Habari maalum kuhusu U.S.A.
2009-10-25
Marekani: Wanandoa wa rangi tofauti wanyimwa cheti cha ndoa
Juma lililopita huko Hammond, Louisiana, wapenzi wawili walituma maombi ya kibali cha kufunga ndoa na walikataliwa kwa misingi ya rangi zao tofauti. Afisa wa kutathmini na kuandikisha nyaraka (Muamuzi wa Amani) alidai kuwa “ndoa baina ya watu wa rangi hazidumu” na alisema kuwa anafanya hivyo “kwa ajili ya watoto.”
2009-04-10
Irani: Mwaka Mpya Waanza na Ujumbe Kutoka Kwa Obama
Siku Wairani waliposherehekea Norouz (Nowruz) kama sikukuu ya mwaka mpya nchini Irani, raisi wa Marekani Barak Obama alituma ujumbe kwa watu wa Irani na kwa viongozi wa Jamhuri ya kiislamu, ujumbe huo ulitoa rai ya kutaka mwanzo mpya kati ya nchi hizo mbili. Wanablogu kadhaa wametoa maoni kuhusu ujumbe huo, angalia baadhi ya maoni hayo.
2009-02-26
Misri: Wanablogu Wafuatilia Milipuko ya Mabomu Mjini Kairo
Mtalii wa Kifaransa ameuwawa na watu wapatao 20 wamejeruhiwa wakati bomu lilipolipuka nje ya msikiti wa Al Hussein uliopo katika eneo la utalii la Khan Al Khalili mjini Kairo. Na wakati dunia ilipokuwa inaanza kufahamu ni kipi kilichokuwa kinatokea, wanablogu wa Misri waliingia kazini haraka, wakipashana habari za yanayotukia, taarifa, uchambuzi na hofu zao.
2009-02-15
Haiti: Fanmi Lavalas na Uchaguzi Ujao
Mwishoni mwa juma lililopita, ulimwengu wa wanablogu wa Kihaiti ulijaa habari za kutengwa kwa vyama vya siasa na Tume ya Muda ya Uchaguzi kwenye uchaguzi wa maseneta utakaofanyika mwezi Aprili 2009 , na siku ya tarehe 6 Januari, tume hiyo CEP ilichapisha orodha ya wagombea ubunge watakaokwaana kwenye uchaguzi ujao wa bunge nchini Haiti. Wanablogu wanaandika mawazo yao kuhusu wagombea walioachwa.
2009-02-02
Mashariki ya Kati: Vikwazo kama Silaha ya Kisiasa
Watu wengi wa Mashariki ya Kati wamesusia bidhaa za Israeli na Marekani kama jibu la mashambulizi ya Israeli huko Gaza. Tarek Amr anapitia yale wanablogu wanayosema kuhusu suala hili.
2009-01-26
MENA: Maoni Wakati Wa Kuapishwa Obama
Tukio la kihistoria limetokea Marekani leo wakati Barack Obama alipoapishwa kuwa rais wa 44. Wakati kuungwa mkono kwa Obama kati ya Waarabu kumekuwa kukipungua katika miezi michache iliyopita kufuatia uteuzi wake wa baraza la mawaziri na ukimya wake kuhusu mashambulio ya Israeli huko Gaza, wanablogu wa Mashariki ya Kati na ...
2008-11-09
Iraki:OBAMAAAAA!!! Huraaah Oyee!!
Hivyo ndivyo asemavyo Neurotic Iraqi Wife. Kwa ujumla blogu nyingi za Iraki zimemchukulia vyema rais mteule Obama, lakini sio wanablogu wote waliofurahia. Salam Adil anaorodhesha maoni baada ya Uchaguzi wa rais huko Marekani.







