<?xml version="1.0" encoding="UTF-8"?>
<rss version="2.0"
	xmlns:content="http://purl.org/rss/1.0/modules/content/"
	xmlns:wfw="http://wellformedweb.org/CommentAPI/"
	xmlns:dc="http://purl.org/dc/elements/1.1/"
	xmlns:atom="http://www.w3.org/2005/Atom"
	xmlns:sy="http://purl.org/rss/1.0/modules/syndication/"
	xmlns:slash="http://purl.org/rss/1.0/modules/slash/"
	>

<channel>
	<title>Global Voices in Swahili &#187; U.S.A.</title>
	<atom:link href="http://sw.globalvoicesonline.org/category/world/americas/usa/feed/" rel="self" type="application/rss+xml" />
	<link>http://sw.globalvoicesonline.org</link>
	<description>Dunia inaongea, je unasikiliza?</description>
	<lastBuildDate>Wed, 02 Dec 2009 12:35:07 +0000</lastBuildDate>
	<generator>http://wordpress.org/?v=2.8.4</generator>
	<language>en</language>
	<sy:updatePeriod>hourly</sy:updatePeriod>
	<sy:updateFrequency>1</sy:updateFrequency>
			<item>
		<title>Afrika Kusini: Kikaragosi Kiliochoathirika na VVU Kwenye Kipindi cha Sesame Chaelimisha Kuhusu Ukimwi</title>
		<link>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/11/afrika-kusini-kikaragosi-kiliochoathirika-na-vvu-kwenye-kipindi-cha-sesame-chaelimisha-kuhusu-ukimwi/</link>
		<comments>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/11/afrika-kusini-kikaragosi-kiliochoathirika-na-vvu-kwenye-kipindi-cha-sesame-chaelimisha-kuhusu-ukimwi/#comments</comments>
		<pubDate>Mon, 23 Nov 2009 10:38:13 +0000</pubDate>
		<dc:creator>Christian Bwaya</dc:creator>
				<category><![CDATA[Arts & Culture]]></category>
		<category><![CDATA[Children]]></category>
		<category><![CDATA[Education]]></category>
		<category><![CDATA[English]]></category>
		<category><![CDATA[Feature]]></category>
		<category><![CDATA[General]]></category>
		<category><![CDATA[Health]]></category>
		<category><![CDATA[South Africa]]></category>
		<category><![CDATA[U.S.A.]]></category>
		<category><![CDATA[Weblog]]></category>
		<category><![CDATA[Youth]]></category>

		<guid isPermaLink="false">http://sw.globalvoicesonline.org/?p=696</guid>
		<description><![CDATA[Wakati kipindi cha watoto cha Mtaa wa Sesame (Sesame Street) kikisherehekea maadhimisho ya miaka 40 mwezi huu, kwa kizindua msimu wake  mpya leo, kikaragosi kizuri kinachovutia cha Muppet katika toleo la Afrika Kusini kinaendelea kusaidia kupambana na kuelimisha kuhusu VVU/UKIMWI. ]]></description>
			<content:encoded><![CDATA[<em>Ilichapwa kwanza na<a href="http://globalvoicesonline.org/author/juhie-bhatia/">Juhie Bhatia</a>  &middot; Imetafsiriwa na <a href='http://sw.globalvoicesonline.org/author/bwaya/'>Christian Bwaya</a> &middot;  <a href='http://globalvoicesonline.org/2009/11/11/south-africa-sesame-streets-hiv-positive-muppet-raises-awareness/'>Angalia ujumbe mama</a></em> 
<br /><p><img alt="" src="http://globalvoicesonline.org/wp-content/uploads/2009/11/Kami22.jpg" title="Kami" class="alignright" width="200" height="260" /><br />
Wakati kipindi cha watoto cha <a href="http://www.sesamestreet.org/home/">Mtaa wa Sesame</a> (Sesame Street) kikisherehekea maadhimisho ya miaka 40 mwezi huu, kwa kizindua msimu wake  mpya leo, kikaragosi kizuri kinachovutia cha Muppet katika toleo la Afrika Kusini kinaendelea kusaidia kupambana na kuelimisha kuhusu VVU/UKIMWI. </p>
<p>Wakati kipindi cha Sesame Street kinatazamwa katika zaidi ya <a href="http://www.sesameworkshop.org/newsandevents/sesameupdates/sesame_40thbirthday">nchi 140</a>, kila toleo huzungumzia masuala yanayotokea kwenye jamii husika na kwa kumtumia vikaragosi tofauti. <a href="http://muppet.wikia.com/wiki/Kami">Kami</a> mwenye rangi ya Njano-dhahabu alionekana kwa mara ya kwanza kwenye kipindi mwenza cha Sisame Street cha Afrika Kusini kinachoitwa <a href="http://www.schooltv.co.za/TakHome.htm">Takalani Sesame</a>, mwaka 2002 kujibu matatizo ya nchi yanayohusiana na UKIMWI. Kama kikaragosi cha kwanza duniani chenye VVU, kinasaidia kuwaelimisha watoto kuhusu ugonjwa na kushughulikia masuala yanayohusiana na kuwa mwathirika wa UKIMWI. Jina la Kami <a href="http://www.sesameworkshop.org/aroundtheworld/southafrica">linatoka</a> kwenye neno la kiSetswana “Kamogelo”, lenye maana ya “kukubalika.” Sunshinestar110, anayeblogu kwenye <em>U dont Like My Opinion&#8230;That’s Fine!</em> <a href="http://thatsfine2009.blogspot.com/2009/11/happy-birthday-to-you.html">anazungumzia zaidi</a> kuhusu Kami:</p>
<blockquote><p>“Kami ni mwathirika wa VVU mwenye afya, yatima wa miaka mitano mwenye bashasha ambaye ana aibu kidogo lakini huchangamka akijongelewa kwa njia ya kirafiki, pia anajua mengi kuhusu Virusi vya UKIMWI, alimpoteza mama yake kwa ugonjwa huo. Kami alipozinduliwa, akiwa na nywele zake za kahawia na pia alivaa fulana, na kutembea kwenye mtaa wa Susame na kujiuliza huku akihofu kama wenyeji watataka kucheza nae. Hakuwa na haja ya kuogopa kwa sababu vikaragosi vingine vilimpokea kwa bashasha”</p></blockquote>
<p>Kami aliletwa kuwasaidia watoto wengi wa Afrika Kusini wanaotaabika na janga la VVU/UKIMWI. Inaaminika kuwa Afrika Kusini ina idadi kubwa zaidi ya watu walio na VVU duniani – inakadiriwa kuwa watu <a href="http://www.unaids.org/en/CountryResponses/Countries/south_africa.asp">milioni 5.7</a> Kwa makadirio, kati ya walioathirikia, 280,000 ni watoto wa umri wa miaka chini ya 14 na kuna yatima milioni 1.4 nchini kutokana na UKIMWI. Zaidi ya madhara ya kimwili ya kuwa na VVU, vilevile kuna unyanyapaa na miiko inayotokana na kuwa na ugonjwa, ambayo husababisha ugumu kwa watu kupata matibabu stahiki na msaada. Takalani Sesame, ambayo inajumuisha lugha zote rasmi 11 za Afrika Kusini, inajaribu kuwasaidia watoto kuyatazama masuala haya kwa ujasiri kupitia Kami.</p>
<p>Hata hivyo, kulikuwa na mkanganyiko wakati Kami alipoanza kuonyeshwa, hasa hasa nchini Marekani, ambapo wengi walikasirishwa na kuwa kipindi cha watoto kinanamchezesha mhusika mwenye VVU. <em>Haven on Earth</em> <a href="http://haven-on-earth.spaces.live.com/blog/cns!C13DE188EF218F14!382.entry?sa=500695506">anafafanua</a> mjadala huo:</p>
<blockquote><p>“Ingawa ilitaarifiwa kuwa ujio wa Kami kwenye kipindi cha Sesame Street nchini Afrika Kusini ulikuwa unakaribishwa.(Nina wakati mgumu kukubaliana na ukweli huu kwa sababu kiwango kikubwa cha kukataa bado kipo), kulikuwa na mkanganyiko ulio wazi hapa Marekani. Ninakumbuka kusoma kuhusu suala hili (hii ni sababu ya mimi kufurahia kukutana na kipindi kikirushwa kutokea Afrika Kusini – nisingelifikiria kukitafuta). Iliondokea kuwa kundi la wabunge wa Congress wa chama cha Republican walituma barua kwa Rais wa Shirika la Utangazaji la Umma (PBS) linalorusha kipindi cha Sesame Street. Barua ilidai kwamba mipango ya kuleta mhusika kama huyo ambaye ni mwathirika wa UKIMWI nchini Marekani haikuwa sahihi, kwa kuzingatia umri wa watazamaji. Walipendekeza kwamba hatua hiyo ingeathiri ufadhili wa umma kwa Shirika hilo (PBS).”</p></blockquote>
<p>Kami hajawahi kuonekana kwenye kipindi cha Sesame Stree cha Marekani, ingawa amedhihirisha kuwa mhusika aliyefanikiwa sana kwenye kipindi cha Takalani Sesame na zaidi. Mwaka 2003, UNICEF <a href="http://www.unicef.org/media/media_16631.html">ilimteua</a> kuwa “Shujaa wa Watoto” duniani. Katika <a href="http://www.youtube.com/watch?v=9eXlNn-C8BY">video</a> hii, anaungana na Rais wa zamani wa Marekani Bill Clinton kutoa ujumbe kuhusu VVU/UKIMWI. Jamie, anayeblogu kwenye <em>No day but Today</em>&#8230;, <a href="http://phaino.blogspot.com/2006/12/world-according-to-sesame-street.html">anajadili</a> mafanikio mengine ya Kami:</p>
<blockquote><p> “Kwa sababu watoto wengi wa Afrika Kusini wanamfahamu mtu fulani mwenye UKIMWI, mhusika huyo amekuwa shujaa wa taifa, anayependwa na watu wa nchi hiyo. Kami ameonekana kwenye Umoja wa Mataifa na Benki ya Dunia na alihojiwa na Katie Couric. Ameteuliwa kuwa balozi wa UNICEF wa watoto na ameonekana kwenye vipande vya onyesho la Takalami pembeni mwa Desmond Tutu na Nelson Mandela.”</p></blockquote>
<p>Pamoja na mafanikio ya Kami, wanablogu wengine bado wanaamini kuwa si mhusika sahihi kwa toleo la Kimarekani la Sesame Street. Emily Meyer, anayeblogu kwa ajili ya darasa lake la heshima, <a href="http://hons101fall09eem.blogspot.com/2009/10/kami-hiv-muppet.html">anasema</a>:</p>
<blockquote><p>“Ingawa ni muhimu kwa Wamerekani kufahamu kuhusu VVU/UKIMWI na hatari ya ugonjwa wenyewe, nadhani kuwafundisha watoto katika umri wa miaka miwili na mitatu ni kwenda mbali sana. Watoto wadogo kiasi hiki hawataweza kuelewa kuhusu VVU na hawataelewa madhara yake. Kama Kami alitakiwa aletwe Marekani kama njia kueneza elimu na kudhibiti UKIMWI, sidhani kama matokeo yaliyokusudiwa yangetokea&#8230;Watoto nchini Marekani hawalazimishwi kuhusika na masuala ya UKIMWI katika umri huo mdogo. Nadhani wakati sahihi kwa watoto nchini Marekani kujifunza kuhusu hatari ya virusi vya UKIMWI ni wanapokuwa wakubwa, kadri ya miaka kumi ama kumi na moja au wakati mwanafunzi anapoanza kujihusisha na vitendo vya mapenzi kimwili”</p></blockquote>
<p>Bado, wanablogu wengi, kama huyu hapa <a href="http://beckyluz.wordpress.com/2008/12/16/kami-the-hiv-positive-muppet/">anayeandika kwenye</a> <em>Muppets and History</em>, anamwona Kami kama mfano mwingine wa namna Sesame Street inavyosukuma mipaka. Wengine <a href="http://joburgjoblog.blogspot.com/2006/03/celebrating-aids-research.html">wanaonyesha upendo</a> wao kwa kikaragosi huyo na ujumbe anaowaletea watoto. Na wengine wanadhani anatakiwa atumike kwenye matoleo mengine ya Sesame Street. Katika blogu yake binafsi, Steisha Pintado <a href="http://steishapintado.wordpress.com/2008/12/18/final-grades-kami/">anasema</a>:</p>
<blockquote><p>“Anawaonyesha watoto kwamba ni sawa kumkumbatia mtu mwenye virusi vya UKIMWI, na anaeleza nini cha kufanya anapokuwa na kidonda kwenye kidole chake au kama umejikata mwenyewe. Anaifundisha hadhira ya watoto wadogo kuhusu kukabiliana na kuumwa na kupotelewa&#8230;.Ingawa ngono huwa haitajwi kamwe katika kuzungumzia hali ya Kami, watu wengine wamesema kuwa kuwepo kwa mhusika mwenye virusi vya UKIMWI lisingekuwa jambo sahihi kwa hadhira ya watazamaji wadogo. Mbunge mmoja hata alidai kuwa Warsha ya Sesame ingepoteza msaada wa kifedha kutoka serikalini kama ingerusha kipindi chenye mhusika huyo kwenye nchi yetu. Inashangaza kusikia maneno haya. Wazazi wanatumia muda mfupi (na unaopungua kila siku) na watoto wao, na wanaruhusu runinga kuwaelimisha zaidi na zaidi. Ni wazi wazazi wengi hawawafundishi watoto wao namna ya kuyakabili masuala nyeti  ya uelewa na kukubalika. Wazazi tayari wamewaruhusu Warsha ya Sesame kuingiza suala la kukubalika kwa wale wenye ulemavu na kuugua, na pia kwa wale wenye rangi na dini tofauti. Je, hii ina tofauti gani? </p></blockquote>
]]></content:encoded>
			<wfw:commentRss>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/11/afrika-kusini-kikaragosi-kiliochoathirika-na-vvu-kwenye-kipindi-cha-sesame-chaelimisha-kuhusu-ukimwi/feed/</wfw:commentRss>
		<slash:comments>0</slash:comments>
		</item>
		<item>
		<title>China: Obama ni Mshabiki Mkubwa wa Kutokuchuja Habari</title>
		<link>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/11/china-obama-ni-mshabiki-mkubwa-wa-kutokuchuja-habari/</link>
		<comments>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/11/china-obama-ni-mshabiki-mkubwa-wa-kutokuchuja-habari/#comments</comments>
		<pubDate>Tue, 17 Nov 2009 10:06:54 +0000</pubDate>
		<dc:creator>j nambiza tungaraza</dc:creator>
				<category><![CDATA[China]]></category>
		<category><![CDATA[East Asia]]></category>
		<category><![CDATA[English]]></category>
		<category><![CDATA[Freedom of Speech]]></category>
		<category><![CDATA[International Relations]]></category>
		<category><![CDATA[Politics]]></category>
		<category><![CDATA[Roundups]]></category>
		<category><![CDATA[U.S.A.]]></category>

		<guid isPermaLink="false">http://sw.globalvoicesonline.org/?p=690</guid>
		<description><![CDATA[Ilichapwa kwanza naOiwan Lam  &#183; Imetafsiriwa na j nambiza tungaraza &#183;  Angalia ujumbe mama 
Adam Minter amesikitishwa na maoni ya Obama kwenye Mkutano uliofanyika kwenye Ukumbi wa Jiji la Shanghai, hasa, maelezo yake kuwa &#8220;Mimi ni muunga mkono mkubwa wa kutokuchuja habari&#8220;.
]]></description>
			<content:encoded><![CDATA[<em>Ilichapwa kwanza na<a href="http://globalvoicesonline.org/author/oiwan/">Oiwan Lam</a>  &middot; Imetafsiriwa na <a href='http://sw.globalvoicesonline.org/author/j-nambiza-tungaraza/'>j nambiza tungaraza</a> &middot;  <a href='http://globalvoicesonline.org/2009/11/17/china-obama-as-a-big-supporter-of-non-censorship/'>Angalia ujumbe mama</a></em> 
<br /><p>Adam Minter amesikitishwa na maoni ya Obama kwenye Mkutano uliofanyika kwenye Ukumbi wa Jiji la Shanghai, hasa, maelezo yake kuwa &#8220;<a href="http://shanghaiscrap.com/?p=3920">Mimi ni muunga mkono mkubwa wa kutokuchuja habari</a>&#8220;.</p>
]]></content:encoded>
			<wfw:commentRss>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/11/china-obama-ni-mshabiki-mkubwa-wa-kutokuchuja-habari/feed/</wfw:commentRss>
		<slash:comments>0</slash:comments>
		</item>
		<item>
		<title>Marekani: Mauaji ya Fort Hood Yasababisha Kumulikwa kwa Waislamu Walio Jeshini</title>
		<link>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/11/marekani-mauaji-ya-fort-hood-yasababisha-kumulikwa-kwa-waislamu-walio-jeshini/</link>
		<comments>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/11/marekani-mauaji-ya-fort-hood-yasababisha-kumulikwa-kwa-waislamu-walio-jeshini/#comments</comments>
		<pubDate>Sat, 14 Nov 2009 09:35:25 +0000</pubDate>
		<dc:creator>Deogratias Simba</dc:creator>
				<category><![CDATA[Americas]]></category>
		<category><![CDATA[English]]></category>
		<category><![CDATA[Ethnicity]]></category>
		<category><![CDATA[General]]></category>
		<category><![CDATA[Racism]]></category>
		<category><![CDATA[Religion]]></category>
		<category><![CDATA[U.S.A.]]></category>
		<category><![CDATA[Video]]></category>
		<category><![CDATA[Weblog]]></category>

		<guid isPermaLink="false">http://sw.globalvoicesonline.org/?p=641</guid>
		<description><![CDATA[Shambulizi la upigaji risasi la kushtukiza lililofanywa na mwanajeshi wa Jeshi la Marekani, Meja Nidal Malik Hassan, na kusababisha vifo vya watu 13 na kujeruhi wengine 31 katika kambi ya kijeshi ya Fort Hood, jimbo la Texas, kwa mara nyingine limesababisha Waislamu nchini Marekani kumulikwa - hasa wale wanolitumikia jeshi. ]]></description>
			<content:encoded><![CDATA[<em>Ilichapwa kwanza na<a href="http://globalvoicesonline.org/author/bhumika-ghimire/">Bhumika Ghimire</a>  &middot; Imetafsiriwa na <a href='http://sw.globalvoicesonline.org/author/simbadeo/'>Deogratias Simba</a> &middot;  <a href='http://globalvoicesonline.org/2009/11/12/usa-fort-hood-massacre-puts-spotlight-on-muslims-in-army/'>Angalia ujumbe mama</a></em> 
<br /><p><a href="http://en.wikipedia.org/wiki/Fort_Hood">Shambulizi la upigaji risasi la kushtukiza</a> lililofanywa na mwanajeshi wa Jeshi la Marekani, Meja Nidal Malik Hassan, na kusababisha vifo vya watu 13 na kujeruhi wengine 31 katika kambi ya kijeshi ya Fort Hood, jimbo la Texas, kwa mara nyingine limesababisha Waislamu nchini Marekani kumulikwa - hasa wale wanaolitumikia jeshi. </p>
<p>Kitambo kifupi baada ya Meja Hassan kutangazwa kama mfyatuaji aliyetuhumiwa, kulikuwa na kukosa raha kuliko wazi kabisa miongoni mwa warusha habari na watoa maoni kuhusu usuli wake wa kidini na asili yake.  Iliripotiwa pia kwa wingi kwamba wanajeshi wengine wa Kiislamu mara nyingine walikabiliana na mashambulizi kutoka kwa wanajeshi wenzao.</p>
<p>Howard M. Friedman, Profesa Mwandamizi wa Sheria katika Chuo Kikuu cha Toledo, anasema katika blogu yake ijulikanayo kama <em><a href="http://religionclause.blogspot.com/2009/11/muslim-soldiers-in-us-military-face.html">ReligionClause</a></em>:</p>
<blockquote><p> “Jeshi limekuwa likiandikisha Waislamu walio na ujuzi wa lugha na welewa wa utamaduni, vitu vinavyohitajika ili kupigana vita huko Iraki na Afganistani. Hata hivyo, Waislamu walio jeshini sasa wanatiliwa shaka na baadhi ya maofisa wao.&#8221;</p></blockquote>
<p>Bila kujali mashaka dhidi ya wanajeshi Waislamu yaliyokuwapo kabla ya shambulizi hili, mtu anaweza kuwa na hofu kwamba mashaka hayo yamepata msukumo mpya baada ya mauaji ya watu kule Fort Hood. Maswali bado yanaendelea kuibuliwa endapo Meja Hassan alikuwa mwenye siasa kali na ambaye alifanya mashambulizi hayo kwa msukumo wa itikadi ya kidini au labda tu alikuwa na tatizo la kiakili. </p>
<p>Kule Kanada, mwandishi Gwynne Dyer wa gazeti huru la kila wiki la Vancouver kupitia mtandao wa <em><a href="http://www.straight.com/article-269513/gwynne-dyer-us-media-overlook-obvious-explanation-maj-nidals-mass-murder">Straight.com</a></em>, anabuni kwamba kuelekeza fikra kwenye dini ya muuaji ni kufumbia macho baadhi ya masuala mengine muhimu:</p>
<blockquote><p>“Baada ya siku chache wakati watoa maoni wakisitasita kutoa maelezo yanayoshindana, vyombo vya habari vinaanza kujikita katika maelezo kwamba ilikuwa ni unyanyasaji wa kirangi/kiasili/kidini ndiko kulikomsukuma Nidal kupata ukichaa. Watu wabaya, wanaofanya vitu kinyume na Wamarekani mwisho wa siku ndiyo wenye kuhusika na msiba huo, na kuna mwisho wake. </p>
<p>Maelezo yanayokwepwa ni kwamba vita vya Wamarekani vinavyoendeshwa ng&#39;ambo katika ardhi za Waislamu vinawajenga Waislamu nyumbani kuchukua msimamo mkali. Usijali sana kwamba magaidi wa Kiislamu waliokuzwa nyumbani walioshambulia mfumo wa usafiri jijini Landani mwaka 2005, na wafanya njama wa Kiislamu kadhaa ambao wamekamatwa katika nchi za Magharibi kabla njama zao hazijazaa matunda, wote wamelaumu uvamizi unaofanywa na mataifa ya Magharibi kwenye nchi za Kiislamu kama kitendo kilichowasukuma wao kuwa na msimamo mkali. Zaidi sana, usijali kwamba kile kilichowafanya kuwa na msimamo mkali ni ukweli kwamba uvamizi huo haukuwa na maana kwa masuala ya usalama wa Magharibi.&#8221;</p></blockquote>
<p>Fox News, ambayo mara nyingi hukosolewa kwa kuelemea kwake upande mmoja katika masuala yanayohusiana na uhamiaji na siasa mgando, inasemekana kuitisha wazo la <a href="http://www.salon.com/news/politics/war_room/2009/11/06/fox_friends/index.html">&#8220;uchunguzi kwa Waislamu&#8221; </a>walio jeshini. Katika tovuti ya <em><a href="http://www.veteranstoday.com/modules.php?name=News&#038;file=article&#038;sid=9280">Veterans Today</a></em>, ofisa mstaafu wa Jeshi la Ulinzi wa Pwani ya Marekani, United States Coast Guard, Tom Barnes, anasema chombo hicho cha habari kinachochea mtazamo uleule wa siku zote kwa kujaribu kujenga imani potofu ya &#8220;sisi dhidi ya wao&#8221;:</p>
<blockquote><p>
“… chombo hicho cha habari kinazidi kuwa &#8220;kisichosaidia&#8221;, yaani kwa lugha nyepesi, hasa kama swali hili la msingi linageuka kuwa vita nyingine ya Fox Channel dhidi &#8220;yao&#8221;.  Taarifa kama hizi siyo tu zinazidi kupitwa na wakati bali ni za hatari pia. <a href="http://www.salon.com/news/politics/war_room/2009/11/06/fox_friends/index.html">Hapa</a> ndipo palipo na habari nzima.</p>
<p>Kama nilivyoonyesha hapo kabla, jambo kama hili limewahi kutokea katika Jeshi la Ulinzi la Marekani. Ninazidi kuchoshwa na habari za Fox News zinazoniambia kuwa adui zangu ni akina nani. Kila wakati. Bila kukoma. Sikuwa na habari kwamba &#8220;wao&#8221; wapo wengi!&#8221;</p></blockquote>
<p><a href="http://news.google.com/news/url?sa=t&#038;ct2=us%2F0_0_s_0_0_t&#038;usg=AFQjCNFUhLnrNP-D9fmObNIMr6pSA-X1sg&#038;cid=1465293836&#038;ei=oXL4Spi5FIqGmQfJnPI9&#038;rt=SEARCH&#038;vm=STANDARD&#038;url=http%3A%2F%2Fwww.csmonitor.com%2F2009%2F1108%2Fp02s08-usmi.html">Magazeti mengi</a> hivi sasa yanachunguza ni kwa namna gani vitendo vya Hassan vitawaathiri Waislamu wanaotumikia katika Jeshi la Marekani, na wakazi Waislamu wanaoishi karibu na kambi ya Fort Hood.</p>
<p>Hapa kuna taarifa ya habari ya video ya <em><a href="http://www.youtube.com/watch?v=N8Azg9TxYkM">euroamericannews</a></em> katika YouTube kuhusu maoni ya Waislamu walio Fort Hood kuhusiana na tukio hilo.</p>
<p><object width="425" height="344"><param name="movie" value="http://www.youtube.com/v/N8Azg9TxYkM&#038;color1=0xb1b1b1&#038;color2=0xcfcfcf&#038;hl=en&#038;feature=player_embedded&#038;fs=1"></param><param name="allowFullScreen" value="true"></param><param name="allowScriptAccess" value="always"></param><embed src="http://www.youtube.com/v/N8Azg9TxYkM&#038;color1=0xb1b1b1&#038;color2=0xcfcfcf&#038;hl=en&#038;feature=player_embedded&#038;fs=1" type="application/x-shockwave-flash" allowfullscreen="true" allowScriptAccess="always" width="425" height="344"></embed></object></p>
<p>Wakati ambapo uchunguzi wa mauaji hayo unaendelea, bila shaka jicho litaendelea kutupwa wa Waislamu wanaotumikia jeshi.</p>
]]></content:encoded>
			<wfw:commentRss>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/11/marekani-mauaji-ya-fort-hood-yasababisha-kumulikwa-kwa-waislamu-walio-jeshini/feed/</wfw:commentRss>
		<slash:comments>0</slash:comments>
		</item>
		<item>
		<title>Video: Dunia Yaadhimisha Kuanguka kwa Ukuta wa Berlini</title>
		<link>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/11/video-dunia-yaadhimisha-kuanguka-kwa-ukuta-wa-berlini/</link>
		<comments>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/11/video-dunia-yaadhimisha-kuanguka-kwa-ukuta-wa-berlini/#comments</comments>
		<pubDate>Wed, 11 Nov 2009 12:50:28 +0000</pubDate>
		<dc:creator>Deogratias Simba</dc:creator>
				<category><![CDATA[Americas]]></category>
		<category><![CDATA[Cyprus]]></category>
		<category><![CDATA[English]]></category>
		<category><![CDATA[Feature]]></category>
		<category><![CDATA[Film]]></category>
		<category><![CDATA[General]]></category>
		<category><![CDATA[German]]></category>
		<category><![CDATA[Germany]]></category>
		<category><![CDATA[History]]></category>
		<category><![CDATA[Human Rights]]></category>
		<category><![CDATA[Law]]></category>
		<category><![CDATA[Mexico]]></category>
		<category><![CDATA[Politics]]></category>
		<category><![CDATA[Protest]]></category>
		<category><![CDATA[U.S.A.]]></category>
		<category><![CDATA[Video]]></category>
		<category><![CDATA[War & Conflict]]></category>
		<category><![CDATA[Weblog]]></category>
		<category><![CDATA[Western Europe]]></category>

		<guid isPermaLink="false">http://sw.globalvoicesonline.org/?p=620</guid>
		<description><![CDATA[Leo ni Kumbukumbu ya 20 ya kuanguka kwa Ukuta wa Berlini, kizingiti madhubuti cha kiusalama ambacho kiliwahi kuligawa jiji la Berlini katika pande mbili za Mashariki na Magharibi huko Ujerumani. Leo tunaonyesha baadhi ya picha za video zinazotoka pande mbalimbali za dunia zinazopandishwa ili kusherehekea siku hii na nini ukuta huo ulimaanisha siyo Ujerumani tu bali duniani kote. ]]></description>
			<content:encoded><![CDATA[<em>Ilichapwa kwanza na<a href="http://globalvoicesonline.org/author/juliana-rincon-parra/">Juliana Rincón Parra</a>  &middot; Imetafsiriwa na <a href='http://sw.globalvoicesonline.org/author/simbadeo/'>Deogratias Simba</a> &middot;  <a href='http://globalvoicesonline.org/2009/11/09/video-the-world-commemorates-the-fall-of-the-berlin-wall/'>Angalia ujumbe mama</a></em> 
<br /><p><div class="wp-caption aligncenter" style="width: 310px"><img alt="Ukuta wa Berlini na Natalie Maynor" src="http://globalvoicesonline.org/wp-content/uploads/2009/11/127094076_0624cc7780-300x214.jpg" title="Berlin Wall by Natalie Maynor" width="300" height="214" /><p class="wp-caption-text">Ukuta wa Berlini na Natalie Maynor</p></div><br />
Leo ni <a href="http://www.mauerfall09.de/">Kumbukumbu ya 20 ya kuanguka kwa Ukuta wa Berlini</a>, kizingiti madhubuti cha kiusalama ambacho kiliwahi kuligawa jiji la Berlini katika pande mbili za Mashariki na Magharibi huko Ujerumani. Leo tunaonyesha baadhi ya picha za video zinazotoka pande mbalimbali za dunia zinazopandishwa ili kusherehekea siku hii na nini ukuta huo ulimaanisha siyo Ujerumani tu bali duniani kote. </p>
<p>Huko Ujerumani, mfululizo wa mifano ya vipande vya mchezo wa domino iliundwa kutumia maboya na kisha kunyanyuliwa ili baadaye yaangushwe kama ishara ya kumaliika kwa zama za Vita Baridi. <a href="http://www.youtube.com/watch?v=rsDNfQqnET4">Video hii iliyotayarishwa na NoCommentTV</a> inaonyesha vipande hivyo vya domino, ambavyo <a href="http://www.spiegel.de/international/germany/0,1518,615014,00.html">vilichorwa na watoto huko Ujerumani</a> na p<a href="http://www.heiditrautmann.com/category.aspx?CID=2676368777">ia na wasanii wanaoishi maeneo mengine ambapo kuna migawanyiko na kuta</a>, vikisimamishwa. Kipande cha kukupa vitu vya kuchagua kimezuiwa kufanya kazi, lakini <a href="http://www.youtube.com/watch?v=0y5eGXy_laQ">unaweza kuona jinsi vipande hivyo vya domino vilivyoangushwa kwa kubofya kiungo hiki ili kuiona katika ukurasa wake wa YouTube</a>.</p>
<p><object width="425" height="344"><param name="movie" value="http://www.youtube.com/v/rsDNfQqnET4&#038;color1=0x234900&#038;color2=0x4e9e00&#038;hl=es&#038;feature=player_embedded&#038;fs=1"></param><param name="allowFullScreen" value="true"></param><param name="allowScriptAccess" value="always"></param><embed src="http://www.youtube.com/v/rsDNfQqnET4&#038;color1=0x234900&#038;color2=0x4e9e00&#038;hl=es&#038;feature=player_embedded&#038;fs=1" type="application/x-shockwave-flash" allowfullscreen="true" allowScriptAccess="always" width="425" height="344"></embed></object></p>
<p>Kule <a href="http://www.youtube.com/watch?v=hDCHrnZdwcs">Kolombia</a>, wanafunzi waliigiza uangukaji wa ukuta huo, kwa kupokezana kuvunjilia mbali ukuta wa zege:</p>
<p><object width="425" height="344"><param name="movie" value="http://www.youtube.com/v/hDCHrnZdwcs&#038;color1=0x234900&#038;color2=0x4e9e00&#038;hl=es&#038;feature=player_embedded&#038;fs=1"></param><param name="allowFullScreen" value="true"></param><param name="allowScriptAccess" value="always"></param><embed src="http://www.youtube.com/v/hDCHrnZdwcs&#038;color1=0x234900&#038;color2=0x4e9e00&#038;hl=es&#038;feature=player_embedded&#038;fs=1" type="application/x-shockwave-flash" allowfullscreen="true" allowScriptAccess="always" width="425" height="344"></embed></object></p>
<p>Kutoka Ujerumani, mshabiki wa kuangusha domino <a href="http://www.youtube.com/watch?v=dKLiooarpkA">Annodomino2007</a> amepandisha mtandaoni domino yake mwenyewe ili kuenzi kuanguka kwa ukuta huo, na pia kama kuadhimisha kumbukumbu ya miaka 10 tangu alipoanza mapenzi yake makubwa kwa michezo ya domino:</p>
<p><object width="425" height="344"><param name="movie" value="http://www.youtube.com/v/dKLiooarpkA&#038;color1=0x234900&#038;color2=0x4e9e00&#038;hl=es&#038;feature=player_embedded&#038;fs=1"></param><param name="allowFullScreen" value="true"></param><param name="allowScriptAccess" value="always"></param><embed src="http://www.youtube.com/v/dKLiooarpkA&#038;color1=0x234900&#038;color2=0x4e9e00&#038;hl=es&#038;feature=player_embedded&#038;fs=1" type="application/x-shockwave-flash" allowfullscreen="true" allowScriptAccess="always" width="425" height="344"></embed></object></p>
<p><a href="http://www.youtube.com/watch?v=UF_o1KYQIWU">Kule Marekani</a>, wanachuo waliinua mfano wa Ukuta wa Berlini ambao mtu angeweza kuandika juu yake, yaani kama njia ya kuiamsha jamii:</p>
<p><object width="425" height="344"><param name="movie" value="http://www.youtube.com/v/UF_o1KYQIWU&#038;color1=0x234900&#038;color2=0x4e9e00&#038;hl=es&#038;feature=player_embedded&#038;fs=1"></param><param name="allowFullScreen" value="true"></param><param name="allowScriptAccess" value="always"></param><embed src="http://www.youtube.com/v/UF_o1KYQIWU&#038;color1=0x234900&#038;color2=0x4e9e00&#038;hl=es&#038;feature=player_embedded&#038;fs=1" type="application/x-shockwave-flash" allowfullscreen="true" allowScriptAccess="always" width="425" height="344"></embed></object></p>
<p>Kutoka Mexico, <a href="http://www.youtube.com/watch?v=kffLolfYcfU">VarinVxx alipandisha picha ya video</a> ikionyesha ukuta mwingine ambao bado uko imara, <em>Si Berlini, si Palestina, bali ni kwenye mpaka wa Marekani na Mexico, Ukuta wa Aibu huko Marekani</em>:</p>
<p><object width="425" height="344"><param name="movie" value="http://www.youtube.com/v/kffLolfYcfU&#038;color1=0x234900&#038;color2=0x4e9e00&#038;hl=es&#038;feature=player_embedded&#038;fs=1"></param><param name="allowFullScreen" value="true"></param><param name="allowScriptAccess" value="always"></param><embed src="http://www.youtube.com/v/kffLolfYcfU&#038;color1=0x234900&#038;color2=0x4e9e00&#038;hl=es&#038;feature=player_embedded&#038;fs=1" type="application/x-shockwave-flash" allowfullscreen="true" allowScriptAccess="always" width="425" height="344"></embed></object></p>
<p><a href="http://www.youtube.com/watch?v=cGpVyCovo70">Krista Schyler</a> pia analinganisha ukuta ulio kwenye mpaka wa Mexico na Marekani na ule wa Berlini, safari hii siyo tu kukazia kuhusu madhara ya uhamaji wa binadamu, lakini kutoka kwa mtazamo wa utunzaji wanyama pori pia:</p>
<p><object width="425" height="344"><param name="movie" value="http://www.youtube.com/v/cGpVyCovo70&#038;color1=0x234900&#038;color2=0x4e9e00&#038;hl=es&#038;feature=player_embedded&#038;fs=1"></param><param name="allowFullScreen" value="true"></param><param name="allowScriptAccess" value="always"></param><embed src="http://www.youtube.com/v/cGpVyCovo70&#038;color1=0x234900&#038;color2=0x4e9e00&#038;hl=es&#038;feature=player_embedded&#038;fs=1" type="application/x-shockwave-flash" allowfullscreen="true" allowScriptAccess="always" width="425" height="344"></embed></object></p>
<p>Mradi huu wa majaribio (Mradi Rubani) kwa ajili ya <a href="http://www.youtube.com/watch?v=7QeaIChuJ4c">makala ya video ya Ziashere</a> inaonyesha kuta nyingine ambazo bado ziko imara, mojawapo ikiwa kule Ireland:</p>
<p><object width="425" height="344"><param name="movie" value="http://www.youtube.com/v/7QeaIChuJ4c&#038;color1=0x234900&#038;color2=0x4e9e00&#038;hl=es&#038;feature=player_embedded&#038;fs=1"></param><param name="allowFullScreen" value="true"></param><param name="allowScriptAccess" value="always"></param><embed src="http://www.youtube.com/v/7QeaIChuJ4c&#038;color1=0x234900&#038;color2=0x4e9e00&#038;hl=es&#038;feature=player_embedded&#038;fs=1" type="application/x-shockwave-flash" allowfullscreen="true" allowScriptAccess="always" width="425" height="344"></embed></object></p>
<p>Video hiyo ya mwisho ina umri wa miaka 2 sasa, lakini bado ujumbe wake una maana: <a href="http://www.youtube.com/watch?v=Pu4OztB_Zyo">mtengeneza filamu Adam</a> aliwahoji vijana kutoka pande zote mbili za ukuta Kaskazini na Kusini mwa Cyprus, ukanda wa kijani unaolindwa na vikosi vya helmeti za kibuluu vya Umoja wa Mataifa ambao unatenganisha WaCyprus wa Kituruki na Wacyprus wa Kigiriki, jambo linaoufanya mji huo uwe na heshima ya kuwa <a href="http://en.wikipedia.org/wiki/Nicosia">mji wa mwisho uliogawanyika</a>.</p>
<p><object width="425" height="344"><param name="movie" value="http://www.youtube.com/v/Pu4OztB_Zyo&#038;color1=0x234900&#038;color2=0x4e9e00&#038;hl=es&#038;feature=player_embedded&#038;fs=1"></param><param name="allowFullScreen" value="true"></param><param name="allowScriptAccess" value="always"></param><embed src="http://www.youtube.com/v/Pu4OztB_Zyo&#038;color1=0x234900&#038;color2=0x4e9e00&#038;hl=es&#038;feature=player_embedded&#038;fs=1" type="application/x-shockwave-flash" allowfullscreen="true" allowScriptAccess="always" width="425" height="344"></embed></object></p>
]]></content:encoded>
			<wfw:commentRss>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/11/video-dunia-yaadhimisha-kuanguka-kwa-ukuta-wa-berlini/feed/</wfw:commentRss>
		<slash:comments>0</slash:comments>
		</item>
		<item>
		<title>Ujauzito na Magereza: Afya na Haki za Wanawake Magerezani</title>
		<link>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/11/ujauzito-na-magereza-afya-na-haki-za-wanawake-magerezani/</link>
		<comments>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/11/ujauzito-na-magereza-afya-na-haki-za-wanawake-magerezani/#comments</comments>
		<pubDate>Thu, 05 Nov 2009 13:24:11 +0000</pubDate>
		<dc:creator>Christian Bwaya</dc:creator>
				<category><![CDATA[Americas]]></category>
		<category><![CDATA[Argentina]]></category>
		<category><![CDATA[Brazil]]></category>
		<category><![CDATA[Conversations for a Better World]]></category>
		<category><![CDATA[East Asia]]></category>
		<category><![CDATA[Eastern & Central Europe]]></category>
		<category><![CDATA[Ecuador]]></category>
		<category><![CDATA[English]]></category>
		<category><![CDATA[Feature]]></category>
		<category><![CDATA[General]]></category>
		<category><![CDATA[Health]]></category>
		<category><![CDATA[Human Rights]]></category>
		<category><![CDATA[Humanitarian]]></category>
		<category><![CDATA[Laos]]></category>
		<category><![CDATA[Peru]]></category>
		<category><![CDATA[Photography]]></category>
		<category><![CDATA[Russia]]></category>
		<category><![CDATA[Spain]]></category>
		<category><![CDATA[Spanish]]></category>
		<category><![CDATA[U.S.A.]]></category>
		<category><![CDATA[Video]]></category>
		<category><![CDATA[Weblog]]></category>
		<category><![CDATA[Western Europe]]></category>

		<guid isPermaLink="false">http://sw.globalvoicesonline.org/?p=493</guid>
		<description><![CDATA[Mapambano bado yanaendelea kuhakikisha haki za binadamu kwa wanawake wajawazito duniani pote, ni inaelekea kwamba katika mchakato huo, wanawake waliopo magerezani wanasahauliwa. Je ni hatua zipi zilizochukuliwa kuhakikisha kuwa nao wanaangaliwa kwa utu, kwa kuzingatia uhai wanaoubeba.]]></description>
			<content:encoded><![CDATA[<em>Ilichapwa kwanza na<a href="http://globalvoicesonline.org/author/juliana-rincon-parra/">Juliana Rincón Parra</a>  &middot; Imetafsiriwa na <a href='http://sw.globalvoicesonline.org/author/bwaya/'>Christian Bwaya</a> &middot;  <a href='http://globalvoicesonline.org/2009/10/24/pregnancy-and-prisons-womens-health-and-rights-behind-bars/'>Angalia ujumbe mama</a></em> 
<br /><p><img alt="" src="http://globalvoicesonline.org/wp-content/uploads/2009/10/2044749780_4ade9e2e3f-300x225.jpg" title="2044749780_4ade9e2e3f" class="aligncenter" width="300" height="225" /></p>
<p><strong>Je, wanawake wote wajawazito wanastahili haki sawa za binadamu, au wanawake wajawazito walio jela huziacha haki hizo? </strong></p>
<p>Kuna maswali machache yanayokuja akilini kuhusu haki ya mwanamke mjamzito kuishi na kumlea mwanae anapokuwa kapatikana na hatia kwa kosa la jinai la namna fulani:<br />
•	Inakuwaje kwao wanapokuwa wajawazito na kupata mtoto wakiwa gerezani?<br />
•	Je, wanapaswa kuwa kipaumbele wakati kuna wanawake wengine nje ya vyuo vya mafunzo bila msaada wa kitabibu?<br />
•	Je, ujauzito unapaswa kuwa juu ya hali nyinginezo za kisheria kumhakikishia mwanamke mjamzito haki zake za kibinadamu? </p>
<p><strong>Marekani: wanawake walio kwenye uchungu wa kuzaa hawatafungwa tena minyororo.  </strong></p>
<p>Je unaweza kufikira mwanamke akijifungua huku mikono yake ikiwa kwenye pingu na miguu yake ikiwa imefungwa na minyororo kwenye kitanda? <a href="http://www.rhrealitycheck.org/user/malika-sadaa-saar">Malika Saada Saar</a>, mwanzilishi na Mkurugenzi Mtendaji wa <a href="http://www.rebeccaproject.org/">Mradi wa Rabecca kwa Haki za Binadamu</a>, <a href="http://www.rhrealitycheck.org/blog/2009/10/06/in-labor-and-in-chains">anatuelezea</a> kuhusu kitendo hiki ambacho bado kinatokea nchini Marekani, ambapo wanawake wajazito wanaotumikia kifungo wamekuwa wakifungwa minyororo wakati wa uchungu na kujifungua na kuwa hiki ni kitendo kilichozoeleka katika baadhi ya magereza (ya kurekebishia tabia), ingawa ni hatari kwa afya ya mama na mtoto. Ifuatayo ni video ya mahojiano yaliyoambatanishwa kwenye makala iliyoandikwa kwa ajili ya mradi wa <em>RH Reality Check</em>, jamii ya mtandaoni kuhusu afya na haki ya uzazi na jinsia inatupa taarifa na uchambuzi kwa afya ya uzazi:</p>
<p><object width="425" height="344"><param name="movie" value="http://www.youtube.com/v/CWj1uHdxnt8&#038;color1=0x234900&#038;color2=0x4e9e00&#038;hl=es&#038;feature=player_embedded&#038;fs=1"></param><param name="allowFullScreen" value="true"></param><param name="allowScriptAccess" value="always"></param><embed src="http://www.youtube.com/v/CWj1uHdxnt8&#038;color1=0x234900&#038;color2=0x4e9e00&#038;hl=es&#038;feature=player_embedded&#038;fs=1" type="application/x-shockwave-flash" allowfullscreen="true" allowScriptAccess="always" width="425" height="344"></embed></object><br />
<strong><br />
Kitu gani hutokea kwa mtoto mchanga wa wa mfungwa baada ya kuzaliwa?</strong></p>
<p>Nchi mbalimbali zina kanuni tofauti kuhusiana na watoto magerezani. Kwa mfano, nchini Argentina, kwa mujibu wa <em>Ajintem</em>, chombo cha mawasiliano cha taarifa za uhamamiaji,  <a href="http://portal.ajintem.com/archivo/80-argentina-prision-domiciliaria-para-embarazadas-y-madres.html">sheria ilipitishwa</a> mwaka uliopita ikifafanua kwamba wanawake wajawazito, wanawake wenye watoto wadogo chini ya miaka mitano na wale wenye watoto walemavu wangenufaika na mpango wa kutumikia kifungo chao makwao chini ya ulinzi wa nyumbani. Sheria hii ingewanufaisha si tu akina mama, ambao kwa kuwa gerezani wasingepata huduma za afya wakati wa ujauzito, lakini pia (ingemnufaisha) mtoto, ambaye angelelewa ama katika mazingira yasiyo salama yanayokosa uhuru na upungufu wa udhibiti wa afya na chakula, au wangelelewa mbali na mama, na hivyo kusababisha mlolongo wa matatizo mengine. Hata hivyo, ujumbe ni kwa ajili ya mahakimu kufuatilia kiini cha sheria na kutoa ruhusa hii kwa wanawake wale ambao hawahusishwi na mashitaka ya jinai ya matumizi ya nguvu, kuhakikisha kwamba idadi kubwa ya raia iliyobaki haiuchukulii ujauzito kama kadi ya kumtoa mtu jela bure.</p>
<p>Katika visiwa vya Canary, kwa mujibu wa blogu ya <em>Prisiones y penas</em>, ambayo huandika kuhusu habari zinazohusu jela na magereza, wanawake wanaruhusiwa <a href="http://prisionesypenas.blogspot.com/2009/09/detenidas-con-hijos-en-carceles.html">kuishi na watoto wao hadi umri wa miaka mitatu</a> ndani ya selo zao, lakini wakiwa pamoja na wafungwa wenzao, kitu ambacho sio mazingira mazuri sana kwako. Kwa hiyo, wanawake wajawazito au wanawake wenye watoto wenye umri wa chini ya miaka 3 huambiwa kuhusiana na kuingia kwenye magereza kuwa si vizuri kwa mtoto kukualia gerezani, na hupewa uchaguzi wa kumpeleka mtoto kwa wanafamilia wengine. Hali ni hii hii huko <a href="http://www.reuters.com/article/worldNews/idUSTRE5085ZV20090109">Peru</a> na <a href="http://russiatoday.com/Top_News/2009-07-27/russia-s-prison-born-children-marked-for-life.html">Urusi</a>. Nchini Marekani, kuna magereza mawili tu yenye kuruhusu jambo hili, huko New York na Nebraska, <a href="http://www.amnestyusa.org/women/custody/toomuchtime/pt_02/e_moms.html">kama ilivyoonyeshwa na mpiga picha maarufu Jane Evelyn Atwood</a> kwenye insha ya picha zake tatu kwa ajili ya <a href="http://www.amnestyusa.org/women/custody/toomuchtime/"><em>Shirika la kimataifa la Amnesty International</em>, inayoitwa <em>Too Much Time</em></a>, ambapo alitembelea dazani nyingi za magereza kote duniani kurekodi na kuweka kumbukumbu za maisha ya wafungwa.</p>
<p>Kwa nini mfumo wa magereza nchini Marekani hauruhusu, kwa ujumla, wanawake wenye watoto kubaki nao? Atwood anaeleza kwamba kwa sababu ya mazingira ufungwa, hairuhusiwi. Kwenye <a href="http://prisonphotography.wordpress.com/2009/10/07/women-behind-bars-jane-evelyn-atwoods-too-much-time/"><em>blogu ya Prison Photography</em> wanaelezea madai haya</a>: </p>
<blockquote><p>Watoto hawahusishwi kwenye magereza yote isipokuwa mawili tu nchini Marekani. Tishio la usalama linatajwa kama sababu: mtoto ndani ya gereza ni dhaifu na atakuwa shabaha ya malengo maovu siku zote. Madai yanaonekana kuwa hayana maana kwa kiasi fulani kwa unapofananisha na mifumo ya adhabu kwa nchi nyinginezo.</p></blockquote>
<p>Insha ya Atwood kwenye wavuti ya <em>Amnesty International</em> inaonyesha mambo mawili, sehemu inayohusu taratibu za kujifungua huku umefungwa minyororo kama yalivyoelezwa kwenye <a href="http://www.amnestyusa.org/women/custody/toomuchtime/pt_02/f_vanbab.html">Mtoto wa Vanessa</a> na pia inaonyesha jambo jingine kuhusu mfumo wa magereza na umama, kwa kutumia picha za wanawake wakati mpigapicha akisoma insha kuhusu uzoefu wake wa kutembelea magereza huku akipiga picha. </p>
<p><strong>Ujauzito kama zana ya mapatano? </strong></p>
<p>Kwa nini haki za wanawake wajawazito gerezani zinatatanisha? Katika  <em>Russia Today</em>, idhaa ya matangazo ya Kirusi, <a href="http://russiatoday.com/Top_News/2009-07-27/russia-s-prison-born-children-marked-for-life.html">mada hii inatajwa</a> panapojadiliwa suala la watoto kuzaliwa na kulelewa katika mfumo wa magereza wa Kirusi:</p>
<blockquote><p>Wenye kutilia mashaka (suala hili) wanadhani akina mama wengine hupata ujauzito kwa makusudi ili tu kurahisisha maisha huko gerezani. Ruhusa ya kwenda hospitali, halafu kuwa na ratiba iliyojaa muda mwingi na mwanao –ni afadhali kuliko kukaa kwenye seli ya magereza, wanadai. </p></blockquote>
<p>Na kuna wanawake ambao wanaona kwamba kuwa na mimba ni njia pekee ya kukwepa hukumu, kama ilivyotokea mwezi Juni, pale mwanamama wa Kiingereza aliwekwa ndani na kuhukumiwa kifo huko Laos kwa sababu ya kusafirisha madawa ya kulevya akapata ujauzito gerezani na akanusurika kunyongwa, kwa sababu serikali ya Laos isingemnyonga mwanamama mjamzito. <a href="http://www.dailyexpress.co.uk/posts/view/105278/No-firing-squad-for-girl-who-fell-pregnant-in-jail">Madai yaliyotolewa </a>kwa mujibu wa jarida la Kiingereza la <em>Daily Express</em>, ni kwamba alipata ujauzito kwa kupandikiziwa mbegu za kiume ‘ili kupata hukumu nyepesi zaidi” </p>
<p><strong>Kwa maneno yao: Wanawake wanaeleza kuhusu watoto wao na maisha ya gerezani</strong></p>
<p>Geraldin Rodríguez, Mwajentina aliye kwenye jela za Ecuador kwa sababu ya biashara ya madawa ya kulevya anamueleza <a href="http://marcosbrugiati.blogspot.com/2009/07/carcel-de-mujeres.html">Marcos Brugiati</a>, mwandishi mshiriki katika chapisho la mtandaoni linalohusiana na masuala ya sanaa liitwalo <em><a href="http://www.indexarte.com.ar/noticias/562/las-rejas-de-la-carcel-el-arte-de-la-espera.htm">Plastica-Argentina</a></em>, masimulizi kuhusu kuigiza na kufanya maonyesho ndani ya jela, kupata ujauzito gerezani na kumpata mwanae. Aliruhusiwa kuwa na mwanae, lakini akaamua kwamba mwanae anahitaji kukua akiwa mtu huru:</p>
<blockquote><p> “Decidí que salga para vivir, tenía miedo que sufra de grande los traumas que hoy tengo. Se lo llevó al año mi hermano quien se hice cargo con su esposa”.</p></blockquote>
<div class="translation">Niliamua aondoke ili aishi, nilikuwa na wasiwasi angeteswa na msongo wa mawazo nilionao leo. Baada ya mwaka kaka yangu alimchukua na anamtunza kwa kushirikiana wa mke wake. </div>
<p>Juvinete yuko kwenye <a href="http://www.nortecastilla.es/20080908/vida/quedarse-embarazada-prision-irresponsable-20080908.html">gereza la Kihispania</a>, na alikuwa mjamzito wakati alipofungwa kwa kusafirisha madawa ya kulevya. Anasimulia habari zake kwenye gazeti la kanda huko Uhispania linaloitwa <em><a href="http://www.nortecastilla.es/20080908/vida/quedarse-embarazada-prision-irresponsable-20080908.html">NorteCastilla</a></em>. Miaka mitatu baada ya kujifungua mwanae akiwa gerezani, mwanae ilibidi aondoke, na alipelekwa kwa familia ya kufikia. Juvinete humuona mwanae huyo wa kike kila baada ya siku 15 na kila miezi miwili hupata ruhusa ya wiki mbili kukaa na mwanae. Hata hivyo, mambo hayaonekani kuwa mazuri sana: kuna uwezekano kwamba Juvinete atapelekwa Brazil alikozaliwa, na anahofia matokeo ya mabadiliko haya kwa mwanae. Anao ushauri kwa mwanamke yeyote anayeamua kupata ujauzito akiwa jela:</p>
<blockquote><p>-Intento convencerlas para que no se queden en estado dentro porque ver a un niño privado de libertad es muy duro, es irresponsable. Ellos no tienen que pagar nuestros errores.</p></blockquote>
<div class="translation">
Ninajaribu kuwashawishi wasipate ujauzito wakiwa bado ndani kwa sababu kumuona mtoto akikosa uhuru wake ni vigumu sana, ni kutokuwajibika. (Watoto wanaozaliwa jela) wasilipie gharama ya makosa yetu</div>
<p>.  </p>
<p>Kwenye wavuti ya <em><a href="http://www.womenandprison.org/motherhood/kebby-warner.html">Woman and Prison</a></em>, iliyojikita katika kuyatazama maisha ya wanawake wakiwa kwenye mifumo ya magereza , <a href="http://www.womenandprison.org/motherhood/kebby-warner.html">mfungwa Kebby Warner anaongelea ujauzito wake</a> mwenyewe alipokuwa akitumikia kifungo kwenye gereza la Kimarekani, na jinsi alivyotendewa wakati wa ujauzito wake, utungu na baadae, wakati alipokuja kunyang’anywa mwanae. Hapa ni muhtasari anapoandika kuhusu hatua za kujifungua: </p>
<blockquote><p>Wakati wa utungu, hakuna mtu anaruhusiwa kuwa kwenye chumba cha kujifungulia. Familia yangu wala haikujua kwamba nilikuwa ninajifungua au nimempata (mwanagu) mpaka nilipokuwa nimetoka hospitali. Wakati huo wa siku tatu baadhi ya walinzi walikuwa ndani ya chumba, lakini muda mwingi, wakati wauguzi walipowaomba kukaa nje ya mlango, walitii. Nimesikia simulizi za kutisha za wanawake wakifungwa kwa mnyororo kwenye kitanda cha uzazi. Ninashukuru kwa kutokukumbana na hali hiyo. Wauguzi wengi walinitendea kama binadamu badala ya mfungwa.</p></blockquote>
<p>Unaweza kusoma shuhuda zaidi kuhusu kukua na mzazi gerezani na madhara mbalimbali ambayo kufunga wanawake kunaweza kuyawasababisha kwa watoto wao <a href="http://www.womenandprison.org/motherhood/index.html">kwenye Wanawake na Magereza</a>.</p>
<p>Kwa hiyo unafikiriaje? Kwa wanawake wajawazito duniani kote kutokupata huduma za afya za namna yoyote, je jitihada zaidi zinahitajika kuwanufaisha wanawake walio gerezani? Je, kuna tofauti kati ya wanawake wanaotumikia kifungo kwenye magereza (ya mafunzo) na wale wanaoishi nje? Je, ni lazima kuwatendea tofauti?<br />
<em><br />
Picha iliyotumika kwenye makala hii ni “17 de noviembre” ya <a href="http://www.flickr.com/photos/daquellamanera/2044749780/">daquella manera</a>.</em></p>
]]></content:encoded>
			<wfw:commentRss>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/11/ujauzito-na-magereza-afya-na-haki-za-wanawake-magerezani/feed/</wfw:commentRss>
		<slash:comments>0</slash:comments>
		</item>
		<item>
		<title>Marekani: Wanandoa wa rangi tofauti wanyimwa cheti cha ndoa</title>
		<link>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/10/marekani-wanandoa-wa-rangi-tofauti-wanyimwa-cheti-cha-ndoa/</link>
		<comments>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/10/marekani-wanandoa-wa-rangi-tofauti-wanyimwa-cheti-cha-ndoa/#comments</comments>
		<pubDate>Sun, 25 Oct 2009 04:44:20 +0000</pubDate>
		<dc:creator>Christian Bwaya</dc:creator>
				<category><![CDATA[Americas]]></category>
		<category><![CDATA[Children]]></category>
		<category><![CDATA[English]]></category>
		<category><![CDATA[Ethnicity]]></category>
		<category><![CDATA[Freedom of Speech]]></category>
		<category><![CDATA[General]]></category>
		<category><![CDATA[Governance]]></category>
		<category><![CDATA[Law]]></category>
		<category><![CDATA[Religion]]></category>
		<category><![CDATA[U.S.A.]]></category>
		<category><![CDATA[Weblog]]></category>

		<guid isPermaLink="false">http://sw.globalvoicesonline.org/?p=392</guid>
		<description><![CDATA[Juma lililopita huko Hammond, Louisiana, wapenzi wawili walituma maombi ya kibali cha kufunga ndoa na walikataliwa kwa misingi ya rangi zao tofauti. Afisa wa kutathmini na kuandikisha nyaraka (Muamuzi wa Amani) alidai kuwa “ndoa baina ya watu wa rangi hazidumu” na alisema kuwa anafanya hivyo “kwa ajili ya watoto.”]]></description>
			<content:encoded><![CDATA[<em>Ilichapwa kwanza na<a href="http://globalvoicesonline.org/author/jillian-york/">Jillian C. York</a>  &middot; Imetafsiriwa na <a href='http://sw.globalvoicesonline.org/author/bwaya/'>Christian Bwaya</a> &middot;  <a href='http://globalvoicesonline.org/2009/10/21/usa-interracial-couple-denied-marriage-license/'>Angalia ujumbe mama</a></em> 
<br /><p>Juma lililopita, huko Hammond, Louisiana, Beth Humphrey (ambaye ni mzungu) na Terence McKay (ambaye ni mweusi) walituma maombi ya kupata cheti cha ndoa na <a href="http://www.msnbc.msn.com/id/33332436/ns/us_news-race_and_ethnicity">walinyimwa</a> kwa misingi ya rangi zao. Afisa wa kutathmini na uandikishaji (Muamuzi wa Amani), Keith Bardwell, alidai kwamba katika uzoefu wake, “ndoa za rangi tofauti hazidumu kwa muda mrefu” na akasema alikuwa “akiamua hivyo kwa ajili ya watoto wa wanandoa hao”. </p>
<p>“<a href="http://en.wikipedia.org/wiki/Jim_Crow_laws">Sheria za Jim Cro</a>w” ambazo ziliwataka Wamerekani weusi na weupe kuwa na huduma tofauti zilikomeshwa mwaka 1965, na <a href="http://en.wikipedia.org/wiki/Anti-miscegenation_laws">sheria zilizozuia ndoa na mahusiano ya kimapenzi kati ya watu wenye rangi tofauti</a> zilikomeshwa katika majimbo yote ya Marekani mwaka 1967. </p>
<p>Lakini ubaguzi wa rangi bado upo. Ingawa muda mwingi huwa upo chini ya  ardh, mara nyingine ubaguzi huo hunyanyua kichwa chake kibaya kwa namna ambayo si haiwezekani kutoonekana; habari hii ilitawala vichwa vya habari katika vyombo vya habari nchini kote Marekani, na kusababisha makala za wanablogu kutokea kwenye jamii za sehemu hizo na zaidi.</p>
<p>Katika majibu yaliyotokana na “utetezi” wa Bardwell kwamba huwafungisha ndoa watu weusi mara zote, blogu ya kupinga ubaguzi wa rangi iitwayo <em>Stuff White People Do</em> ilionyesha kuchukizwa kwake, <a href="http://stuffwhitepeopledo.blogspot.com/2009/10/still-ask-that-old-camouflaging.html">kwa kusema</a>: </p>
<blockquote><p>Sawa, u mtenda haki na mema wa namna gani, Jaji Bardwell. Bila kutaja, uingiliaji wako (katika maisha ya watu) na ubaba wa kulazimisha. </p>
<p>Nikizungumzia nyumba ya Bardwell, ambayo nina hakika imezidiwa na kundi kubwa lenye furaha la watoto weusi kwa weupe wakicheza pamoja, alikuwa na haya pia ya kusema:<br />
<em><br />
Nina mabiwi na mabiwi ya marafiki weusi. Huja nyumbani kwangu, ninawaoza, wanatumia msala wangu. Ninawafanyia kama ninavyomfanyia yeyote. </em></p>
<p>Mh ndio, marafiki weusi pia, wengi mno. Pale kwake, hadi bafuni kwake! </p></blockquote>
<p>Mtoa maoni kwenye blogu hiyo, <em>Siditty </em>(ambaye pia aliandika makala yake <a href="http://siditty.blogspot.com/2009/10/interracial-couple-denied-marriage.html">hapa</a>), aligusia hali ya kinyume cha hasira ya Bardwell: </p>
<blockquote><p>Huwa ninajiuliza kuhusu mtu ambaye katokea Louisiana, mwenye historia ndefu ya kujichanganya na watu wa rangi tofauti, kwa kupitia mfumo wa utamaduni wa ukazi kati ya watu weupe na wanawake weusi (placage) kadhalika na utamaduni mchanganyiko wa  jamii ya Kispania na Kifaransa nma Weusi (Creole), sasa hivi ghafla tu anaonekana kujali sana watoto. Jamii yake haikuwa inajali hivi kwenye miaka ya 1700, hapaswi kuwa hivyo anavyodai leo.</p></blockquote>
<p>Blogu ya <em>Racism Review </em>ililichachafya suala la Bardwell “ kujali watoto” kwa <a href="http://www.racismreview.com/blog/2009/10/15/interracial-couple-denied-marriage-license/">ushahidi</a> wa watoto waliotakana na uhusiano wa rangi tofauti: </p>
<p>Na, ili kuutazama zaidi ushahidi, <a href="http://www.jstor.org/pss/352395">watoto wa ndoa za wenzi wenye tofauti ya rangi</a> huwa hawateseki ukilinganisha na watoto wengine kwa kigezo kwamba wanakulia katika mazingira yanayokubali tofauti za watu na watoto wa ndoa za rangi tofauti. Kama watoto wa namna hii watakutana na ubaguzi wa rangi (na matatizo mengine ya kimfumo), basi <a href="http://www.ajph.org/cgi/content/abstract/93/11/1865">wana uwezekano mkubwa wa kukumbana na msongo</a>, matatizo ya kiafya yanayohusiana na msongo wa mawazo, kama vile uvutaji sigara na matumizi ya madawa ya kulevya. Hayo ndiyo <strong><em>matokeo</em> </strong>ya ubaguzi wa rangi, na hiyo ni sababu nyingine ya kufanya kazi ili kuukomesha ubaguzi wa rangi. <strong><em>Isitumike</em></strong> – kwa kupindua mantiki juu chini –kama sababu ya kuendeleza ubaguzi.</p>
<p>Na <em>Black Girl in Maine</em> aligusia pia kuhusu swali la “vipi kuhusu watoto?”, kwa <a href="http://blackgirlinmaine.wordpress.com/2009/10/15/what-about-the-kids/">kuelezea uzoefu</a> wa mwanae ambaye ni chotara: </p>
<blockquote><p>Na kwa watoto, vipi kuhusu watoto? Ndio, watoto chotara mara nyingine hupata usumbufu kutoka kwa wengine lakini sio mara zote na nadhani kati ya vijana wa leo inaonekana poa sana kuwa chotara. Kama rafiki yangu alivyoniambia mwanangu hapati matatizo na kupata marafiki wa kiume na wa kike. Nadhani wakati pekee ambapo watoto machotara huweza  kupata shida ni pale wanapokosa mtu wa kuongea nao kuhusu asili yao. Nadhani wakati ambapo watoto wameunganishwa na historia ya asili yao na ya jamii yao, hiyo huwatengenezea nafasi salama kwao. </p></blockquote>
<p>Nchini Marekani, s<a href="http://en.wikipedia.org/wiki/Anti-miscegenation_laws#Anti-miscegenation_Laws_enacted_in_the_Thirteen_Colonies_and_the_United_States">heria ya kuwazuia watu wa rangi tofauti kuoana ama kuwa na uhusiano wa kimapenzi</a> katika majimbo mengi ilipiga marufuku ndoa za Wamarekani weupe na Wamerekani weusi (na wale wa asili nyinginezo) katika majimbo kadhaa. Wakati katika majimbo mengine, sheria hizi zilibatilishwa mwanzoni mwa miaka ya 1780, katika majimbo 16 sheria hizi hazikuondoshwa mpaka wakati wa kesi ya mwaka 1967 , kati ya <a href="http://en.wikipedia.org/wiki/Anti-miscegenation_laws#Loving_v._Virginia">Loving na Virginia</a>, ambapo wenzi hawa wa rangi tofauti waliokuwa wameoana mjini Washington, D.C walitiwa chini ya ulinzi kwenye chumba chao cha kulala. Vita yao ya kisheria ilifika mpaka Mahakama Kuu ya Marekani, ambapo sheria hizi zilifika mahali zikatupiliwa mbali.</p>
<p>Wanablogu kadhaa waligusia mtazamo wa kisheria kwa suala hili. Mwanablogu mmoja, <em>Jay Says</em>, <a href="http://jaysays.com/2009/10/louisiana-judge-refuses-to-preside-over-interracial-marriage/">anaandika</a>:</p>
<blockquote><p>Kama Jaji wa masuala ya Amani, anatakiwa kuelewa kwamba ndoa za rangi tofauti si kinyume cha sheria tena – baada ya kuonekana ni kinyume cha katiba miaka 40 iliyopita. Tukio hili limegusa hisia baada ya Maandamano ya Usawa Kitaifa mwishoni mwa wiki ambapo <a href="http://vidly.com/aenC">nilifanya mahojiano mafupi</a> na wanandoa wa rangi tofauti, Bwana na Bibi Newman (pichani) kuhusu kwa nini wanaandamana.</p>
<p>Ubaguzi wa rangi, Uwepo wa matabaka, Ubaguzi wa watu wa jinsia tofauti, Hofu ya Ushoga, Kutovumiliana kidini pamoja na upendeleo wa aina nyingine vinaweza kuwapo na vipo katika jamii yetu, lakini havipaswi kuwepo kisheria. Kumruhusu mwajiriwa wa Serikali anayelipwa kwa kodi za watu “huru” wa Marekani (au katika mukhtadha huu jimbo lililo nchini Marekani) kutumia imani zake binafsi kuamua masuala yanayotawaliwa kwa sheria za kiraia ni kichefuchefu. Kama hakubaliani na ndoa za rangi tofauti, basi anahitaji kutafuta kazi nyingine –labda Mkuu wa Ku Klux Klan?</p></blockquote>
<p>Mwisho, mwanablogu mmoja amechukua fursa ya kuligeuza suala hili kuwa wakati muafaka wa kujifunza. Yeye, ambaye blogu yake inatwa <em>Ni Nini Ninachojua?</em>, anawasihi wasomaji kufikiri kuhusu hisia zao wenyewe kuhusu mada husika: </p>
<blockquote><p>Kama una wasi wasi kwamba ubaguzi wa rangi bado unaishi ndani yetu wote, fikiria unavyojisikia unapopata wazo la kuoa au kuolewa nje ya watu wa rangi yako, hasa wewe ukiwa ni mzungu na mwingine ni mweusi. Ndio, ni sawa kwa watu wengine, lakini hivi usingetafuta sababu nzuri zenye hoja zinzoshawishi za kuelezea kwa nini binti yako atayafanya maisha yake yawe magumu sana atakapomleta nyumbani mchumba wake mweusi? Kuwa mkweli. Hata kama ulisema, “Hakuna shida” hivi kweli haukusita hata kidogo kupata jibu? Kama haikuwa hivyo, basi wewe si wa kawaida. </p></blockquote>
<p>Wakati Bardwell <a href="http://www.google.com/url?sa=t&#038;source=web&#038;oi=news_result&#038;ct=res&#038;cd=1&#038;ved=0CA0QqQIwAA&#038;url=http%3A%2F%2Fblogs.usatoday.com%2Fondeadline%2F2009%2F10%2Flouisiana-jp-says-he-wont-resign-over-interracial-marriage-issue.html&#038;ei=KarbSoWDBM_L8QaKh_m2BQ&#038;usg=AFQjCNHLMtP_RWImJP00A7ZrzL06uU4Www&#038;sig2=44ZFnEHaEEs78URKZiQV-g">anasema sasa</a> kuwa hatajiuzulu kwa sababu ya suala hili, jambo moja ni la hakika: bila ya shaka kuna habari zaidi zaja.</p>
]]></content:encoded>
			<wfw:commentRss>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/10/marekani-wanandoa-wa-rangi-tofauti-wanyimwa-cheti-cha-ndoa/feed/</wfw:commentRss>
		<slash:comments>0</slash:comments>
		</item>
		<item>
		<title>Marekani: Stempu ya Iddi Yachochea Chuki Huko Tennessee</title>
		<link>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/09/marekani-stempu-ya-iddi-yachochea-chuki-huko-tennessee/</link>
		<comments>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/09/marekani-stempu-ya-iddi-yachochea-chuki-huko-tennessee/#comments</comments>
		<pubDate>Sat, 26 Sep 2009 10:32:16 +0000</pubDate>
		<dc:creator>j nambiza tungaraza</dc:creator>
				<category><![CDATA[Americas]]></category>
		<category><![CDATA[English]]></category>
		<category><![CDATA[Feature]]></category>
		<category><![CDATA[Freedom of Speech]]></category>
		<category><![CDATA[Governance]]></category>
		<category><![CDATA[Media]]></category>
		<category><![CDATA[Politics]]></category>
		<category><![CDATA[Religion]]></category>
		<category><![CDATA[U.S.A.]]></category>
		<category><![CDATA[Weblog]]></category>

		<guid isPermaLink="false">http://sw.globalvoicesonline.org/?p=323</guid>
		<description><![CDATA[Barua pepe yenye madai ya uongo kuwa Rais Obama ametoa stempu mpya kuadhimisha sikukuu ya Waislamu Eid al-Fitr imemfikia Meya wa Tennessee ambaye aliisambaza kwa wafanyakazi wake na waasa waisusie stempu hiyo.]]></description>
			<content:encoded><![CDATA[<em>Ilichapwa kwanza na<a href="http://globalvoicesonline.org/author/jillian-york/">Jillian C. York</a>  &middot; Imetafsiriwa na <a href='http://sw.globalvoicesonline.org/author/j-nambiza-tungaraza/'>j nambiza tungaraza</a> &middot;  <a href='http://globalvoicesonline.org/2009/09/21/usa-eid-postage-stamp-provokes-hate-in-tennessee/'>Angalia ujumbe mama</a></em> 
<br /><p><div class="wp-caption alignleft" style="width: 210px"><img alt="Toleo la stempu la mwaka 2008, kabla bei haijapanda" src="http://globalvoicesonline.org/wp-content/uploads/2009/09/eid.jpg" title="eid" width="200" height="200" /><p class="wp-caption-text">Toleo la stempu la mwaka 2008, kabla bei haijapanda</p></div><br />
Wakati Waislamu nchini Marekani wanasherehekea <a href="http://en.wikipedia.org/wiki/Eid_ul-Fitr">Eid al-Fitr</a>, sherehe inayoadhimisha mwisho wa mwezi wa Ramadhani, barua pepe yenye nia mbaya imekuwa ikizunguka. Barua pepe hiyo ina maddai ya uongo kuwa Rais Obama ametoa stempu mpya kuadhimisha sherehe mbili za Eid na kuwataka wasomaji wa barua pepe hiyo kuigomea hiyo stempu, huku ikiorodhesha mashambulizi ya kigaidi yalifonywa nchini Marekani katika kipindi cha miaka ishirini iliyopita. Maandishi ya hiyo barua pepe yanaonekana kwenye <a href="http://missivesfrommarx.wordpress.com/2009/09/20/this-stuff-makes-me-sick/#comment-1096">makala hii</a> ya <em>Missives from Marx</em>, ambaye anaelezea kughafirika kwake kulikotokana na barua hiyo:</p>
<blockquote><p>Nilipokea barua pepe ifuatayo leo kutoka kutoka kwa ndugu yangu. Kutokana na mambo kama haya  ndiyo maana nitazitumia wiki nne za mafunzo yangu ya dini (Western Religious Course) kuzisambaratisha imani potofu juu ya Uislamu. Ndio maana uchambuzi yakinifu ni lazima uwe sehemu muhimu ya masomo yangu.</p></blockquote>
<p>Na kama ilivyoondokea, hakuna jipya kuhusu hii barua, au stempu. <a href="http://urbanlegends.about.com/library/bl-muslim-stamp.htm">About.com</a> inafafanua kuwa barua hii imekuwepo tangu mwaka 2002, wakati stempu yenyewe ilitolewa tarehe 1, Septemba 2001.</p>
<p>Aziz Poonwalla, katika blogu ya <em>City of Brass</em> kwenye BeliefNet  <a href="http://blog.beliefnet.com/cityofbrass/2009/09/terror-mail-the-eid-stamp.html">anafafanua</a> habari ya hii barua pepe:</p>
<blockquote><p>Matoleo ya hiyo barua pepe, ambayo yamekuwa yakizungushwa kwa miaka kadhaa, <a href="http://www.snopes.com/politics/stamps/eidstamp.asp">yameshachambuliwa</a> lakini bado yanaendelea kusambazwa. Nimeblogu kwa kirefu kuhusu <a href="http://cityofbrass.blogspot.com/2007/10/eid-stamp.html">historia ya stempu hiyo</a> ya Eid, utata uliombatana nayo wakati ilipotolewa (hasa kutoka kwa wahafidhina wa chama cha Republicans), na utetezi wa stempu hiyo uliofanywa na Rais Bush pamoja na Spika Hastert. Kwa kifupi, stempu hiyo ilitolewa tarehe 1 Septemba 2001, siku kumi kabla ya mashambulizi ya 9-11, wakati wa serikali ya Bush. Meya Piper anajiunga na orodha ndefu ya wanasiasa wahafidhina ambao hawana pingamizi na stempu zinazoadhimisha sikukuu za Hanukkah, Kwanzaa, na hata mwaka mpya wa Kichina – bali stempu iliyotolewa kwa ajili ya sikukuu ya Kiislamu ya Eid imetengwa kama tishio, na kuwataka Wamarekani wazalendo waiwajibikie?</p></blockquote>
<p><a href="http://www.clarksvilleonline.com/2009/09/04/the-mayors-anti-islamic-email-is-a-major-embarrassment/">Makala</a> kwenye <em>Clarksville Online</em>, blogu ya mji wa Clarkstown, Tennessee, inaelezea ni kwa nini hii barua pepe imesababisha vichwa vikubwa vya habari mwaka huu:</p>
<blockquote><p>
Meya wa Clarksville Tennessee, Johnny Piper ametuma barua pepe ya kichochezi inayopinga Uislamun kwa wafanyakazi wa mji huo, inayowaasa waisusie hiyo stempu iliyotolewa na husduma ya posta ya Marekani…</p>
<p>… Meya Piper anajaribu kutetea vitendo yake, lakini vitendo hivyo ni vigumu kutetewa. Waislamu ni sehemu mojawapo ya nchi hii. Wanatumikia kiadilifu kwenye majeshi yetu ya ulinzi, wanalilinda taifa, na uhuru wetu. Hakuna mtu nayepaswa kuchukuliwa kama raia wa tabaka la pili kwa misingi ya imani yake ya kidini, au kutokana na vitendo vya watu wenye siasa kali wachache. Tukio hili lililotengenezwa na Meya wetu limekuwa ni aibu kwa mji wetu, jimbo, na nchi yetu.</p></blockquote>
<p>Sheila Musaji amekuwa akifuatilia mzunguko wa barua pepe hiyo inayohusu stempu kwa ajili ya jarida la <em>The American Muslim (TAM)</em> tangu mwaka 2005, na katika moja ya habari zake, <a href="http://theamericanmuslim.org/tam.php/features/articles/through_the_looking_glass_eid_stamp_continues_to_provoke_religious_right/">anatoa maoni</a> juu ya vitendo vichafu vya Meya Piper:</p>
<blockquote><p>Nina hakika kuwa Meya wetu mzuri alishangazwa na <a href="http://www.theamericanmuslim.org/tam.php?URL=http%3A%2F%2Fwww.theamericanmuslim.org%2Ftam.php%2Ffeatures%2Farticles%2Fwhite_house_iftar%2F0017527">ghafla ya iftar iliyofanywa na Obama kwenye Ikulu ya Marekani</a>.</p>
<p>Na, kama ilivyo kawaida maneno ya mwisho ya wabaguzi wote huwa: <em>‘nina marafiki kasha wa Kiislamu,” aliongeza.”</em></p>
<p>Pengine marafiki hao wazuri wa Kiislamu wanaweza kumuelimisha ni kwa nini makala <a href="http://www.theamericanmuslim.org/tam.php?URL=http%3A%2F%2Fwww.theleafchronicle.com%2Fassets%2Fpdf%2FDA14202394.PDF">HII</a> (PDF) inagadhabisha.</p></blockquote>
]]></content:encoded>
			<wfw:commentRss>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/09/marekani-stempu-ya-iddi-yachochea-chuki-huko-tennessee/feed/</wfw:commentRss>
		<slash:comments>0</slash:comments>
		</item>
		<item>
		<title>Irani: Mwaka Mpya Waanza na Ujumbe Kutoka Kwa Obama</title>
		<link>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/04/irani-mwaka-mpya-waanza-na-ujumbe-kutoka-kwa-obama/</link>
		<comments>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/04/irani-mwaka-mpya-waanza-na-ujumbe-kutoka-kwa-obama/#comments</comments>
		<pubDate>Fri, 10 Apr 2009 07:17:32 +0000</pubDate>
		<dc:creator>j nambiza tungaraza</dc:creator>
				<category><![CDATA[Americas]]></category>
		<category><![CDATA[Arts & Culture]]></category>
		<category><![CDATA[Farsi]]></category>
		<category><![CDATA[Governance]]></category>
		<category><![CDATA[International Relations]]></category>
		<category><![CDATA[Iran]]></category>
		<category><![CDATA[Middle East & North Africa]]></category>
		<category><![CDATA[Politics]]></category>
		<category><![CDATA[U.S.A.]]></category>
		<category><![CDATA[Video]]></category>
		<category><![CDATA[Weblog]]></category>

		<guid isPermaLink="false">http://sw.globalvoicesonline.org/?p=106</guid>
		<description><![CDATA[Siku Wairani waliposherehekea Norouz (Nowruz) kama sikukuu ya mwaka mpya nchini Irani, raisi wa Marekani Barak Obama alituma ujumbe kwa watu wa Irani na kwa viongozi wa Jamhuri ya kiislamu, ujumbe huo ulitoa rai ya kutaka mwanzo mpya kati ya nchi hizo mbili. Wanablogu kadhaa wametoa maoni kuhusu ujumbe huo, angalia baadhi ya maoni hayo.]]></description>
			<content:encoded><![CDATA[<em>Ilichapwa kwanza na<a href="http://globalvoicesonline.org/author/hamid-tehrani/">Hamid Tehrani</a>  &middot; Imetafsiriwa na <a href='http://sw.globalvoicesonline.org/author/j-nambiza-tungaraza/'>j nambiza tungaraza</a> &middot;  <a href='http://globalvoicesonline.org/2009/04/06/iran-the-new-year-starts-with-a-message-from-obama/'>Angalia ujumbe mama</a></em> 
<br /><p><img alt="" src="http://globalvoicesonline.org/wp-content/uploads/2009/03/norouz.jpg" class="aligncenter" width="400" height="378" /></p>
<p>Mwaka huu, sherehe za mwaka mpya wa Ki-Irani zilianza na ujumbe usiotarajiwa kutoka kwa rais wa Marekani Barak Obama, uliolekezwa kwa watu wa Irani na kwa mara ya kwanza, kwa viongozi wa Jamhuri ya Kiislamu, ujumbe huo ulitoa rai ya kuanza upya kati ya nchi hizo mbili. Wanablogu kadhaa wametoa maoni kuhusu ujumbe huo, na wengine wanaanza kuziona zama mpya baada ya zaidi ya miaka 30 ya misukosuko kati ya mataifa haya mawili.</p>
<p><object width="425" height="344"><param name="movie" value="http://www.youtube.com/v/0ee0wrjVtkk&#038;color1=0xb1b1b1&#038;color2=0xcfcfcf&#038;hl=cs&#038;feature=player_embedded&#038;fs=1"></param><param name="allowFullScreen" value="true"></param><embed src="http://www.youtube.com/v/0ee0wrjVtkk&#038;color1=0xb1b1b1&#038;color2=0xcfcfcf&#038;hl=cs&#038;feature=player_embedded&#038;fs=1" type="application/x-shockwave-flash" allowfullscreen="true" width="425" height="344"></embed></object></p>
<p><em>Mohammad Ali Abtahi,</em> makamu wa rais wa zamani, anadhani ujumbe wa Obama ni wa muhimu sana na <a href="http://www.webneveshteha.com/en/weblog/?id=2146309980">anaandika:</a></p>
<blockquote><p>Kwa jina la jamhuri ya Kiislamu ya Irani, pia nawapongeza taifa la Irani na viongozi wake. Bila ya shaka hii ni fursa ya kihistoria. Hatuwezi kudharau umuhimu wa Marekani katika hali ya sasa ya Irani. Bila ya shaka hatuwezi kupuuza nyayo za Marekani katika kila majalada ya wasifu wa Irani hasa yale ya kiuchumi hata kama ni kwa uchache, kutokana na vikwazo vilivyowekwa dhidi ya taifa la Irani. Kutuma ujumbe wa pongezi kunaweza kuwa ni fursa muhimu kisiasa, kiuchumi na kihistoria, leo hii na hata baada ya kubadilishwa serikali ya Marekani.  Kadhalika kupuuza kunaweza kuifanya hali izidi kuwa ya hatari zaidi ya ilivyokuwa wakati wa utawala wa Bush kwa sababu Obama anaweza kukusanya viongozi wa kisiasa na maoni ya wananchi dhidi ya Irani.</p></blockquote>
<p>Mwanablogu ambaye pia ni mwanahabari <em>Masih Alinejad </em><a href="http://masihalinejad.com/?p=304">anaandika</a> [fa] kuhusu sababu zilizoifanya Idhaa ya Taifa ya Televisheni kutotangaza ujumbe wa Obama. Anaongeza:</p>
<blockquote><p>kama Obama angeongea kama Bush na kuitathmini Irani kama tishio, Idhaa ya Televisheni ya Taifa ingetangaza mara kadhaa. Mwanablogu huyu anatukumbusha ile hotuba ya mashuhuri ya Bush ambayo aliita Irani mwanachama wa kundi la waovu ilitangazwa mara kadhaa kwenye televisheni ya taifa.</p></blockquote>
<p><em>Zandgieh Sagi </em><a href="http://zendegisagi.com/">ameuita</a> [fa] ujumbe wa Obama kama ujumbe chanya na jambo ambalo linawastahili watu wa Irani. Mwanablogu huyu anasema kuwa jambo la kwanza ambalo serikali ya Irani inaweza kulifanya ni kutumia lugha inayofaa kisiasa.</p>
<p>Katika blogu ya <em>In View from Iran </em><a href="http://viewfromiran.blogspot.com/2009/03/obamas-norouz-message.html">tunasoma</a>:</p>
<blockquote><p>Kuna hatua nyingi ambazo serikali ya Marekani inaweza kuzichukua ili kujenga imani. Siyo zote ambazo zitategemea nia ya serikali ya Irani ya kuanzisha mazungumzo na Marekani. Nauona ujumbe wa Obama wa mwaka mpya kama ujumbe chanya, lakini tunahitaji zaidi ya hilo.</p></blockquote>
<p><em>Mmoeeni </em><a href="http://mmoeeni.blogspot.com/2009/03/blog-post_3630.html">anaandika</a> [fa] kwamba wakati televisheni ya Irani haikutangaza habari zinazohusu ujumbe wa Obama, rais wa Irani aliweza kuwatukana viongozi wa Marekani huko Marekani. Mwanablogu huyo anaongeza, kwa kejeli, kwamba Ahmedinejad atasema kwamba kuna uhuru wa kweli nchini Irani.</p>
<p><strong>Sherehe za Mwaka Mpya</strong><br />
Wairani walisherehekea Norouz (Nowruz) kunako siku ya kwanza ya msimu wa kuchipuka mimea. Katika dhifa hii, baadhi ya Wairani huweka maua kwenye kaburi la <a href="http://en.wikipedia.org/wiki/Cyrus_the_Great">Cyrus Mkuu</a>, mwanzilishi wa ufalme wa kwanza wa Persia katika <a href="http://en.wikipedia.org/wiki/Pasargad">Pasargad</a> (pichani juu). Kwenye tovuti ya <em>Okoa Pasargad </em><a href="http://www.savepasargad.com/2009-March/Nowruz/Nowruz-dar%20pasargad.htm">imeandikwa</a> [fa] kwamba utawala wa jamhuri ya Kiislamu hausaidii wageni wanaozuru sehemu hii ya kihistoria, lakini katika miaka ya hivi karibuni watu wengi wamekuwa wakizuru ili kuusherekea mwaka mpya huko Pasargad.</p>
]]></content:encoded>
			<wfw:commentRss>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/04/irani-mwaka-mpya-waanza-na-ujumbe-kutoka-kwa-obama/feed/</wfw:commentRss>
		<slash:comments>0</slash:comments>
		</item>
		<item>
		<title>Clinton Azuru Indonesia</title>
		<link>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/02/clinton-azuru-indonesia/</link>
		<comments>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/02/clinton-azuru-indonesia/#comments</comments>
		<pubDate>Thu, 26 Feb 2009 13:59:57 +0000</pubDate>
		<dc:creator>j nambiza tungaraza</dc:creator>
				<category><![CDATA[East Asia]]></category>
		<category><![CDATA[English]]></category>
		<category><![CDATA[Governance]]></category>
		<category><![CDATA[Indonesia]]></category>
		<category><![CDATA[International Relations]]></category>
		<category><![CDATA[Politics]]></category>
		<category><![CDATA[U.S.A.]]></category>
		<category><![CDATA[Weblog]]></category>

		<guid isPermaLink="false">http://sw.globalvoicesonline.org/?p=79</guid>
		<description><![CDATA[Pamoja na kukutana na viongozi wa Indonesia, Katibu wa Mambo ya Nje wa Marekani, Hillary Clinton alipata muda wa kutembelea makazi ya watu masikini mjini Jakarta. Kadhalika alitokea kwenye kipindi cha televisheni cha vijana. Ni nini maoni ya wanablogu?]]></description>
			<content:encoded><![CDATA[<em>Ilichapwa kwanza na<a href="http://globalvoicesonline.org/author/mong/">Mong Palatino</a>  &middot; Imetafsiriwa na <a href='http://sw.globalvoicesonline.org/author/j-nambiza-tungaraza/'>j nambiza tungaraza</a> &middot;  <a href='http://globalvoicesonline.org/2009/02/20/clinton-visits-indonesia/'>Angalia ujumbe mama</a></em> 
<br /><p>Katibu wa Mambo ya Nje wa Marekani Hillary Clinton aliwasili nchini Indonesia Jumatano iliyopita. <a href="http://www.thejakartapost.com/news/2009/02/19/us-ri-pledge-closer-comprehensive-ties.html">Alitilia mkazo</a>  &#8220;jukumu la Indonesia katika kudhibiti matatizo ya dunia, yanayojumuisha ugaidi, uchumi wa kujihami, mabadiliko ya hali ya hewa(kuongezeka kwa joto) na matatizo ya kiuchumi.&#8221; Indonesia ndio taifa kubwa la Kiislamu duniani na nchi ya tatu kwa ukubwa kati ya zile zinazoongozwa kidemokrasia.</p>
<p>Pamoja na  kukutana na viongozi wa Indonesia, Clinton alipata muda wa kutembelea <a href="http://indosnesos.blogspot.com/2009/02/clinton-cheered-in-visit-to-indonesian.html">makazi ya watu masikini mjini</a> Jakarta. Kadhalika alitokea kwenye <a href="http://indosnesos.blogspot.com/2009/02/clinton-talks-with-teens-on-local.html">kipindi cha televisheni cha vijana</a>.</p>
<p><object width="425" height="344"><param name="movie" value="http://www.youtube.com/v/PgAjAY6ERiI&#038;color1=0xb1b1b1&#038;color2=0xcfcfcf&#038;hl=en&#038;feature=player_embedded&#038;fs=1"></param><param name="allowFullScreen" value="true"></param><embed src="http://www.youtube.com/v/PgAjAY6ERiI&#038;color1=0xb1b1b1&#038;color2=0xcfcfcf&#038;hl=en&#038;feature=player_embedded&#038;fs=1" type="application/x-shockwave-flash" allowfullscreen="true" width="425" height="344"></embed></object></p>
<p>Bloga <em>Everything Indonesia</em> <a href="http://everythingindonesia.blogspot.com/2009/02/hillary-in-jakarta-lovefest-begins.html">anaamini</a> kuwa ziara ya Clinton nchini Indonesia inafungua zama mpya ya sera ya nje ya Marekani:</p>
<blockquote><p>Ziara ya katibu wa Mambo ya Nje wa Marekani Clinton nchini Indonesia inafungua zama mpya za sera ya nje ya Marekani. Sera iliyopungua dharau, inayojumuisha zaidi kama inavyoitwa nguvu-zenye-akili.</p></blockquote>
<p>Bloga Mbak Rita amegundua kwamba <a href="http://mbakrita.wordpress.com/2009/02/19/kompas-and-jurnas/">Clinton anaonekana kijana sana leo</a>:</p>
<blockquote><p>&#8220;kwa kweli nafikiri anaonekana kijana na mrembo, pengine inatokana na tabasamu lake alilotoa wakati wa ziara yake hapa… Watu wengine katika kipindi cha maongezi cha televisheni nilichokitaja kabla walisema kwamba watu wa Jakarta walijawa jazba za bure kuhusu ziara yake. Nafarijika kuwa nilikosea.&#8221;</p></blockquote>
<p>Devi Girsang <a href="http://devigirsang.blogspot.com/2009/02/snapshots-of-hillary-clintons-arrival.html">alishangazwa</a> na hali ya barabarani siku aliyowasili Clinton:</p>
<blockquote><p>Kama mkazi wa Jakarta niliyozoea kukwama kwenye foleni za magari, huwa nafadhaika kama barabara zikiwa tulivu na zenye watu pungufu. Ni mambo mawili yaliyoingia akilini mwangu; kuna vitisho vya mabomu au ghasia. Unakumbuka machafuko ya Jakarta ya mwaka 1998 au shambulio la Hoteli ya Marriot la mwaka 2003? Umeshahamu namaanisha nini</p>
<p>Majira ya saa 8 za mchana leo, iliondokea kuwa ni kuwasili kwa Katibu wa Mambo ya Nje wa Marekani mjini Jakarta ndio kulikosimamisha magari. Bahati yangu nilikuwa bado nina mawe kwenye kamera yangu ya kidijitali nikaweza kupiga picha kadhaa.</p></blockquote>
<p>Katika safu ya maoni, <a href="http://devigirsang.blogspot.com/2009/02/snapshots-of-hillary-clintons-arrival.html">Therry</a>, anajiuliza kama Marekani ilimtuma Clinton wa uongo:</p>
<blockquote><p>Niliangalia hotuba aliyoitoa Clinton kwenye televisheni na sina hakika kama ni mimi tu, lakini yule mwanamke hafanani na Hillary.</p>
<p>Naanza kufikiri kuwa serikali ya Marekani ilimtumia Clinton wa uongo, kwa sababu yule mwanamke anaonekana mzee sana na jimama kuwa Clinton wa kweli.</p></blockquote>
<p><img alt="" src="http://globalvoicesonline.org/wp-content/uploads/2009/02/clinton1.jpg" class="alignnone" width="413" height="281" /><br />
<em>Siyo kila mmoja aliyeshangilia ziara ya Hillary Clinton nchini Indonesia. Picha kutoka kwa <a href="http://jakartanews-update.tumblr.com/post/79223596/welcoming-message-from-kids-to-hillary-clinton">Jakarta Today</a>.</em></p>
<p>Andreas Harsono alitaka Clinton <a href="http://andreasharsono.blogspot.com/2009/02/clintons-chance-to-push-beyond-cliches.html">aongelee masuala </a>ya uhuru wa kidini, usawa katika sheria na mageuzi ya kijeshi wakati wa ziara yake:</p>
<blockquote><p>&#8220;(Clinton) awe muangalifu na asiseme kuwa Waislamu wa Indonesia wana &#8220;siasa za wastani&#8221; kama wanavyosema wanadiplomasia wageni. Kwa wanachama wa makundi ya kidini yanayokandamizwa nchini Indonesia, tamko hilo halina maana na ni kauli mbiu potofu.</p>
<p>&#8220;Mashaka ya ongezeko la kutokuvumiliana kidini sio suala pekee ambalo Clinton angeliongelea na Rais Susilo Bambang Yudhoyono. Uhuru wa kujieleza pia ni tatizo kubwa katika visiwa vidogo ambako makabila madogo yanaonyesha upinzani kwa dola ya Indonesia. Katika Indonesia, hata vitendo vya amani kama vile kupandisha bendera vinaweza kukupeleka jela kwa muda mrefu.</p>
<p>Clinton anaweza kushawishika kupamba masuala kama uhuru wa kidini, usawa katika sheria na mageuzi ya kijeshi ili kuboresha uhusiano wa Marekani na Indonesia. Na kama akifanya hivyo, atapoteza fursa ya kubadilisha maisha ya watu wengi nchini Indonesia ambao wanataka serikali  ishinikizwe kutambua haki zao.</p></blockquote>
<p>Kupitia huduma ya Twita yafuatayo ni maoni yanayohusu ziara ya Clinton:</p>
<blockquote><p><a href="http://twitter.com/waxinglyrical/statuses/1225412528">waxinglyrical:</a> kuna mtu ameuliza hillary Clinton ni nani?</p>
<p><a href="http://twitter.com/mirageinblue/statuses/1225228545">mirageinblue</a>: Nimemuona hillary clinton mapokezi. Safi sana</p>
<p><a href="http://twitter.com/oplet/statuses/1225013899">oplet</a>: Klabu ya mashabiki wa Obama wanafanya maandamano kumopinga Hillary Clinton mjini Jakarta, wanasema hawampendi tangu wakati wa kugombea nafasi ya kugombea urais.</p></blockquote>
<p><img alt="" src="http://globalvoicesonline.org/wp-content/uploads/2009/02/clinton2.jpg" class="alignnone" width="350" height="234" /><br />
<em>Picha kutoka ukurasa wa Flickr wa Idara ya Mambo ya <a href="http://flickr.com/photos/statephotos/3290368997/">Nje ya Marekani</a></em></p>
]]></content:encoded>
			<wfw:commentRss>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/02/clinton-azuru-indonesia/feed/</wfw:commentRss>
		<slash:comments>0</slash:comments>
		</item>
		<item>
		<title>Misri: Wanablogu Wafuatilia Milipuko ya Mabomu Mjini Kairo</title>
		<link>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/02/misri-wanablogu-wafuatilia-milipuko-ya-mabomu-mjini-kairo/</link>
		<comments>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/02/misri-wanablogu-wafuatilia-milipuko-ya-mabomu-mjini-kairo/#comments</comments>
		<pubDate>Thu, 26 Feb 2009 03:46:44 +0000</pubDate>
		<dc:creator>j nambiza tungaraza</dc:creator>
				<category><![CDATA[Breaking News]]></category>
		<category><![CDATA[Disaster]]></category>
		<category><![CDATA[Egypt]]></category>
		<category><![CDATA[English]]></category>
		<category><![CDATA[Feature]]></category>
		<category><![CDATA[France]]></category>
		<category><![CDATA[Middle East & North Africa]]></category>
		<category><![CDATA[Politics]]></category>
		<category><![CDATA[Travel]]></category>
		<category><![CDATA[U.S.A.]]></category>
		<category><![CDATA[Weblog]]></category>

		<guid isPermaLink="false">http://sw.globalvoicesonline.org/?p=76</guid>
		<description><![CDATA[Mtalii wa Kifaransa ameuwawa na watu wapatao 20 wamejeruhiwa wakati bomu lilipolipuka nje ya msikiti wa Al Hussein uliopo katika eneo la utalii la Khan Al Khalili mjini Kairo. Na wakati dunia ilipokuwa inaanza kufahamu ni kipi kilichokuwa kinatokea, wanablogu wa Misri waliingia kazini haraka, wakipashana habari za yanayotukia, taarifa, uchambuzi na hofu zao.]]></description>
			<content:encoded><![CDATA[<em>Ilichapwa kwanza na<a href="http://globalvoicesonline.org/author/lasto-adri/">Lasto Adri</a>  &middot; Imetafsiriwa na <a href='http://sw.globalvoicesonline.org/author/j-nambiza-tungaraza/'>j nambiza tungaraza</a> &middot;  <a href='http://globalvoicesonline.org/2009/02/22/egypt-bloggers-react-to-cairo-bombings/'>Angalia ujumbe mama</a></em> 
<br /><p></a>Mtalii wa Kifaransa <a href="http://english.aljazeera.net/news/middleeast/2009/02/2009222175234931911.html">ameuwawa</a> na watu wapatao 20 wamejeruhiwa wakati bomu lilipolipuka nje ya <a href="http://www.answers.com/Al%20Hussein%20Mosque">msikiti wa Al Hussein</a> uliopo katika eneo la utalii la <a href="http://www.answers.com/Khan%20Al%20Khalili">Khan Al Khalili</a> mjini Kairo mapema leo.</p>
<p>Na wakati dunia ilipokuwa inaanza kufahamu ni kipi kilichokuwa kinatokea, wanablogu wa Misri waliingia kazini haraka, wakipashana habari za yanayotukia, taarifa, uchambuzi na hofu zao.</p>
<p>Yote yalianza wakati <a href="http://twitter.com/Zeinobia/status/1237624709"><em>Zenobia</em></a> alipotundika ujumbe katika ukurasa wa Twita akiripoti kuwa “Kumetokea mlipuko wa aina fulani kwenye mgahawa uliopo Al Azhar.” Dakika chache baadaye <a href="http://twitter.com/3arabawy/status/1237645532"><em>Arabawy</em></a> alifuatia na ujumbe mwingine uliothibitisha: “Mlipuko katika mtaa wa el-mashhad el-Husseini mjini Kairo.”</p>
<p><img alt="" src="http://globalvoicesonline.org/wp-content/uploads/2009/02/moftasa-300x131.png" class="aligncenter" width="300" height="131" /></p>
<p><a href="http://twitter.com/moftasa/status/1237694368"><em>Moftasa</em></a> ndiye alikuwa wa kwanza kuuhisi uhusiano wa milipuko na sheria mpya ya kuzuia-ugaidi, ambayo itajadiliwa katika siku chache zijazo kwenye bunge la Misri. Rasimu ya sheria hiyo imekumbana na vipingamizi vikubwa.</p>
<p>Hakuna lililothibitishwa mpaka sasa, na uvumi unaenea; hata hivyo, <em>Zeinobia </em>alijaribu <a href="http://egyptianchronicles.blogspot.com/2009/02/breaking-news-blast-in-al-hussein.html">kukusanya habari kama zinavyotokea kutoka vyanzo tofauti vya magazeti na idhaa za televisheni </a>katika muhtasari. </p>
<p>Mwanablogu <a href="http://arabist.net/archives/2009/02/22/report-explosion-in-cairo/"><em>Arabist</em></a>, ambaye alikuwa Karibu na eneo na kuusikia mlipuko huo yeye mwenyewe, aliandika:</p>
<blockquote><p>Nimesikia taarifa za mabomu yanayolipuka katika mji mkongwe wa Kairo Karibu na Khan al-Khalili, sehemu maarufu kwa watalii. Nitawapasha kadri habari zitakapopatikana.</p>
<p>Habari mpya: Al Jazeera inaripoti <del datetime="2009-02-26T03:13:58+00:00">vifo 11, Wamisri watatu, Wajerumani watatu, Mfaransa mmoja,</del> 16 wamejeruhiwa, Mfaransa mmoja amefariki, haya na mengineyo bado hayajathibitishwa.</p>
<p>Habari mpya 2: Tayari wanaharakati wanasema kuwa tukio hili limetukia Karibu sana na mwezi ujao ambapo Sheria ya Dharura itajadiliwa Bungeni…</p>
<p>Habari mpya 3: Wanne wamefariki (Wajerumani na Wafaransa) 12 wamejeruhiwa, wa mataifa mbalimbali.</p></blockquote>
<p>Halafu <a href="http://twitter.com/moftasa/status/1237863455"><em>moftasa</em></a> alibandika kiungo cha picha kutoka kwenye eneo la mlipuko kwenye Twita.</p>
<p>Wakati <a href="http://egypt4.wordpress.com/"><em>Msfour</em></a>, mfanyakazi wa Kimarekani anayeishi Kairo, <a href="http://twitter.com/msfour/status/1237956556">alikuwa wa kwanza kuwataka wanablogu wanaotumia Twita</a> kutumia kielelezo cha <a href="http://search.twitter.com/search?q=%23cairobomb">#cairobomb</a>, <em>Arabawy</em> ndiye <a href="http://twitter.com/3arabawy/status/1237819035">alikuwa wa kwanza kuwataka wanablogu watumie kielelezo jumuishi cha delicious</a>: <em>El-HusseinExplosion</em> ili kukusanya viunganishi vyote chini ya <a href="http://delicious.com/tag/El-HusseinExplosion">anwani pepe moja</a>.</p>
<p>Wanablogu <a href="http://www.gaberism.net/2009/02/22/explosion-in-cairo/"><em>Yassary Masry </em></a>[Ar], <a href="http://carlincairo.blogspot.com/2009/02/explosion-at-khan.html"><em>Carl</em>, <a href="http://egypt4.wordpress.com/2009/02/22/we-are-fine/"><em>Msfour</em></a>, <a href="http://egytimes.org/2009/02/fuck-terrorism/"><em>Maree</em></a>, <a href="http://arabicsource.wordpress.com/2009/02/22/blast-in-cairo/"><em>Rob</em></a>, <a href="http://www.sandmonkey.org/2009/02/22/terrorist-attack-in-cairo/"><em>SandMonkey</em></a> pamoja na <a href="http://www.greywoolknickers.net/?p=178"><em>Grey wool Knickers </em></a>walikuwa ni miongoni mwa wanablogu wa kwanza kuandika kuhusu tukio hilo, ama kuwafariji marafiki na familia au kujadili uhusiano wa milipuko ya mabomu na sheria ya kuzuia ugaidi. <a href="http://www.greywoolknickers.net/?p=178"><em>Grey wool Knickers </em></a>aliandika ujumbe mfupi unaohusianisha matukio ya mwisho yaliyotokea Misri, akijaribu kuyaunganisha na milipuko ya hivi karibuni: </p>
<blockquote><p>Kama <a href="http://moftasa.jaiku.com/presence/54233060">watu</a> <a href="http://arabist.net/arabawy/2009/02/22/explosion-in-al-azhar-area/">kadhaa</a> wanavyoona, matukio haya yametokea katika wakati wa kushuku, tukizingatia kwamba <a href="http://www.fidh.org/spip.php?article1397">Sheria ya Dharura</a> (iliyokuwepo tangu mwaka 1967 wakati wa vita vya Waarabu-na-Waisraeli, vilivyositishwea kwa muda wakati wa utawala wa Rais Sadat) ilitaka kuanzishwa tena. Serikali ya Rais Mubarak <a href="http://www.arabicnews.com/ansub/Daily/Day/050818/2005081819.html">imekuwa ikiahidi kwa miaka mingi</a> kuanzisha sheria ya kuzuia ugaidi ambayo ingechukua nafasi ya sheria za kijeshi, ambayo ingewapa raia angalau kinga kidogo kwenye katiba ya Misri.  Utawala wa sasa unao uwezo wa kurejesha Sheria ya Dharura na kutenda inavyotaka, kama wasomaji watakavyogundua katika <a href="http://www.greywoolknickers.net/?p=143">kutekwa kwa Philip Rizk</a> na <a href="http://prisonersforgaza.wordpress.com/">Diaa Gad</a>, kati yaw engine wengi. Huku kukiwa na matarajio ya mabadiliko katika serikali za Marekani na Israeli – pamoja na makundi ya upinzani yenye sauti na yaliyo mitandao ya ndani na ile inayovuka mipaka na kuingia Gaza – inaonekana kuwa utawala unaozeeka wa Mubarak unaanza kuingiwa na kihoro na kujikuta una machaguo machache ya kuendeleza mshiko wake madarakani isipokuwa kwa kutumia <a href="http://en.wikipedia.org/wiki/Strategy_of_tension">mikakati ya kuongeza hali ya vuguvugu</a>. Nafikiri <a href="http://globalvoicesonline.org/2009/02/22/2009/02/19/egypt-ayman-nour-released/">kuachiwa kwa mfungwa wa kisiasa Ayman Nour hivi karibuni </a>kunaweza kuwa ni ushahidi wa mchechetu unaozikumba ngazi za juu za utawala huu wa kiimla. Ili kupata habari kama zinavyotukia, angalia <a href="http://delicious.com/tag/El-HusseinExplosion">ukurasa huu wa delicious</a>.</p></blockquote>
<p>Mpaka wakati makala hii ilipokuwa ikiandikwa imethibitishwa kwamba msichana wa Kifaransa mwenye umri wa miaka 21 ameuwawa, na watu wengine wapatao 20 wa mataifa mbalimbali wamejeruhiwa. Hata hivyo, bado ni mapema mno kurukia hitimisho la ni nani aliyehusika na milipuko.</p>
<p>Picha zinaweza kupatikana katika <a href="http://yalally.blogspot.com/2009/02/blog-post_22.html">blogu ya AbdelFatah</a> na wasomaji wanaweza kuwafuatilia wanablogu wa Misri kwenye twita <a href="http://search.twitter.com/search?q=%23cairobomb">hapa</a>.</p>
]]></content:encoded>
			<wfw:commentRss>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/02/misri-wanablogu-wafuatilia-milipuko-ya-mabomu-mjini-kairo/feed/</wfw:commentRss>
		<slash:comments>0</slash:comments>
		</item>
	</channel>
</rss>
