Habari kuhusu Teknolojia kutoka Aprili, 2012
Bolivia: Wanaharakati Washinikiza Upatikanaji Nafuu wa Mtandao wa Intaneti
Nchini Bolivia, kuunganishwa na mtandao wa intaneti ni miongoni mwa huduma ghali zaidi duniani. Huduma hiyo haina kasi na bado haijaweza kupatikana kwa idadi kubwa ya watu. Kikundi cha wanaharakati kwa kutumia mtandao na nje ya mtandao kinadai huduma nafuu na bora zaidi.
Mali: Kimya cha Wanablogu wa Nchini Humo
Wakati mtandao wa intaneti umetawaliwa na blogu, ujumbe wa twita na video kutoka nchi mbalimbali, watumiaji wa intaneti wenyeji wa Mali wangali kimya. Mji mkuu, Bamako, umeathirika kwa kukatika kwa umeme kwa kile kinachodaiwa kuwa kuadimika kwa mafuta. Katika mazingira kama haya, kipaumbele si kutuma ujumbe, bali kutafuta kutafuta taarifa kuhusu viongozi wapya wa sehemu ya Kaskazini ya Nchi hiyo.
Ghana: Matumizi ya Vyombo vya Habari vya Kiraia katika Uchaguzi wa Mwaka 2012
Wananchi wa Ghana wanajitayarisha kwa ajili ya uchaguzi wa rais na wabunge ambao utafanyika tarehe 7 Disemba 2012, Jumuiya ya wanablogu wa Ghana imezindua mradi wa uanahabari wa kijamii ambao una nia ya kufunza wanaharakati, vikundi vya kisiasa na wanafunzi kutumia zana za uanahabari wa kijamii kwa ajili ya kwa ajili ya kuafuatilia na kuripoti shughuli za uchaguzi.