<?xml version="1.0" encoding="UTF-8"?>
<rss version="2.0"
	xmlns:content="http://purl.org/rss/1.0/modules/content/"
	xmlns:wfw="http://wellformedweb.org/CommentAPI/"
	xmlns:dc="http://purl.org/dc/elements/1.1/"
	xmlns:atom="http://www.w3.org/2005/Atom"
	xmlns:sy="http://purl.org/rss/1.0/modules/syndication/"
	xmlns:slash="http://purl.org/rss/1.0/modules/slash/"
	>

<channel>
	<title>Global Voices in Swahili &#187; Media</title>
	<atom:link href="http://sw.globalvoicesonline.org/category/topics/media/feed/" rel="self" type="application/rss+xml" />
	<link>http://sw.globalvoicesonline.org</link>
	<description>Dunia inaongea, je unasikiliza?</description>
	<lastBuildDate>Wed, 02 Dec 2009 12:35:07 +0000</lastBuildDate>
	<generator>http://wordpress.org/?v=2.8.4</generator>
	<language>en</language>
	<sy:updatePeriod>hourly</sy:updatePeriod>
	<sy:updateFrequency>1</sy:updateFrequency>
			<item>
		<title>Urusi: Jinsi Abiria wa &#8220;Nevsky Express&#8221; Walivyoeleza Habari Kupitia Vyombo Vya Habari Vya Kijamii</title>
		<link>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/12/urusi-jinsi-abiria-wa-nevsky-express-walivyoeleza-habari-kupitia-vyombo-vya-habari-vya-kijamii/</link>
		<comments>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/12/urusi-jinsi-abiria-wa-nevsky-express-walivyoeleza-habari-kupitia-vyombo-vya-habari-vya-kijamii/#comments</comments>
		<pubDate>Tue, 01 Dec 2009 11:11:27 +0000</pubDate>
		<dc:creator>j nambiza tungaraza</dc:creator>
				<category><![CDATA[Breaking News]]></category>
		<category><![CDATA[Eastern & Central Europe]]></category>
		<category><![CDATA[English]]></category>
		<category><![CDATA[Feature]]></category>
		<category><![CDATA[Internet & Telecoms]]></category>
		<category><![CDATA[Media]]></category>
		<category><![CDATA[Politics]]></category>
		<category><![CDATA[Russia]]></category>
		<category><![CDATA[Russian]]></category>
		<category><![CDATA[Technology]]></category>
		<category><![CDATA[Weblog]]></category>

		<guid isPermaLink="false">http://sw.globalvoicesonline.org/?p=738</guid>
		<description><![CDATA[Ajali ya treni la "Nevsky Express" ilitokea mbali na makazi ya watu. Ilichukua masaa kadhaa kwa wanahabari kufika kwenye eneo. Na hapo ndio picha na video za kwanza zilipoanza kuonekana kila mahali. je nini kilichotokea kwenye upashanaji habari wa kiraia ambao uliongoza njia ya kupashana habari wakati wa ajali ya ndege huko Urusi mwaka mmoja uliopita?]]></description>
			<content:encoded><![CDATA[<em>Ilichapwa kwanza na<a href="http://globalvoicesonline.org/author/gregory-asmolov/">Gregory Asmolov</a>  &middot; Imetafsiriwa na <a href='http://sw.globalvoicesonline.org/author/j-nambiza-tungaraza/'>j nambiza tungaraza</a> &middot;  <a href='http://globalvoicesonline.org/2009/11/29/russia-how-passengers-of-nevsky-express-tell-their-stories-through-social-media/'>Angalia ujumbe mama</a></em> 
<br /><p>Mamlaka nchini Urusi yanaendelea <a href="http://globalvoicesonline.org/2009/11/28/russia-at-least-25-people-killed-in-the-neva-express-train-crash/">kuchunguza ajali ya treni la &#8220;Nevsky Express&#8221; </a>[ENG] ambayo ilitokea kati ya Moscow na St Petersburg usiku wa Ijumaa. Kwa mujibu wa maofisa, dhahama hiyo iliyochukua maisha ya angalau abiria 25 ilikuwa ni shambulio la kigaidi. Ajali hiyo imezua maswali mengi. Watu wengi wanauliza ni nini kilichotokea katika masaa ya mwanzo baada ya ajali na ni kwa nini ilichukua muda mrefu kuanza kutoa taarifa za ajali hiyo.</p>
<p>Kwa kuwa dhahama hiyo ilitokea mbali na maeneo yenye makazi ya watu, ilichukua muda mrefu kwa wanahabari kuwasili kwenye eneo la ajali. Na ndipo picha za kwanza na video zilipoanza kuonekana kila mahali. Je nini kilichoyatokea majukwaa ya uanahabari wa kijamii ambayo yalitaarifu vilivyo kuhusu <a href="http://news.bbc.co.uk/2/hi/europe/7614951.stm">ajali ya ndege mjini Perm</a> [ENG] mwezi Septemba 2008.</p>
<p>Abira pekee ambaye alitoa taarifa mara moja kuhusu ajali ya “Nevsky Express” alikuwa mtumiaji wa Twita <a href="http://twitter.com/lazy_frog">Lazy Frog</a>. Aliandika mara 12 kuhusu ajali hiyo kabla ya kuwasili nyumbani. Haya ndio aliyoandika: </p>
<blockquote><p>Nipo hai. Lakini nitaeleza kuhusu (ajali) baadaye. Kama mtu ataeleza chochote kwenye habari, tafadhali niandikie. Hawatuambii kila kitu hapa.</p></blockquote>
<p>Baadaye, abiria wengi kutoka mabehewa ya kwanza – ni mabehewa ya mwisho ambayo yaliteguliwa kutoka kwenye reli –walisema kuwa kwa saa zima baada ya ajali hawakufahamu chochote. <a href="http://twitter.com/lazy_frog">Lazy frog</a> alituma habari mpya za nyongeza: </p>
<blockquote><p>Tumepanda treni jingine. Nilifanya kila nilichoweza.</p>
<p>Hivi sasa tupo SAPSAN (treni mpya ambyo iliwachukua abiria kwenda St. Petersburg – G.A). Natamani ingekuwa inakwenda polepole.</p>
<p>Wametangaza sasa hivi kuwa watu walitayarishwa rasmi wangetulaki kwenye kituo cha treni.</p></blockquote>
<p>Siku iliyofuata baada ya dhahama, <a href="http://twitter.com/lazy_frog">Lazy Frog </a>aliandika muhtasari wa uzoefu wake:</p>
<blockquote><p>Nilizihisi hisia za kwanza kuhusu kilichotokea wakati tulipofika karibu na Piter (St. Petersburg G.A). Sikuwa na wasiwasi nilipokuwa katika eneo la ajali. Nilikuwa na hofu kidogo na viatu vyangu – kulikuwa na tope kila mahali na mawe yenye ncha.</p></blockquote>
<p>Jumamosi habari nyingi zilijitokeza wakati abiria walipoanza kublogu kuhusu yaliyowakuta. Makala ya blogu maarufu zaidi inayohusiana na mada hii iliandikwa na mtumiaji wa LJ <em>paltus_mk</em> [RUS] ambaye alikuwemo ndani ya mabehewa ya mwisho yaliharibiwa vibaya na mlipuko. <a href="http://paltus-nk.livejournal.com/23747.html">Aliandika </a>[RUS]:</p>
<blockquote><p>Yote yanatokea ndani ya sekunde 10 wakati unapofahamu ni nini kitakachotokea. Nilikuwa na muda wa kutosha kuutayarisha mwili wangu. Lakini hakuna linaloweza kusaidia dhidi ya kanuni za Newton wakati dazeni za tani za vyuma zinaposimama mara moja wakati zikiwa katika mwendo wa kasi – ni bahati tu… kwa hiyo nilikuwa na bahati tu. Kaka yangu alikuwa na bahati, pia, ukiachilia mbali ukweli kuwa majeraha yake yalikuwa yanatisha kuliko yangu.<br />
[…]</p></blockquote>
<blockquote><p>Kila kitu ambacho kilikwenda mrama hadi kusimama kabisa kulichukua kama sekunde 30 hivi. Ilikuwa giza na kimya. Watu walioumia walianza kulia. Nilikuwa sakafuni, nimekandamizwa na miili mingine. Niliisogeza ile miili. Niliona kuwa nimelowana na damu lakini damu ile haikuwa yangu. Niliona kuwa ni mzima na miguu yangu na mikono vuinafanya kazi. Kichwani nilikuwa na jeraha linalovuja damu. Ilinibidi ninyanyuke na kusubiri kwa muda kiasi kabla ya watu wenye majeraha mado waliposafisha njia ya kutoka.<br />
[…]<br />
Mateso yalikuwepo kila mahali. Tulikuwa tumeketi mwishoni mwa behewa na mikoba yote ilipaa ikituelekea. Watu wengi waliojeruhiwa. Katika dakika chahce baada ya ajali, behewa lilikuwa ni kama fungu la miili, viti na sehemu za treni ambazo zilikuwa zimesambaa sawia kila mahali.</p></blockquote>
<p><em>Paltus_mk </em>anasimulia habari za uokoaji zenye maelezo ya kina kuanzia dakika za mwanzo baada ya ajali, lakini wakati huo huo anaepuka ufafanuzi ambao ungeweza kuwastua wasomaji. Anaandika kuwa abiria walianza kupeana huduma ya kwanza kwa ushujaa bila kuogopa. Anasema haikuwezekana kuhesabu ni wagtu wangapi waliofariki. Waokoaji waliwasili saa moja na nusu baada ya ajali. <em>Paltus_mk</em> na kaka yake hatimaye waliokolewa na kupelekwa kwenye hospitali jirani na baadaye aliwasili mjini St. Petersburg. </p>
<p>Hadithi nyingine ya kunusurika ilichapishwa na mwanablogu pancakyes katika huduma nyingine ya kublogu ya Kirusi Ya.Ru. behewa lake halikuharibiwa na mlipuko. Alichapisha makala yake ya kwanza saa 4:11 za usiku – nusu saa baada ya ajali – pale pale kwenye eneo la ajali.  Aliandika kuwa treni ilisimama kutokana na ajali ya namna fulani, mabehewa machache yaliteguliwa na kwamba angewasili nyumbani kwa uchelevu kuliko ilivyotarajiwa. Karibu saa zima baadaye, aliongeza kuwa kulikuwa na waathirika katika mabehewa mawili ya mwisho. Jumamosi,  <em>pancakyes</em> <a href="http://pancakyes.ya.ru/replies.xml?item_no=30442">alichapisha habari nzima kuhusu ajali</a> [RUS] kama alivyoshudia mwenyewe:</p>
<blockquote><p>Tulihisi mitetemo michache ambayo ilikuwa ikiongezeka nguvu. Vitu vilianza kuanguka kutoka mezani. Haikuwa wazi ni nini kilichotokea. Hapakuwa na matangazo. Kwanza tulidhani kuwa halikuwa jambo lenye uzito. Pengine kuna mtu aliyesimamisha treni kwa makosa. Lakini makondakta wenye sura zenye hofu walianza kukimbia kila mahali wakikusanya magodoro, vitambaa vya mezani na maji. Walitutaka tusiondoke kwenye viti vyetu isipokuwa kama ni madaktari. Tulisikia mambo mabaya kutoka kwenye redio zao. Uvumi ulianza kusambaa. Hatukuamini kuwa mabehewa mawili yalikuwa yametengana na yalikuwa mbali sana. Baadaye tuligundua kuwa ilikuwa kweli.</p>
<p>Tulitoka nje na tulitaka kusaidia. Tulikwenda mpaka behewa la tatu. […] hatukutaka kuwa waduwazi ambao wanaongeza wingi wa watu bila fursa yoyote ya kusaidia. Pia hatukutaka kuona yale ambayo watu waliotoka huko walikwishatueleza.</p></blockquote>
<p>Mara baada ya ajali, majukwaa ya uanahabari wa kijamii yalikuwa sehemu ya kwanza ambayo wanahabari wa Kirusi  walikuwa wakitafuta habari. Mwandishi kutoka Shirika la Habari la RIA-Novosty aliacha maoni kwenye blogu ya <em>pancakyes</em> na kumtaka mwanablogu huyo ampigie simu mara moja. Tatyana Landa (mtumiaji wa LJ mwenye jina la Elada) <a href="http://elada.livejournal.com/220534.html">aliandika kwenye blogu yake</a> [RUS] kuhusu rafiki aliyenusurika ambaye alikuwemo kwenye treni. Mara moja wanahabari wawili waliacha maoni ya kumtaka awasiliane nao. Baadaye Tatyana <a href="http://elada.livejournal.com/220866.html">alichapisha makala ya hasira</a> [RUS] ambamo alisema kuwa mwanahabari kutoka “Komsomolskaya pravda” (gazeti la udaku la Kirusi) alikuwa akijaribu kumpata kwa simu mara kadhaa usiku huo. Makala hiyo iligeukia mahali ambapo watu walianza kujadili kama wanahabari wanaweza kuwatumia wanablogu kama chanzo cha taarifa zinazohusu hii ajali ya treni. Wanahabari pia walijaribu kuwasiliana na mwanablogu ambaye <a href="http://naechst-naechst.livejournal.com/105582.html#comments">aliandika</a> [RUS] kuwa aliamua kutopanda treni la “Nevsky Express” katika dakika ya mwisho.</p>
<p>Baadhi ya wanablogu <a href="http://tema.livejournal.com/509436.html">walieza kughafirika kwao </a>[RUS] na ukweli kuwa ni watu wachache mno kutoka kwenye treni walitumia vyombo vya habari vya kijamii kutoa taarifa za kile kilichokuwa kinatokea., Na, inavyoonekana, kuna fafanuzi kadhaa zinazoelea ni kwa nini  uanahabari wa kijamii haukuchukua nafasi kubwa katika upashaji wa habari za ajali ya “Nevsky express”.</p>
<p>Twita, jukwaa zuri la kublogu moja kwa moja, si maarufu nchini Urusi. Kwa mujibu wa <a href="http://twitter.com/twitRU">twitRU </a>[RUS], kuna watumiaji wa Twita 2,700 tu ambao wanaandika kwa lugha ya Kirusi. Wakati huo huo, majukwaa maarufu ya kublogu nchini Urusi kama vile Livejournal.com au ya.ru yangeweza kutumika ili kublogu moja kwa moja lakini, kama ilivyojadiliwa hapo juu, kuna mifano michache tu ya matumizi hayo.</p>
<p>Ufafanuzi wa pili unahusiana na nafasi ya zana za mkononi na uunganishaji. Zana za mkononi zinaongezeka nchini. Warusi zaidi na zaidi wanaweza kutumia mtandao wa intaneti na zana nyingine za mtandaoni. Tabia hii ina nguvu katika maeneo ya Moscow na St. Petersburg. Lakini ajali ilitokea mbali na maeneo ya mjini ambako, kama mashihidi walivyotaarifu, uwezo wa kupatikana kwa mawasiliano ya simu za mkononi ulikuwa mdogo. Mwanablogu  <em>pancakyes </em><a href="http://pancakyes.ya.ru/replies.xml?item_no=30442&#038;ncrnd=2805">anasimulia</a> tatizo la mawasiliano:</p>
<blockquote><p>
Mawasilian ya simu yalikuwa mabaya sana. Inawezekana kuwa kila mtu alijaribu kupiga simu kwa wakati mmoja na mtandao ulielemewa. Nilianza kupata jumba za maandishi pale tu nilipokuwa kwenye treni la pili (treni ambalo liliwachukua abiria kwenda Saint- Petersburg G.A.). Ningeliweza kutumia mtandao wa intaneti, lakini ilikuwa ni vigumu mno.</p></blockquote>
<p>Hii ni tofauti, ajali ya ndege kule Perm mwaka jana ambayo ilitoa fursa nyingi kwa uanahabari wa kiraia:</p>
<p>1. Ndege ilianguka ndani ya mipaka ya mji ambako watu wengi waliweza kuona ni nini kilichokuwa kinatokea kutokea madirishani. Ajali ya “Nevsky express”, kama ilivyoelezwa awali, ilitokea sehemu za vijijini.</p>
<p>2.Habari zilizoandikwa kwa uanahabari wa kijamii kule Perm zilitokana na maelezo ya walioishuhudia ajali ambao hawakuwamo katika ajali (kwa bahati mbaya, hapakuwa na walionusurika kutoka katika ile ndege). Mashahidi wote wa tukio la “Nevsky Express”  walikuwa ni abiria katika treni. </p>
<p>3. Watu wengi walituma habari mpya juu ya ajali ya ndege kule Perm kwa kutumia tarakilishi za nyumbani. Walionusurika kwenye “Nevsky Express” walitegemea zana za mikononi.</p>
<p>Tofauti hizi zinabainisha kwa nini vyombo vya habari vya kiraia vilikuwa mbele katika ajali ya  ndege na vilikaribia kutokuwepo kwenye tukio la “Nevsky Express.” </p>
<p>Pia inawezekana kudai kuwa urusi bado haijaendeleza utamaduni wa utoaji taarifa kupitia uanahabari wa kiraia. Na ndiyo sababu abiria wawili tu walikuwa na msukumo wakutosha kwenda kwenye mtandao na kujipa kazi ya uanahabari wa kijamii. Na pia inaweza kufafanua upinzani wa abiria na wanablogu kwa wanahabari ambao walikuwa wanatafuta taarifa za ajali kwenye vyombo vya habari vya kijamii. </p>
<p>Inaonekana kana kwamba ulimwengu wa blogu wa Kirusi bado uko mbali na kuwa chanzo kikuuu cha kutangaza habari mpya. Bado unabaki kuwa sehemu ya usambazaji wa habari na mijadala mipana inayohusu nini kilichotokea. </p>
]]></content:encoded>
			<wfw:commentRss>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/12/urusi-jinsi-abiria-wa-nevsky-express-walivyoeleza-habari-kupitia-vyombo-vya-habari-vya-kijamii/feed/</wfw:commentRss>
		<slash:comments>0</slash:comments>
		</item>
		<item>
		<title>Somalia: Kuufahamisha mtandao wa waandishi na wanablogu wa Kisomali</title>
		<link>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/11/somalia-kuufahamisha-mtandao-wa-waandishi-na-wanablogu-wa-kisomali/</link>
		<comments>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/11/somalia-kuufahamisha-mtandao-wa-waandishi-na-wanablogu-wa-kisomali/#comments</comments>
		<pubDate>Tue, 24 Nov 2009 12:45:45 +0000</pubDate>
		<dc:creator>Christian Bwaya</dc:creator>
				<category><![CDATA[English]]></category>
		<category><![CDATA[General]]></category>
		<category><![CDATA[Media]]></category>
		<category><![CDATA[Somalia]]></category>
		<category><![CDATA[Sub-Saharan Africa]]></category>
		<category><![CDATA[Weblog]]></category>

		<guid isPermaLink="false">http://sw.globalvoicesonline.org/?p=705</guid>
		<description><![CDATA[Kituo cha habari cha Somalia ni jukwaa la waandishi na wanablogu wa Kisomali wanaoishi ndani na nje ya Somalia. Kituo kinasambaza machapicho ya habari na kuchapisha blogu zilizoandikwa na waandishi wa habari. ]]></description>
			<content:encoded><![CDATA[<em>Ilichapwa kwanza na<a href="http://globalvoicesonline.org/author/ndesanjo-macha/">Ndesanjo Macha</a>  &middot; Imetafsiriwa na <a href='http://sw.globalvoicesonline.org/author/bwaya/'>Christian Bwaya</a> &middot;  <a href='http://globalvoicesonline.org/2009/11/05/somalia-introducing-a-network-of-somali-journalists-and-bloggers/'>Angalia ujumbe mama</a></em> 
<br /><p><a href="http://somalimedia.ning.com/">Kituo cha habari cha Somalia</a> ni jukwaa la waandishi na wanablogu wa Kisomali wanaoishi ndani na nje ya Somalia. Kituo kinasambaza machapicho ya habari na kuchapisha blogu zilizoandikwa na waandishi wa habari. </p>
<blockquote><p>Kituo cha Habari cha Somalia ni jukwaa linalojitegemea kwa ajili ya waandishi wa Kisomali ndani na nje ya nchi hiyo. (Kituo hicho) kimeanzishwa kukuza wasifu wa waandishi werevu, na wachapa kazi waliyoyatoa maisha yao kuwatumiakia watu dunia nzima.<br />
Somalia imekuwa ikichukuliwa kama nchi iliyoshindwa, nchi inayohusishwa na vifo, mapigano ya wenyewe kwa wenyewe yasiyoisha, vita, ugaidi na uharamia wa kisasa. Lakini moja wapo ya habari za mafanikio kwa miaka mingi imekuwa ni kukua kwa uhuru wa habari na maoni. Hata hivyo, kuupa kipaumbele na kuutangaza ukweli huja kwa gharama kubwa.</p>
<p>Kituo hicho huchapisha blogu za waandishi hawa. Pia, kituo kinatawanya habari na taarifa za waandishi wa habari. Kituo pia kinaratibu waandishi wa Kisomali na wale wasio Wasomali. Kinawapa waandishi wasio Wasomali wanaoweza kuwa wanasafiri kwenda Somalia ushauri na mawasiliano ya awali. Kituo pia kinafanya kazi na mashirika makubwa ya kimataifa ya habari kwa ushirikiano, kuzalisha na kujazia habari na taarifa kuhusu Somalia na eneo lote la Pembe ya Afrika. </p></blockquote>
<p>Solana Larsen anaandika kuhusu <a href="http://somalimedia.ning.com/profiles/blogs/the-new-somali-media-centre">asili ya Mradi wa Kituo cha Habari cha Somalia</a>:</p>
<blockquote><p>Kama haujahisi bado, mimi si Msomali. </p>
<p>Katika shule ya Uandishi wa Habari jijini London mwaka 2002 nilikuwa na mwanafunzi mwenzangu aitwaye Harun Hassan ambaye nilizoea kumuuliza maswali mengi kuhusu maisha yake  ya Mogadishu na Siasa za Somalia. Baada ya kuhitimu, tulibaki kuwa marafiki na nilimfahamisha kuhusu uwezekano wa yeye kuandikia mtandao wa openDemocracy.net ambapo nilikuwa mhariri kwa miaka michache. Baadaye, nikawa mhariri mtendaji wa Global Voices Online, ambapo mara chache tulikuwa na habari kuhusiana na wanablogu wa kiSomali. </p>
<p>Harun alizoea kuniambia kuhusu mawazo aliyokuwanayo kwa ajili ya Mradi wa Habari uliojumuisha jamii ya Kisomali mjini London. Alianzisha gazeti la Kisomali, na wakati fulani alinifuata nimsaidie kutengeneza tovuti kwa ajili ya kitu alichokiita Kituo cha Habari cha Somalia.</p>
<p>Habari za jamii ya KiSomali kwenye vyombo vya habari nchini Uingereza zilikuwa hasi na zisizo sahihi, Harun alifikiria kuwa namna pekee ya kusahihisha hilo,ilikuwa ni kuwarahisishia waandishi wa Uingereza kuwapata waandishi wa Kisomali na watafiti wa kuongea nao.</p>
<p>Tulitengeneza tovuti na blogu, lakini baadae kidogo tukakabiliwa na kazi nyingine na mradi ukadumaa.</p>
<p>Wavuti unayoipitia sasa, ni jaribio letu  lapili la kutengeneza nyenzo ya mtandao kwa ajili ya waandishi wa Kisomali na wengine kuitumia ili kusaidia kuboresha uwelewa wa kidunia wa Wasomali na Somalia yenyewe.</p></blockquote>
<p>Hapa chini ni baadhi ya makala za blogu za hivi karibuni kabisa kutoka kwenye Kituo cha Habari cha Somalia: </p>
<p>Katika makala yenye kichwa cha habari, <a href="http://somalimedia.ning.com/profiles/blogs/affair-to-remember">Uzinifu wa Kukumbuka</a>, Fathia Absie anaandika kuhusu kushitakiwa kwa Joshua Asisam mlinzi wa amani katika Somalia, kwa kujihusisha na uhusiano wa kimapenzi na mwanamke wa Kisomali:</p>
<blockquote><p>Mahakama ya Kijeshi ya Kampala ilimhukumu Joshua Asisa kifungo cha mwaka mmoja na nusu jela. Bw. Asisa ambaye ni mwanachama wa walinzi wa amani wa AMASOM nchini Somalia alipatiaka na hatia ya kujuhusisha na uhusiano wa kimapenzi na mwanamke wa Kisomali aitwaye Nimco Omar na kumpa ujauzito baada ya kumuoa kwa kumdanganya kuwa alikuwa Mwislamu.<br />
Habari hii ilitokea mwaka uliopita huko Mogadisho lakini hakuna aliyesikia mpaka mwanamke huyu mdogo alipokwenda Kampala na kumshitaki Bw. Asisa mahakamani kwa kumdanganya. Mohamed Abubakar Ahmed ambaye ni mwandishi aliyeiibua habari hiyo aliniambia kuwa aliipata habari hiyo baada ya kuwa imeripotiwa na magazeti ya Uganda. Baada ya hapo, Bw. Ahmed alijaribu kuonana na viongozi wa jamii ya Kisomali waishio Kampala na akaweza kukutana na msichana huyo. Aliniambia kuwa Bi. Omar alimwambia kuhusu habari hiyo na jinsi alivyokutana na Bw. Asisa ambaye ni daktari. Alikuwa akifanya kazi kwenye hospitali binafsi kwa ajili ya jeshi la Uganda mjini Mogadisho.</p></blockquote>
<p>“<a href="http://somalimedia.ning.com/profiles/blogs/in-the-spirit-of-spreading-the">kwa nia ya kutawanya neno..</a>,” anaandika Idil Osman: </p>
<blockquote><p>Mafunzo ya kijeshi yanayofanyika katika makambi ya wakimbizi wa Kisomali huko Dadaab, Kaskazini mashariki ya Kenya yamechochea kelele zinazochanganya wengi ndani na nje ya eneo. Hata hivyo ninashangazwa sana na msimamo wa serikali ya Kenya. Nilifanya ripoti ya uchunguzi katika suala hili mapema kazini ambapo waziri wa ulinzi wa Kenya alidai kwa msimamo kwamba Kenya haikutoa ruhusa kwa mafunzo haya kufanyika.<br />
Wakati huo huo mashahidi na wanaharakati wa haki za binadamu wanarekodi na kuweka kumbukumbu za ushahidi wa vijana hawa wanaowekwa  katika magari ya kijeshi ya Kenya na kusafirishwa kwa magari kwenda kwenye vyuo vya mafunzo ya Kijeshi vya Kenya.<br />
Wengi wa vijana hawa wanachukuliwa kwa kudanganywa na kuahidiwa mshahara mzuri pamoja na kazi inayoaminika kwenye miradi ya kijeshi ya Umoja wa Mataifa/Umoja wa Ulaya/Umoja wa Afrika..<br />
Kiukweli wanafunzwa kwenda na kupigana kwenye vita ile ile waliyoikimbia na kuwafanya wawe wakimbizi. Wengi wa wakimbizi hawa vijana wanaarifiwa kuwa chini ya umri unaotakikana na wamechukuliwa bila ridhaa ya wazazi wao.<br />
Imevunja haki zao za kimataifa za binadamu kama wakimbizi kwa mujibu wa tangazo la kwenye vyombo vya habari lilitolewa hivi karibuni na Shirika la Human Rights Watch, kwa sababu wakimbizi wanatakiwa kuwekwa kwenye mazingira ya kiraia. </p></blockquote>
<p>Solana anajadili suala la ‘chanzo kisichotaka kufahamika’ katika taarifa za vyombo vya habari vya Kimagharibi kwenye makala yake aliyoipa jina la “<a href="http://somalimedia.ning.com/profiles/blogs/when-local-sources-go-unnamed">Wakati vyanzo vya mahali vinapochagua kutokuwa na jina</a>”</p>
<blockquote><p>nimechukua toleo la hivi karibuni la jarida la National Geographic Magazine kwa habari yao inayohusu ‘Somalia iliyovunjika’. Picha za Mogadishu zilizopigw ana Pascal Maitre ni nzuri, ingawa zinaonyesha uharibifu mkubwa. Na mwandishi, Robert Draper anatoa muhtasari wa haki na wenye mguso kuhusu historia tata. Pia anaziweka wazi changamoto za upashaji habari wa kigeni.  </p>
<p>Katika hali inayoacha maswali, mwandishi wa Kisomali Harun Hassan anatajwa kwa jina kwenye maelezo ya picha inayomwonyesha mlinzi wa barabarani mjini Mogadishu, lakini kwa kiwango ninachoona haionekani kwenye habari yenyewe. Kwa nini kuna ugumu wa kuweka wazi chanzo?  Kama Draper alihangaika kuwasiliana na kuvihoji vyanzo vya Habari vya Somalia, kwa nini asiwaeleze wasomaji wake habari hiyo?</p>
<p>Je, huu ndio uzoefu wa wandishi wa Kisomali wanaowasaidia waandishi wa Kimagharibi kuhabarisha? Ninatumainii wanachama wa Kituo cha Habri cha Somalia watasaida kutupa mwanga wa jinsi inavyokuwa kwenye sehemu hiyo ya timu inayotengeneza ripoti.  </p></blockquote>
<p>Unaweza kuona orodha ya wanachama waliopo wa Kituo hicho <a href="http://somalimedia.ning.com/profiles/members/">hapa</a>.</p>
]]></content:encoded>
			<wfw:commentRss>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/11/somalia-kuufahamisha-mtandao-wa-waandishi-na-wanablogu-wa-kisomali/feed/</wfw:commentRss>
		<slash:comments>0</slash:comments>
		</item>
		<item>
		<title>Brazil: Mtazamo wa Wakazi wa Vitongoji Maskini</title>
		<link>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/11/brazil-mtazamo-wa-wakazi-wa-vitongoji-maskini/</link>
		<comments>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/11/brazil-mtazamo-wa-wakazi-wa-vitongoji-maskini/#comments</comments>
		<pubDate>Mon, 23 Nov 2009 11:21:58 +0000</pubDate>
		<dc:creator>j nambiza tungaraza</dc:creator>
				<category><![CDATA[Americas]]></category>
		<category><![CDATA[Brazil]]></category>
		<category><![CDATA[Cyber-Activism]]></category>
		<category><![CDATA[Governance]]></category>
		<category><![CDATA[Media]]></category>
		<category><![CDATA[Photos]]></category>
		<category><![CDATA[Portuguese]]></category>
		<category><![CDATA[War & Conflict]]></category>
		<category><![CDATA[Weblog]]></category>

		<guid isPermaLink="false">http://sw.globalvoicesonline.org/?p=716</guid>
		<description><![CDATA[Katika makala hii, tunasikia mitazamo ya wanahabari raia kutoka mradi wa Viva Favela kuhusiana ya vurugu inayotokana na mihadarati huko Rio de Janeiro na jinsi inavyofagia makazi ya walalahoi, kama wanavyoiona mbele ya milango ya nyumba zao.]]></description>
			<content:encoded><![CDATA[<em>Ilichapwa kwanza na<a href="http://globalvoicesonline.org/author/diego-casaes/">Diego Casaes</a>  &middot; Imetafsiriwa na <a href='http://sw.globalvoicesonline.org/author/j-nambiza-tungaraza/'>j nambiza tungaraza</a> &middot;  <a href='http://globalvoicesonline.org/2009/11/01/brazil-a-view-from-slum-dwellers-on-rios-drugs-war/'>Angalia ujumbe mama</a></em> 
<br /><p>Wiki iliyopita, picha za vita kati ya wasafirishaji na wafanyabiashara ya madawa ya kulevya mjini Rio de Janeiro zilitapakaa duniani. Tarehe 17 Oktoba, mapambano kati ya magenge yanayotokea vilima vya Morro Sao Joao na Morro dos Macacos yaliwatisha watu. Mamia ya askari wa jimbo walipelekwa katika juhudi za kudhibiti magenge hayo yanayoshindana lakini haikusaidia: ugomvi kati ya wafanyabiashara wa madawa ya kulevya na polisi yalipelekea kutunguliwa kwa helikopta ya polisi na vifo vya polisi watatu, na kuchukua maisha ya zaidi ya watu 30 wengine, miongoni mwao wakiwemo watu wanaotuhumiwa kuwa wanachama wa magenge na wapiti njia. </p>
<div class="wp-caption aligncenter" style="width: 610px"><img alt="Wakati helikopta inalipuka. Picha na Taiane Oliveira kwenye Twitpic." src="http://globalvoicesonline.org/wp-content/uploads/2009/10/36736952.jpg" title="The moment the helicopter exploded. Photo by Taiane Oliveira On Twitpic." width="600" height="450" /><p class="wp-caption-text">Wakati helikopta inalipuka. Picha na Taiane Oliveira kwenye Twitpic.</p></div>
<p>Blogu ya <em><a href="http://inblogs.com.br/censurado/">Censurado</a></em> inaukosoa mtizamo wa gavana katika mgogoro huu, baada ya kusikia habari zinazoashiria kuwa <a href="http://inblogs.com.br/censurado/politicanacional/carnaval-fora-de-epoca-no-rio-de-janeiro-chove-bala-rio-2016-socorro-ja">polisi hawakujua chochote juu a uvamizi</a>:</p>
<blockquote><p>Vocês viram as cenas na televisão este fim de semana? Helicóptero caindo, policial morrendo queimado, inocente metralhado nas ruas e traficante invadindo a favela do outro em plena luz do dia, uma verdadeira cena de filme de guerra. Dizem no Rio que até o serviço secreto israelense sabia que um morro atacaria o outro, mas mesmo assim o governador Sérgio Cabral diz que a policia carioca não sabia de nada? Acho que ele anda passando muito tempo com o Lula. Só isso explica essa ‘ignorância&#39; sobre o tema.</p></blockquote>
<div class="translation">Je uliiona habari katika televisheni mwishoni mwa juma hili? Helikopta akianguka, polisi wanaungua moto, watu wasio na hatia wanapigwa kwa risasi mitaani na wauza madawa ya kulevya wakivamia vitongoji vya wauzaji wengine mchana kweupe; kama picha kutoka kwenye sinema ya vita. Mjini Rio, watu wanasema kuwa hata shirika la kijasusi la Israel lilikuwa linafahamu kuwa wauza madawa ya kulevya wangeeenda kuwashambulia wauzaji wengine, lakini bado gavana Sergio Cabral alisema kuwa polisi wa carioca walikuwa hawafahamu lolote? Nadhani anatumia muda mwingi na [rais wa Brazil] Lula. Hiyo ndiyo sababu pekee ya “kutokufahamu kwake” juu ya suala hili.</div>
<p>Mwanablogu <em><a href="http://anamvc.blogspot.com/">Ana Maria</a> </em>[pt] anasema kuwa kuitungua helikopta siyo kazi rahisi na kuonyesha kuwa huu unaweza ukawa ni mwanzo tu. <a href="http://anamvc.blogspot.com/2009/10/desespero-do-trafico.html">Anasema</a>[pt]:</p>
<blockquote><p>Mas os senhores do tráfico, donos dos morros cariocas possuem não apenas as armas capazes disso, possuem indivíduos capazes de manuseá-las e causar um desastre como o do sábado.<br />
Isso vai ficar marcado para sempre na memória da PM e do cidadão de bem, morador do estado do Rio de Janeiro.<br />
Se eles podem fazer isso com um helicóptero da polícia tripulado por homens treinados, que dão a vida pela segurança pública, o que podem fazer com o cidadão comum?<br />
Não vou “tapar o sol com peneira”.<br />
As coisas podem piorar.</p></blockquote>
<div class="translation">Sio tu vigogo wa madawa ya kulevya, bali pia wamiliki wa makazi ya masikini katika carioca, wanazo bunduki zenye uwezo wa kufanya jambo kama hilo mikononi mwao, na pia wanao watu waliofundishwa kuzitumia na kusababisha janga kama la Jumamosi iliyopita.<br />
Tukio hili litaacha lama katika kumbukumbu za Polisi na raia wa kawaida, wakazi wa jimbo la Rio de Janeiro.<br />
Kama wanaweza kufaifanyia hivi helikopta inayoendeshwa na watu waliofuzu, ambao wametoa maisha yao ili kutoa usalama kwa umma, je wanaweza kufanya nini kwa raia wa kawaida?<br />
Siwezi “kulificha jua kwa chujio”.<br />
Mambo yanaweza kuwa mabaya zaidi.</div>
<p><strong><br />
Maelezo ya wakazi juu ya vita vya madawa ya kulevya</strong></p>
<div class="wp-caption aligncenter" style="width: 410px"><img alt="Mwanamke aliyembeba mtoto anatembea bila kujali mbele ya maofisa wa polisi wanaofanya doria katika Morro dos Macacos" src="http://globalvoicesonline.org/wp-content/uploads/2009/10/Macacos-010.jpg" title="Macacos-010" width="400" height="300" /><p class="wp-caption-text">Mwanamke aliyembeba mtoto anatembea bila kujali mbele ya maofisa wa polisi wanaofanya doria katika Morro dos Macacos</p></div>
<p>Mradi wa habari wa jamii <em><a href="http://www.vivafavela.com.br/">Viva Favela</a></em> [pt] unatoa <a href="http://www.vivafavela.com.br/publique/cgi/cgilua.exe/sys/start.htm?infoid=46399&#038;sid=87">maelezo ya wakazi walioshuhudia kwa macho ugomvi huu</a>. Waandishi wao wa kiraia – ambao wote wanaishi katika mstari wa mbele wa mapambano – wamekusanya maoni kutoka kwa wakazi wa kwenye maeneo hayo na picha za siku ambayo vita vya madawa ya kulevya vilianza jijini Rio de Janeiro.</p>
<p>Mtu wa kwanza kusikilizwa na <em>Viva Favela</em> alikuwa Hugo Mattos, ambaye anaishi kwenye mtaa ambao ndio njia ya kuelekea kwenye eneo ambalo matukio yalijiri (Morro dos Macacos). Alisema kuwa wauza madawa ya kulevya walitumia bunduki zenye nguvu ya juu na akaongeza kuwa kuna aina fulani ya hofu ya jumla kwamba ikiwa polisi watalichukua tena eneo linalokaliwa na wauza madawa ya kulevya, patazuka machafuko mabaya kama jibu kutoka kundi linalotawala Morro dos Macasos: </p>
<blockquote><p>O tiroteio começou por volta das duas da manhã e só terminou às oito horas, quando a policia chegou. Muita gente teve que dormir fora de casa nesse dia.</p>
<p>As pessoas dizem que ninguém deve sair de casa depois das 10 horas, porque algo pode acontecer.</p></blockquote>
<div class="translation">Kutupiana risasi kulianza kwenye majira ya saa 8 za usiku na kumalizika saa 2 asubuhi wakati polisi walipowasili. Iliwabidi watu wengi walale nje ya nyumba zao usiku ule. Watu wanasema kuwa hakuna anayepaswa kutoka nyumbani kwake baada ya saa 4 za usiku, kwa kuwa lolote linaweza kutokea.</div>
<p>Kwa mujibu wa <em>Viva Favela</em>, taarifa kama hizi huletwa wakati wote kutoka kwa wakazi wa maeneo hayo, ambao hawana uwezo wa kufanya lolote. Jioni ya Jumanne tarehe 20 Oktoba, wakazi wa Morro Sao Joao waliandamana kutokana na hofu ya kuvamiwa kama majibu (ya wauza madawa walioshambuliwa awali), hofu ambayo ilitajwa kuwa haikuwa na msingi wowote na Mkuu wa jeshi la Polisi, Kanali Mario Sergio Duarte. Hata hivyo, watu walikwishaingiliwa na hofu. Mkazi mwingine wa Morro dos Macacos, Karen Carolina Nascimento anasema kuwa kutupiana risasi kati ya wauza madawa ya kulevya na polisi kumekuwa kukiendelea kwa miezi miwili. Anahofu mgogoro mpya:</p>
<blockquote><p>Já era praticamente uma rotina, mas no último sábado foi diferente. O confronto aconteceu por causa de uma tentativa de invasão e não foi a primeira vez que os traficantes do Morro São João tentam. O comentário que se escuta no morro é que a facção rival deu uma ordem para tomar o Morro dos Macacos até dezembro e que esses bandidos tiveram ajuda de policiais para tentar invadir.</p>
<p>O policiamento não está reforçado e os moradores estão muito apreensivos com medo de uma outra invasão. Eu trabalho no pé do Morro São João e vou para a minha casa andando. Ontem só havia um único carro com dois policiais dentro parado em uma esquina. Em cima do morro não existe policiamento nenhum. Uma vez ou outra um carro blindado sobe e faz uma ronda. Estamos com muito medo porque com certeza a facção rival vai tentar tomar novamente.</p></blockquote>
<div class="translation">[Vita vya Magenge] vimekuwa ni kama kama kawaida, lakini jumamosi hii ilikuwa tofauti. Mgogoro ulianza kwa sababu ya jaribio la kuivamia Morro dos Macacos lililofanywa na wauza madawa ya kulevya kutoka Morro Sao Joao, na hili halikuwa jaribio la kwanza. Neno lililokuwa kwenye kwenye makazi ni kuwa kundi shindani limetoa amri ya kuiteka Morro dos Macacos ifikapo mwezi Desemba na kwamba maofisa wa polisi walikuwa wanawaunga mkono wauzaji hao.<br />
Doria ya polisi haitekelezwi na wakazi wana wasiwasi mkubwa, wanahofia uvamizi mpya. Ninafanya kazi chini ya bonde la Morro Sao Joao na hutembea ninaporudi nyumbani. Jana, kulikuwa na gari moja tu lililokuwa na maofisa wawili wa polisi ndani yake lililoegeshwa kwenye kona. Hakuna doria ya polisi juu kwenye makazi. Mara moja moja kwa nadra gari iliyokingwa (mithili ya gari ya jeshi) huja huku juu na kufanya doria. Tumo kwenye hofu kubwa kwani tuna hakika kuwa kundi shindani litajaribu kulikomboa eneo.</div>
<p><em><a href="http://www.vivafavela.com.br/publique/cgi/cgilua.exe/sys/start.htm?infoid=46400&#038;sid=87">Viva Favela</a></em> [pt] pia inatoa maoni ya <em>Wagner da Silva de Barros</em>, mwenye umri wa miaka 29 ambaye ni mkazi wa Vila Penheiro kutoka Complexo da Mare, anayesema kuwa athari za mgogoro katika Morro dos Macacos umefika mbali kiasi hiki kwa sababu ya helikopta iliyotunguliwa na anaongeza kuwa vita hii itaenea pia kwenye  jamii nyingine nyingi:</p>
<blockquote><p>A queda do helicóptero e a morte dos três policiais chocou parte da população, mas na Maré, durante cinco meses, nós vivemos um confronto entre facções que matou muita gente, inclusive moradores que nada tinham a ver com o tráfico, e não teve nem metade da divulgação que esse tiroteio dos Macacos está tendo.</p>
<p>Esses tiroteios reforçam de que na favela só existe bandido e violência, mas o que muitas pessoas ignoram é que trabalhadores morrem durante os conflitos e são logo identificados como traficantes pela polícia.</p></blockquote>
<div class="translation">Kuanguka kwa helikopta na vifo vya maofisa watatu wa polisi kulishtua sehemu ya wakazi wa kwenye vitongoji, lakini Mare [vitongoji hivyo vya hali ya chini], kwa miezi mitano, tumeishi katika ugomvi baina ya makundi ambao umeua watu wengi zaidi, pamoja na wakazi ambao hawakuwa na uhusiano wowote na biashara ya madawa ya madawa ya kulevya, na hawa hawakupata hata nusu ya habari zilizotangazwa na vyombo vya habari juu ya mapambano ya risasi katika Morro dos Macacos.<br />
Mapambano haya ya risasi yanasisitiza ukweli kuwa katika maeneo ya maskini (favelas) kuna majambazi na machafuko, ila jambo ambalo watu wengi hawafahamu ni kuwa wafanyakazi hufariki wakati wa machafuko na haraka polisi huwatangaza kama wauza madawa ya kulevya.</div>
<p>Kwa mujibu wa <em><a href="http://www.vivafavela.com.br/publique/cgi/cgilua.exe/sys/start.htm?infoid=46400&#038;sid=87">Viva Favela</a></em> [pt], katika kesi ya Morro dos Macacos, vijana watatu wa kiume wasio na hatia ambao waliuwawa kwa risasi walijumuishwa kwenye orodha ya majambazi waliouwawa. Katibu wa Usalama Jose Mariano Beltrame alijirudi na kuomba msamaha kwa familia za Marcelo Costa Gomes, 26, Leonardo Fernandes Paulino, 27, na Francisco Haílton Vieira Silva, 24. Walikuwa wanarudi nyumbani kutokea kwenye hafla wakati uvamizi ulipotokea. Kijana wa nne, mhudumu wa hoteli Francisco Alaílton Vieira da Silva, 22, aliokolewa na wakazi na hivi sasa yuko hospitali katika kitengo cha huduma maalum. Mpenzi wake wa kike ni mjamzito wa miezi 3.</p>
<p>Walter Mesquista wa <em>Viva Favela</em> pia <a href="http://www.vivafavela.com.br/publique/cgi/cgilua.exe/sys/start.htm?infoid=46399&#038;sid=87">anatoa picha za mgogoro huo</a> zilizopigwa na mpiga picha <em>Guillermo Planel</em> siku ambayo watu wanaiita “Vita vya Mihadarati”.</p>
<p><img alt="" src="http://globalvoicesonline.org/wp-content/uploads/2009/10/Macacos-001.jpg" title="Macacos-001" class="aligncenter" width="400" height="300" /></p>
<p><img alt="" src="http://globalvoicesonline.org/wp-content/uploads/2009/10/Macacos-002.jpg" title="Macacos-002" class="aligncenter" width="400" height="300" /></p>
<p><img alt="" src="http://globalvoicesonline.org/wp-content/uploads/2009/10/Macacos-003.jpg" title="Macacos-003" class="aligncenter" width="400" height="300" /></p>
<p><img alt="" src="http://globalvoicesonline.org/wp-content/uploads/2009/10/Macacos-004.jpg" title="Macacos-004" class="aligncenter" width="400" height="300" /></p>
<p><img alt="" src="http://globalvoicesonline.org/wp-content/uploads/2009/10/Macacos-005.jpg" title="Macacos-005" class="aligncenter" width="400" height="300" /></p>
<p><img alt="" src="http://globalvoicesonline.org/wp-content/uploads/2009/10/Macacos-006.jpg" title="Macacos-006" class="aligncenter" width="400" height="300" /></p>
<p><img alt="" src="http://globalvoicesonline.org/wp-content/uploads/2009/10/Macacos-007.jpg" title="Macacos-007" class="aligncenter" width="400" height="300" /></p>
<p><img alt="" src="http://globalvoicesonline.org/wp-content/uploads/2009/10/Macacos-008.jpg" title="Macacos-008" class="aligncenter" width="400" height="300" /></p>
<p><img alt="" src="http://globalvoicesonline.org/wp-content/uploads/2009/10/Macacos-009.jpg" title="Macacos-009" class="aligncenter" width="400" height="300" /></p>
<p><img alt="" src="http://globalvoicesonline.org/wp-content/uploads/2009/10/macacos011_trat.jpg" title="macacos011_trat" class="aligncenter" width="400" height="300" /></p>
<p><img alt="" src="http://globalvoicesonline.org/wp-content/uploads/2009/10/macacos012_trat.jpg" title="macacos012_trat" class="aligncenter" width="400" height="300" /></p>
<p><img alt="" src="http://globalvoicesonline.org/wp-content/uploads/2009/10/macacos013_trat.jpg" title="macacos013_trat" class="aligncenter" width="400" height="300" /></p>
<p>Kuna mauaji takriban 6,000 kwa mwaka katika jimbo zima la Rio, ambalo lina wakazi milioni 14. Operesheni “Eneza Amani” yenye doria ya kudumu imekuwa ikitekelezwa kwa mwaka mzima katika vitongoji vitano. Ongezeko la uwepo wa polisi vitongojini kunayalazimisha magenge kupigania maeneo mengine.</p>
<p><img alt="" src="http://globalvoicesonline.org/wp-content/uploads/2009/10/viva_favela_logoweb-300x136.jpg" title="viva_favela_logoweb" class="alignnone" width="300" height="136" /></p>
<p><em><a href="http://www.vivafavela.com.br/publique/cgi/cgilua.exe/sys/start.htm?infoid=40489&#038;sid=74">Viva Favela</a> ni mradi wa uanahabari wa kijamii ambao unafanya kazi na wanablogu malum pamoja na wapiga picha ambao wanaishi katika maeneo maskini ya Rio de Janeiro. Mradi huo uko chini ya uongozi wa Mhariri <a href="http://twitter.com/rodrigonogueira">Rodrigo Nogueira</a>. Unaweza kupata taarifa zaidi katika <a href="http://twitter.com/vivafavela">akaunti yao rasmi ya Twita</a></em> [pt] <em>na katika <a href="http://www.orkut.com.br/Main#Community?cmm=33684890">jamii </a>ya Orkut </em>[pt].</p>
]]></content:encoded>
			<wfw:commentRss>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/11/brazil-mtazamo-wa-wakazi-wa-vitongoji-maskini/feed/</wfw:commentRss>
		<slash:comments>0</slash:comments>
		</item>
		<item>
		<title>Misri na Aljeria: Pambano la Twita</title>
		<link>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/11/misri-na-aljeria-pambano-la-twita/</link>
		<comments>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/11/misri-na-aljeria-pambano-la-twita/#comments</comments>
		<pubDate>Mon, 16 Nov 2009 12:04:35 +0000</pubDate>
		<dc:creator>j nambiza tungaraza</dc:creator>
				<category><![CDATA[Algeria]]></category>
		<category><![CDATA[Egypt]]></category>
		<category><![CDATA[International Relations]]></category>
		<category><![CDATA[Media]]></category>
		<category><![CDATA[Middle East & North Africa]]></category>
		<category><![CDATA[Sport]]></category>
		<category><![CDATA[Weblog]]></category>

		<guid isPermaLink="false">http://sw.globalvoicesonline.org/?p=673</guid>
		<description><![CDATA[Katika sehemu nyingi duniani, hakuna linalounganisha zaidi – au wakati mwingine kutenganisha – zaidi ya pambano la mpira wa miguu. Washabiki wa Misri na Aljeria, katika ulimwengu wote wa Waarabu na zaidi, walilidhihirisha hilo Jumamosi hii wakati timu zao zilipokwenda sambamba wakati wa kuwania kuingia fainali za Kombe la Dunia huko Afrika Kusini. ]]></description>
			<content:encoded><![CDATA[<em>Ilichapwa kwanza na<a href="http://globalvoicesonline.org/author/jillian-york/">Jillian C. York</a>  &middot; Imetafsiriwa na <a href='http://sw.globalvoicesonline.org/author/j-nambiza-tungaraza/'>j nambiza tungaraza</a> &middot;  <a href='http://globalvoicesonline.org/2009/11/15/egypt-vs-algeria-the-twitter-match/'>Angalia ujumbe mama</a></em> 
<br /><p>Katika sehemu nyingi duniani, hakuna linalounganisha zaidi – au wakati mwingine kutenganisha – zaidi ya pambano la mpira wa miguu. Washabiki wa Misri na Aljeria, katika ulimwengu wote wa Waarabu na zaidi, walilidhihirisha hilo Jumamosi hii wakati timu zao zilipokwenda sambamba wakati wa kuwania kuingia fainali za Kombe la Dunia huko Afrika Kusini. Wakati vihoro vilipanda juu huko mjini Cairo, pia vilikuwa hai na katika hali nzuri kwenye uwanja yakini mtandaoni, pamoja na kwenye <a href="http://twitter.com/">Twita</a>, ambako watumiaji walitaarifu kuwa skrini zao zilijaa hisia za mpira. Mtumiaji wa Twita <em><a href="http://twitter.com/mbaa">mbaa</a></em> alituma picha ya skrini yake, ambayo ilifurika mazungumzo ya pambano hilo:</p>
<p><img alt="" src="http://globalvoicesonline.org/wp-content/uploads/2009/11/mbaa2.jpg" title="mbaa" class="aligncenter" width="535" height="410" /></p>
<p>Ujumbe wa twita kutoka kwa Mmisri <em><a href="http://twitter.com/embee">embee</a></em> <a href="http://twitter.com/embee/status/5718935256">ulionyesha</a> ushabiki uliokithiri wa baadhi ya washabiki:</p>
<p><img alt="" src="http://globalvoicesonline.org/wp-content/uploads/2009/11/embee-status-5718935256-300x113.PNG" title="embee-status-5718935256" class="aligncenter" width="300" height="113" /></p>
<p>Baadhi ya taarifa zinadai kuwa tiketi zote zimekwishauzwa hivi sasa! Wakati huo huo, Mmisri <em><a href="http://twitter.com/norayounis">NoraYounis</a></em> <a href="http://twitter.com/norayounis/status/5718108814">alielezea kutoamini</a> kwake katika nguvu ya kuunganisha ya mpira wa miguu kwa Wamisri:</p>
<p><img alt="" src="http://globalvoicesonline.org/wp-content/uploads/2009/11/NoraYounis-status-5718108814-300x152.PNG" title="NoraYounis-status-5718108814" class="aligncenter" width="300" height="152" /></p>
<p><a href="http://twitter.com/nohaatef/status/5718339271">Ujumbe wa twita</a> wa Mmisri <em><a href="http://twitter.com/nohaatef">NohaAtef</a></em>, kwa upande mwingine, ulionyesha vitu vinavyoweza kuinua mioyo katika mpira wa miguu:</p>
<p><img alt="" src="http://globalvoicesonline.org/wp-content/uploads/2009/11/NohaAtef-status-5718339271-300x151.PNG" title="NohaAtef-status-5718339271" class="aligncenter" width="300" height="151" /></p>
<p>Katika mifano mingi, mpira wa miguu ulichimbua ushindani wa kitaifa. Waaljeria na Wamisri walikwenda kichwa kwa kichwa kwenye twita wakati pambano likiendelea. Mmisri <em><a href="http://twitter.com/sandmonkey">Sandmonkey</a></em> <a href="http://twitter.com/sandmonkey/status/5714575409">aling’aka</a>: </p>
<p><img alt="" src="http://globalvoicesonline.org/wp-content/uploads/2009/11/Sandmonkey-status-5714575409-300x86.PNG" title="Sandmonkey-status-5714575409" class="aligncenter" width="300" height="86" /></p>
<p>Mualjeria-Mmarekani <em><a href="http://twitter.com/themoornextdoor">themoornextdoor</a></em> alijibu mapigo <a href="http://twitter.com/themoornextdoor/status/5715301341">akitania</a>:</p>
<p><img alt="" src="http://globalvoicesonline.org/wp-content/uploads/2009/11/themoornextdoor-status-5715301341-300x124.PNG" title="themoornextdoor-status-5715301341" class="aligncenter" width="300" height="124" /></p>
<p>Mwishowe, Mualjeria <em><a href="http://twitter.com/reemba">reemba</a></em> <a href="http://twitter.com/reemba/status/5717755317">alitukumbusha</a> kuwa mambo bado hayajaisha mpaka yaishe:</p>
<p><img alt="" src="http://globalvoicesonline.org/wp-content/uploads/2009/11/reemba-status-5717755317-300x147.PNG" title="reemba-status-5717755317" class="aligncenter" width="300" height="147" /></p>
]]></content:encoded>
			<wfw:commentRss>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/11/misri-na-aljeria-pambano-la-twita/feed/</wfw:commentRss>
		<slash:comments>0</slash:comments>
		</item>
		<item>
		<title>Jordan: Barua kwa MBC</title>
		<link>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/11/jordan-barua-kwa-mbc/</link>
		<comments>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/11/jordan-barua-kwa-mbc/#comments</comments>
		<pubDate>Sat, 14 Nov 2009 09:24:15 +0000</pubDate>
		<dc:creator>j nambiza tungaraza</dc:creator>
				<category><![CDATA[English]]></category>
		<category><![CDATA[Jordan]]></category>
		<category><![CDATA[Media]]></category>
		<category><![CDATA[Middle East & North Africa]]></category>
		<category><![CDATA[Roundups]]></category>

		<guid isPermaLink="false">http://sw.globalvoicesonline.org/?p=648</guid>
		<description><![CDATA[Ilichapwa kwanza naAmira Al Hussaini  &#183; Imetafsiriwa na j nambiza tungaraza &#183;  Angalia ujumbe mama 
M-jordan Ola Eliwat, kutoka Cinnamon Zone, anaandika barua ya wazi kwa makapuni ya televisheni ya MBC. Katika barua hiyo anaandika: &#8220;Na tafadhali fikirieni kufunga 90% ya idhaa zenu, nadhani itakuwa hisani KUBWA kwa taifa la Kiarabu!&#8221;
]]></description>
			<content:encoded><![CDATA[<em>Ilichapwa kwanza na<a href="http://globalvoicesonline.org/author/amira-al-hussaini/">Amira Al Hussaini</a>  &middot; Imetafsiriwa na <a href='http://sw.globalvoicesonline.org/author/j-nambiza-tungaraza/'>j nambiza tungaraza</a> &middot;  <a href='http://globalvoicesonline.org/2009/11/14/jordan-letter-to-mbc/'>Angalia ujumbe mama</a></em> 
<br /><p>M-jordan Ola Eliwat, kutoka <em><a href="http://oeliwat.jeeran.com/archive/2009/11/970286.html">Cinnamon Zone</a></em>, anaandika barua ya wazi kwa makapuni ya televisheni ya MBC. Katika barua hiyo anaandika: &#8220;Na tafadhali fikirieni kufunga 90% ya idhaa zenu, nadhani itakuwa hisani KUBWA kwa taifa la Kiarabu!&#8221;</p>
]]></content:encoded>
			<wfw:commentRss>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/11/jordan-barua-kwa-mbc/feed/</wfw:commentRss>
		<slash:comments>0</slash:comments>
		</item>
		<item>
		<title>Naijeria: Wanablogu Wajadili Sifa Mbaya ya Naijeria</title>
		<link>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/11/naijeria-wanablogu-wajadili-sifa-mbaya-ya-naijeria/</link>
		<comments>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/11/naijeria-wanablogu-wajadili-sifa-mbaya-ya-naijeria/#comments</comments>
		<pubDate>Wed, 11 Nov 2009 12:22:55 +0000</pubDate>
		<dc:creator>j nambiza tungaraza</dc:creator>
				<category><![CDATA[English]]></category>
		<category><![CDATA[Media]]></category>
		<category><![CDATA[Nigeria]]></category>
		<category><![CDATA[Sub-Saharan Africa]]></category>
		<category><![CDATA[Weblog]]></category>

		<guid isPermaLink="false">http://sw.globalvoicesonline.org/?p=622</guid>
		<description><![CDATA[Inajulikana vyema kuwa Naijeria ina tatizo la muonekano – utapeli wa 419 kwenye intaneti, rushwa, uharamia wa mafuta katika jimbo la Delata – kwa watu wengi, huu ndio uhusiano unaokuja akilini wakati nchi yenye watu wengi zaidi Afrika inapotajwa. ]]></description>
			<content:encoded><![CDATA[<em>Ilichapwa kwanza na<a href="http://globalvoicesonline.org/author/eremipagamo-amabebe/">Eremipagamo Amabebe</a>  &middot; Imetafsiriwa na <a href='http://sw.globalvoicesonline.org/author/j-nambiza-tungaraza/'>j nambiza tungaraza</a> &middot;  <a href='http://globalvoicesonline.org/2009/11/02/nigeria-bloggers-debate-nigerias-negative-image/'>Angalia ujumbe mama</a></em> 
<br /><p><img alt="" src="http://globalvoicesonline.org/wp-content/uploads/2009/10/nigeria-300x225.jpg" title="photo from Oluniyi Ajao: http://www.flickr.com/photos/niyyie/2212651560/" class="alignleft" width="300" height="225" /> Inajulikana vyema kuwa Naijeria ina tatizo la muonekano – utapeli wa 419 kwenye intaneti, rushwa, uharamia wa mafuta katika jimbo la Delta – kwa watu wengi, huu ndio uhusiano unaokuja akilini wakati nchi yenye watu wengi zaidi Afrika inapotajwa. Hata hivyo, mwaka uliopita umekuwa mgumu kwa watu wa Najeria walio ughaibuni: katika miezi michache iliyopita, mfululizo wa matukio  yanayoionyesha Naijeria katika mwanga wa utata ulizua majadiliano kwenye ulimwengu wa blogu.</p>
<p>Mwezi Septemba, Sony ilitoa <a href="http://naijablog.blogspot.com/2009/09/that-sony-ps3-419-ad-if-you-havent-seen.html">tangazo la mchezo wa Playstation 3</a> ambalo lilikuwa na mstari unaosema, “Usiamini kila kitu unachosoma kwenye intaneti – vinginevyo, ningekuwa milionea wa Kinaijeria hivi sasa.” Tangazo hilo lilikumbana na mawazo ya kuchanganyikiwa kutoka kwa Wanaijeria wengi, na Serikali ya Shirikisho iliitaka Sony kuomba radhi (Sony iliomba msamaha na baadaye ikaliondoa tangazo).</p>
<p>Katika wakati huo huolilikuja toleo la filamu ya <em>District 9 </em>– filamu ya kisayansi ambayo ilipokewa kwa mapitio mazuri lakini yaliyowakasirisha Wanaijeria. <a href="http://news.bbc.co.uk/2/hi/8264180.stm">Serikali ya Naijeria ilichukizwa</a> na jinsi filamu hiyo ilivyowaonyesha Wanaijeria kama wahalifu na wala watu, na iliipiga marufuku ndani ya Naijeria na kulitaka Baraza la Udhibiti kuikamata kutoka kwenye majumba ya sinema. Kwenye mtandao, filamu hiyo ilisababisha maoni yaliyopishana, huku baadhi ya watu wakichukua mtizamo kuwa filamu ina mtizamo wa kibaguzi dhidi ya Wanaijeria, wakati wengine waliitetea kama wakilisho la kubuni lenye chembe ndogo ya ukweli.</p>
<p>Adamu Waziri katika EVCL <a href="http://evclvisuals.blogspot.com/2009/09/nigeria-and-district-9.html">anasema</a> kuwa mara nyingi jinsi Wanaijeria wanavyoonyeshwa na Wanaijeria pia huwa hakufurahishi:</p>
<blockquote><p>Nollywood, kiwanda cha filamu cha wazawa, kimetuonyesha katika mwanga mbaya zaidi kwa wote, watazamaji wa kitaifa na wale wa kimataifa. Kuna wakati usingeweza kupata filamu ya Nollywood ambayo haikuwa na haya yafuatayo au mchanganyiko wake: utapeli, uchawi, ujambazi wa kutumia silaha, ngono kati wanandugu, mapenzi nje ya ndoa, kula watu na pia suala tunalolipenda, rushwa. Nollywood imekuwa ikitoa maelfu ya filamu zenye maudhui haya kwa miaka bila pingamizi la kweli kutoka kwa umma wa kawaida au wizara.<br />
… kupiga marufuku filamu kunaanzisha mfano mbaya; na kunaweza kuwa hatari. Tuachieni sisi umma tujadili hili suala. Tumekomaa vya kutosha kufanya hivyo. Kwa kweli, waziri wetu amefanikiwa kuipatia filamu hiyo matangazo zaidi jambo ambalo nina hakika hakulikusudia.</p></blockquote>
<p>Nicole Stamp <a href="http://www.racialicious.com/2009/08/18/district-9-is-racist-alternate-perspective/">anatoa maoni</a> kuhusu masuala ya rangi katika <em>District 9</em>:</p>
<blockquote><p>
Jambo ambalo linanikera ni kuwa watu wengi wanaoiangalia filamu hii hawaulizi, au hata hawaoni, muonekano huu usioaminika wa kibaguzi…. Kwa nini Wanaijeria wasiweze kuwa watu wenye kutaka vitu vyenye  mantiki kama vile pesa na silaha? Kwa nini wanaenda nje ya njia zao na kuwa washenzi wa ki-ooga-booga?&#8230;  haiwezekani kutojali jinsi Wanaijeria wanavyoonyeshwa ambavyo kukiangaliwa katika muktadha mpana, kumepita hali ya kuumiza au kudhalilisha lakini ni hali ya hatari.</p></blockquote>
<p>Unaweza kusoma <a href="http://nigerianstalk.org/?p=261">zaidi mjadala huu kwenye tovuti ya Nigerianstalk.org</a> au tafuta kwenye google kwa kutumia maneno haya “district 9 race”.</p>
<p>Katika siku za karibuni zaidi, gazeti la Time <a href="http://www.time.com/time/photogallery/0,29307,1926470,00.html">lilichapisha onyesho la picha</a> na mpiga picha wa Afrika Kusini <a href="http://www.pieterhugo.com/">Pieter Hugo</a> ambazo zilionyesha picha kutoka kwenye kiwanda cha sinema cha &#8220;<a href="http://en.wikipedia.org/wiki/Nollywood">Nollywood</a>&#8221; huko Naijeria. Japokuwa halikuwa onyesho tata kama ilivyokuwa District 9 au tangazo la Playstation, mpiga picha huyo hata hivyo alichochea mdahalo katika ulimwengu wa blogu, na mjadala kuhusu kama uonyeshwaji huo wa Wanaijeria uko chini ya fungu la uhuru wa kisanii au upendeleo wa kitamaduni.</p>
<p>Solomon Sydelle kwenye blogu ya Nigerian Curiosity <a href="http://www.nigeriancuriosity.com/2009/10/time-magazines-nollywood-pictorial.html">anaandika</a>:</p>
<blockquote><p>Ninaelewa fika haja ya kusogeza mipaka, kwani shauku hiyo imepelekea kupatikana kwa ubunifu wa kazi za hali juu sana na mafanikio ya wakati wote. Hata hivyo, <strong>kwa picha hizi, ninahangaika kuzithamini pamoja na kile kinachoonyeshwa na ninaamini kuwa bila ulazima wowote zilitegemea upendeleo ambao unathibitisha imani fulani potofu za kadamnasi ya Hugo ambayo kwa kiasi kikubwa ni ya Magharibi.</strong></p></blockquote>
<p>Matukio haya yametukia katika wakati mbaya kwani yanawiana na mpango mpya uliozinduliwa mwanzoni mwa mwaka huu wa “kutengeneza chapa mpya ya Naijeria” (Re-brand Nigeria). Mpango huo unadhaminiwa na Dk. Dora Akunyili, Waziri wa Habari na Mawasiliano wa Naijeria, na ambao umekumbana na yote mawili, sifa na kukosolewa (angalia <a href="http://globalvoicesonline.org/2009/04/03/nigeria-on-rebranding-nigeria/comment-page-2/">hapa</a> ili kusoma mjadala huo kwenye Global Voices) </p>
<p>Bunmi Oloruntoba katika blogu ya A Bombastic Element <a href="http://bombasticelements.blogspot.com/2009/10/nigeria-super-villains-of-modern-age_22.html">anajadili kampeni ya kutengeneza chapa mpya</a> katika muktadha wa <a href="http://www.bbc.co.uk/worldservice/documentaries/2009/10/091021_rebranding_nigeria.shtml">mjadala wa hivi karibuni kwenye BBC</a> juu ya suala hilo:</p>
<blockquote><p>Waziri alikuwa na shauri zuri aliposema kuwa Naijeria haiyatazami mengi yaliyo chanya, haielezi simulizi zake na inafanya makosa ya kuiachia dunia kufafanua taswira yake inayoelemea kwenye sifa zake mbaya pekee. Na anayo mifano mizuri ya mambo chanya. Lakini BBC ilitafuta maafisa uhusiano na wataalamu wa chapa wachache ambao wanapinga kwa kusema, kama nchi inataka kujitengenezea chapa mpya, inapaswa kuipatia timu yoyote ya mahusiano nyenzo zaidi. Wale waliohojiwa walisema, ugavi wa umeme wa uhakika na mwisho wa uchumi unaotegemea mashjine za jenereta kutaizifanya jitihada za kutengeneza chapa mpya ya Naijeria kuwa “rahisi.” Na kuthibitisha  maneno yao, dakika 13:40 baada ya kipindi kuanza… naam, haupaswi kuwa Mnaijeria kujua ni nini kilichotokea.</p></blockquote>
<p>Sehemu angavu ya mjadala wa taswira ya Naijeria ilikuwa ni video iliyosambazwa sana ya mwandishi wa Kinaijeria <a href="http://en.wikipedia.org/wiki/Chimamanda_Ngozi_Adichie">Chimamanda Ngozi Adichie</a> akiongelea juu ya “<a href="http://www.ted.com/talks/chimamanda_adichie_the_danger_of_a_single_story.html">Hatari ya simulizi moja.</a>”  Adichie anatoa maoni juu ya mitegoya taswira kubwa ya Afrika kama sehemu ya majanga; anatahadharisha kuwa kujekea upeo wa “simuli moja” kunasiliba uzoefu na kutengeneza imani potofu. Kwa wanablogu wengi, maneno ya Adichie yalitoa mwangwi wa kughafirika kwao na taswira ya Naijeria iliyozoeleka nje ya nchi. </p>
<p><object width="446" height="326"><param name="movie" value="http://video.ted.com/assets/player/swf/EmbedPlayer.swf"></param><param name="allowFullScreen" value="true" /><param name="wmode" value="transparent"></param><param name="bgColor" value="#ffffff"></param><param name="flashvars" value="vu=http://video.ted.com/talks/dynamic/ChimamandaAdichie_2009G-medium.flv&#038;su=http://images.ted.com/images/ted/tedindex/embed-posters/ChimamandaAdichie-2009G.embed_thumbnail.jpg&#038;vw=432&#038;vh=240&#038;ap=0&#038;ti=652&#038;introDuration=16500&#038;adDuration=4000&#038;postAdDuration=2000&#038;adKeys=talk=chimamanda_adichie_the_danger_of_a_single_story;year=2009;theme=new_on_ted_com;theme=words_about_words;theme=speaking_at_tedglobal2009;theme=the_creative_spark;theme=master_storytellers;event=TEDGlobal+2009;&#038;preAdTag=tconf.ted/embed;tile=1;sz=512x288;" /><embed src="http://video.ted.com/assets/player/swf/EmbedPlayer.swf" pluginspace="http://www.macromedia.com/go/getflashplayer" type="application/x-shockwave-flash" wmode="transparent" bgColor="#ffffff" width="446" height="326" allowFullScreen="true" flashvars="vu=http://video.ted.com/talks/dynamic/ChimamandaAdichie_2009G-medium.flv&#038;su=http://images.ted.com/images/ted/tedindex/embed-posters/ChimamandaAdichie-2009G.embed_thumbnail.jpg&#038;vw=432&#038;vh=240&#038;ap=0&#038;ti=652&#038;introDuration=16500&#038;adDuration=4000&#038;postAdDuration=2000&#038;adKeys=talk=chimamanda_adichie_the_danger_of_a_single_story;year=2009;theme=new_on_ted_com;theme=words_about_words;theme=speaking_at_tedglobal2009;theme=the_creative_spark;theme=master_storytellers;event=TEDGlobal+2009;"></embed></object></p>
<p>Mwanablogu Shade NonConformist  <a href="http://shadenonconformist.blogspot.com/2009/10/danger-of-intellectualization-long-post.html">anaandika kuhusu uhusiano wa rissala ya Adichie na taswira ya Naijeria</a>:</p>
<blockquote><p>Ninaamini kuwa hivi ndivyo Adichie alivyomaanisha katika hotuba ya <strong>Hatari ya Simulizi Moja</strong> aliyoitoa kwenye TED. Inageuka kuwa tatizo pale sura <strong>pekee</strong> ya Afrika tunayoiona ni ile inayohusisha wanyama waliokufa, umaskini, majanga, vifo, ufisadi, watu mashuhuri wanaasili watoto… unafahamu yadi zote tisa. Sasa sisemim kuwa Afrika haina mambo hayo. Wote tunaweza tukaafikiana kuwa tunayo. Ninachosema ni kuwa mambo hayo si ya nchi za Kiafrika peke yake.<br />
…Mimi/sisi hatutasikoma kukosoa taswira za Afrika ambazo hazina mizani na zenye ubaguzi. Kuonyesha taswira zenye mizani iliyolingana ni jambo muhimu. Kama Waafrika pia tunapaswa kiujifanya kuwa kama vyombo ambavyo viko <strong>radhi kutumika katika mabadiliko</strong> tunayotakja kuyaona (ambayo tutayaona) katika bala letu tunalolienzi. </p></blockquote>
]]></content:encoded>
			<wfw:commentRss>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/11/naijeria-wanablogu-wajadili-sifa-mbaya-ya-naijeria/feed/</wfw:commentRss>
		<slash:comments>0</slash:comments>
		</item>
		<item>
		<title>Afrika: Chungu cha Kuiyeyusha Afrika</title>
		<link>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/11/afrika-chungu-cha-kuiyeyusha-afrika/</link>
		<comments>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/11/afrika-chungu-cha-kuiyeyusha-afrika/#comments</comments>
		<pubDate>Thu, 05 Nov 2009 13:36:02 +0000</pubDate>
		<dc:creator>j nambiza tungaraza</dc:creator>
				<category><![CDATA[English]]></category>
		<category><![CDATA[Kenya]]></category>
		<category><![CDATA[Media]]></category>
		<category><![CDATA[Nigeria]]></category>
		<category><![CDATA[Roundups]]></category>
		<category><![CDATA[Sub-Saharan Africa]]></category>

		<guid isPermaLink="false">http://sw.globalvoicesonline.org/?p=536</guid>
		<description><![CDATA[Ilichapwa kwanza naNdesanjo Macha  &#183; Imetafsiriwa na j nambiza tungaraza &#183;  Angalia ujumbe mama 
Marvin anaandika kuhusu Afripot, tovuti ya habari inayotilia makini habari za Afrika: “Hivi sasa anatambulisha chungu cha kuyeyushia Afrika – Afripot. Tayari nimo ndani ninayeyuka na ninatumaini kukuona pale na wewe pia kwani mazungumzo kuhusu Afrika na Waafrika yanachukua [...]]]></description>
			<content:encoded><![CDATA[<em>Ilichapwa kwanza na<a href="http://globalvoicesonline.org/author/ndesanjo-macha/">Ndesanjo Macha</a>  &middot; Imetafsiriwa na <a href='http://sw.globalvoicesonline.org/author/j-nambiza-tungaraza/'>j nambiza tungaraza</a> &middot;  <a href='http://globalvoicesonline.org/2009/11/05/africa-africas-melting-pot/'>Angalia ujumbe mama</a></em> 
<br /><p><a href="http://marvintumbo.wordpress.com/2009/11/04/africa%E2%80%99s-melting-pot/">Marvin anaandika kuhusu Afripot</a>, tovuti ya habari inayotilia makini habari za Afrika: “Hivi sasa anatambulisha chungu cha kuyeyushia Afrika – Afripot. Tayari nimo ndani ninayeyuka na ninatumaini kukuona pale na wewe pia kwani mazungumzo kuhusu Afrika na Waafrika yanachukua kasi na kupamba moto. Ni nani ajuaye, inaweza kutengeneza joto la kutosha na kulazimisha mabadiliko tuayoyahitaji sana.” </p>
]]></content:encoded>
			<wfw:commentRss>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/11/afrika-chungu-cha-kuiyeyusha-afrika/feed/</wfw:commentRss>
		<slash:comments>0</slash:comments>
		</item>
		<item>
		<title>Saudia Arabia: Ambako Kuiga Kazi Kinyume cha Haki Miliki ni Kosa la Jinai</title>
		<link>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/11/saudia-arabia-ambako-kuiga-kazi-kinyume-cha-haki-miliki-ni-kosa-la-jinai/</link>
		<comments>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/11/saudia-arabia-ambako-kuiga-kazi-kinyume-cha-haki-miliki-ni-kosa-la-jinai/#comments</comments>
		<pubDate>Tue, 03 Nov 2009 12:06:46 +0000</pubDate>
		<dc:creator>Christian Bwaya</dc:creator>
				<category><![CDATA[English]]></category>
		<category><![CDATA[General]]></category>
		<category><![CDATA[Internet & Telecoms]]></category>
		<category><![CDATA[Law]]></category>
		<category><![CDATA[Media]]></category>
		<category><![CDATA[Middle East & North Africa]]></category>
		<category><![CDATA[Protest]]></category>
		<category><![CDATA[Saudi Arabia]]></category>
		<category><![CDATA[Weblog]]></category>

		<guid isPermaLink="false">http://sw.globalvoicesonline.org/?p=458</guid>
		<description><![CDATA[Wanablogu wa Kisaudia wanaungana ili kumuunga mkono mwanablogu mwenzao anayelituhumu gazeti moja kuwa limetumia picha na kuzinakili kutoka mwenye blogu yake bila ruhusa. ]]></description>
			<content:encoded><![CDATA[<em>Ilichapwa kwanza na<a href="http://globalvoicesonline.org/author/amira-al-hussaini/">Amira Al Hussaini</a>  &middot; Imetafsiriwa na <a href='http://sw.globalvoicesonline.org/author/bwaya/'>Christian Bwaya</a> &middot;  <a href='http://globalvoicesonline.org/2009/10/20/saudi-arabia-where-plagiarism-is-a-crime/'>Angalia ujumbe mama</a></em> 
<br /><p>Wanablogu wa Kisaudia wanaungana ili kumuunga mkono mwanablogu mwenzao anayelituhumu gazeti moja kuwa limetumia picha na kuzinakili kutoka mwenye blogu yake bila ruhusa. </p>
<p><em><a href="http://saudijeans.org/2009/10/14/alyaum-steals-kaust-blogger/">Saudi Jeans</a></em>‘ Ahmed Al Omran anazo sifa kiduchu mno kwa gazeti hilo linalotuhumiwa kwa kitendo cha kutumia kazi za wengine kinyume cha haki miliki: </p>
<blockquote><p>Ingawa gazeti la al – Yaum, kwa muda mrefu limefurahia nafasi kubwa katika Jimbo la Mashariki, (EP) linabaki kuwa kati ya machapicho duni zaidi nchini. Nilizaliwa na kukuzwa katika Jimbo la Mashariki, na nilizoea kusoma magazeti ya Ashraq al-Awsat, al-Hayat na al-Watan lakini sio al-Yaum. </p></blockquote>
<p>Kutofurahishwa kwa Al Omran kulichochewa zaidi baada ya <em><a href="http://saudiaggie.blogspot.com/2009/10/i-should-be-getting-paid-for-this.html">Saudi Aggie</a></em>, mwanafunzi mwenye jina la Nathan wa <em>Chuo Kikuu cha Sayansi na Teknolojia cha Mfalme Abdulla</em> (KAUST) <a href="http://globalvoicesonline.org/2009/09/26/saudi-arabia-kaust-to-inspire-scientific-achievement-and-more/">kilichofunguliwa hivi karibuni</a> alipoleta malalamiko kwamba gazeti hilo limetumia picha zake pamoja na uchambuzi wake kuhusu uchaguzi wa wanafunzi hivi majuzi. Ameweka nakala ya habari hizo kutoka gazetini na kuwauliza wasomaji wake:</p>
<blockquote><p>Siwezi kuamini hili! Angalia makala hii iliyochapishwa hivi majuzi kwenye gazeti maarufu la Saudi Arabia, Al Yaum. Je, picha hizi zinaonekana kana kwamba zinafahamika? Vipi kuhusu maneno? Kama huwezi kusoma Kiarabu, hii ilichukuliwa karibu neno kwa neno kutoka kwenye makala ya blogu yangu niliyoipa jina la ‘<a href="http://saudiaggie.blogspot.com/2009/10/elections.html">uchaguzi</a>’ na kuichapa Oktoba 5, 2009. Hii haiwezi kuwa sahihi kisheria, hata hapa Saudi Arabia!</p></blockquote>
<p>Mwanafuzi huyo wa Kimarekani anaongeza: </p>
<blockquote><p>
Kama ningekuwa Marekani ningefungua kesi ya haki miliki ya utaaluma dhidi ya Al Yaum. Kama lingekuwa ni Gazeti la New York Times limetumia kazi yangu bila ruhusa, ningekuwa tajiri sasa hivi. Hivi haki miliki za utaaluma kwa mawazo na picha zilizochapishwa zina thamani yoyote hapa?</p></blockquote>
<p>Al Omran anazingatia: </p>
<blockquote><p>Nathan anafikiria kuwashitaki, jambo ambalo nadhani litakuwa zuri sana, lakini labda wameshajitia aibu vilivyo wao wenyewe.  </p></blockquote>
<p>Watoa maoni kwenye blogu ya Nathan wanaguswa na yaliyompata mwanablogu: </p>
<p><em>Mazoo</em> anaandika: </p>
<blockquote><p>Ninasikitika kuona hili linatokea kwako&#8230;<br />
Lakini, hili ni jambo lililozoeleka hapa Saudi Arabia&#8230;</p>
<p>Nimesikia kesi nyingi ambazo kazi za marafiki zangu (maandiko ya blogu, picha na mawazo) yameibwa na waandishi habari wavivu. Walilalamikia hali hii na wengine waliaandikia wahariri wakuu –wengine wao huandika taarifa za kuomba msamaha na wengine wao humfukuza kazi mtu aliyeiba maudhui</p></blockquote>
<p><em>Al Hanouf</em>, anayejielezea mwenyewe kuwa ni mwanafunzi wa sheria, anataka haki itendeke: </p>
<blockquote><p>Kama kitendo hiki kikiangaliwa chini ya makosa ya jinai yanayohusiana na kompyuta, basi huyu – mwana habari – inatakiwa awe jela kwa zaidi ya miezi sita na kukulipa si chini ya fedha ya Riyali za Saudia 250,000.<br />
Unapaswa uende kwa mwanasheria, na tafadhali usilimalize hili kwa kuliandikia gazeti barua pepe! Kuna sheria, na (gazeti) halitaweza kurekebisha makosa yake kama tutalimaliza suala hili kwa njia zatu za kizembe!</p></blockquote>
<p>Na Chiara anashauri: </p>
<blockquote><p>Nami ninashiriki katika kuchefuka na uvunjifu huu wa sheria ya haki miliki, na njia iliyozoeleka ya kutafsiri na ‘kuiba’ kazi za wengine si nafuu. Unaweza kuweka blogu yako nzima chini ya haki miliki kama ambavyo wanablogu wengine wamefanya, na kufanya namna ambayo jina lako litaonekana kwenye picha. </p></blockquote>
<p>Kwenye makala fuatilizi, Nathan anaandika:  </p>
<blockquote><p>Nchini Saudi Arabia, umbea huenea kama vile ugonjwa wa mlipuko. Blogu hii imepokea makumi elfu ya watembeleaji wapya katika juma moja tu </p>
<p>[…] </p>
<p>Nilikuja Saudia kujenga madaraja (ushirikiano), sio kutengeneza maadui. Nilikuja kusoma na kutafiti katika Chuo kikuu ambacho kinajitahidi kwa nguvu zote kuwa moja wapo ya vyuo vikuu bora vya utafiti duniani, na sio kupata fedha kutoka kwa watu ama mashirika. </p>
<p>Ninataka uwajibikaji. Ilichokifanya <em>Al Yaum</em> kilikuwa ni makosa, lakini mwenendo wa mjadala pia una makosa. </p></blockquote>
<p>Na maneno yake ya mwisho kwa wasomaji wake ni: </p>
<blockquote><p>Kama unataka kuazima kitu kutoka kwenye blogu yangu, tafadhali omba kwanza. Hakuna mtu, nikijijumuisha na mimi, anayependa kutokuelewana. </p></blockquote>
<p>Kwa kutumia kifaa cha kutafsiri, <a href="http://saudiaggie.blogspot.com/2009/10/i-should-be-getting-paid-for-this.html?showComment=1255467311093#c5285446355482995533">mwandishi husika</a> anamwandikia Nathan akilielezea vyema suala lake.</p>
]]></content:encoded>
			<wfw:commentRss>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/11/saudia-arabia-ambako-kuiga-kazi-kinyume-cha-haki-miliki-ni-kosa-la-jinai/feed/</wfw:commentRss>
		<slash:comments>0</slash:comments>
		</item>
		<item>
		<title></title>
		<link>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/10/380/</link>
		<comments>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/10/380/#comments</comments>
		<pubDate>Sat, 17 Oct 2009 06:35:44 +0000</pubDate>
		<dc:creator>j nambiza tungaraza</dc:creator>
				<category><![CDATA[Botswana]]></category>
		<category><![CDATA[Elections]]></category>
		<category><![CDATA[English]]></category>
		<category><![CDATA[Media]]></category>
		<category><![CDATA[Politics]]></category>
		<category><![CDATA[Roundups]]></category>
		<category><![CDATA[Sub-Saharan Africa]]></category>
		<category><![CDATA[Technology]]></category>

		<guid isPermaLink="false">http://sw.globalvoicesonline.org/?p=380</guid>
		<description><![CDATA[Ilichapwa kwanza naNdesanjo Macha  &#183; Imetafsiriwa na j nambiza tungaraza &#183;  Angalia ujumbe mama 
Mradi Wa Uchaguzi Afrika (AEP) www.africanelections.org utakuwa unafuatilia uchaguzi mkuu wa wa 10 wa Botswana, unaofanyika Oktoba 16, 2009.
]]></description>
			<content:encoded><![CDATA[<em>Ilichapwa kwanza na<a href="http://globalvoicesonline.org/author/ndesanjo-macha/">Ndesanjo Macha</a>  &middot; Imetafsiriwa na <a href='http://sw.globalvoicesonline.org/author/j-nambiza-tungaraza/'>j nambiza tungaraza</a> &middot;  <a href='http://globalvoicesonline.org/2009/10/15/botswana-african-elections-project-to-cover-elections/'>Angalia ujumbe mama</a></em> 
<br /><p>Mradi Wa Uchaguzi Afrika (AEP) www.africanelections.org <a href="http://www.africanelections.org/botswana/blogs/?post=475">utakuwa unafuatilia uchaguzi mkuu wa wa 10 wa Botswana</a>, unaofanyika Oktoba 16, 2009.</p>
]]></content:encoded>
			<wfw:commentRss>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/10/380/feed/</wfw:commentRss>
		<slash:comments>0</slash:comments>
		</item>
		<item>
		<title>Marekani: Stempu ya Iddi Yachochea Chuki Huko Tennessee</title>
		<link>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/09/marekani-stempu-ya-iddi-yachochea-chuki-huko-tennessee/</link>
		<comments>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/09/marekani-stempu-ya-iddi-yachochea-chuki-huko-tennessee/#comments</comments>
		<pubDate>Sat, 26 Sep 2009 10:32:16 +0000</pubDate>
		<dc:creator>j nambiza tungaraza</dc:creator>
				<category><![CDATA[Americas]]></category>
		<category><![CDATA[English]]></category>
		<category><![CDATA[Feature]]></category>
		<category><![CDATA[Freedom of Speech]]></category>
		<category><![CDATA[Governance]]></category>
		<category><![CDATA[Media]]></category>
		<category><![CDATA[Politics]]></category>
		<category><![CDATA[Religion]]></category>
		<category><![CDATA[U.S.A.]]></category>
		<category><![CDATA[Weblog]]></category>

		<guid isPermaLink="false">http://sw.globalvoicesonline.org/?p=323</guid>
		<description><![CDATA[Barua pepe yenye madai ya uongo kuwa Rais Obama ametoa stempu mpya kuadhimisha sikukuu ya Waislamu Eid al-Fitr imemfikia Meya wa Tennessee ambaye aliisambaza kwa wafanyakazi wake na waasa waisusie stempu hiyo.]]></description>
			<content:encoded><![CDATA[<em>Ilichapwa kwanza na<a href="http://globalvoicesonline.org/author/jillian-york/">Jillian C. York</a>  &middot; Imetafsiriwa na <a href='http://sw.globalvoicesonline.org/author/j-nambiza-tungaraza/'>j nambiza tungaraza</a> &middot;  <a href='http://globalvoicesonline.org/2009/09/21/usa-eid-postage-stamp-provokes-hate-in-tennessee/'>Angalia ujumbe mama</a></em> 
<br /><p><div class="wp-caption alignleft" style="width: 210px"><img alt="Toleo la stempu la mwaka 2008, kabla bei haijapanda" src="http://globalvoicesonline.org/wp-content/uploads/2009/09/eid.jpg" title="eid" width="200" height="200" /><p class="wp-caption-text">Toleo la stempu la mwaka 2008, kabla bei haijapanda</p></div><br />
Wakati Waislamu nchini Marekani wanasherehekea <a href="http://en.wikipedia.org/wiki/Eid_ul-Fitr">Eid al-Fitr</a>, sherehe inayoadhimisha mwisho wa mwezi wa Ramadhani, barua pepe yenye nia mbaya imekuwa ikizunguka. Barua pepe hiyo ina maddai ya uongo kuwa Rais Obama ametoa stempu mpya kuadhimisha sherehe mbili za Eid na kuwataka wasomaji wa barua pepe hiyo kuigomea hiyo stempu, huku ikiorodhesha mashambulizi ya kigaidi yalifonywa nchini Marekani katika kipindi cha miaka ishirini iliyopita. Maandishi ya hiyo barua pepe yanaonekana kwenye <a href="http://missivesfrommarx.wordpress.com/2009/09/20/this-stuff-makes-me-sick/#comment-1096">makala hii</a> ya <em>Missives from Marx</em>, ambaye anaelezea kughafirika kwake kulikotokana na barua hiyo:</p>
<blockquote><p>Nilipokea barua pepe ifuatayo leo kutoka kutoka kwa ndugu yangu. Kutokana na mambo kama haya  ndiyo maana nitazitumia wiki nne za mafunzo yangu ya dini (Western Religious Course) kuzisambaratisha imani potofu juu ya Uislamu. Ndio maana uchambuzi yakinifu ni lazima uwe sehemu muhimu ya masomo yangu.</p></blockquote>
<p>Na kama ilivyoondokea, hakuna jipya kuhusu hii barua, au stempu. <a href="http://urbanlegends.about.com/library/bl-muslim-stamp.htm">About.com</a> inafafanua kuwa barua hii imekuwepo tangu mwaka 2002, wakati stempu yenyewe ilitolewa tarehe 1, Septemba 2001.</p>
<p>Aziz Poonwalla, katika blogu ya <em>City of Brass</em> kwenye BeliefNet  <a href="http://blog.beliefnet.com/cityofbrass/2009/09/terror-mail-the-eid-stamp.html">anafafanua</a> habari ya hii barua pepe:</p>
<blockquote><p>Matoleo ya hiyo barua pepe, ambayo yamekuwa yakizungushwa kwa miaka kadhaa, <a href="http://www.snopes.com/politics/stamps/eidstamp.asp">yameshachambuliwa</a> lakini bado yanaendelea kusambazwa. Nimeblogu kwa kirefu kuhusu <a href="http://cityofbrass.blogspot.com/2007/10/eid-stamp.html">historia ya stempu hiyo</a> ya Eid, utata uliombatana nayo wakati ilipotolewa (hasa kutoka kwa wahafidhina wa chama cha Republicans), na utetezi wa stempu hiyo uliofanywa na Rais Bush pamoja na Spika Hastert. Kwa kifupi, stempu hiyo ilitolewa tarehe 1 Septemba 2001, siku kumi kabla ya mashambulizi ya 9-11, wakati wa serikali ya Bush. Meya Piper anajiunga na orodha ndefu ya wanasiasa wahafidhina ambao hawana pingamizi na stempu zinazoadhimisha sikukuu za Hanukkah, Kwanzaa, na hata mwaka mpya wa Kichina – bali stempu iliyotolewa kwa ajili ya sikukuu ya Kiislamu ya Eid imetengwa kama tishio, na kuwataka Wamarekani wazalendo waiwajibikie?</p></blockquote>
<p><a href="http://www.clarksvilleonline.com/2009/09/04/the-mayors-anti-islamic-email-is-a-major-embarrassment/">Makala</a> kwenye <em>Clarksville Online</em>, blogu ya mji wa Clarkstown, Tennessee, inaelezea ni kwa nini hii barua pepe imesababisha vichwa vikubwa vya habari mwaka huu:</p>
<blockquote><p>
Meya wa Clarksville Tennessee, Johnny Piper ametuma barua pepe ya kichochezi inayopinga Uislamun kwa wafanyakazi wa mji huo, inayowaasa waisusie hiyo stempu iliyotolewa na husduma ya posta ya Marekani…</p>
<p>… Meya Piper anajaribu kutetea vitendo yake, lakini vitendo hivyo ni vigumu kutetewa. Waislamu ni sehemu mojawapo ya nchi hii. Wanatumikia kiadilifu kwenye majeshi yetu ya ulinzi, wanalilinda taifa, na uhuru wetu. Hakuna mtu nayepaswa kuchukuliwa kama raia wa tabaka la pili kwa misingi ya imani yake ya kidini, au kutokana na vitendo vya watu wenye siasa kali wachache. Tukio hili lililotengenezwa na Meya wetu limekuwa ni aibu kwa mji wetu, jimbo, na nchi yetu.</p></blockquote>
<p>Sheila Musaji amekuwa akifuatilia mzunguko wa barua pepe hiyo inayohusu stempu kwa ajili ya jarida la <em>The American Muslim (TAM)</em> tangu mwaka 2005, na katika moja ya habari zake, <a href="http://theamericanmuslim.org/tam.php/features/articles/through_the_looking_glass_eid_stamp_continues_to_provoke_religious_right/">anatoa maoni</a> juu ya vitendo vichafu vya Meya Piper:</p>
<blockquote><p>Nina hakika kuwa Meya wetu mzuri alishangazwa na <a href="http://www.theamericanmuslim.org/tam.php?URL=http%3A%2F%2Fwww.theamericanmuslim.org%2Ftam.php%2Ffeatures%2Farticles%2Fwhite_house_iftar%2F0017527">ghafla ya iftar iliyofanywa na Obama kwenye Ikulu ya Marekani</a>.</p>
<p>Na, kama ilivyo kawaida maneno ya mwisho ya wabaguzi wote huwa: <em>‘nina marafiki kasha wa Kiislamu,” aliongeza.”</em></p>
<p>Pengine marafiki hao wazuri wa Kiislamu wanaweza kumuelimisha ni kwa nini makala <a href="http://www.theamericanmuslim.org/tam.php?URL=http%3A%2F%2Fwww.theleafchronicle.com%2Fassets%2Fpdf%2FDA14202394.PDF">HII</a> (PDF) inagadhabisha.</p></blockquote>
]]></content:encoded>
			<wfw:commentRss>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/09/marekani-stempu-ya-iddi-yachochea-chuki-huko-tennessee/feed/</wfw:commentRss>
		<slash:comments>0</slash:comments>
		</item>
	</channel>
</rss>
