GlobalVoices katika

Technology

Hifadhi ya mada · 79 jumbe


Habari mpya Kuhusu Technology

6 Mei 2013

TEDXSão Tomé: Mkutano Wanukia São Tomé na Príncipe

TEDXSão Tomé

TEDXSão Tomé

Uandikishaji wa awali kwa ajili ya mkutano wa TEDXSão Tomé umezinduliwa rasmi. Mkutano huo una kaulimbiu inayosema “Visiwa Vimeunganishwa : São Tomé + Príncipe = Áfrika Vimeunganishwa na Ulimwengu” na utafanyika tarehe 20 Juni. Wasemaji katika mkutano huo waliothibitishwa ni pamoja: Dynka Amorim, Ismael Sequeira, Profesa Robert Drewes na Aoaní d'Alva. Tiketi linapatikana kwa Euro 20. Zaidi kuhusu mkutano huo tembelea ukurasa wa Facebook na tovuti [viungo vyote katika lugha ya Kireno].

24 Aprili 2013

Washindi wa Tuzo za Kwanza za Uandishi wa Kiraia Nchini Ghana

Soma makala hii.

Tumepata matokeo ya Tuzo za kwanza kabisa za Uandishi wa Kiraia nchini Ghana.

13 Aprili 2013

AZISE ya Uwazi Yajiandaa kwa Uchaguzi wa Jumapili Nchini Venezuela

Soma makala hii. Technology for Transparency Network

Wakati wapiga kura wa Venezuela wakijiandaa kuelekea kwenye uchaguzi wa mara ya pili katika kipindi cha miezi sita, kikundi cha Asasi Zisizo za Kiserikali kimekusanya nguvu ili kuhakikisha kuwa wanakuza uwazi katika mchakato wa uchaguzi.

22 Januari 2013

Jukwaa la Kiafrika Lenye Makala za Bure za Kitaaluma

Video inayoonesha namna www.hadithi.org inavyofanya kazi kuboresha upatikanaji wa zana za utafiti kwa Afrika

Januari 24, ni siku ambayo inategemewa kuwa ya kuzindua rasmi Hadithi, ambalo ni jukwaa la kuhifadhia zana za bure za kitaaluma mjini Nairobi, Kenya. Wasomi mbalimbali na wadau wa mitandao watakusanyika pamoja kujadili upatikanaji wa zana huru za kitaaluma katika elimu ya juu nchini Kenya. Hadithi itasaidia kutafuta, kuona na kushusha makala kutoka katika taasisi za kitafiti duniani kote. Kujiandikisha kwa tukio hili, itafute Hadithi mtandaoni kupitia Facebook na tovuti ya Eventbrite.

1 Januari 2013

Kuhusiana na Vuguvugu la Mabadiliko ya Umma

Gaurav Mishra anachambua nguvu ya vuguvugu la mabadiliko linaloanzia kwa watu wa kawaida na namna inavyofanya kazi kuleta mabadiliko chanya katika utendaji wa vyombo vikuu vya habari kwa kutumia vyombo vya habari vya kiraia.

30 Septemba 2012

Video jumbe
Mbinu za Kugundua Dawa Bandia katika Nchi Zinazoendelea

Soma makala hii.

Watu 700,000 hufa kila mwaka kwa kutumia dawa bandia za malaria na saratani pekee. Shirika la Afya Duniani, WHO linasema katika ripoti yake kuwa, mapato kutoka kwa dawa hizi kila mwaka hukaribia dola bilioni 200.

27 Agosti 2012

Mgogoro wa Umoja wa Ulaya: Kitabu cha Kwanza cha Global Voices cha Kieletroni

Soma makala hii.

"Umoja wa Ulaya katika Mgogoro" (EU in Crisis) ni chapisho letu la kwanza katika Mradi wa Vitabu wa Global Voices na ambao unahusisha makala bora zaidi kuhusu mazungumzo ya kijamii, ushiriki na uhamasishaji unaopewa nguvu na raia wanaopitia nyakati ngumu za kubana matumizi katika bara la kale zaidi na kwingineko.

7 Juni 2012

Kenya: Wanaharakati wapigana vita dhidi ya ufisadi kwa intaneti

Soma makala hii.

I Paid a Bribe ni njia mojawapo inayotumiwa na wanaharakati dhidi ya ufisadi nchini, kwa kutumia teknolojia mpya ili kuwawezesha kupata ripoti za utoaji wa hongo.' I paid a Bribe' imefuatia muundo wa ‘India Anti-Corruption Portal (IPAB)' na ni ushirkiano kati ya IPAB na Wamani Trust ya Kenya ili kuleta IPAB katika Afrika Mashariki na Kati.

30 Aprili 2012

Bolivia: Wanaharakati Washinikiza Upatikanaji Nafuu wa Mtandao wa Intaneti

Soma makala hii.

Nchini Bolivia, kuunganishwa na mtandao wa intaneti ni miongoni mwa huduma ghali zaidi duniani. Huduma hiyo haina kasi na bado haijaweza kupatikana kwa idadi kubwa ya watu. Kikundi cha wanaharakati kwa kutumia mtandao na nje ya mtandao kinadai huduma nafuu na bora zaidi.

Photos jumbe
Mali: Kimya cha Wanablogu wa Nchini Humo

Soma makala hii.

Wakati mtandao wa intaneti umetawaliwa na blogu, ujumbe wa twita na video kutoka nchi mbalimbali, watumiaji wa intaneti wenyeji wa Mali wangali kimya. Mji mkuu, Bamako, umeathirika kwa kukatika kwa umeme kwa kile kinachodaiwa kuwa kuadimika kwa mafuta. Katika mazingira kama haya, kipaumbele si kutuma ujumbe, bali kutafuta kutafuta taarifa kuhusu viongozi wapya wa sehemu ya Kaskazini ya Nchi hiyo.

Sehemu za Dunia

Nchi

Lugha