Habari kuhusu Siasa kutoka Oktoba, 2009
Trinidad & Tobago: Kampeni ya 350
“Trinidad na Tobago ni kisiwa tajiri na nchi inayoendelea tajiri kwa mafuta na gesi asilia. Lakini pia tunashuhudia madhara mabaya ya maendeleo ya haraka kwenye nyanja za viwanda katika visiwa vyetu. Hii ni fursa ya sauti za wanawake kusikika”: Attillah Springer anajihusisha na kampeni ya hali ya hewa 350.
Bhutan: Mpito Usio na Mikwaruzo Kuelekea Demokrasi
Tshering Tobgay, kiongozi wa chama cha upinzani katika Bunge la Taifa la Bhutan, anatoa maoni kuwa: “mpito wetu kuelekea demokrasi, kwa hakika, umetukia bila mikwaruzo. Umetukia bila mikwaruzo kiasi kwamba wengi wetu walikuwa hata hawaufuatilii.”
Trinidad & Tobago: Mtrini Mpaka Kwenye Mifupa?
“Kila siku ambayo ninapitia habari ninazidi kushawishika kuwa ninataka kuachana na klabu ya ‘Mimi ni Mtrini’ na kwenda sehemu nyingine”: Coffeewallah ameshachoka na kila kitu kuanzia uhalifu mpaka kodi.
Uanaharakati na Umama Barani Asia
Je, mwanamke anatoa sadaka zipi ili kupigania jambo analiamini? Je, watoto wake wanaathiriwa vipi na mateso yanayoelekezwa kwake? Makala hii inachambua kwa kifupi maisha ya wanawake wanaharakati katika Asia ambao pia ni ma-mama.
Uganda: Wanablogu wa Uganda Wajadili Muswada Unaopinga Ushoga
Muswada ambao utaufanya ushoga kuwa kingyume cha sheria nchini Uganda umewasilishwa bungeni na sasa unasubiri tu saini ya rais Yoweri Museveni. Wanablogu mashoga nchini uganda wanajadili.
Somalia: Je Serikali Inawaandikisha Vijana Wa Kikenya Kwa Ajili Ya Vita?
Huu ni muhtasari wa kwanza wa blogu za Kisomali mwaka 2009. Naam, ni zaidi ya mwaka mmoja tangu nilipochukua likizo ya muda mrefu kutoka kwenye shughuli za kublogu lakini sasa nimerudi, moja kwa moja. Hii ni makala ya kwanza na tarajieni makala zaidi zinazohusu ulimwengu wa blogu za Kisomali.
Gabon: Upinzani waendelea kupinga matokeo ya Uchaguzi
Wapinzani wa kisiasa wa Gabon wanaonyesha muungano wa vyama vya siasa kupinga matokeo ya uchaguzi wa mwezi Agosti, ambayo yalimkabidhi urais mwana wa mtawala wa kiimla aliyepita, Omar Bongo. Wanasiasa na raia wanaikemea Ufaransa kwa kuingilia siasa za nchi hiyo.
Australia: Wanawake wa Kenya wakataliwa haki ya ukimbizi
Wanawake wawili wanakabiliwa na uwezekano wa kutimuliwa kutoka Australia baada ya maombi yao ya kuomba hifadhi kukataliwa, pamoja na hatari wanayoweza kuipata ya kulazimishwa tohara ya kike ikiwa watarudishwa nyumbani.