Habari kutoka Muhtasari wa Habari na Uhuru wa Kujieleza
Baada ya Maandamano Burkina Faso na Burundi, Naija na Togo Zinafuata?
Wanaija 20,000 wameingia mitaani mjini Niamey, Naija mnamo Juni, 6. Kuna ababu nyingi za maandamano hayo: umaskini uliokithiri, utawala mbovu na kubanwa kwa uhuru wa kujieleza yakiwa ni moja wapo ya malalamiko ya asasi za kiraia nchini humo. Maandamano kama haya yalitokea katika nchi za Burkina Faso, Burundi na Togo....
Ramani Hizi Zaonesha Mahali Walipotesewa na Kuuawa Wanahabari wa Kambodia
Kituo cha Haki za Binadamu cha kambodia kimezindua jarida linaloelezea ukiukwaji wa haki za binadamu unaofanywa kwa waandishi wa habari nchini Kambodia. Katiba ya nchini Kambodia inatoa uhuru wa kupashana habari lakini wanahabari wanazidi kunyanyaswa na kuuawa, hususani kwa waandishi wanaopasha habari kuhusiana na ukiukwaji wa maadili unaofanywa na maafisa...
Je, Blogu Zinaelekea Kutoweka?
Makala haya ni sehemu ya 46 ya #LunesDeBlogsGV (#JumatatuYaBloguGlobalVoices) siku ya Machi 23, 2015. Kwenye #LunesDeBlogsGV (#JumatatuyaBloguGlobalVoices), tunajitahidi kuzitunza blogu mithili ya “viumbe wanaoelekea kutoweka”, kwa kushughulikia changamto zinazokabili uwepo wa blogu kwenye ulimwengu wa kidijitali. Jitihada kama hizi zinamfanya mwanablogu Iván Lasso kuchambua mustakabali wa kublogu na matatizo yanayowakabili wanablogu leo,...
Video: Mwanasheria wa Swaziland Aliyefungwa Jela Azungumza Kupitia Wanaharakati wa Haki za Binadamu
#swazijustice ni kampeni inayotoa wito wa kuachiliwa huru kwa Bheki Makhubu, mhariri wa gazeti la Taifa na Thulani Maseko, mwanasheria wa haki za binadamu, ambao walifungwa jela nchini Swaziland kwa miaka miwili kwa sababu ya kuandika makala kukosoa mfumo wa mahakama nchini humo. Wawili hao walikamatwa tarehe 17 Machi 2014...
Uhuru wa Vyombo vya Habari nchini Liberia Wawekwa Shakani Kufuatia Vita Dhidi ya Ebola
Umoja wa wanahabari wa Liberia wasikitishwa na hali ya kukosekana kwa uhuru wa upashanaji habari kufuatia hatua ya serikali ya kuzuia kuenea kwa virusi vya ebola. Umoja huu ulimwandikia barua Waziri wa sheria kumtaka kutafakari upya madhila wanayokabiliana nayo waandishi wa vyombo vya habari. Ufuatao ni muhtasari wa barua yenyewe:...
Jinsi Wanablogu Walifikia Gerezani kwa Kuandika Kuhusu Haki za Binadamu Nchini Ethiopia
Melody Sundberg anachambua uhuru wa kujieleza nchini Ethiopia baada ya wanablogu wa Ethiopia waliokamatwa kukaa siku 100 gerezani: Ethiopia ina idadi ya watu 94,000,000 na ni nchi ya pili yenye wakazi wengi katika bara la Afrika. Hata hivyo, hailingani na mahojiano ya Endalkhachew Chala kupitia Global Voices, kuwa na gazeti...
Umuhimu wa Haki kwa Wanablogu wa Ethiopia
Justice Matters ni blogu inayoripoti kuhusu kesi ya wanablogu wa Zone9 waliokamatwa na waandishi wa habari nchini Ethiopia kwa ajili ya kutoa maoni yao: Blogu hii ina habari zaidi za hivi karibuni kuhusu jitihada za utetezi, ripoti za vyombo vya habari, na hadhi ya kisheria ya wanablogu wa Zone9 nchini...
Ethiopia: #FreeZone9Bloggers Yavuma Kwenye Mtandao wa Tumblr
Global Voices Advocacy ilianzisha mtandao wa Tumblr mapema mwezi Mei kutafuta uungwaji mkono kwa wanablogu tisa na waandishi wa habari – ambao wanne kati yao ni wanachama wa Global Voices – ambao kwa sasa wako kizuizini nchini Ethiopia shauri ya kazi zao. Washirika kutoka duniani kote waliwasilisha picha, ujumbe wa...
‘Hali Mbaya’ ya Haki za Binadamu Nchini Vietnam
Mtandao wa haki za Binadamu illitoa ripoti yake ya 2013 kuhusu ‘hali mbaya’ ya haki za binadamu nchini Vietnam: …. Hali ya haki za binadamu nchini Vietnam iligeuka na kuwa mbaya mwaka 2013. Idadi ya watu waliotiwa kizuizini kwa kutoa maoni ya kisiasa yaliyo kinyume na wale wa chama tawala...
Kwa Nini Kublogu ni Tishio kwa Serikali ya Ethiopia
Beza Tesfaye anaelezea kwa nini kublogu ni tishio kwa serikali ya Ethiopia kufuatia kukamatwa kwa wanablogu tisa Ethiopia: Ninapoandika haya, Kwa uwoga nakumbushwa kwamba nchini Ethiopia, kutoa maoni yako kunaweza kukufanya uakapewa tiketi ya daraja la kwanza gerezani. Kutoka Aprili 25 hadi 26, 2014, wanablogu tisa wa Ethiopia na waandishi...