Habari kuhusu Vyombo na Uandishi wa Habari kutoka Septemba, 2010
Colombia: maoni ya Awali Kuhusu Kifo cha Kiongozi wa FARC ‘Mono Jojoy’
Víctor Julio Suárez, ambaye anajulikana zaidi kama Jorge Briceño or Mono Jojoy, mmoja wa viongozi wa juu wa Majeshi ya Ukombozi wa Colombia (FARC), aliuwawa katika kile kilichoitwa "Operesheni Sodoma." Watumiaji wa Twita wa Colombia walianza mara moja kuandika maoni yao kuhusu habari hiyo.
Karibeani: Kwa Heri, Arrow
Wanablogu wa Karibeani wanaomboleza kifo cha mmoja wa waasisi wa muziki wa soca katika kanda hiyo - Alphonsus Cassell, ambaye anayejulikana zaidi kama “arrow” – na ambaye kibao chake kikali, Hot, Hot, Hot kinapewa sifa ya kuutambulisha mtindo wa soca kwa kadamnasi duniani kote. Taarifa za habari zinathibitisha kuwa muimbaji huyo allikuwa akisumbuliwa na ugonjwa wa saratani kwa muda; rambirambi za wanablogu zimekuwa na mguso pia zinaelezea masikitiko binafsi...