Habari kuhusu Siasa kutoka Machi, 2012
Hong Kong: Raia wasema ‘Hapana’ kwa uchaguzi wa meya usio wa kidemokrasi
Kati ya wajumbe wa Kamati ya Kumchagua Kiongozi Mkuu wa Hong Kong wapatao 1,200, wajumbe 689 walimchagua Leung Chun-ying kuwa meya mpya wa jiji la Hong Kong mnamo tarehe 25 Machi. Matokeo yalipotangazwa, maelfu waliandamana ili kupinga jinsi ambavyo Beijing imekuwa ikiuchezea na mchakato wa uchaguzi.
Zambia: Ban Ki-Moon atoa wito kwa taifa kuheshimu haki za mashoga
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban Ki-Moon aliitembelea Zambia mnamo Februari 21; ambapo alilihutubia bunge, alikutana wanasiasa maarufu na kutembelea Maporoko ya Viktoria, hakuna katika haya yaliyogonga vichwa vya habari kama mwito wake wa taifa hili kuheshimu haki za mashoga.
Dondoo za Video: Utetezi wa haki za binadamu
Kuna masimulizi kusisimua katika siku za hivi karibuni kwenye tovuti ya Global Voices Video za Utetezi ikiwa ni pamoja na haki za wananchi wenyeji na habari za hivi karibuni kutoka Amerika ya Kusini, Mashariki ya Mbali, Ulaya Magharibi na Afrika kusini mwa Jangwa la Sahara zilizochaguliwa na Juliana Rincón Parra.
Palestina: Gaza yashambuliwa, watu 12 wauwawa na wengine wengi kujeruhiwa
Usiku kucha wa tarehe 9 Machi na asubuhi ya Machi 10, ndege za kivita za Israel zilishambulia maeneo maalumu katika Ukanda wa Gaza, na kuua takribani watu 12 na kujeruhi wengine 20.