<?xml version="1.0" encoding="UTF-8"?>
<rss version="2.0"
	xmlns:content="http://purl.org/rss/1.0/modules/content/"
	xmlns:wfw="http://wellformedweb.org/CommentAPI/"
	xmlns:dc="http://purl.org/dc/elements/1.1/"
	xmlns:atom="http://www.w3.org/2005/Atom"
	xmlns:sy="http://purl.org/rss/1.0/modules/syndication/"
	xmlns:slash="http://purl.org/rss/1.0/modules/slash/"
	>

<channel>
	<title>Global Voices in Swahili &#187; Science</title>
	<atom:link href="http://sw.globalvoicesonline.org/category/topics/science/feed/" rel="self" type="application/rss+xml" />
	<link>http://sw.globalvoicesonline.org</link>
	<description>Dunia inaongea, je unasikiliza?</description>
	<lastBuildDate>Wed, 02 Dec 2009 12:35:07 +0000</lastBuildDate>
	<generator>http://wordpress.org/?v=2.8.4</generator>
	<language>en</language>
	<sy:updatePeriod>hourly</sy:updatePeriod>
	<sy:updateFrequency>1</sy:updateFrequency>
			<item>
		<title>Afya Duniani: Siku ya Vyoo Duniani Yatoa Harufu</title>
		<link>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/11/afya-duniani-siku-ya-vyoo-duniani-yatoa-harufu/</link>
		<comments>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/11/afya-duniani-siku-ya-vyoo-duniani-yatoa-harufu/#comments</comments>
		<pubDate>Wed, 25 Nov 2009 10:46:39 +0000</pubDate>
		<dc:creator>j nambiza tungaraza</dc:creator>
				<category><![CDATA[Brunei]]></category>
		<category><![CDATA[Development]]></category>
		<category><![CDATA[English]]></category>
		<category><![CDATA[Environment]]></category>
		<category><![CDATA[Ethiopia]]></category>
		<category><![CDATA[Feature]]></category>
		<category><![CDATA[Gender]]></category>
		<category><![CDATA[Health]]></category>
		<category><![CDATA[India]]></category>
		<category><![CDATA[Oman]]></category>
		<category><![CDATA[Science]]></category>
		<category><![CDATA[Singapore]]></category>
		<category><![CDATA[Thailand]]></category>
		<category><![CDATA[United Kingdom]]></category>
		<category><![CDATA[Weblog]]></category>

		<guid isPermaLink="false">http://sw.globalvoicesonline.org/?p=731</guid>
		<description><![CDATA[Ingawa inaweza kusikika kama masihara, Siku ya Vyoo Duniani inatilia maanani kwenye suala ambalo si la mzaha linalowakwaza karibu nusu ya watu wote duniani – ukosefu wa vyoo na mfumo wa usafi.]]></description>
			<content:encoded><![CDATA[<em>Ilichapwa kwanza na<a href="http://globalvoicesonline.org/author/juhie-bhatia/">Juhie Bhatia</a>  &middot; Imetafsiriwa na <a href='http://sw.globalvoicesonline.org/author/j-nambiza-tungaraza/'>j nambiza tungaraza</a> &middot;  <a href='http://globalvoicesonline.org/2009/11/19/global-health-world-toilet-day-raises-a-stink/'>Angalia ujumbe mama</a></em> 
<br /><p><img alt="" src="http://globalvoicesonline.org/wp-content/uploads/2009/11/1019110937_99be0d6df3_m.jpg" title="Tiled Toilet" class="alignright" width="180" height="240" /><br />
Ingawa inaweza kusikika kama vile masihara, <a href="http://www.worldtoiletday.com/">Siku ya Vyoo Duniani</a> inatilia maanani kwenye suala ambalo si la mzaha linalowakwanza karibu nusu ya watu wote duniani – ukosefu wa vyoo na mfumo wa usafi.</p>
<p>Watu wanaweza kuwa wanaona aibu kuongea wazi kuhusu hili suala, lakini kila mmoja hujisaidia, kwenye choo au la. Siku ya Vyoo Duniani inasaidia watu kusherehekea umuhimu wa usafi na kuwaelimisha watu bilioni 2.5 ambao hawana vyoo na mfumo wa usafi wenye uhakika. Video hii iliyotengenezwa na asasi isiyo ya kibiashara WaterAid <a href="http://www.youtube.com/watch?v=-T2eH7zrDJg">inaonyesha</a> starehe ya kuwa na choo.</p>
<p>Kusherehekea kopo lako kunaweza kuonekana kama ujinga, lakini kutokuwa na kopo siyo tu kunaweza kukusababishia aibu, kukosa heshima na masuala mengine ya kiusalama, bali pia kunaweza kukusababishia magonjwa yanayoweza kuzuilika na hata kifo. Pale watu wanapokosa vyoo, wanalazimika kujisaidia mitaani kweupe, kwenye viwanja au vichochoroni. Matokeo? Uchafuzi wa maji ya kunywa na vyanzo vya chakula, jambo ambalo linapelekea hatari nyingi za kiafya. Ukosefu wa mfumo wa usafi ndiyo sababu kubwa ya maambukizi na huua <a href="http://worldtoiletday.com/about.html">watu milioni 1.8</a>, hasa watoto, kila mwaka. Hata nchi zenye vyoo vya kutosha huwa zinakabiliana na matatizo yanayotokana na vyoo vichafu vya umma mpaka utupaji majitaka unaoharibu njia za maji.</p>
<p>Vanilla, anayeblogu kwenye <em>Let&#39;s Look At It This Way</em> kutokea Singapore, <a href="http://whatsayyouvanilla.blogspot.com/2009/11/world-toilet-day.html">anasema</a> kuwa watu wanapaswa kutilia maanani vyoo:</p>
<blockquote><p> “ Ninajua kwamba hii ni mada chafu kwa watu wengi. Ni bahati mbaya kwamba hii mada bado ni ‘mwiko’ kuiongelea wazi na watu wengi hawana uelewa kuhusu ukubwa wa tatizo. Ninashindwa kuelewa ni kwa jinsi gain hii inaweza kuwa mada isiyo na maana wakati, kwa wastani, huwa tunakwenda chooni mara 2500 kwa mwaka, au mara 6-8 kwa siku. Wakati wa maisha yetu, hutumia muda wa miaka 3 vyooni.&#8221; </p></blockquote>
<p>Chini ya maandalizi ya asasi isiyo ya kibiashara <a href="http://worldtoiletday.com/wto.html">The World Toilet Organisation</a>, Siku ya Vyoo Duniani inasherehekewa dunia nzima kwa matukio mbalimbali. Ili kuuelimisha umma zaidi, wiki hii WaterAid <a href="http://wateraidnews.blogspot.com/2009/11/launch-of-new-iphone-application-brings.html">ilitangaza</a> uzinduzi wa zana mpya ya Kutafutia Vyoo nchini Uingereza ya simu za mkononi za iPhone. Zana hiyo ya bure inawasaidia Waingereza kutafuta choo cha umma kilicho karibu zaidi  wakati pia inawakumbusha jinsi walivyo na bahati ya kuwa na vyoo safi na salama. Tukio kubwa zaidi leo, linaloitwa <a href="http://worldtoiletday.com/squat/">Mchuchumao Mkubwa</a>, linawataka watu wasimame na wachuchumae kwa dakika moja katika sehemu za umma ili kuongeza utambuzi. <a href="http://www.flickr.com/groups/1216217@N24/">Picha</a> hizi zinaonyesha watu waliochuchumaa dunia nzima, pamoja <a href="http://www.flickr.com/photos/25532596@N04/4116769214/in/pool-1216217@N24">na hii ya</a> watoto wa chekechea huko Singapore:</p>
<p><img alt="" src="http://globalvoicesonline.org/wp-content/uploads/2009/11/4116769214_1b876f8640.jpg" title="Singapore Squat" class="aligncenter" width="500" height="273" /></p>
<p>Blogu inayotokea Brunei, <em>the world according to panyaluru </em>…, pia <a href="http://panyaluru.blogspot.com/2009/11/cut-paste-toilets.html">inaonyesha kuridhika</a> na vyoo kwa kuliweka suala hili kwenye muktadha sawia:</p>
<blockquote><p> “Fikiria ikiwa tunatembea mbele ya mlolongo wa maduka kule Kiulap au Gadong. Mara tu tumbo linaunguruma kama vile ambavyo haujawahi kusikia. Halisimami kukupa mapumziko. Linaunguruma na kuunguruma. Ngurumo. Taa ni ya manjano tayari kubadilika kuwa ya kijani. Lakini hakuna vyoo unavyoviona. Hakuna hata choo kimoja cha umma kwenye mlolongo wa maduka… ongezea pia kuwa hakuna maji, karatasi ya chooni, hakuna chochote! Hiyo inaweza kuwa siku mbaya zaidi katika maisha yako, jinamizi baya, au jinamizi baya zaidi ya yale yaliyowakuta watoto kwenye filamu za Elm Street. Katika siku hii, hebu na tuvienzi vyoo.”</p></blockquote>
<p>Ukiachilia mbali upande makini wa suala hili, watu wengi wametumia mzaha kuadhimisha siku ya Vyoo Duniani. Huko Uingereza blogu ya <em>London City Drains</em> imeweka chemsha bongo ya vyoo yenye maswali 10, wakati katika <a href="http://www.youtube.com/watch?v=zx2oVPjnUXs">video</a> hii mwalimu wa sekondari Matt Cheplic anaimba kuhusu siku hii.</p>
<p>Baadhi ya wanablogu wanasema kuwa vyoo pekee vinaweza visiwe jibu. Sandhya, anayeblogu kwenye <em>Maradhi Manni </em>nchini India, <a href="http://maradhimanni.blogspot.com/2009/11/big-squat-to-take-stand-on-sanitation.html">anasema</a> wanaume wengi hawatumii vyoo vilivyopo:</p>
<blockquote><p>Kwenye mji kama Chennai, ambako hali ya hewa ni ya joto kwa karibu miezi 10 ya mwaka, huwaona wanaume wanakojoakando ya barabara kila wakati. Wkati wanawake wanaweza kujidhibiti  na kwenda nyumbani kujisaidia, kwa nini wanaume hawawezi kufanya hivyo, sijui kwa nini. Kwa hiyo, kwanza watu wote wanabidi wapigwe faini kali kwa kufanya kosa hili (naam, ni kosa) pale pale wanapokamatwa. Nimewahi kuwaona wakifanya hivyo kwenye ukuta wa vyoo vya umma! Kule Srinagam, nimewahi kuwaona wakikojoa kwenye ukutra wa boma la hekalu pamoja na kuwa kila mtaa unaolizunguka hekalu una vyoo, ambavyo vilikuwa visafi, lakini vya kulipia!”</p></blockquote>
<p>Wakati ukosefu wa mfumo wa usafi unaathiri kila mtu, miiko inayozunguka suala la vyoo inawaathiri vikubwa wanawake zaidi ya  wengine. <a href="http://worldtoiletday.com/squat">Katika baadhi ya nchi</a>, staha huwalazimisha wanawake kufanya shughuli zao kwenye makonde kabla ya jua kuchomoza au kujizuia mpaka mpaka baada ya jua kuzama, jambo ambalo linasababisha madhara ya kiusalama na kiafya. Joanne Sprague, anayeblogu kwenye <em>Overturning Boulders</em> nchini India, <a href="http://overturningboulders.blogspot.com/2009/11/but-where-do-women-do-their-business.html">anabaini</a> kuwa wanawake hawapo kwenye mzunguko wa kwenda haja asubuhi mijini Chennai, wakati huko Ethiopia blogu ya <em>AN ADVENTURE IN ADDIS</em> <a href="http://anadventureinaddis.com/2009/11/17/world-toilet-day/">inabaini </a>hali kama hiyo pia:</p>
<blockquote><p>“Nimekuwa nikisikia mara nyingi juu ya ukosefu wa vyoo kwa wanawake au ukosefu wa vyoo kwa ujumla; kwamba wasichana wa rika la kuwa wali huko mashambani huamka saa 10 za alfajiri kwenda nje kwenye giza kufanya shughuli zao ili wasitaniwe na wavulana shuleni au huacha kwenda shule kabisa. Wanaume hukojoa kila mahali, sigara mkononi na kuna kuna dhana kuwa wanawake hawapaswi kufanya hivyo, kama wanafikiriwa hata kidogo… ninataka kuona bango kubwa kwa lugha ya Ki-Amhara linalosema “wasichana nendeni pia’ lenye picha ya mwanasesere anayevutia wa kike aliyeketi chooni.” </p></blockquote>
<p>Kusherehekea Siku ya Vyoo Duniani, mwanablogu Jonathan Stray, anawachukua wasomaji kwenda <a href="http://jonathanstray.com/world-toilet-day">ziara ya kimataifa ya vyoo </a>ambavyo ameshawahi kuvizuru, kuanzia Thailand na Uingereza mpaka Afrika Magharibi na Oman, na anahitimisha:</p>
<blockquote><p> “Sisi watu wa Magharibi na vyoo vyetu vya kuvuta na karatasi za chooni na chemchemi zinazong’ara ni tofauti na wengine wengi; wengine wote waliobaki hufikiri kuwa bafu ni sehemu iliyolowana, inayonuka, ikiwa wanayo hayo mabafu. Choo kizuri kinamaanisha kuwa pengine una kiwango kizuri cha maisha, kwa hiyo burudika na choo chako. Siku njema ya Vyoo Duniani!  </p></blockquote>
<p><em>Picha ya <a href="http://www.flickr.com/photos/nedrichards/1019110937/">choo cha vigae</a> imepigwa na <a href="http://www.flickr.com/photos/nedrichards/">nedrichards</a> kwenye Flickr, Haki Miliki Huru.</em></p>
]]></content:encoded>
			<wfw:commentRss>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/11/afya-duniani-siku-ya-vyoo-duniani-yatoa-harufu/feed/</wfw:commentRss>
		<slash:comments>0</slash:comments>
		</item>
		<item>
		<title>Ulaya: Siku ya Kimataifa ya Bahari Nyeusi</title>
		<link>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/11/ulaya-siku-ya-kimataifa-ya-bahari-nyeusi/</link>
		<comments>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/11/ulaya-siku-ya-kimataifa-ya-bahari-nyeusi/#comments</comments>
		<pubDate>Tue, 03 Nov 2009 11:47:14 +0000</pubDate>
		<dc:creator>j nambiza tungaraza</dc:creator>
				<category><![CDATA[Bulgaria]]></category>
		<category><![CDATA[Cyber-Activism]]></category>
		<category><![CDATA[English]]></category>
		<category><![CDATA[Environment]]></category>
		<category><![CDATA[Georgia]]></category>
		<category><![CDATA[Governance]]></category>
		<category><![CDATA[International Relations]]></category>
		<category><![CDATA[Middle East & North Africa]]></category>
		<category><![CDATA[Romania]]></category>
		<category><![CDATA[Roundups]]></category>
		<category><![CDATA[Russia]]></category>
		<category><![CDATA[Science]]></category>
		<category><![CDATA[Turkey]]></category>
		<category><![CDATA[Ukraine]]></category>

		<guid isPermaLink="false">http://sw.globalvoicesonline.org/?p=504</guid>
		<description><![CDATA[Ilichapwa kwanza naVeronica Khokhlova  &#183; Imetafsiriwa na j nambiza tungaraza &#183;  Angalia ujumbe mama 
Katika Th!nk About It, Adela anaandika kuhusu Siku ya Kimataifa ya Bahari Nyeusi.
]]></description>
			<content:encoded><![CDATA[<em>Ilichapwa kwanza na<a href="http://globalvoicesonline.org/author/neeka/">Veronica Khokhlova</a>  &middot; Imetafsiriwa na <a href='http://sw.globalvoicesonline.org/author/j-nambiza-tungaraza/'>j nambiza tungaraza</a> &middot;  <a href='http://globalvoicesonline.org/2009/11/03/zimbabwe-is-tsvangirai-righting-sadcs-wrongs/'>Angalia ujumbe mama</a></em> 
<br /><p>Katika <em>Th!nk About It</em>, Adela <a href="http://climatechange.thinkaboutit.eu/think2/post/international_black_sea_action_day/#When:20:43:06Z">anaandika</a> kuhusu Siku ya Kimataifa ya Bahari Nyeusi.</p>
]]></content:encoded>
			<wfw:commentRss>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/11/ulaya-siku-ya-kimataifa-ya-bahari-nyeusi/feed/</wfw:commentRss>
		<slash:comments>0</slash:comments>
		</item>
		<item>
		<title>Afrika ya Kusini: VVU na UKIMWI na mabadiliko ya sera</title>
		<link>http://sw.globalvoicesonline.org/2008/10/afrika-ya-kusini-vvu-na-ukimwi-na-mabadiliko-ya-sera/</link>
		<comments>http://sw.globalvoicesonline.org/2008/10/afrika-ya-kusini-vvu-na-ukimwi-na-mabadiliko-ya-sera/#comments</comments>
		<pubDate>Sun, 26 Oct 2008 08:21:20 +0000</pubDate>
		<dc:creator>Deogratias Simba</dc:creator>
				<category><![CDATA[English]]></category>
		<category><![CDATA[Feature]]></category>
		<category><![CDATA[General]]></category>
		<category><![CDATA[Health]]></category>
		<category><![CDATA[Politics]]></category>
		<category><![CDATA[Science]]></category>
		<category><![CDATA[South Africa]]></category>
		<category><![CDATA[Sub-Saharan Africa]]></category>
		<category><![CDATA[Weblog]]></category>

		<guid isPermaLink="false">http://sw.globalvoicesonline.org/?p=33</guid>
		<description><![CDATA[Ilichapwa kwanza nahttp://globalvoicesonline.org/author/juhie-bhatia/  &#183; Imetafsiriwa na Deogratias Simba &#183;  Angalia ujumbe mama 

Mwishoni mwa mwezi Septemba, Barbara Hogan, aliteuliwa na Rais wa mpito Kgalema Motlanthe kuwa waziri mpya wa afya wa Afrika ya Kusini, akichukua nafasi ya mtangulizi wake mwenye utata mwingi, Manto Tshabalala-Msimang. Wanaharakati wa masuala ya UKIMWI na raia wengi wa [...]]]></description>
			<content:encoded><![CDATA[<em>Ilichapwa kwanza na<a href="Juhie Bhatia">http://globalvoicesonline.org/author/juhie-bhatia/</a>  &middot; Imetafsiriwa na <a href='http://sw.globalvoicesonline.org/author/simbadeo/'>Deogratias Simba</a> &middot;  <a href='http://globalvoicesonline.org/2008/10/19/south-africa-a-new-era-in-the-fight-against-hivaids/'>Angalia ujumbe mama</a></em> 
<br /><p><img src='http://globalvoicesonline.org/wp-content/uploads/2008/10/166594216_8891fa8210_m1.jpg' alt='' class='alignright' /><br />
Mwishoni mwa mwezi Septemba, Barbara Hogan, <a href="http://www.mediaclubsouthafrica.com/index.php?option=com_content&#038;view=article&#038;id=746:cabinet260908&#038;catid=44:developmentnews&#038;Itemid=111">aliteuliwa</a> na Rais wa mpito Kgalema Motlanthe kuwa waziri mpya wa afya wa Afrika ya Kusini, akichukua nafasi ya mtangulizi wake mwenye utata mwingi, Manto Tshabalala-Msimang. Wanaharakati wa masuala ya UKIMWI na raia wengi wa Afrika ya Kusini wana matumaini makubwa kwamba hatua hii huenda ikaashiria mabadiliko ya sera za serikali kuhusu suala la VVU na UKIMWI.</p>
<p>Hogan, mwanamama mwanaharakati mkongwe dhidi ya ubaguzi wa rangi na mwanachama wa muda mrefu wa ANC, yaani African National Congress, hapo awali alikuwa mwenyekiti wa kamati ya kusimamia masuala ya fedha. Tangu kuteuliwa kwake kuwa waziri wa afya, amebadili mwelekeo wa serikali iliyopita kuhusu VVU na UKIMWI na <a href="http://www.plusnews.org/Report.aspx?ReportId=80715">kuapa</a><br />
kutoa kipaumbele kwa masuala ya UKIMWI. Jambo hili limezua mshawasha miongoni mwa raia wa Afrika ya Kusini, ambapo wengi wao wanaamini kwamba Hogan anaweza kuimarisha vita vya nchi dhidi ya VVU na UKIMWI kwa kufuata sera yenye kuzingatia mtizamo wa kisayansi zaidi. Katika picha hii ya <a href="http://www.beatit.co.za/flash/popup.php?videourl=http://www.youtube.com/v/Ml0baEkwhyA">video</a>, wanaharakati wa masuala ya UKIMWI wanashangilia uteuzi wa Hogan katika nafasi yake hiyo mpya.</p>
<p>Siku za nyuma Hogan alipata <a href="http://www.tac.org.za/community/node/2414">kumkosoa waziwazi </a>Rais wa zamani Thabo Mbeki na msimamo wake juu ya sera ya VVU na UKIMWI. Wastani wa watu milioni 5.7 nchini Afrika ya Kusini wanasemekana <a href="http://www.unaids.org/en/CountryResponses/Countries/south_africa.asp">kuishi na VVU</a> na kiasi cha watu 350,000 walifariki kutokana na UKIMWI mwaka jana nchini humo (wastani wa watu 1,000 kila siku). Kwa upande mwingine Tshabalala-Msimang amelaumiwa vikali kwa kutofanya juhudi za kutosha kukabili tatizo la VVU na UKIMWI nchini humo. Waziri huyo wa zamani wa afya alihamasisha matumizi ya vyakula kama vile beetroot, vitunguu saumu na vinginevyo kama tiba ya VVU na UKIMWI, jambo lililosababisha watu kumbatiza jina la &#8220;Dkt Beetroot&#8221;, na zaidi <a href="http://bunpai.com/2008/10/07/new-era/">ameshutumiwa</a> kwa kusababisha mkanganyo kuhusu matumizi ya dawa za kurefusha maisha (ARV). </p>
<p>Stephen, akiandika kwenye tovuti ya <em>irreverence</em>, <a href="http://www.irreverence.co.za/2008/09/three-cheers-for-barbara-hogan/">alimuita</a> Tshabalala-Msimang kama aibu ya taifa na papo hapo akimwita Hogan kama tumaini lililorejea. Ciaran Parker, akitumia blogu yake ya <em>Ciaran’s Peculier [sic] Blog</em>, <a href="http://ciaranparker.com/2008/09/26/bye-bye-dr-beetroot/">anafafanua</a> kuhusu msimamo wa Tshabalala-Msimang usiokubaliwa na wengi:</p>
<blockquote><p>“Ingawa Kgalema Motlanthe ameahidi kutoleta mabadiliko makubwa, bado ameatosa baadhi wa mawaziri wenye utata mkubwa waliokuwa kwenye serikali ya Mbeki. Mmoja wao akiwa ni Waziri wa Afya, Dkt Manto<br />
Tshabalala-Msimang, aliyekuwa mwananadharia mkubwa katika hoja ya Mbeki ya sera za kukana uwepo wa UKIMWI. Serikali ya Mbeki ilikataa katakata kuona uhusiano uliopo kati ya VVU na UKIMWI, na waziri wake wa afya alijenga hoja kwamba hata dawa za kurefusha maisha, ambazo kwa kweli zimeonyesha kusaidia katika juhudi za kukabili gonjwa hili, zilikuwa ghali mno &#8230; Wataalamu wa afya wanaofanya kazi nchini Afrika ya Kusini na ambao walipingana waziwazi na nadharia za kushangaza za waziri huyu walijikuta wakifanywa kuwa wahanga.&#8221; </p></blockquote>
<p>Mapema juma lililopita, wakati wa  uzinduzi wa <a href="http://www.hivvaccineenterprise.org/conference/2008/">mkutano juu ya Chanjo ya UKIMWI ya Kimataifa ya 2008 </a> (International AIDS Vaccine 2008) huko Cape Town, Hogan, <a href="http://www.tac.org.za/community/node/2421">alitangaza hadharani </a>kwamba VVU husababisha UKIMWI na kwamba ni lazima kukabiliana nao kwa kutumia dawa za hospitalini. Pia alieleza kwamba serikali ilikuwa na nia ya dhati<br />
kuongeza nguvu katika programu za kuzuia uambukizaji wa kutoka kwa mama kwenda kwa mtoto, dawa zinazozuia akina mama wajawazito wenye VVU kuwapatia watoto wao ambao hawajazaliwa maambukizo na kueleza kwamba chango madhubuti ya VVU ilikuwa ikihitajika mno.</p>
<p>Wanasayansi, wanaharakati na wanablogu wengi wameeleza furaha yao kufuatia hotuba iliyotolewa na Hogan. Haley, akiblogu katika tovuti inayoitwa <em>ujasura kama mwanafunzi balozi</em>, ana hili la <a href="http://whereishaley.blogspot.com/2008/10/hallelujah-south-african-health.html">kusema</a>:</p>
<blockquote><p>“Kusema kweli, watu wengi ninaozungumza nao wanashangazwa na jambo hili - kwamba maafisa wa serikali waliochaguliwa kwa njia za kidemokrasi wanakana fikra &#8230; kwamba &#8230; VVU husababisha UKIMWI. Hata hivyo, kwa bahati mbaya, hapa Afrika ya Kusini hivyo ndivyo hali ilivyokuwa &#8230; lakini sasa mambo yamebadilika, msimamo si huo tena.”</p></blockquote>
<p>Ray Hartley, anayeandika katika <em>The Times, Afrika ya Kusini</em>, anablogu <a href="http://blogs.thetimes.co.za/hartley/2008/10/14/hogans-simple-bold-statement-ends-era-of-aids-denialism/">akiongeza</a>: </p>
<blockquote><p>“‘Tunajua kwamba VVU husababisha UKIMWI.&#39;</p>
<p>Kwa kauli hii, Waziri wa Afya, Barbara Hogan, amehitimisha muongo mzima wa aibu ya kukana uwepo wa UKIMWI jambo ambalo limeigharimu Afrika ya Kusini idadi isiyohesabika ya maisha ya binadamu, wakati huohuo wale waliokuwa wakiishi na VVU wakiishia kuishi kana kwamba kwenye kivuli chao wenyewe.”</p></blockquote>
<p>Ni vigumu kueleza idadi kamili ya watu walioathiriwa na sera zilizopita juu ya VVU na UKIMWI, lakini Shirika la Treatment Action Campaign (TAC) (Kampeni ya Kutetea Tiba) <a href="http://www.tac.org.za/community/node/2414">linakadiria</a> kwamba kiasi cha raia milioni mbili wa Afrika ya Kusini walikufa kutokana na kuugua UKIMWI katika kipindi ambapo Mbeki alikuwa madarakani, na kwamba walau jumla ya vifo 300,000 vingeweza kuepukwa endapo tu angetimiza baadhi ya mambo ya msingi ya kikatiba. Baadhi ya wanablogu wanasema kwamba wote wawili, Mbeki na Tshabalala-Msimang wametapakaa damu mikononi mwao. Soneka Kamuhuza, anayeandika kupitia blogu ya <em>Things That Make You Go Mmmh!</em> <a href="http://thingsthatmakeyougommmh.blogspot.com/2008/10/mbeki-war-criminal.html">anamshutumu</a> vikali Mbeki.</p>
<blockquote><p>“Umawazo mgando wao [Mbeki na Tshabalala-Msimang], umbumbumbu wa kukusudia na kujitia kwao kuwa wanyofu kulichochea tu uendelevu wa janga hili. Kutumia njia ya kutazama tatizo zima kwa upana badala ya chanzo chake, pasipo kuingiza na njia nyingine, hakuwezi kuwa njia madhubuti ya kutibu VVU, waliingiza nchi katika wakati mgumu kwa kutumia umbumbumbu wao ambao waliulinda kwa njia zote. Hivi sasa inakadiriwa kwamba Afrika ya Kusini inaongoza duniani kwa kuwa na idadi kubwa ya watu wanaoishi na VVU. Kwa namna fulani, naona ushawishi wa Mbeki katika jambo hili &#8230; Katika nchi ambayo ina utajiri mkubwa wa maliasili, amehadaa rasilimali watu iliyo muhimu sana, kwa kuwanyima fursa ya watu kuamua na kuanza kupambana na tatizo hili la UKIMWI kikamilifu.”</p></blockquote>
<p>Wengi wanaamini kwamba Hogan atarekebisha mambo yaliyoharibika kwa sehemu fulani. Makala katika <em>Peripheries</em> <a href="http://www.peripheries.org/2008/09/26/south-africa-appoints-new-health-minister/">inaonyesha kwamba </a>watu wanatarajia kwamba wakati wa kuwa na ukanaji wa UKIMWI huku ukipewa nguvu na msukumo wa kisiasa nchini Afrika ya Kusini tayari umefikia kikomo. Hata hivyo, wapo ambao hawako kupaparikia mambo haraka hivyo. BillyC, akitoa maoni yake juu ya makala iliyoandikwa katika <em>The Times, la Afrika ya Kusini </em><a href="http://blogs.thetimes.co.za/hartley/2008/10/14/hogans-simple-bold-statement-ends-era-of-aids-denialism/">anasema</a>:</p>
<blockquote><p>“Barbara Hogan ana kazi kubwa mbele yake ili kurekebisha mambo ambayo kwa kiasi fulani tayari amekwishasababisha madhara kwa mfumo wa afya katika uangalizi wa Manto. Uwezo wa wafanyakazi, ari ya kazi, na viwango vya utendaji ukiachia mbali sera za afya na sheria, yote ni mambo ambayo hayana budi kushughulikiwa. Zaidi ya hilo, kuna uhamasishaji wa matumizi ya dawa na upungaji pepo wa kivuduu, vilevile uhusianishaji wa kishetani na sayansi ya magharibi vyote vikiwa vimejikita sawasawa katika mfumo wa kufikiri wa taifa. Itachukua miaka mingi ya kazi ngumu, yenye kujaa ujasiri na unyoofu ili kuturejesha katika mfumo wa afya ulio wa heshima na wenye ufanisi. Tumwombee Barbara Hogan apate kasi. Kusema kweli anaihitaji.”</p></blockquote>
<p><em>Picha ya <a href="http://flickr.com/photos/mvcorks/166594216/">Utepe wa Ukimwi wa Afrika ya Kusini </a>imetoka kwa <a href="http://flickr.com/photos/mvcorks/">mvcorks</a> katika mtandao wa picha wa Flickr.</em></p>
]]></content:encoded>
			<wfw:commentRss>http://sw.globalvoicesonline.org/2008/10/afrika-ya-kusini-vvu-na-ukimwi-na-mabadiliko-ya-sera/feed/</wfw:commentRss>
		<slash:comments>0</slash:comments>
		</item>
	</channel>
</rss>
