<?xml version="1.0" encoding="UTF-8"?>
<rss version="2.0"
	xmlns:content="http://purl.org/rss/1.0/modules/content/"
	xmlns:wfw="http://wellformedweb.org/CommentAPI/"
	xmlns:dc="http://purl.org/dc/elements/1.1/"
	xmlns:atom="http://www.w3.org/2005/Atom"
	xmlns:sy="http://purl.org/rss/1.0/modules/syndication/"
	xmlns:slash="http://purl.org/rss/1.0/modules/slash/"
	>

<channel>
	<title>Global Voices in Swahili &#187; Chile</title>
	<atom:link href="http://sw.globalvoicesonline.org/category/world/americas/chile/feed/" rel="self" type="application/rss+xml" />
	<link>http://sw.globalvoicesonline.org</link>
	<description>Dunia inaongea, je unasikiliza?</description>
	<lastBuildDate>Wed, 02 Dec 2009 12:35:07 +0000</lastBuildDate>
	<generator>http://wordpress.org/?v=2.8.4</generator>
	<language>en</language>
	<sy:updatePeriod>hourly</sy:updatePeriod>
	<sy:updateFrequency>1</sy:updateFrequency>
			<item>
		<title>Amerika ya Kati: Kasi Kubwa ya Ueneaji wa Jangwa</title>
		<link>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/11/amerika-ya-kati-kasi-kubwa-ya-ueneaji-wa-jangwa/</link>
		<comments>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/11/amerika-ya-kati-kasi-kubwa-ya-ueneaji-wa-jangwa/#comments</comments>
		<pubDate>Fri, 06 Nov 2009 13:24:23 +0000</pubDate>
		<dc:creator>Deogratias Simba</dc:creator>
				<category><![CDATA[Americas]]></category>
		<category><![CDATA[Argentina]]></category>
		<category><![CDATA[Brazil]]></category>
		<category><![CDATA[Chile]]></category>
		<category><![CDATA[Conversations for a Better World]]></category>
		<category><![CDATA[English]]></category>
		<category><![CDATA[Environment]]></category>
		<category><![CDATA[Feature]]></category>
		<category><![CDATA[Spanish]]></category>
		<category><![CDATA[Weblog]]></category>

		<guid isPermaLink="false">http://sw.globalvoicesonline.org/?p=556</guid>
		<description><![CDATA[Ueneaji wa jangwa unasambaa kimyakimya lakini kwa kasi kubwa mahali pengi duniani na Amerika ya Kati haijaweza kukwepa hali hii iliyo na athari mbaya za kutisha. Wakati ambapo majangwa ni maumbo ya asili, ueneaji wa jangwa ni mchakato wa kuharibika kwa nyanda za ardhi kutokana na mabadiliko ya hali ya hewa na uharibifu unaofanywa na binadamu. ]]></description>
			<content:encoded><![CDATA[<em>Ilichapwa kwanza na<a href="http://globalvoicesonline.org/author/belen-bogado/">Belen Bogado</a>  &middot; Imetafsiriwa na <a href='http://sw.globalvoicesonline.org/author/simbadeo/'>Deogratias Simba</a> &middot;  <a href='http://globalvoicesonline.org/2009/11/04/latin-america-the-rapid-spread-of-desertification/  '>Angalia ujumbe mama</a></em> 
<br /><p>Pengine maneno ueneaji jangwa yanaweza kusikika sawa na jangwa, lakini kuna tofauti kubwa ya msingi kati ya maneno hayo: wakati ambapo majangwa ni moja kati ya maumbo mazuri ya kipekee ya asili, ueneaji jangwa ni mchakato wa kuharibika ambako kanda za ardhi hupitia baada ya kuathiriwa vibaya na mabadiliko ya hali ya hewa, shughuli za binadamu na majanga ya asili mpaka hatimaye zinageuka na kuwa majangwa.</p>
<div class="wp-caption aligncenter" style="width: 410px"><img alt="Picha na Macnolete na inatumika chini ya leseni ya Creative Commons." src="http://globalvoicesonline.org/wp-content/uploads/2009/11/desertification.jpg" title="desertification" width="400" height="258" /><p class="wp-caption-text">Picha na Macnolete na inatumika chini ya leseni ya Creative Commons.</p></div>
<p>Ingawa athari ya mabadiliko ya hali ya hewa katika ueneaji jangwa bado haijaeleweka vema, yaani kwa mujibu wa GreenFacts, inafahamika kwamba <a href="http://www.greenfacts.org/en/desertification/index.htm">viwango vya juu vya joto vinavyotokana na kuongezeka kwa viwango vya dioksidii ya kaboni kunaweza kuwa na athari mbaya kutokana na kuongezeka kwa upotevu wa maji kutoka ardhini na kupungua kwa viwango vya mvua katika maeneo yenye ukame</a>. Wakati huohuo ueneaji jangwa nao huchangia katika mabadiliko ya hali ya hewa kwa kuruhusu kaboni iliyohifadhiwa kwenye mimea ya maeneo yenye ukame na udongo kurushwa kwenye anga.</p>
<p>Ueneaji jangwa unazidi kuwa na athari mahali pote duniani. Kwa sasa hivi ueneaji huo unaathiri mavuno, unasababisha kupanda kwa bei za vyakula vilivyopo, na katika baadhi ya maeneo, hata wanyama wanakufa. Watu wanalazimika kuhamia maeneo mengine ya mbali na nyumbani kwao, kama anavyoeleza mwanablogu Miguel Angel Alvarado anayetokea El Salvador <a href="http://www.ecoportal.net/content/view/full/61308/">kuhusu mpango wa kuhamisha makazi ya rais kwa sababu ya ueneaji jangwa[es]</a>:</p>
<blockquote><p>El traslado de casa presidencial, del Barrio san Jacinto al local en donde estaba el Ministerio de Relaciones exteriores, según informes extrajudiciales, obedece a la prevención del ejecutivo ante un posible hundimiento del suelo generado por cárcavas en este sector.</p></blockquote>
<div class="translation">Kwa mujibu wa nyaraka zisizo rasmi kisheria, kuhamishwa kwa makazi ya rais kutoka maeneo ya San Jacinto kwenda ilipokuwa Wizara ya Mambo ya Nje hapo awali, ilikuwa ni hatua ya kujihami iliyofanywa na mhimili wa dola ili kuepuka kutitia kwa ardhi kutokana na makorongo yaliyotokea pale.</div>
<p>Bara lililoathiriwa zaidi ni Afrika, na jambo hili linaweza kuonekana zaidi nchini Kenya, ambapo moja ya sekta zinazoweza kupata athari kubwa za ueneaji jangwa na ukame ni wasichana. Pale maji yaliyohifadhiwa kwenye matenki yalipokuwa yametumika yote katika Nyumba ya Watoto Yatima ya Dago Dala Hera huko Magharibi mwa Kenya, akina mama wanaojitolea na watoto wanalazimika kuteka maji yasiyo salama kutoka katika mto ulio karibu kwa ajili ya kupikia na kunywa. <a href="http://us.oneworld.net/article/367320-africa-famine-deepens-drought-worst-decades">“Kwenda mtoni kuteka maji peke yao nyakati za jioni kunawaweka wasichana katika hatari ya kukumbana na wanaume wanaoweza kuwanyanyasa kingono,”</a> alisema Edwin Odoyo, ambaye mama yake anayeitwa Pamela ndiye aliyeanzisha makazi hayo ya watoto yatima.</p>
<p>Ingawa ueneaji jangwa una athari kubwa zaidi barani Afrika, hali ya mazingira ya Amerika ya Kati nayo inapitia mabadiliko makubwa, kama ilivyojadiliwa siku za karibuni katika Mkutano wa Tisa wa Kongamano kuelekea Mkataba wa Umoja wa Mataifa wa Kukabili Ueneaji Jangwa uliofanyika jijini Buenos Aires, Ajentina. Mtaalamu wa Kiitaliano, Massimo Candelori, aliyekuwa mwakilishi wa Mkataba wa Kukabili Uenejaji Jangwa, <a href="http://www.tierramerica.info/nota.php?lang=esp&#038;idnews=3422">alisema katika mahojiano na  Tierramerica</a> kwamba hali ilivyo Amerika ya Kati inatisha kwa kuzingatia kwamba hakuna taarifa za kutosha kuhusu kiwango cha ueneaji jangwa katika eneo hilo. “Hatuna takwimu za sasa hivi. Moja ya lengo lililojadiliwa katika Mkutano wa Tisa lilikuwa ni kupata viashirio vinavyoturuhusu kuelewa vizuri zaidi hali halisi &#8230; takwimu tulizonazo mpaka sasa ni zile za miaka kumi iliyopita,” alisema Candelori.</p>
<p>Katika nchi za Amerika ya Kati ambapo kilimo na ufugaji ni moja ya sekta kuu za uchumi, ueneaji jangwa unaweza kuwa wa kimyakimya, lakini wenye madhara makubwa kama mnyama hatari mwindaji. Walau <a href="http://www.tierramerica.info/nota.php?lang=eng&#038;idnews=3207">asilimia 25 ya sehemu ya eneo zima</a> tayari imeharibiwa na wakati huohuo watu wanazidi kuwa na wasiwasi juu ya suala hili, kama inavyojionyesha katika blogu mbalimbali. </p>
<p><em>Eco Briefings [pt]</em>, blogu ya KiBrazili, inaonyesha kwamba <a href="http://ecobriefings.com/2009/10/05/desertificao/">WaBrazili waishio Kaskazini Mashariki mwa nchi wanashuhudia ueneaji wa kasi sana wa jangwa[pt]</a>:</p>
<blockquote><p>Mais um alerta está ligado. Temos pouco tempo para corrigir as coisas. (…)</p>
<p>No Brasil a desertificação tem avançado na caatinga, e zonas do polígono da seca no Nordeste e Norte de Minas Gerais, e também em Estados que antes não tinham áreas secas ou desertificadas como o Rio Grande do Sul. O Rio Amazonas viveu já uma grande seca a pouco tempo, grande com mortandade de peixes.</p></blockquote>
<div class="translation">Kiitia hatari kingine kinanguruma. Tuna muda mfupi sana wa kurekebisha mambo (…)</p>
<p>Nchini Brazili, ueneaji jangwa umeongezeka sana katika Caatinga, katika ukanda wa maeneo kame Kaskazini Mashariki na Kaskazini mwa jimbo la Minas Gerais, na vilevile katika majimbo ambayo hayakukumbwa na ukame wala ueneaji jangwa hapo kabla kama vile Rio Grande do Sul. Mto Amazon umepitia ukame mkubwa kabisa katika kipindi kifupi kilichopita, jambo lililosababisha samaki kufa kwa idadi kubwa.</p></div>
<p>Ajentina nayo ina maeneo kadhaa yaliyoathiriwa. Katika mkoa wa Valles Aridos, Kaskazini Mashariki, ambapo shughuli kuu ya kiuchumi ni ufugaji kondoo, inakadiriwa kwamba <a href="http://globalvoicesonline.org/2009/11/04/latin-america-the-rapid-spread-of-desertification/www.inta.gov.ar/salta/info/documentos/Desertificaci%C3%B3n.pdf">katika miaka 100 iliyopita, walau watu 180,000 walilazimika kuhama. [es] (katika mfumo wa .pdf)</a>. Kusini mwa nchi ya Ajentina nako hakujapona na ueneaji jangwa. Mwanablogu Ailen Romero, anaandika maoni katika blogu inayoitwa <em>Geoperspectivas [es]</em> <a href="http://geoperspectivas.blogspot.com/2009/06/dia-mundial-de-la-desertificacion-2009.html">kwamba katika mkoa wa Patagonia, juhudi za serikali za kukabili ueneaji jangwa bado hazitoshi</a>:</p>
<blockquote><p>En la Patagonia, la amplitud del problema es de tal magnitud que ha comenzado a adquirir estado público. Pocos ignoran el tema, pero pocos tienen la posibilidad de actuar de alguna forma o con el conocimiento para hacerlo. El problema de la desertificación en el caso de la Patagonia supera a los planes que se han elaborado para combatirlo. Es por eso que no deben ahorrarse esfuerzos, ni limitar la imaginación de soluciones alternativas.”Si la geografía es la manifestación de la sociedad en el espacio físico, un espacio físico deteriorado refleja una sociedad deteriorada” afirman del Valle y Coronato(investigadores del Centro Nacional Patagónico)</p></blockquote>
<div class="translation">Katika Patagonia, ukali wa tatizo ni mkubwa kiasi kwamba umma wote umetambua tatizo hilo. Ni watu wachache tu ndiyo wanaolipuuza na ni wachache tu walio na nafasi au maarifa ya kufanya juhudi kulikabili. Tatizo la ueneaji jangwa huko Patagonia unazidi mipango iliyokwishaainishwa kulikabili. Ndiyo sababu kila juhudi haina budi kufanywa, wala kusiwe na mipaka katika kufikiria ufumbuzi mwingine wowote. ‘Kama Jiografia ni kielelezo cha jamii katika nafasi halisia, kuharibika kwa nafasi halisia huko kunaakisi kuharibika kwa jamii, wanasema  Valle na Coronato (watafiti kutoka katika Kituo cha Taifa cha Patagonia).</div>
<p>Huko Chile, ambapo <a href="http://www.conaf.cl/?seccion_id=8ad00d8dd61d22aa152575a1e5c08e58&#038;unidad=0&#038;PHPSESSID=db19e79870c9e01418e62b8576a26daf">takribani asilimia 62 ya eneo la taifa tayari imeathiriwa na ueneaji jangwa [es]</a>, mwanablogu Alfredo Erlwein alieleza wasiwasi kupitia katika blogu inayoitwa <em>El Ciudadano [es]</em>(Raia) kuhusu jinsi gani watu <a href="http://www.elciudadano.cl/2009/03/26/desertificacion-y-sequia-el-gran-problema-ambiental-de-chile-y-el-mundo/">wasiyo na maarifa ya kutosha kuhusu ueneaji jangwa</a>.</p>
<blockquote><p>
Efectivamente la desertificación es el problema ambiental más grave de Chile y muy poco conocido. Existen grandes zonas, como en la costa de la octava región, donde la erosión severa supera el 50% de la superficie: esto es que literalmente más de la mitad de los suelos se ha perdido por completo. En esas zonas se encuentran cárcavas de más de 50 metros de profundidad. Una tasa normal de formación de suelo puede ser de 0.2 cm por año, lo que evidencia la gravedad del asunto.</p></blockquote>
<div class="translation">Ueneaji jangwa kwa hakika ni tatizo kubwa kabisa lakini lisilofahamika miongoni mwa matatizo ya kimazingira nchini Chile. Kuna maeneo makubwa, kama vile pwani ya Nane ya Mkoa, ambapo mmomonyoko mkali wa udongo unazidi asilimia 50 ya ardhi: hii ina maana kwamba zaidi ya nusu ya ardhi imepotea, huo ndiyo ukweli. Katika maeneo hayo kuna makorongo yenye kina cha mpaka mita 50. Kiwango cha kawaida cha utengenezekaji ardhi ni kama sm 0.2 kwa mwaka, huo ndiyo uthibitisho wa ukali wa tatizo lililopo.</div>
<p>Kwa mujibu wa mtaalamu Mwitaliano Candelori, <a href="http://www.tierramerica.info/nota.php?lang=eng&#038;idnews=3207">kutumia udongo katika soko la Kaboni kutasaidia kupambana na ueneaji jangwa</a>; jambo hili pengine litaamuliwa katika Kongamano litakalofanyika jijini Copenhagen. Tayari kongamano hilo limeanza kuhesabiwa siku na ulimwengu unalisubiri kwa hamu.</p>
]]></content:encoded>
			<wfw:commentRss>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/11/amerika-ya-kati-kasi-kubwa-ya-ueneaji-wa-jangwa/feed/</wfw:commentRss>
		<slash:comments>0</slash:comments>
		</item>
		<item>
		<title>Chile: Mkutano wa McCain na Pinochet Mwaka 1985</title>
		<link>http://sw.globalvoicesonline.org/2008/10/chile-mkutano-wa-mccain-na-pinochet-mwaka-1985/</link>
		<comments>http://sw.globalvoicesonline.org/2008/10/chile-mkutano-wa-mccain-na-pinochet-mwaka-1985/#comments</comments>
		<pubDate>Tue, 28 Oct 2008 13:58:56 +0000</pubDate>
		<dc:creator>j nambiza tungaraza</dc:creator>
				<category><![CDATA[Americas]]></category>
		<category><![CDATA[Chile]]></category>
		<category><![CDATA[Elections]]></category>
		<category><![CDATA[English]]></category>
		<category><![CDATA[Feature]]></category>
		<category><![CDATA[International Relations]]></category>
		<category><![CDATA[Politics]]></category>
		<category><![CDATA[Spanish]]></category>
		<category><![CDATA[U.S.A.]]></category>
		<category><![CDATA[Weblog]]></category>

		<guid isPermaLink="false">http://sw.globalvoicesonline.org/?p=34</guid>
		<description><![CDATA[Mwaka 1985, Mbunge wa bunge la Marekani aitwaye John Mccain alizuru nchini Chile na kukutana na mtawala wa kiimla Augusto Pinochet, akiwa na viongozi wengine wa serikali. Mkutano huo ambao haujawahi kuripotiwa hapo awali umewekwa wazi na mwandishi wa habari John Dinges, ambaye amechapisha habari hiyo kwenye blogu yake CIPHER [es], kadhalika katika blogu ya Huffington Post, ambako huwa anaandika masuala yanayomhusu John McCain "ambaye amekuwa akishutumu vikali dhana ya kuketi na watawala wa kiimla bila ya masharti yoyote, inaonekana kuwa alifanya jambo hilo hilo analolipinga. ]]></description>
			<content:encoded><![CDATA[<em>Ilichapwa kwanza na<a href="http://globalvoicesonline.org/author/eduardo-avila/">Eduardo Avila</a>  &middot; Imetafsiriwa na <a href='http://sw.globalvoicesonline.org/author/j-nambiza-tungaraza/'>j nambiza tungaraza</a> &middot;  <a href='http://globalvoicesonline.org/2008/10/27/chile-the-1985-meeting-between-mccain-and-pinochet/'>Angalia ujumbe mama</a></em> 
<br /><p>Mwaka 1985, Mbunge wa bunge la Marekani aitwaye John Mccain alizuru nchini Chile na kukutana na mtawala wa kiimla <a href="http://en.wikipedia.org/wiki/Augusto_pinochet">Augusto Pinochet</a>, akiwa na viongozi wengine wa serikali. Mkutano huo ambao haujawahi kuripotiwa hapo awali umewekwa wazi na mwandishi wa habari John Dinges, ambaye amechapisha habari hiyo kwenye blogu yake <a href="http://ciperchile.cl/2008/10/24/la-desconocida-cita-entre-john-mccain-y-pinochet/"><em>CIPHER [es]</em></a>, kadhalika katika blogu ya Huffington Post, <a href="http://www.huffingtonpost.com/john-dinges/mccain-meets-a-bloody-dic_b_137422.html">ambako huwa anaandika masuala yanayomhusu John McCain</a> &#8220;ambaye amekuwa akishutumu vikali dhana ya kuketi na watawala wa kiimla bila ya masharti yoyote, inaonekana kuwa alifanya hivyo na &#8220;Pinochet, mmoja wa watawala wakiukaji wa haki za binaadamu ambaye anashutumiwa kuua zaidi ya raia 3,000 na kuwasweka gerezani makumi ya maelfu wengine&#8221; </p>
<p>Bloga wa KiChile juan Guillermo Tedeja anaandika kuhusu <a href="http://juanguillermotejeda.wordpress.com/2008/10/25/mccain-pinochet-y-el-sigilo/">baadhi ya yaliyojiri kwenye mkutano huo [es]:</a></p>
<blockquote><p>Seneta aliketi kwa saa moja na nusu na ka-zimwi ketu, pia alikutana na Jenerali wa jeshi Merino, ambaye utesi wake tunaujua fika… Mkutano huo, ulioandaliwa na aliyekuwa balozi wakati huo Hernán Felipe Errázuriz, haukutokea kwenye vyombo vya habari na Seneta hakutoa maoni yoyote.</p></blockquote>
<p>Dinges aliandika kuhusu <a href="http://ciperchile.cl/2008/10/24/la-desconocida-cita-entre-john-mccain-y-pinochet">baadhi ya mazingira ya mkutano huo </a>katika blogu ya Kituo cha uandishi wa Habari na Upelelezi (CIPER kwa kifupi katika lugha ya KiHispania)</p>
<blockquote><p>Wakati wa mkutano, majira ya alasiri mnamo Desemba 30, Idara ya Sheria ya Marekani ilikuwa ikiwasaka maswahiba watatu wa Pinochet - aliyekuwa mkuu wa DINA (Idara ya Taifa ya Upelelezi) Manuel Contreras na maafisa wengine wa DINA Pedro Espinoza pamoja na Armando Fernández Larios - kwa vitendo vya kigaidi walivyovifanya jijini Washington D.C. Kesi iliyoendeshwa huko Washington ilibaini kwamba watu hao walipaswa kushitakiwa kwa ajili ya mauaji ya aliyekuwa balozi wa Chile nchini Marekani na Waziri wa Mambo ya Nje Bwana Orlando Letelier na pia mauaji ya raia wa Marekani Ronny Moffit, ambaye alikuwapo na Letelier. Mlipuko wa bomu kwenye gari sehemu za Sheridan Cirlce katika mji mkuu wa Marekani ulielezewa wakati huo kama moja ya tendo la kuchefua zaidi katika ugaidi wa kimataifa ambalo limewahi kufanywa na taifa la nje katika ardhi ya Marekani. </p>
<p>Wakati wa mkutano wa McCain na Pinochet, makundi ya upinzani wa kidemokrasia nchini Chile yalikuwa yakitafuta kuungwa mkono na viongozi wa Kidemokrasia duniani katika juhudi zao za kumshinikiza Pinochet aruhusu kurejeshwa demokrasi na kusitisha utawala wa kiimla kwa njia za amani, utawala ambao tayari ulikuwa umeshadumu kwa miaka 12. Viongozi wengine wa Bunge la Marekani waliozuru Chile walitoa matamko rasmi ya wazi yaliyopinga utawala wa kimabavu na kuunga mkono kurejeshwa kwa demokrasi, na wakati mwingine viongozi hao wa Bunge walilengwa kwenye maandamo yalioandaliwa na mashabiki wenye ghasia wa Pinochet. </p></blockquote>
<p>Bloga Mchile-Mmarekani Tomás Dinges ameweka viunganishi vya makala zilizoandikwa katika blogu yake ya <em>Chile From Within,</em> na &#8220;mtaalamu-mahiri pamoja na baba&#8221; kadhalika ameweka viunganishi vya ziada vinavyohusiana na habari hiyo, <a href="http://miamiherald.typepad.com/nakedpolitics/2008/10/blog-mccain-met.html">kikiwemo cha majibu kutoka kwenye Kampeni ya Bwana McCain</a> ambayo imetokea kwenye blogu ya gazeti la Miami Herald, <em>Naked Politics</em>. </p>
<p>Mabloga wengi wa kutoka Marekani ya Kusini na Chile wanaichapa makala ya John Dinges, kama njia ya kusambaza habari hiyo.</p>
]]></content:encoded>
			<wfw:commentRss>http://sw.globalvoicesonline.org/2008/10/chile-mkutano-wa-mccain-na-pinochet-mwaka-1985/feed/</wfw:commentRss>
		<slash:comments>0</slash:comments>
		</item>
	</channel>
</rss>
