Eman katika AquaCool anatoa maoni kuhusu mtaa wa kwanza kupata jina linalotokana na huduma ya Twita, katika kambi ya wakambizi huko ukingo wa Magharibi.
Habari mpya Kuhusu Refugees
12 Februari 2013
Hali ya Hatari kwa Watoto nchini Syria: Namna Utakavyo Saidia.
Hadi sasa,inakadiriwa watoto 4,355 wameshauawa katika mgogoro unaoendelea hivi sasa nchini Syria. Mapema wiki hii, tulitoa taarifa juu ya madhila wanayokabiliana nayo watoto wa Syria kufuatia vita hii inayoisambaratisha nchi yao vipande vipande. Leo tunaangalia namna ambavyo watu wanaweza kusaidia kukabiliana na baadhi ya changamoto wanazokumbana nazo.
11 Januari 2012
Afrika: TEKNOHAMA Kwa Ajili ya Wakimbizi na Watu Wasio na Makazi
Barani Afrika na kwingineko TEKNOHAMA imeondokea kuwa nyenzo muhimu wakati wa matatizo wakati teknolojia kama vile Ujumbe mfupi wa Simu za Mkononi, VOIP, na Simu za mkononi zinapozidi kuwa na manufaa kwa wakimbizi na kwa watu waliokosa makazi.
4 Januari 2012
Suluhisho la Kiradikali la Umaskini Duniani: Ufunguzi wa Mipaka
Wataalamu kadhaa wanasema kuwa umaskini uliokithiri hauepukiki. Suluhisho la kiradikali zaidi la kupunguza umaskini kwa haraka duniani kwa wataalamu wengi wa uchumi ni kufungua mipaka kati ya nchi na kuruhusu wafanyakazi kuhamia sehemu ambazo nguvukazi inahitajika zaidi.
27 Julai 2010
Palestina: Mateso ya Kuwa Uhamishoni
Wakimbizi wa Kipalestina ni miongoni mwa watu ambao wamejikuta wakikimbilia uhamishoni ulimwenguni kote, Umoja wa Mataifa unatoa msaada kwa jumla ya wakimbizi waliosajiliwa wapatao milioni 4.7 katika ukanda unaokaliwa kwa nguvu huko Palestina, Jordan, Lebanoni na Syria. Mamilioni ya wakimbizi wa Kipalestina na wale walioteguliwa kutoka kwenye makazi yao wanaishi sehemu mbalimbali duniani. However, their Hata hivyo, watu hawa daima mioyo yao ipo nyumbani kwao, au kwa wazazi au mababu na mabibi zao waliobaki nyuma. Wanablogu wawili wa huko Gaza wameandika kuhusu mateso ya kuwa uhamishoni.
29 Disemba 2009
Rwanda: Video za Wanaojitolea
Mfululizo wa video zilizopakiwa na mtumiaji kdarpa kwenye YouTube, zinaonyesha wafanyakazi wa kujitolea na watu waliokutana nao wakiwa safarini nchini Rwanda ambapo walifanya kazi na jamii za sehemu hiyo.
28 Disemba 2009
Palestina/Gaza: Matayarisho ya Maandamano ya Uhuru Gaza
Ni kama wiki moja hivi mpaka Maandamano ya Uhuru Gaza yatakapoanza. Lengo lake ni kuonyesha mshikamano na Wapalestina na kuongeza ufahamu kuhusu vikwazo vinavyoizingira Gaza. Katharine Ganly anatazama baadhi ya matukio yaliyotokea katika maandalizi ya maandamano hayo.
15 Novemba 2009
24 Oktoba 2009
Uanaharakati na Umama Barani Asia

Je, mwanamke anatoa sadaka zipi ili kupigania jambo analiamini? Je, watoto wake wanaathiriwa vipi na mateso yanayoelekezwa kwake? Makala hii inachambua kwa kifupi maisha ya wanawake wanaharakati katika Asia ambao pia ni ma-mama.
11 Oktoba 2009
Australia: Wanawake wa Kenya wakataliwa haki ya ukimbizi
Wanawake wawili wanakabiliwa na uwezekano wa kutimuliwa kutoka Australia baada ya maombi yao ya kuomba hifadhi kukataliwa, pamoja na hatari wanayoweza kuipata ya kulazimishwa tohara ya kike ikiwa watarudishwa nyumbani.
4 Oktoba 2009
Indonesia: Tetemeko Kubwa Laikumba Sumatra
Mji wa mwambao wa Padang, Sumatra Magharibi umeharibiwa tena na tetemeko la ardhi.




























Kiungo cha RSS kwa Refugees 






mambo vipi wanablog muko powa wote.kama mumenisoma nijibuni.
Asante. Nimepita hapa natafuta japan na china wamemalizaje ugomvi wao kuhusu visiwa,pia chanzo cha ugomvi...