· Februari, 2009

Habari kuhusu Vita na Migogoro kutoka Februari, 2009

Sudani: Maombolezo ya Mwandishi Maarufu wa Riwaya na Mahakama ya Kimataifa

Baada ya kimya kirefu, wanablogu wa Kisudani, wamerejea kwenye ulimwengu wa blogu kuongea, na kubadilishana mawazo kuhusu matukio ya hivi karibuni. Mawazo hayo yanayojumuishwa katika muhtasari huu ni pamoja na yale ya wanablogu tuliowazoea. Baada ya malalamiko kuhusu hali mbaya ya usalama wa afya kwenye Uwanja wa Ndege wa Khartoum, Msudani mwenye matumaini anaomboleza kifo cha mwandishi wa riwaya mashuhuri, Al- Tayeb Saleh.

Madagaska: Zaidi ya 25 Wauwawa Katika Maandamano Kuelekea Ikulu

  9 Februari 2009

Watu wapatao 25 walipigwa risasi na kuuwawa leo katika mji mkuu wa Madagaska, Antananarivo, wakati wa maandamano ya kuelekea ikulu ya nchi hiyo yaliyoitishwa na meya wa jiji Andry Rajoelina baada ya kujitangaza kama kiongozi wa serikali mpya ya mpito katika mkutano wa hadhara wa kisiasa. Katika majuma yaliyopita, ugombeaji wa nguvu za kisiasa kati ya Meya na Rais Marc Ravolamanana kumesababisha ghasia na uporaji.