangili wa tembo, Hong Kong kwa Tembo, uliandamana Oktoba 4, wakiitaka Hong Kong kuteketeza hifadhi yake ya tani 25 za pembe za ndovu.
PICHA: Maisha Nchini Myanmar
Mpiga picha Geoffrey Hiller ameweka kumbukumbu ya maisha yake nchini Myanmar kuanzia mwaka 1987 mpaka kipindi cha kihistoria kutokea nchini humo
Korea Kusini: Mwandishi Msafiri, Utamaduni Tofauti, na Jamii ya Wageni
John Bocskay, mwanablogu asiyeandika mara nyingi sana alifanya mahojiano na mwandishi wa utalii Rolf Potts aliyetumia miaka kadhaa kwenye jiji la pili kwa ukubwa nchini Korea Kusini, Pusan, anasema: Kila mtu niliyeonana naye katika vilabu vya wageni alidai kuwa mwandishi au msanii, lakini hungeweza kuona maandishi mengi au sanaa. Ilikuwa...
China: Miitikio ya Raia wa Mtandaoni Kufuatia Muswada wa Sheria ya Kurithi Kodi
Watumiaji wa mtandao nchini China walionyesha kutokuridhishwa kwao na muswada wa sheria unaopendekeza uwezekano wa kurithiwa kodi zinazoanzia yuan RMB 800,000 [yuan ni sarafu ya nchi hiyo]. Badala ya kuziba pengo la kipato miongoni mwa wananchi, watumiaji wa mtandao wanaamini kuwa sheria mpya inakusudia kuiba fedha kutoka kada ya wafanyakzi....