GlobalVoices katika

Labor

Hifadhi ya mada · 12 jumbe


Habari mpya Kuhusu Labor

16 Oktoba 2012

Ghana: Vikwazo Vinavyowakabili Wanawake Kimaendeleo

Betty Mould Iddrisu, Jaji na Waziri wa Sheria wa Ghana, anaandika [fr] kwenye blogu ya pambazuka.org:

Kufikia ngazi za juu kabisa za utawala si rahisi, na hata unapopanda mpaka juu kabisa, bado unajikuta unakabiliwa na hisia za watu zenye uadui na watu wanakuwa na mashaka na uwezo wako, kwa sababu tu wewe ni mwanamke. Mwanamke akikamata madaraka ya juu humbidi kufanya kazi kwa bidii zidi kuliko mwanaume ili kuthibitisha uwezo wake, lakini bado hata akifanya hivyo anakumbana na uadui pamoja na mfumo unaomwona kuwa duni, iwe katika majukumu yake kama meneja na kiongozi, na hata katika mazingira yoyote ya kazi ambayo yanatawaliwa kwa kiasi kikubwa na wanaume.

10 Oktoba 2012

Côte d'Ivoire: Wafanyakazi wa Afya Wagoma baada Miezi Minne Bila Mshahara

S.B anatoa maoni juu ya kuanza kwa mgomo usio na ukomo unaoratibiwa na wafanyakazi wa taasisi za afya mjini Abidjan. Katika mtandao wa Connection Ivorienne, anabainisha [fr] kwamba:

Kufuatia mabadiliko ya utolewaji wa huduma za afya ambazo zilitolewa bure kabisa baada tu ya kumalizika kwa mgogoro wa baada ya uchaguzi, sera iliyoanzishwa na serikali ya Côte d'Ivoire, ambayo sasa imeelekeza baadhi ya huduma tu ndizo zitakuwa bure, wafanyakazi wa taasisi kadhaa za afya hawajapata mishahara yao kwa wakati. Kibaya zaidi ni kwamba wakubwa wao hawakupata fungu lolote kwa ajili hiyo kwa zaidi ya miezi kumi na sita.

8 Oktoba 2012

Tunisia: Mgomo Waanza jijini Thala

Kupitia mtandao wa twita, Tounsia Hourra (m-Tunisia huru) anasema [ar] kuna mgomo mkubwa umeanza jijini Thala, kwenye jimbo la Kasserine, leo [Oktoba 8, 2012]. Mgomo huo umekuja kama hatua ya kupinga kukua kwa kasi kwa ukosefu wa ajira na kuzorota kwa maendeleo ya jiji hilo.


@tounisiahourra
: اضراب عام في تالة ( ولاية القصرين ) اليوم احتجاجا على ارتفاع معدلات البطالة واهمال صيانة المدينة

@tounisiahourra: Mgomo mkubwa jijini Thala (jimbo la Kasserine) leo kupinga kuongezeka kwa ukosefu wa ajira na kuzorota kwa maendeleo ya jiji hilo.

23 Agosti 2012

Photos jumbe
Mauritania: Wafanyakazi wa Migodini Wapinga ‘Aina Mpya ya Utumwa’

Soma makala hii.

Zaidi ya wafanyakazi 2,300 wako kwenye mgomo nchini Mauritania katika mji wa kaskazini wa Zouerat, jambo ambalo limesababisha kuzorota kwa maeneo mengine kumi ya Kampuni la Taifa la Madini na Viwanda, huku kazi zikiwa kwenye mvurugiko mkubwa. Madai yamejikita katika suala zima la maslahi bora ya wafanyakazi.

12 Juni 2012

Kenya: Intani walipwe au wasilipwe?

Soma makala hii.

Mada hapa ni kuhusu kama inafaaa au haifai kwa intani kulipwa,mjadala ulioanzishwa na @RobertAlai.

4 Januari 2012

Suluhisho la Kiradikali la Umaskini Duniani: Ufunguzi wa Mipaka

Soma makala hii.

Wataalamu kadhaa wanasema kuwa umaskini uliokithiri hauepukiki. Suluhisho la kiradikali zaidi la kupunguza umaskini kwa haraka duniani kwa wataalamu wengi wa uchumi ni kufungua mipaka kati ya nchi na kuruhusu wafanyakazi kuhamia sehemu ambazo nguvukazi inahitajika zaidi.

3 Aprili 2011

Saudi Arabia: Mfalme Awaahidi Wananchi wa Saudia Fedha Zaidi

Fedha zaidi zimeahidiwa kutolewa kwa wananchi wa Saudia, ahadi ambayo Mfalme Abdulla ameitoa kupitia hotuba yake kwa taifa leo. Katika hotuba hiyo iliyokuwa fupi, Mlinzi wa Misikiti Miwili Mitukufu aliwashukuru viongozi wa dini, waandishi na Wizara ya Mambo ya Ndani kwa juhudi walizofanya kutetea ufalme. Matamko na Amri vilifuata ya kwamba mabilioni yatagawanywa kwa watu wa Saudia.

31 Machi 2010

Serikali ya Japani: Kuhusu Kuanguka kwa Mfumo wa Ajira

Chombo kinachotumika kufanya tafakari nzito cha Baraza la Mawaziri la Japani, Taasisi ya Utafiti wa Kiuchumi na Kijamii (内閣府 経済社会総合研究所)(ESRI) kimechapisha matokeo ya utafiti yaliyopima hadhi ya sasa ya ajira...

21 Machi 2010

Lebanoni: Wafanyakazi wa Ndani Wanaotoroka

“Mfanyakazi wa ndani anapotoroka kutoka kwenye nyumba ya mwajiri wake, kituo cha polisi hakiwezi kufanya lolote kwa sababu hakuna sheria dhidi ya wafanyakazi wa ndani wanaotoroka. Kwa hiyo ofisa wa kituo cha polisi anamwambia mwajiri wa ki-Lebanoni aseme kuwa (mtoro huyo) aliiba pesa,” anaandika Ethiopian Suicides.

6 Januari 2010

Lebanoni: Matukio ya Wafanyakazi Kujiua ‘Yanadharauliwa’

Matthew Cassel anaripoti tukio la kujia la Theresa Seda, mfanyakazi wa ndani wa Kifilipino jijini Beirut. Soma habari za kina za kutisha za jinsi vifo vya namna hiyo vinavyoongezeka kwa idadi – vinaendelea kutotiliwa maanani kwenye Justimage.

Sehemu za Dunia

Nchi

Lugha