Habari kutoka Muhtasari wa Habari na Kihispania
‘Escopetarra': Chombo cha Kipekee
Kama unaamini kuwa hakuna jambo zuri linaloweza kutokana na bunduki aina ya gobore, basi unapaswa kukifahamu kifaa kiitwacho “escopetarra”— mchanganyiko uliotokana na kubadilisha silaha mbili “hatari” (an AK-47 na gitaa) na kuwa kifaaa cha amani. “Escopetarra” ni neno lililotokana na muunganiko wa maneno ya Kispaniola, “escopeta” (bunduki) na “guitarra” (gitaa). Kwenye...
Je, Utoaji wa Mimba Unaweza Kujadiliwa Kwenye Treni za Medellín?
Wakazi wa jiji la Medellín, Colombia, wanajiuliza kama treni inaweza kuwa eneo la kuzungumzia masuala ya utoaji mimba, kutokana na tangazo la kampeni ya #ladecisiónestuya (uamuzi ni wako) inayoendeshwa kwa mifumo mbalimbali ndani ya vyombo vya usafiri wa umma, hasa magari, kama inavyosimuliwa na mtumiaji wa twita aitwaye Jaime Andrés (@JAIM3_ANDR3S):...
‘Kulea Mtoto Ukiwa Mtoto': Idadi Kubwa ya Mimba za Utotoni Nchini Venezuela
Desireé Lozano, anayeblogu kwenye blogu ya Voces Visibles, anatoa mwito kwa ongezeko kubwa la mimba za utotoni nchini Venezuela, ambapo asilimia 25 ya mimba ni za vijana, na kukosekana kwa sera sahihi za kudhibiti tatizo hili na matokeo yake. Takwimu za Venezuela zinaonesha kwamba nchi hiyo ina idadi kubwa ya...
Je, Blogu Zinaelekea Kutoweka?
Makala haya ni sehemu ya 46 ya #LunesDeBlogsGV (#JumatatuYaBloguGlobalVoices) siku ya Machi 23, 2015. Kwenye #LunesDeBlogsGV (#JumatatuyaBloguGlobalVoices), tunajitahidi kuzitunza blogu mithili ya “viumbe wanaoelekea kutoweka”, kwa kushughulikia changamto zinazokabili uwepo wa blogu kwenye ulimwengu wa kidijitali. Jitihada kama hizi zinamfanya mwanablogu Iván Lasso kuchambua mustakabali wa kublogu na matatizo yanayowakabili wanablogu leo,...
Kulinda Taarifa Binafsi Nchini Ajentina Bado Kuna Safari Ndefu
Kwenye makala iliyoandikwa kwa ajili ya gazeti la mtandaoni Haki za Kidijitali: Amerika Kusini & Visiwa vya Caribbean, No.21, Mmwanasheria wa ki-Ajentina Valeria Milanés anaeleza kwamba hata kama Marekani ni kiranja wa dunia kwenye kuchakata taarifa (data), bado haina sheria ya kulinda taarifa za watu. Marekani pia inachukuliwa kama nchi yenye “kiwango...
Nini Tofauti ya Kusoma na Kuelimika?
Pedro Muller anatafakari kuhusu matatizo yanayoukabili mfumo wa shule, taasisi anayosema ilimaanisha mazingira tofauti ya kihistoria. Kwa kusema hayo, anabainisha umuhimu wa dhana hizi mbili zinazofanana lakini zikimaanisha nyakati mbili tofauti: “Kusoma” na “kuelimika”: El educar se va más allá de memorizarse un par de nombres y olvidarlos al siguiente...
Umoja wa Ulaya Hautatoa Nafuu ya Kodi ya VAT kwa Vitabu ya Kidigitali
Mnamo Machi 5, 2015, Mahakama ya Haki ya Umoja wa Ulaya ilitoa hukumu kwamba punguzo la kodi ya ongezeko la thamani (VAT) lililotolewa kwa vitabu vinavyochapishwa halitahusisha vitabu vya kidijitali, kwa kuzingatia kwamba kila kinachosambazwa au kutolewa kwa mfumo wa kieletroniki au kwa mtandao wa intaneti ni huduma. Amalia Lopez anahoji...
Mwizi Akamatwa, Aomba Msamaha na Kusamehewa
Labda alidhani ingekuwa vyepesi kuiba shampoo mali ya mmiliki wa duka nchini Peru, lakini mambo yalimwendea mrama mwizi huyu. Mtu mmoja akiwa ameongozana na mwenzake waliingia kwenye duka lililoko kwenye jiji la Huancayo nchini Peru, wakisema walikuwa wanataka kununua pombe, na mmiliki alipokuwa amepumbazwa kidogo, jamaa walibeba boksi la shampoo....
Kuelimisha Wasichana Leo, Kuwawezesha Wanawake Kesho
Marita Seara, anayeblogu kwenye Voces Visibles (Sauti Zinazoonekana), anatukaribisha kutafakari suala la ubaguzi unaowaathiri wasichana na vijana wanaopevuka —kupata elimu– na hitaji ya kuwaelimisha wasichana wetu leo ili waweze kuwa wanawake waliowezeshwa kesho na keshokutwa. Kwa mujibu wa takwimu za shirika la kutetea haki za binadamu duniani Amenisty International, wasichana...
Kufanyiwa Kazi na Faida za Matokeo ya Utafiti, Tafiti za Vyuo Vikuu Zina Tija?
Mawazo ikiwa umma wa wananchi unathamini tafiti zinazofanywa na vyuo vikuu, yamewachokoza mwanazuoni César Viloria kutoa mwangaza kidogo kuhusu suala hili kwenye blogu yake. Kuhusu utafiti, lazima tufahamu kwamba kuna aina mbili kuu: utafiti msingi na utafiti tumizi. Utafiti msingi hufanywa kwa minajili ya kuongeza au kuja na maarifa mapya...