Habari kuhusu Maandamano kutoka Februari, 2014
Orodha ya Waliouawa Katika Maandamano ya Venezuela Yapatikana kwa Lugha Tano
Katika blogu ya Panfleto Negro [es], John Manuel Silva na Emiliana Duarte wanafuatilia orodha ya vifo vilivyotokea kufuatia maandamano yanayoendelea nchini Venezuela. Orodha hiyo -ambayo awali ilikuwa kwa lugha ya Kihispania-imetafsiriwa kwenda lugha ya Kiingereza, Kijerumani, Kiitaliano/a> na Kifaransa.
Caribian: Namna Vyombo vya Habari Vinavyoathiri Mitazamo
Venezuela na Haiti zimekuwa zikikabiliwa na maandamano ya kupinga serikali. Hata hivyo, ukuzaji wa mgogoro wa Venezuela unaofanywa na vyombo vya habari vya kimataifa na ukimya wake kwa mgogoro wa Haiti, unaibua maswali muhimu kuhusu kuyumba kwa Marekani katika kuimaisha tunu ya haki za binadamu na demokrasia. Kevin Edmonds anatoa...
PICHA: Vyama vya Wafanyakazi na Asasi za Kiraia Vyaandaa Mgomo
Huku ukiwa umepangiliwa ufanyike mwanzo wa kipindi cha pili cha Rais Park Geun-hye madarakani, takribani wa-Korea elfu 40 (polisi wanadai ni elfu 15) walifanya mgomo nchini kote. Mgomo huo, ulipangwa na Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi nchini Korea, ukiwa na wito wa kusitishwa kwa kudhibitiwa kwa vyama vya wafanyakazi, hatua...
Shirika la UNICEF Latoa Wito wa Kutokuweko kwa Watoto Katika Maandamano Nchini Thailand
Baada ya mlipuko wa bomu la kurushwa kwa mkono nakuwauwa watoto watatu katika maandamano ya kupambana na serikali katika eneo la Bangkok, Shirika la Kuhudumia Watoto la Umoja wa Mataifa lilitoa wito kwa serikali na viongozi wa maandamano kuwalinda watoto na kuwaweka mbali na maandamano. Bijaya Rajbhandari, Mwakilishi wa UNICEF...
Sababu 10 Kwa nini Siafiki Shariah Nchini Pakistan
Mmoja wa msemaji wa Taliban alijitoa kwenye majadiliano ya hivi karibuni na serikali ya Pakistan na kudai kuwa ajenda ni pamoja na kuanzishwa kwa sharia kali. Mwanablogu wa Pakistan na Mwandishi wa Habari Beena Sarwar alipinga wazo hilo kupitia tamko aliloliweka katika mtandao wa Facebook lenye kichwa cha habari ‘sababu...
Rais Yanukovych wa Ukraine ang'olewa madarakani
Baada ya maandamano, vurugu na upinzani dhidi ya serikali uliosababisha vifo vya watu wapatao 100, Bunge la Ukraine hatimaye limepiga kura ya kumwondoa Rais Viktor Yanukovych kama hatua ya kujibu shinikizo la waandamanaji. Tayari Rais Yanukovych amenukuliwa akisema hana mpango wa kutoroka nchi. Soma zaidi kupitia kiungo hiki [en]
Wavenezuela Waishio Mexico Wawambia Waandamanaji: “Hamko Pekeyenu”
Hali ya mambo nchini Venezuela yaendelea kuzorota, huku pakiwa na maandamano na mikusanyiko nchi nzima ayalisababisha vifo vya watu kumi na mamia kujeruhiwa mpaka sasa. Wavenezuela duniani kote wanaopinga serikali yao wameandaa mikusanyiko ya amani kupaza sauti zao na kuzifanya serikali za nchi wanazoishi kuelewa mwenendo wa mambo. Mexico haija...
Vyombo Vikuu vya Habari Vyaihujumu Facebook
Mwanablogu wa Teknolojia Amitha Amarasinghe anadai kwamba mtandao wa Facebook unapewa taswira hasi na vyombo vikuu vya habari nchini Sri Lanka kwa vichwa vya habari kama “Mwanafunzi ajiua shauri ya picha iliyowekwa Facebook”, “Mapenzi ya Facebook yaishia na kifo” na kadhalika. Ghafla tu, kuna mwongezeko mkubwa wa maudhui yanayotoa taswira...
Maandamano ya Venezuela: ‘Vyombo vya Habari vya Kimataifa: Ingilieni Kati!’
Mpendwa Mhariri wa Kimataifa: Sikiliza na uelewe. Hali ya mambo imebadilika nchini Venezuela usiku wa kuamkia leo. Kile kilichokuwa kinaonekana kuwa hali ya kutokuelewana iliyokuwepo kwa miaka sasa imebadilika ghafla. Kile tulichokishuhudia asubuhi hii si habari ya Venezuela uliyodhani unaielewa. Kwenye blogu ya Caracas Chronicles Francisco Toro anashutumu kutokuwepo kwa vyombo...
Kiongozi wa Upinzani Nchini Venezuela Leopoldo López Ajisalimisha Serikalini
Kiongozi wa Upinzani nchini Venezuela Leopoldo López amejisalimisha mwenyewe kwa Vikosi vya Polisi, kama alivyokuwa ametangaza angefanya kwenye video [es] hiyo hapo juu. López, kiongozi wa chama cha Voluntad Popular, alitakiwa kujisalimisha kwa agizo la mahakama jijini Caracas kwa kutuhumiwa kuhusika na makosa ya jinai yanayohusiana na maandamano yanayoendelea nchini...