· Oktoba, 2012

Habari kuhusu Picha kutoka Oktoba, 2012

Kuwait: Ni Maandamano Makubwa Kabisa Kuwahi Kutokea?

Mabomu ya kutoa machozi na maguruneti ya kumfanya mtu kupoteza fahamu yalitumika kutawanya maandamano ya kupinga mabadiliko ya sheria ya uchaguzi nchini Kuwait. Maandamano hayo yaliyofanyika siku ya Jumapili, na kuratibiwa kupitia katika mtandao wa Twita na yaliyowavutia takribani watu 150,000 kati ya watu milioni 3 ambao ndio idadi ya watu wa Kuwait. Taarifa za vyombo vya habari zinaichukulia idadi hii kuwa ni kubwa kabisa katika historia ya Falme za ghuba ndogo.

Venezuela: Tathmini za Baada ya Uchaguzi

  15 Oktoba 2012

Msisimko ulikuwa mkubwa sana usiku wa siku ya Jumapili baada ya matokeo rasmi ya uchaguzi wa Rais wa Venezuela kutangazwa. Sehemu ya nchi ilisherehekea kuendelezwa kwa 'Mapinduzi ya Venezuela' chini ya Rais Hugo Chávez, wakati upande mwingine ulilalamika kwa kushindwa tena kwenye uchaguzi huo.

Guatemala: Waandamanaji Wazawa 7 Wauawa Totonicapán

  13 Oktoba 2012

Raia wasiopungua 7 wameuawa, takribani watu 32 wamejeruhiwa na 35 walidhuriwa na sumu mnamo tarehe 4, Oktoba, 2012 wakati majeshi ya muungano yalipotumia nguvu kuwatawanya waandamanaji kutoka katika njia panda maarufu inayoeleka jiji la Guatemala City.

Venezuela: Picha za Siku ya Uchaguzi

  8 Oktoba 2012

Leo, mitandao ya kijamii nchini Venezuela inatoa taswira ya nchi hiyo kuwa ukingoni mwa zoezi muhimu. Pamoja na shuhuda mbalimbali, taarifa, tetesi na mapendekezo, majukwaa ya vyombo vya habari vya kijamii kama vile Twita, Facebook na Flickr yameonyesha picha zinazoonyesha ushiriki mkubwa wa watu katika kumchagua Rais ajaye wa Jamuhuri hiyo.

Venezuela: ‘Sura na Sauti’ za Uchaguzi

  8 Oktoba 2012

Kwa kutumia mfululizo wa picha na nukuu, mpiga picha wa Kireno Eduardo Leal anayateka mawazo na hisia za watu wa Venezuela kwa jinsi zinavyoeleza watakuwa wanampigia nani kura kuwa Rais katika uchaguzi uliofanyika Jumapili ya Oktoba 7.Kwa kutumia mfululizo wa picha na nukuu, mpiga picha wa Kireno Eduardo Leal anayateka mawazo na hisia za watu wa Venezuela kwa jinsi zinavyoeleza watakuwa wanampigia nani kura kuwa Rais katika uchaguzi uliofanyika Jumapili ya Oktoba 7.