Habari kutoka Muhtasari wa Habari na Uhamiaji na Uhamaji
Baada ya Maandamano Burkina Faso na Burundi, Naija na Togo Zinafuata?
Wanaija 20,000 wameingia mitaani mjini Niamey, Naija mnamo Juni, 6. Kuna ababu nyingi za maandamano hayo: umaskini uliokithiri, utawala mbovu na kubanwa kwa uhuru wa kujieleza yakiwa ni moja wapo ya malalamiko ya asasi za kiraia nchini humo. Maandamano kama haya yalitokea katika nchi za Burkina Faso, Burundi na Togo....
Hadithi ya Wakimbizi wa Njaa kutoka Niger katika Algeria Mashariki
Katika wiki chache zilizopita, mamia ya wahamiaji mwa Jangwa la Sahara kutoka Mali au Niger wamehamia miji ya Algeria katika mpaka wa Mashariki. Liberté Algérie anasimulia hadithi ya wale ambao waliamua kuhama na kwa nini [fr] Les conditions de vie au hangar de la cité Bourroh sont inhumaines. A l’intérieur...
Uhamaji wa Watoto Wachukuliwa kuwa ni Baa la Kibinadamu
Kutoka Mexico, Katia D'Artigues, ambaye ni mwandishi wa blogu ya Campos Elíseos (Champs Elysées), aandika kuhusiana na watoto kulazimika kuhama wao wenyewe [es], hali inayompelekea kuiita hali hii kuwa ni “baa la kibinadamu”: Son niños que son orillados a cruzar la frontera solos. No lo hacen por aventura, sino porque...
Video ya Dakika 5, Yaweza Kuwa Tiketi Yako ya Kwenda Mjini New York
Muungano wa Ustaarabu wa Umoja wa Mataifa (UNAOC) inawaalika vijana chini ya umri wa miaka 25 kuwasilisha video walizozitengeneza wenyewe zenye urefu wa dakika 5 juu ya uhamiaji, tofauti na kuingizwa kijamii kwa ajili ya tamasha kubwa la filamu 2014. Video tatu zitakazoshinda zitazawadiwa Dola za Marekani 1000 na watengenezaji...
Ulaya Yamuonya Waziri wa Ufaransa Kuhusu Matamshi Yake Dhidi ya Warumi
Matamshi ya Waziri wa Mambo ya Ndani wa Ufaransa, Manuel Valls, yalifufua uhasama uliokuwepo kati ya Ufaransa na Warumi.
Wahamiaji 87 Wafariki kwa Kukosa Maji Kaskazini mwa Niger
Mnamo tarehe 30 0ctoba, watu 87 waliokuwa wakijaribu kuifikia bahari ya Mediterania walifariki mara baada ya madereva waliokuwa wakiendesha magari waliyoyatumia kusafiria kuwatelekeza wahamiaji hao katika Jangwa la Sahara. Wahamiaji hawa walihangaika kutafuta msaada bila ya mafanikio. Simulizi ya kuhuzunisha kutoka kwa mmoja wa watu walionusurika aliyejulikana kwa jina la...
Picha Nyeusi: Waafrika Nchini Italia
Picha Nyeusi ni kazi za wapiga picha watatu – Marco Ambrosi, Matteo Danesin na Aldo Sodoma – Kituo cha Stadi za Uhamiaji mjini Verona, Majiji ya Verona na Padua, Chuo Kikuu cha Padua Idara ya Sosholojia ikiwaonyesha Waafrika nchini Italia.
Cape Verde: Midahalo Kuhusu Vijana na Siasa Inayoendelea Huko Ureno
Kuna kundi la raia wa Cape Verde ambalo huandaa mikutano mjini Lisbon ili kujadili uhusiano kati ya vijana na siasa, kama anavyoeleza Suzano Costa katika video [pt] kama ilivyowekwa tena na Amilcar Tavares. Katika blogu yao – Tertúlia Crioula [pt] – unaweza kusoma maelezo yaliyochukuliwa kutoka “Cape Verde katika Mdahalo” kadhalika unaweza...
Lebanoni: Wafanyakazi wa Ndani Wanaotoroka
“Mfanyakazi wa ndani anapotoroka kutoka kwenye nyumba ya mwajiri wake, kituo cha polisi hakiwezi kufanya lolote kwa sababu hakuna sheria dhidi ya wafanyakazi wa ndani wanaotoroka. Kwa hiyo ofisa wa kituo cha polisi anamwambia mwajiri wa ki-Lebanoni aseme kuwa (mtoro huyo) aliiba pesa,” anaandika Ethiopian Suicides.
Haiti: Maoni ya Mwanzo Kuhusu Tetemeko la Ardhi Lenye Ukubwa wa 7.0
Posti ya kwanza ya blogu iliyoandikwa kwa lugha ya Kifaransa kuhusu tetemeko la ardhi huko Haiti imetokea nje ya nchi hiyo, ikitangaza habari mbaya za kuanguka kwa Kasri ya Rais, hospitali na majengo mengine na pia tishio la tsunami. Kwa mujibu wa MetropoleHaiti, Marekani tayari imekwishapendekeza misaada ya kibinadamu.