Habari kutoka Muhtasari wa Habari na Matangazo
Ungana nasi kwa Mkutano wa Global Voices Tunis Novemba 1
Ungana nasi kwenye mkutano wa Global Voices nchini Tunis Novemba 1, 2014 kuanzia saa 3 asubuhi mpaka saa 7 mchana kwenye Maabara ya 404.
Misri, Palestina, China, India, Bangladesh, Ukraine Zashinda Katika Tuzo za Bobs
Washindi wa tuzo za The Bobs 2014 zilizoandaliwa na Deutsche Welle wametangazwa! Miradi ya mtandao kutoka Misri, Palestina, China, India, Bangladesh, Ukraine walichaguliwa kama washindi na baraza la waamuzi la kimataifa. Miradi katika lugha 14 ilishiriki kwenye akundi ya Blogu Bora, Harakati ya Kijamii Bora, Mwenye Ubunifu Zaidi na Uhalisi...
Kufuatilia Kongamano la Dunia la Demokrasia 2013
Kongamano la Dunia la Demokrasia kwa sasa linafanyika mjini Strasbourg, Ufaransa kwa mara ya ppili tangu lianze. Kauli mbiu ya mkutano wa mwaka huu ni “kuunganisha Taasisi na Wananchi katika Kizazi hiki cha dijitali”. Fuatilia mada nne na warsha 21 za mkutano kupitia alama ashiria #CoE_WFD.
Madagascar: Global Voices katika Kimalagasi Yapiga Hatua Kubwa
Mradi wa Lingua wa Global Voices katika lugha ya ki-Malagasi umechapisha mtandaoni posti yake ya 5,000. Mradi huo ulianza mwezi Septemba 12, 2007 ukiwa kati ya miradi ya mwanzo kabisa ya Mradi mkubwa wa Lugha za Kiafrika. Kwa sasa mradi huo unaendeshwa na watafsiri wa ki-Malagasi wapatao 16 miongoni mwao...
Global Voices Yashinda Tuzo Ya Highway Africa
Timu ya Global Voices inayoandika habari za Nchi za Afrika zilizo Kusini mwa Jangwa la Sahara imeshinda Tuzo ya Telekom Highway Africa katika kundi la “Blogu bora ya TEHAMA ya Kiafrika”. Mhariri wa Eneo hilo Ndesanjo Macha alikuwepo Afrika Kusini kuipokea tuzo hiyo (na kikombe cha ushindi!) tarehe 11 Sepetemba,...