· Oktoba, 2012

Habari kuhusu Siasa kutoka Oktoba, 2012

Misri: Ushauri kwa Waandamanaji wa Kuwait

Wakati watu wa Kuwait walipoanzisha maandamano makubwa ambayo hayakuwahi kutokea ya kuonesha waziwazi kutokukubaliana na mabadiliko ya sheria ya uchaguzi yaliyopitishwa chini ya mtawala wa kurithi kufuatia kuvunjwa kwa bunge, watu wa Misri wametumia muda wao mwingi katika Twita wakitoa ushauri kwa watu wa Kuwait kuhusiana na yapi ya kufanya na yapi ya kutokufanya.

Kuwait: Ni Maandamano Makubwa Kabisa Kuwahi Kutokea?

Mabomu ya kutoa machozi na maguruneti ya kumfanya mtu kupoteza fahamu yalitumika kutawanya maandamano ya kupinga mabadiliko ya sheria ya uchaguzi nchini Kuwait. Maandamano hayo yaliyofanyika siku ya Jumapili, na kuratibiwa kupitia katika mtandao wa Twita na yaliyowavutia takribani watu 150,000 kati ya watu milioni 3 ambao ndio idadi ya watu wa Kuwait. Taarifa za vyombo vya habari zinaichukulia idadi hii kuwa ni kubwa kabisa katika historia ya Falme za ghuba ndogo.

Kambodia Yaomboleza Kifo cha Mfalme Norodom Sihanouk

  27 Oktoba 2012

Nchi ya Kambodia inaomboleza kifo cha baba Mfalme Norodom Sihanouk aliyefariki tarehe15 Ockoba, 2012. Mamilio ya watu walisubiri pembezoni mwa barabara itokayo uwanja wa ndege kwenye kwenye makazi ya kifalme kutoa heshima zao za mwisho kwa Mfalme.

Ghana: Vikwazo Vinavyowakabili Wanawake Kimaendeleo

  16 Oktoba 2012

Betty Mould Iddrisu, Jaji na Waziri wa Sheria wa Ghana, anaandika [fr] kwenye blogu ya pambazuka.org: Kufikia ngazi za juu kabisa za utawala si rahisi, na hata unapopanda mpaka juu kabisa, bado unajikuta unakabiliwa na hisia za watu zenye uadui na watu wanakuwa na mashaka na uwezo wako, kwa sababu...

Venezuela: Tathmini za Baada ya Uchaguzi

  15 Oktoba 2012

Msisimko ulikuwa mkubwa sana usiku wa siku ya Jumapili baada ya matokeo rasmi ya uchaguzi wa Rais wa Venezuela kutangazwa. Sehemu ya nchi ilisherehekea kuendelezwa kwa 'Mapinduzi ya Venezuela' chini ya Rais Hugo Chávez, wakati upande mwingine ulilalamika kwa kushindwa tena kwenye uchaguzi huo.

China: Hatua za Kubana Uhuru wa Habari Majimboni

  15 Oktoba 2012

Jing Gao kutoka blogu ya Tofu anaeleza namna serikali ya Fuji ilivyo na mikakati michafu dhidi ya Yunnan na jinsi inavyochukua hatua za kuzuia uchapishaji wa habari zinazoweka wazi kashfa za ufisadi zinazomkabili afisa mmoja wa serikali.

Venezuela: Ni Chávez Tena kwa Miaka Sita Zaidi

  11 Oktoba 2012

Baada ya chaguzi zilizokuwa na changamoto na ushindani mkubwa katika muongo uliopita, Venezuela itaongeza miaka mingine sita kwa utawala wa Hugo Chávez Frías ulioanza mwaka 1999. Idadi ya watu waliokuwa mtandaoni hasa kwenye mitandao ya kijamii, hasusani twita, ilikuwa kubwa sana hasa kabla matokeo rasmi hayajatangazwa.

Uganda Yaadhimisha Miaka 50 ya Uhuru

Terehe 9 Oktoba, 1962, Uganda ilijipatia uhuru wake kutoka kwa Mwingereza. Wakati nchi hiyo iliposherehekea Kumbukumbu yake ya Dhahabu hivi karibuni, wa-Ganda wanaotumia mtandao wamekuwa wakitumia zana za kijamii kama Twita na Facebook kusema maoni yao kuhusu sherehe hizo za kutimiza miaka 50!

Trinidad na Tobago: Ufisadi na Utawala wa Sheria

  9 Oktoba 2012

Hivi karibuni, masuala ya utawala wa sheria yamekuwa yamekuwa yakitawala serikali iliyoko madarakani. Kwa kuwa na kipengere cha 34 ambacho hakifahamiki sana miongoni mwa wananchi, hali ya mambo imebadilika na kuwa utawala wa kiimla, na […] tunaweza kuona ufisadi na matumizi mabaya ya madaraka yamebadilisha kabisa tabia za wale tuliowaona...

Uarabuni: Sera ya Romney kwa Mashariki ya Kati Yaibua Mjadala

Hotuba ya Mgombea urais wa Marekani kupitia chama cha Republican Bw. Mitt Romney iliyoelezea sera yake ya nje imeibua mjadala mzito miongoni mwa raia wa mtandaoni leo hasa wale watokao katika nchi za ki-Arabuni. Twiti zinazohoji sera ya mambo ya nje ya Marekani kwa Mashariki ya Kati ziliendelea wakati ambao Romney, anayepeperusha bendera ya chama cha Republican, alipozungumza katika Chuo cha Jeshi cha Virginia. Endapo atachaguliwa, Romney ameahidi kuwa na sera rafiki za mambo ya nje, tofauti na mwelekeo usiotabirika wa sera za Obama wakati huu ambapo mabadiliko ya kisiasa yanaendelea kulikumba eneo la Mashariki ya Kati.