· Oktoba, 2012

Habari kuhusu Asia Mashariki kutoka Oktoba, 2012

‘Mazungumzo ya Kitaifa’ Nchini Singapore Yatafanikiwa?

  27 Oktoba 2012

Katika juhudi za kupangilia mustakabali wa Singapore, serikali imezindua “mazungumzo ya kitaifa” yatakayodumu kwa mwaka mmoja ili kukusanya maoni ya watu. Baadhi ya wananchi wameupokea mpango huo kwa mikono miwili lakini pia wapo wengine wanaoupinga wakiuona kama mbinu tu ya kujiweka karibu na wananchi.

Kambodia Yaomboleza Kifo cha Mfalme Norodom Sihanouk

  27 Oktoba 2012

Nchi ya Kambodia inaomboleza kifo cha baba Mfalme Norodom Sihanouk aliyefariki tarehe15 Ockoba, 2012. Mamilio ya watu walisubiri pembezoni mwa barabara itokayo uwanja wa ndege kwenye kwenye makazi ya kifalme kutoa heshima zao za mwisho kwa Mfalme.

China: Hatua za Kubana Uhuru wa Habari Majimboni

  15 Oktoba 2012

Jing Gao kutoka blogu ya Tofu anaeleza namna serikali ya Fuji ilivyo na mikakati michafu dhidi ya Yunnan na jinsi inavyochukua hatua za kuzuia uchapishaji wa habari zinazoweka wazi kashfa za ufisadi zinazomkabili afisa mmoja wa serikali.