Habari kuhusu Siasa kutoka Mei, 2009
Uchaguzi Malawi: Utabiri wa Wataalamu wa Mambo Wageuka Batili
Wakati uchaguzi umekwisha na rais aliye madarakani Bingu wa Mutharika ameshaapishwa kwa muhula wake wa pili na wa mwisho, wanablogu wa Malawi (mabloga) bado wanashangaa kuona maendeleo kinyume na utabiri wa wengi, haswa ule watalaamu wa mambo. Utabiri wa kwanza ulikuwa kwamba ushindani ungelikuwa wa karibu sana. Haukuwa. Pili kulikuwa...
Tajiri Wa Kimisri Ahukumiwa Kifo
Wamisri walishuhudia hukumu isiyotarajiwa katika historia ya vyombo vya sheria nchini humo: Bilionea Hesham Talaat Moustafa, pamoja na mamluki wake (mpiga risasi wa kukodi) Mohsen El Sokari wamehukumiwa adhabu ya kifo kutokana na kuhusika kwao katika mauaji ya mwimbaji wa Kilebanoni Suzanne Tameem. Mauaji hayo ya kinyama yalitokea huko Dubai, UAE, na hukumu iliyotolewa Alhamisi imesababisha mshtuko na mshangao wakati wanablogu walipojaribu kukubaliana na yaliyotukia.
Uchaguzi wa India 09: India Imepiga Kura, Imeamua kuimarisha Utulivu
Matokeo ya Uchaguzi yanamiminika kutoka kila upande wa nchi na ni dhahiri kwamba India imepiga kura kwa kishindo ili kuchagua serikali imara ya mseto ya UPA, chini ya uongozi wa chama cha Congress. Dr Manmohan Singh atakuwa Waziri Mkuu kwa mara ya pili mfululizo. Hata kabla matokeo hayajatimia, kwa kuangalia tu mwelekeo, kundi la vyama vya mseto la NDA linaloongozwa na chama cha BJP limetangaza rasmi kushindwa kwake katika uchaguzi.