Habari kuhusu Wanawake na Jinsia kutoka Februari, 2010
Misri: Mwanablogu apoteza kazi kwa kufichua ukweli kuhusu habari ya bikra za bandia
Mwanablogu ambaye pia ni mwanahabari wa Kimisri Amira Al Tahawi amefukuzwa kazi kwa kufichua ukweli kuhusu habari ya uongo juu ya bikra za bandia zinazotengenezwa China katika makala alioyoichapa kwenye yake, ndivyo wanavyodai wanablogu. Yafuatayo ni baadhi ya maoni kutoka kwenye ulimwengu wa blogu za Kimisri kuhusu kisa hicho.
Vazi la Burka Lauelemea Utaratibu wa Tamaduni Mbalimbali Kuishi Pamoja
Tangu mapendekezo ya kupiga marufuku uvaaji wa burqa au hijab huko Ufaransa, suala hilo limekuwa likitokota katika ulimwengu wa bloghu wa Australia. Mtangazaji wa redio katika mtindo wa kushtua umma, ambaye pia ni askari polisi wa zamani, alishutumiwa hivi karibuni juu ya kupinga kuvaliwa kwa hilo vazi la burqa.
Malaysia: Harakati za Kutovaa Nguo za Ndani Wakati Wa Siku ya Valentino
Wanafunzi kadhaa wa kike nchini Malaysia wanahamasisha "harakati za kutovaa nguo za ndani" katika siku ya Valentino. Kampeni hiyo imepata umaarufu mno kupitia ujumbe wa mtu kwa mtu na kwa kupitia intaneti. mamlaka za kidini hazijafurahishwa. Wanablogu wanatoa maoni.