Habari kutoka Muhtasari wa Habari na Kiingereza
Wanawake Wanaovaa Nusu Uchi Wataiokoa Sekta ya Utalii Kenya?
Je, kutembea uchi yanaweza kuwa mbinu bora ya kufufua sekta ya utalii nchini Kenya kufuatia mashambulizi ya wanamgambo wa Al Shabaab?: Seneta mteule, Mbura anasemekana kuwaomba wanawake katika mkoa wa pwani kutembea nusu uchi ili kuwavutia watalii zaidi kuzuru eneo hilo. Wito huo umeibua maswali kuhusiana na thamani ya mwanamke...
Baada ya Maandamano Burkina Faso na Burundi, Naija na Togo Zinafuata?
Wanaija 20,000 wameingia mitaani mjini Niamey, Naija mnamo Juni, 6. Kuna ababu nyingi za maandamano hayo: umaskini uliokithiri, utawala mbovu na kubanwa kwa uhuru wa kujieleza yakiwa ni moja wapo ya malalamiko ya asasi za kiraia nchini humo. Maandamano kama haya yalitokea katika nchi za Burkina Faso, Burundi na Togo....
Kwa nini Tarakimu 64, 89 na 535 Hazipatikani Kwenye Mtandao wa Intaneti China?
Leo ni Juni 4, maadhimisho ya 26 ya maandamano ya kudai demokrasia ya Tiananmen mwaka 1989. Katika miaka ya hivi karibuni, baadhi ya tarakimu zimepotea kwenye mtandao wa Intaneti nchini China kwa sababu ya udhibiti wa taarifa. Tarakimu hizi ni 64, 89 na 535 —zenye kuunganisha kupata Mei 35, namna...
Kuhusu Uamuzi wa Mahakama wa Haki ya Kusaidiwa Kufa Nchini Afrika Kusini
Profesa Pierre de Vos anaingia rasmi kwenye mjadala mkali kuhusu uwezekano wa kumsaidia mtu kufa nchini Afrika Kusini baada ya Mahakama Kuu nchini humo kuamua kwamba mtu anayekufa ana haki ya kusaidiwa kufa na daktari ili aweze kuyahitimisha maisha yake: Ni muhimu kuona kwamba hukumu hii haimlazimishi mtu kuyakatisha maisha...
Ramani Hizi Zaonesha Mahali Walipotesewa na Kuuawa Wanahabari wa Kambodia
Kituo cha Haki za Binadamu cha kambodia kimezindua jarida linaloelezea ukiukwaji wa haki za binadamu unaofanywa kwa waandishi wa habari nchini Kambodia. Katiba ya nchini Kambodia inatoa uhuru wa kupashana habari lakini wanahabari wanazidi kunyanyaswa na kuuawa, hususani kwa waandishi wanaopasha habari kuhusiana na ukiukwaji wa maadili unaofanywa na maafisa...
ISIS Yashambulikia Kwa Mara Nyingine Msikiti wa Shia Nchini Saudi Arabia
kwenye dawati lakuthibitisha habari la Global Voices, mradi unaoendeshwa kwa ushirikiano kati ya Meedan Checkdesk, zana ya mtandaoni ya kufuatilia habari, na Global Voices Online, Joey Ayoub anaonesha miitikio ya awali kabisa kuhusu kupigwa bomu kwa msikiti wa pili wa Shia huko Dammam, Jimbo la Mashariki mwa Saudi Arabia, siku...
Je, Saudi Arabia Imelishambulia Bwawa la Kale la Marib Nchini Yemen?
Kuna taarifa zisizodhibitishwa zinazosema kwamba vikosi vya pamoja vya Kisaudi, ambavyo vimekuwa vikiishambulia Yemen kwa mabomu kwa zaidi ya miezi miwili sasa vimelilenga Bwawa la Marib, moja wapo ya maajabu makuu ya katika ulimwengu wa ubunifu wa kale wa kiufundi. Kwenye mtandao wa Twita, Hussain Albukhaiti anadai: Unconfirmed reports: #Saudi...
Uchaguzi wa FIFA Unaendelea
Pamoja na kutiwa nguvuni kwa maafisa kadhaa wa FIFA kufuatia mashitaka yaliyofunguliwa na Wizara ya Sheria ya Marekani, chombo hicho kinachosimamia kandanda duniani kimesema kwamba uchaguzi wake, ambao utaunda baraza la 65 la FIFA, utaendelea kama ulivyopangwa hivi leo. Rais wa FIFA aliye madarakani Sepp Blatter, ambaye ameongoza chombo hicho...
Lugha za Pili Zinazoongozwa Kuzungumzwa Zaidi Afrika
Don Osborne anajadili habari iliyowekwa kwenye tovuti ya Chuo Kikuu cha Olivet Nazarene ikionesha ramani ya “Lugha za pili kuzungumzwa zaidi duniani.” Anaeleza matatizo makuu kutokana na habari hiyo: Suala la kwanza ni kudhani kwamba “lugha inayozungumzwa zaidi kwenye nchi yoyote huwa wazi; mara nyingi, ni lugha ya taifa husika.”...
Tunayoyajua na Tusiyoyajua Baada ya Jaribio la Mapinduzi Nchini Burundi
Celebration and jubilation near Presidential offices in Bujumbura after the overthrow of Nkurunziza. #BurundiCoup pic.twitter.com/WhJzXKfS69 — Robert ALAI (@RobertAlai) May 13, 2015 Shangwe na vifijo karibu na ikulu ya Rais nchini Bujumbura baada ya kupinduliwa kwa Nkurunzisa. Kufuatia nia ya kugombea urais kwa kipindi cha tatu ya Rais wa Burundi...