The Global Voices Lingua project hopes to bring GV content to new linguistic audiences - Details

Also in:

Media Hifadhi ya mada

Kiungo cha RSS kwa Media

2009-07-24

Nchi za Kiarabu: Homa ya Mafua ya Nguruwe Yaendelea

Homa ya mafua ya nguruwe au H1N1 bado inatawala vichwa vya habari vya magazeti katika nchi za Kiarabu kwani wagonjwa wapya wanaendelea kugunduliwa na mamlaka za afya na kutangazwa katika vyombo vya habari kila siku. Huu ni muhtasari wa yale wanayoongea wanablogu huko Bahrain, Jordan, Misri na Syria.

2009-06-09

Uganda: Mradi wa Katine Wawafikisha Wanakijiji Kwenye Ulimwengu wa Blogu

Inakadiriwa kuwa matumizi na uenezi wa intaneti nchini Uganda ni kwa kiwango cha asilimia sita tu, idadi ambayo inazuia sehemu kubwa ya watu kujiunga na ulimwengu wa blogu nchini Uganda au kuweza kuwasiliana na ulimwengu wa blogu duniani. Mradi wa Katine unaoendeshwa na Guardian and Observer unafanya kazi kubadilisha hali hiyo katika kijiji kimoja.

2009-06-08

Malawi: Wasikilize wanablogu wa uchaguzi Malawi

Wamalawi wanapiga kura katika uchaguzi wa Raisi na Bunge. Baadhi ya wanablogu walipatiwa mafunzo na PenPlus Bytes, Taasisi ya kimataifa ya Uandishi wa TEKNOHAMA kwa ushirikiano na New Media Insitute kwa lengo la kuangalia na kutoa maoni yao kuhusu uchaguzi huo kwa kutumia blogu, teknolojia ya twita na simu za viganjani. Hebu na tuziangalie blogu zao, ambazo zimehifadhiwa katika Potal ya chaguzi za Afrika. Poto hii hutoa taarifa za kutosha kuhusu chaguzi mbalimbali katika nchi za kiafrika.

2009-05-29

Uchaguzi Malawi: Utabiri wa Wataalamu wa Mambo Wageuka Batili

Wakati uchaguzi umekwisha na rais aliye madarakani Bingu wa Mutharika ameshaapishwa kwa muhula wake wa pili na wa mwisho, wanablogu wa Malawi (mabloga) bado wanashangaa kuona maendeleo kinyume na utabiri wa wengi, haswa ule watalaamu wa mambo. Utabiri wa kwanza ulikuwa kwamba ushindani ungelikuwa wa karibu sana. Haukuwa. Pili kulikuwa ...

2009-04-22

Jamhuri Ya Kidemokrasi ya Kongo: Mahojiano na Kabila Yaamsha Gadhabu

Wanablogu wa Kikongo wakosoa mahojiano ya hivi karibuni ya rais Joseph Kabila aliyoyafanya kwenye gazeti la New York times, wanauchambua msimamo wa Kabila juu ya Rwanda, ni nani wa kulaumiwa kuhusu rushwa, na jinsi wanahabari wa Magharibi wanavyoripoti kuhusu Afrika.

2009-02-26

Martinique: Uhuru na “Ubeberu” wa Kifaransa

Wakati harakati za wafanyakazi zinaendelea huko Martinique na Guadeloupe, wanablogu wa Martinique wanapima uhuru wa Idara za Ng'ambo utamaanisha nini. Le blog de [moi] anaona dhana ya kuwa Martinique haiwezi kujitegemea ni dhana inayotusi na ya kibeberu. Wasomaji wake wanadhani kuwa ukweli wa kisiwa chochote kidogo ni kuwa kila siku kitakuwa katika kivuli cha wengine.

2009-02-17

Jamaika: Miziki Yenye Maneno Machafu Yazuiwa

Utata wa muda mrefu juu ya usahihi wa kurushwa hewani kwa miziki fulani umezuka tena nchini Jamaika. Wanablogu wa Jamaika wanapaza sauti zao.

2009-01-26

Blogu za Afrika Zapendekezwa Kupokea Tuzo ya Bloggies 2009

Blogu zilizopendekezwa kwa ajili ya Tuzo ya Tisa ya Zawadi za Weblog: Mapendekezo ya blogu katika mashindano ya Bloggies ya 2009 yalifunguliwa tarehe 1 Januari na kufungwa tarehe 19 Januari. Kwa mujibu wa waandalizi, mashindano hayo ya Bloggies ni mashindano ambayo yamedumu kwa muda mrefu zaidi mtandaoni, na mapendekezo pamoja na uchaguaji wa washindani katika fainali, ni juu ya msomaji wa blogu. Mshindi hupata senti 2,009 za Marekani! Je, ni mabloga gani wa Kiafrika waliopendekezwa kwa ajili ya kinyang'anyiro cha blogu bora zaidi?

2009-01-11

Kivu Mpaka Gaza: Namna Vyombo Vya Habari Vinavyochagua Vipaumbele

Mdahalo unaodadisi ni kwa nini vita katika Mashariki ya Kongo vinapewa kipaumbele kidogo ikilinganishwa na migogoro inayotokea Mashariki ya kati. Mwandishi wa habari wa Rue89 anauliza, "ikiwa kifo cha Muisraeli mmoja ni sawa na vifo kadhaa vya Wapalestina, ni maiti ngapi za watu wa Kongo zitakazowekwa kwenye mnara wa mazishi huko Gaza?" Wanablogu wa pande zote mbili wanalichambua swala hilo.

2008-10-14

Marekani ya Kusini:Taarifa,Twita kwa Waandishi wa Habari Yapata Umaarufu

"Reporting On" ni zana mpya ya kublogu kwa kifupi na inachukua umaarufu mkubwa katika kundi la wanahabari wa Marekani ya Kusini (Walatino) ambao wanatumia zana hii ili kupashana habari na wengine kuhusu yale wanayoyaandika.