<?xml version="1.0" encoding="UTF-8"?>
<rss version="2.0"
	xmlns:content="http://purl.org/rss/1.0/modules/content/"
	xmlns:wfw="http://wellformedweb.org/CommentAPI/"
	xmlns:dc="http://purl.org/dc/elements/1.1/"
	xmlns:atom="http://www.w3.org/2005/Atom"
	xmlns:sy="http://purl.org/rss/1.0/modules/syndication/"
	xmlns:slash="http://purl.org/rss/1.0/modules/slash/"
	>

<channel>
	<title>Global Voices in Swahili &#187; Internet &amp; Telecoms</title>
	<atom:link href="http://sw.globalvoicesonline.org/category/topics/internet-telecoms/feed/" rel="self" type="application/rss+xml" />
	<link>http://sw.globalvoicesonline.org</link>
	<description>Dunia inaongea, je unasikiliza?</description>
	<lastBuildDate>Wed, 02 Dec 2009 12:35:07 +0000</lastBuildDate>
	<generator>http://wordpress.org/?v=2.8.4</generator>
	<language>en</language>
	<sy:updatePeriod>hourly</sy:updatePeriod>
	<sy:updateFrequency>1</sy:updateFrequency>
			<item>
		<title>Urusi: Jinsi Abiria wa &#8220;Nevsky Express&#8221; Walivyoeleza Habari Kupitia Vyombo Vya Habari Vya Kijamii</title>
		<link>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/12/urusi-jinsi-abiria-wa-nevsky-express-walivyoeleza-habari-kupitia-vyombo-vya-habari-vya-kijamii/</link>
		<comments>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/12/urusi-jinsi-abiria-wa-nevsky-express-walivyoeleza-habari-kupitia-vyombo-vya-habari-vya-kijamii/#comments</comments>
		<pubDate>Tue, 01 Dec 2009 11:11:27 +0000</pubDate>
		<dc:creator>j nambiza tungaraza</dc:creator>
				<category><![CDATA[Breaking News]]></category>
		<category><![CDATA[Eastern & Central Europe]]></category>
		<category><![CDATA[English]]></category>
		<category><![CDATA[Feature]]></category>
		<category><![CDATA[Internet & Telecoms]]></category>
		<category><![CDATA[Media]]></category>
		<category><![CDATA[Politics]]></category>
		<category><![CDATA[Russia]]></category>
		<category><![CDATA[Russian]]></category>
		<category><![CDATA[Technology]]></category>
		<category><![CDATA[Weblog]]></category>

		<guid isPermaLink="false">http://sw.globalvoicesonline.org/?p=738</guid>
		<description><![CDATA[Ajali ya treni la "Nevsky Express" ilitokea mbali na makazi ya watu. Ilichukua masaa kadhaa kwa wanahabari kufika kwenye eneo. Na hapo ndio picha na video za kwanza zilipoanza kuonekana kila mahali. je nini kilichotokea kwenye upashanaji habari wa kiraia ambao uliongoza njia ya kupashana habari wakati wa ajali ya ndege huko Urusi mwaka mmoja uliopita?]]></description>
			<content:encoded><![CDATA[<em>Ilichapwa kwanza na<a href="http://globalvoicesonline.org/author/gregory-asmolov/">Gregory Asmolov</a>  &middot; Imetafsiriwa na <a href='http://sw.globalvoicesonline.org/author/j-nambiza-tungaraza/'>j nambiza tungaraza</a> &middot;  <a href='http://globalvoicesonline.org/2009/11/29/russia-how-passengers-of-nevsky-express-tell-their-stories-through-social-media/'>Angalia ujumbe mama</a></em> 
<br /><p>Mamlaka nchini Urusi yanaendelea <a href="http://globalvoicesonline.org/2009/11/28/russia-at-least-25-people-killed-in-the-neva-express-train-crash/">kuchunguza ajali ya treni la &#8220;Nevsky Express&#8221; </a>[ENG] ambayo ilitokea kati ya Moscow na St Petersburg usiku wa Ijumaa. Kwa mujibu wa maofisa, dhahama hiyo iliyochukua maisha ya angalau abiria 25 ilikuwa ni shambulio la kigaidi. Ajali hiyo imezua maswali mengi. Watu wengi wanauliza ni nini kilichotokea katika masaa ya mwanzo baada ya ajali na ni kwa nini ilichukua muda mrefu kuanza kutoa taarifa za ajali hiyo.</p>
<p>Kwa kuwa dhahama hiyo ilitokea mbali na maeneo yenye makazi ya watu, ilichukua muda mrefu kwa wanahabari kuwasili kwenye eneo la ajali. Na ndipo picha za kwanza na video zilipoanza kuonekana kila mahali. Je nini kilichoyatokea majukwaa ya uanahabari wa kijamii ambayo yalitaarifu vilivyo kuhusu <a href="http://news.bbc.co.uk/2/hi/europe/7614951.stm">ajali ya ndege mjini Perm</a> [ENG] mwezi Septemba 2008.</p>
<p>Abira pekee ambaye alitoa taarifa mara moja kuhusu ajali ya “Nevsky Express” alikuwa mtumiaji wa Twita <a href="http://twitter.com/lazy_frog">Lazy Frog</a>. Aliandika mara 12 kuhusu ajali hiyo kabla ya kuwasili nyumbani. Haya ndio aliyoandika: </p>
<blockquote><p>Nipo hai. Lakini nitaeleza kuhusu (ajali) baadaye. Kama mtu ataeleza chochote kwenye habari, tafadhali niandikie. Hawatuambii kila kitu hapa.</p></blockquote>
<p>Baadaye, abiria wengi kutoka mabehewa ya kwanza – ni mabehewa ya mwisho ambayo yaliteguliwa kutoka kwenye reli –walisema kuwa kwa saa zima baada ya ajali hawakufahamu chochote. <a href="http://twitter.com/lazy_frog">Lazy frog</a> alituma habari mpya za nyongeza: </p>
<blockquote><p>Tumepanda treni jingine. Nilifanya kila nilichoweza.</p>
<p>Hivi sasa tupo SAPSAN (treni mpya ambyo iliwachukua abiria kwenda St. Petersburg – G.A). Natamani ingekuwa inakwenda polepole.</p>
<p>Wametangaza sasa hivi kuwa watu walitayarishwa rasmi wangetulaki kwenye kituo cha treni.</p></blockquote>
<p>Siku iliyofuata baada ya dhahama, <a href="http://twitter.com/lazy_frog">Lazy Frog </a>aliandika muhtasari wa uzoefu wake:</p>
<blockquote><p>Nilizihisi hisia za kwanza kuhusu kilichotokea wakati tulipofika karibu na Piter (St. Petersburg G.A). Sikuwa na wasiwasi nilipokuwa katika eneo la ajali. Nilikuwa na hofu kidogo na viatu vyangu – kulikuwa na tope kila mahali na mawe yenye ncha.</p></blockquote>
<p>Jumamosi habari nyingi zilijitokeza wakati abiria walipoanza kublogu kuhusu yaliyowakuta. Makala ya blogu maarufu zaidi inayohusiana na mada hii iliandikwa na mtumiaji wa LJ <em>paltus_mk</em> [RUS] ambaye alikuwemo ndani ya mabehewa ya mwisho yaliharibiwa vibaya na mlipuko. <a href="http://paltus-nk.livejournal.com/23747.html">Aliandika </a>[RUS]:</p>
<blockquote><p>Yote yanatokea ndani ya sekunde 10 wakati unapofahamu ni nini kitakachotokea. Nilikuwa na muda wa kutosha kuutayarisha mwili wangu. Lakini hakuna linaloweza kusaidia dhidi ya kanuni za Newton wakati dazeni za tani za vyuma zinaposimama mara moja wakati zikiwa katika mwendo wa kasi – ni bahati tu… kwa hiyo nilikuwa na bahati tu. Kaka yangu alikuwa na bahati, pia, ukiachilia mbali ukweli kuwa majeraha yake yalikuwa yanatisha kuliko yangu.<br />
[…]</p></blockquote>
<blockquote><p>Kila kitu ambacho kilikwenda mrama hadi kusimama kabisa kulichukua kama sekunde 30 hivi. Ilikuwa giza na kimya. Watu walioumia walianza kulia. Nilikuwa sakafuni, nimekandamizwa na miili mingine. Niliisogeza ile miili. Niliona kuwa nimelowana na damu lakini damu ile haikuwa yangu. Niliona kuwa ni mzima na miguu yangu na mikono vuinafanya kazi. Kichwani nilikuwa na jeraha linalovuja damu. Ilinibidi ninyanyuke na kusubiri kwa muda kiasi kabla ya watu wenye majeraha mado waliposafisha njia ya kutoka.<br />
[…]<br />
Mateso yalikuwepo kila mahali. Tulikuwa tumeketi mwishoni mwa behewa na mikoba yote ilipaa ikituelekea. Watu wengi waliojeruhiwa. Katika dakika chahce baada ya ajali, behewa lilikuwa ni kama fungu la miili, viti na sehemu za treni ambazo zilikuwa zimesambaa sawia kila mahali.</p></blockquote>
<p><em>Paltus_mk </em>anasimulia habari za uokoaji zenye maelezo ya kina kuanzia dakika za mwanzo baada ya ajali, lakini wakati huo huo anaepuka ufafanuzi ambao ungeweza kuwastua wasomaji. Anaandika kuwa abiria walianza kupeana huduma ya kwanza kwa ushujaa bila kuogopa. Anasema haikuwezekana kuhesabu ni wagtu wangapi waliofariki. Waokoaji waliwasili saa moja na nusu baada ya ajali. <em>Paltus_mk</em> na kaka yake hatimaye waliokolewa na kupelekwa kwenye hospitali jirani na baadaye aliwasili mjini St. Petersburg. </p>
<p>Hadithi nyingine ya kunusurika ilichapishwa na mwanablogu pancakyes katika huduma nyingine ya kublogu ya Kirusi Ya.Ru. behewa lake halikuharibiwa na mlipuko. Alichapisha makala yake ya kwanza saa 4:11 za usiku – nusu saa baada ya ajali – pale pale kwenye eneo la ajali.  Aliandika kuwa treni ilisimama kutokana na ajali ya namna fulani, mabehewa machache yaliteguliwa na kwamba angewasili nyumbani kwa uchelevu kuliko ilivyotarajiwa. Karibu saa zima baadaye, aliongeza kuwa kulikuwa na waathirika katika mabehewa mawili ya mwisho. Jumamosi,  <em>pancakyes</em> <a href="http://pancakyes.ya.ru/replies.xml?item_no=30442">alichapisha habari nzima kuhusu ajali</a> [RUS] kama alivyoshudia mwenyewe:</p>
<blockquote><p>Tulihisi mitetemo michache ambayo ilikuwa ikiongezeka nguvu. Vitu vilianza kuanguka kutoka mezani. Haikuwa wazi ni nini kilichotokea. Hapakuwa na matangazo. Kwanza tulidhani kuwa halikuwa jambo lenye uzito. Pengine kuna mtu aliyesimamisha treni kwa makosa. Lakini makondakta wenye sura zenye hofu walianza kukimbia kila mahali wakikusanya magodoro, vitambaa vya mezani na maji. Walitutaka tusiondoke kwenye viti vyetu isipokuwa kama ni madaktari. Tulisikia mambo mabaya kutoka kwenye redio zao. Uvumi ulianza kusambaa. Hatukuamini kuwa mabehewa mawili yalikuwa yametengana na yalikuwa mbali sana. Baadaye tuligundua kuwa ilikuwa kweli.</p>
<p>Tulitoka nje na tulitaka kusaidia. Tulikwenda mpaka behewa la tatu. […] hatukutaka kuwa waduwazi ambao wanaongeza wingi wa watu bila fursa yoyote ya kusaidia. Pia hatukutaka kuona yale ambayo watu waliotoka huko walikwishatueleza.</p></blockquote>
<p>Mara baada ya ajali, majukwaa ya uanahabari wa kijamii yalikuwa sehemu ya kwanza ambayo wanahabari wa Kirusi  walikuwa wakitafuta habari. Mwandishi kutoka Shirika la Habari la RIA-Novosty aliacha maoni kwenye blogu ya <em>pancakyes</em> na kumtaka mwanablogu huyo ampigie simu mara moja. Tatyana Landa (mtumiaji wa LJ mwenye jina la Elada) <a href="http://elada.livejournal.com/220534.html">aliandika kwenye blogu yake</a> [RUS] kuhusu rafiki aliyenusurika ambaye alikuwemo kwenye treni. Mara moja wanahabari wawili waliacha maoni ya kumtaka awasiliane nao. Baadaye Tatyana <a href="http://elada.livejournal.com/220866.html">alichapisha makala ya hasira</a> [RUS] ambamo alisema kuwa mwanahabari kutoka “Komsomolskaya pravda” (gazeti la udaku la Kirusi) alikuwa akijaribu kumpata kwa simu mara kadhaa usiku huo. Makala hiyo iligeukia mahali ambapo watu walianza kujadili kama wanahabari wanaweza kuwatumia wanablogu kama chanzo cha taarifa zinazohusu hii ajali ya treni. Wanahabari pia walijaribu kuwasiliana na mwanablogu ambaye <a href="http://naechst-naechst.livejournal.com/105582.html#comments">aliandika</a> [RUS] kuwa aliamua kutopanda treni la “Nevsky Express” katika dakika ya mwisho.</p>
<p>Baadhi ya wanablogu <a href="http://tema.livejournal.com/509436.html">walieza kughafirika kwao </a>[RUS] na ukweli kuwa ni watu wachache mno kutoka kwenye treni walitumia vyombo vya habari vya kijamii kutoa taarifa za kile kilichokuwa kinatokea., Na, inavyoonekana, kuna fafanuzi kadhaa zinazoelea ni kwa nini  uanahabari wa kijamii haukuchukua nafasi kubwa katika upashaji wa habari za ajali ya “Nevsky express”.</p>
<p>Twita, jukwaa zuri la kublogu moja kwa moja, si maarufu nchini Urusi. Kwa mujibu wa <a href="http://twitter.com/twitRU">twitRU </a>[RUS], kuna watumiaji wa Twita 2,700 tu ambao wanaandika kwa lugha ya Kirusi. Wakati huo huo, majukwaa maarufu ya kublogu nchini Urusi kama vile Livejournal.com au ya.ru yangeweza kutumika ili kublogu moja kwa moja lakini, kama ilivyojadiliwa hapo juu, kuna mifano michache tu ya matumizi hayo.</p>
<p>Ufafanuzi wa pili unahusiana na nafasi ya zana za mkononi na uunganishaji. Zana za mkononi zinaongezeka nchini. Warusi zaidi na zaidi wanaweza kutumia mtandao wa intaneti na zana nyingine za mtandaoni. Tabia hii ina nguvu katika maeneo ya Moscow na St. Petersburg. Lakini ajali ilitokea mbali na maeneo ya mjini ambako, kama mashihidi walivyotaarifu, uwezo wa kupatikana kwa mawasiliano ya simu za mkononi ulikuwa mdogo. Mwanablogu  <em>pancakyes </em><a href="http://pancakyes.ya.ru/replies.xml?item_no=30442&#038;ncrnd=2805">anasimulia</a> tatizo la mawasiliano:</p>
<blockquote><p>
Mawasilian ya simu yalikuwa mabaya sana. Inawezekana kuwa kila mtu alijaribu kupiga simu kwa wakati mmoja na mtandao ulielemewa. Nilianza kupata jumba za maandishi pale tu nilipokuwa kwenye treni la pili (treni ambalo liliwachukua abiria kwenda Saint- Petersburg G.A.). Ningeliweza kutumia mtandao wa intaneti, lakini ilikuwa ni vigumu mno.</p></blockquote>
<p>Hii ni tofauti, ajali ya ndege kule Perm mwaka jana ambayo ilitoa fursa nyingi kwa uanahabari wa kiraia:</p>
<p>1. Ndege ilianguka ndani ya mipaka ya mji ambako watu wengi waliweza kuona ni nini kilichokuwa kinatokea kutokea madirishani. Ajali ya “Nevsky express”, kama ilivyoelezwa awali, ilitokea sehemu za vijijini.</p>
<p>2.Habari zilizoandikwa kwa uanahabari wa kijamii kule Perm zilitokana na maelezo ya walioishuhudia ajali ambao hawakuwamo katika ajali (kwa bahati mbaya, hapakuwa na walionusurika kutoka katika ile ndege). Mashahidi wote wa tukio la “Nevsky Express”  walikuwa ni abiria katika treni. </p>
<p>3. Watu wengi walituma habari mpya juu ya ajali ya ndege kule Perm kwa kutumia tarakilishi za nyumbani. Walionusurika kwenye “Nevsky Express” walitegemea zana za mikononi.</p>
<p>Tofauti hizi zinabainisha kwa nini vyombo vya habari vya kiraia vilikuwa mbele katika ajali ya  ndege na vilikaribia kutokuwepo kwenye tukio la “Nevsky Express.” </p>
<p>Pia inawezekana kudai kuwa urusi bado haijaendeleza utamaduni wa utoaji taarifa kupitia uanahabari wa kiraia. Na ndiyo sababu abiria wawili tu walikuwa na msukumo wakutosha kwenda kwenye mtandao na kujipa kazi ya uanahabari wa kijamii. Na pia inaweza kufafanua upinzani wa abiria na wanablogu kwa wanahabari ambao walikuwa wanatafuta taarifa za ajali kwenye vyombo vya habari vya kijamii. </p>
<p>Inaonekana kana kwamba ulimwengu wa blogu wa Kirusi bado uko mbali na kuwa chanzo kikuuu cha kutangaza habari mpya. Bado unabaki kuwa sehemu ya usambazaji wa habari na mijadala mipana inayohusu nini kilichotokea. </p>
]]></content:encoded>
			<wfw:commentRss>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/12/urusi-jinsi-abiria-wa-nevsky-express-walivyoeleza-habari-kupitia-vyombo-vya-habari-vya-kijamii/feed/</wfw:commentRss>
		<slash:comments>0</slash:comments>
		</item>
		<item>
		<title>Palestina: Mtaa wa Twita</title>
		<link>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/11/palestina-mtaa-wa-twita/</link>
		<comments>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/11/palestina-mtaa-wa-twita/#comments</comments>
		<pubDate>Sun, 15 Nov 2009 10:57:21 +0000</pubDate>
		<dc:creator>j nambiza tungaraza</dc:creator>
				<category><![CDATA[English]]></category>
		<category><![CDATA[Ideas]]></category>
		<category><![CDATA[Internet & Telecoms]]></category>
		<category><![CDATA[Middle East & North Africa]]></category>
		<category><![CDATA[Palestine]]></category>
		<category><![CDATA[Refugees]]></category>
		<category><![CDATA[Roundups]]></category>

		<guid isPermaLink="false">http://sw.globalvoicesonline.org/?p=663</guid>
		<description><![CDATA[Ilichapwa kwanza naKatharine Ganly  &#183; Imetafsiriwa na j nambiza tungaraza &#183;  Angalia ujumbe mama 
Eman katika AquaCool anatoa maoni kuhusu mtaa wa kwanza kupata jina linalotokana na huduma ya Twita, katika kambi ya wakambizi huko ukingo wa Magharibi.
]]></description>
			<content:encoded><![CDATA[<em>Ilichapwa kwanza na<a href="http://globalvoicesonline.org/author/katharine-ganly/">Katharine Ganly</a>  &middot; Imetafsiriwa na <a href='http://sw.globalvoicesonline.org/author/j-nambiza-tungaraza/'>j nambiza tungaraza</a> &middot;  <a href='http://globalvoicesonline.org/2009/11/14/palestine-twitter-inspiried-street/'>Angalia ujumbe mama</a></em> 
<br /><p>Eman katika <em>AquaCool</em> anatoa maoni kuhusu <em><a href="http://aquacool.subzeroblue.com/2009/10/06/1st-twitter-inspired-street-name-in-palestine/">mtaa wa kwanza kupata jina linalotokana na huduma ya Twita</a></em>, katika kambi ya wakambizi huko ukingo wa Magharibi.</p>
]]></content:encoded>
			<wfw:commentRss>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/11/palestina-mtaa-wa-twita/feed/</wfw:commentRss>
		<slash:comments>0</slash:comments>
		</item>
		<item>
		<title>Ofisa Aweka Wazi Ufisadi wa Polisi kupitia Mtandao</title>
		<link>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/11/ofisa-aweka-wazi-ufisadi-wa-polisi-kupitia-mtandao/</link>
		<comments>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/11/ofisa-aweka-wazi-ufisadi-wa-polisi-kupitia-mtandao/#comments</comments>
		<pubDate>Tue, 10 Nov 2009 11:10:26 +0000</pubDate>
		<dc:creator>Deogratias Simba</dc:creator>
				<category><![CDATA[Breaking News]]></category>
		<category><![CDATA[Cyber-Activism]]></category>
		<category><![CDATA[English]]></category>
		<category><![CDATA[Feature]]></category>
		<category><![CDATA[Freedom of Speech]]></category>
		<category><![CDATA[General]]></category>
		<category><![CDATA[Human Rights]]></category>
		<category><![CDATA[Internet & Telecoms]]></category>
		<category><![CDATA[Russia]]></category>
		<category><![CDATA[Technology]]></category>
		<category><![CDATA[Weblog]]></category>

		<guid isPermaLink="false">http://sw.globalvoicesonline.org/?p=595</guid>
		<description><![CDATA[Mnamo tarehe 6 Novemba, afisa wa polisi katika Idara ya Mambo ya Ndani huko Novorossiysk alitumia tovuti yake binafsi kuwasiliana na Waziri Mkuu Vladimir Putin na kuzungumzia matatizo lukuki yanayowakabili maafisa wa polisi nchini Urusi. ]]></description>
			<content:encoded><![CDATA[<em>Ilichapwa kwanza na<a href="http://globalvoicesonline.org/author/vadim-isakov/">Vadim Isakov</a>  &middot; Imetafsiriwa na <a href='http://sw.globalvoicesonline.org/author/simbadeo/'>Deogratias Simba</a> &middot;  <a href='http://globalvoicesonline.org/2009/11/09/officer-exposes-police-corruption-using-the-web/'>Angalia ujumbe mama</a></em> 
<br /><p><img alt="" src="http://globalvoicesonline.org/wp-content/uploads/2009/11/YouTube-%D0%92%D0%B8%D0%B4%D0%B5%D0%BE%D0%BE%D0%B1%D1%80%D0%B0%D1%89%D0%B5%D0%BD%D0%B8%D0%B5-%D0%BC%D0%B0%D0%B9%D0%BE%D1%80%D0%B0-%D0%BC%D0%B8%D0%BB%D0%B8%D1%86%D0%B8%D0%B8-%D0%BA-%D0%9F%D1%83%D1%82%D0%B8%D0%BD%D1%83-1_1257748652019-75x75.jpg" title="YouTube - Видеообращение майора милиции к Путину (#1)_1257748652019" class="alignleft" width="75" height="75" /> Mnamo tarehe 6 Novemba, afisa wa polisi katika Idara ya Mambo ya Ndani huko <a href="http://maps.google.com/maps?q=Novorossiysk&#038;oe=utf-8&#038;rls=org.mozilla:en-US:official&#038;client=firefox-a&#038;um=1&#038;ie=UTF-8&#038;hq=&#038;hnear=Russian+Federation,+Region+of+Krasnodar,+Novorossiysk&#038;gl=us&#038;ei=aa73SouZJZDR8QbxpNDzCQ&#038;sa=X&#038;oi=geocode_result&#038;ct=title&#038;resnum=1&#038;ved=0CAoQ8gEwAA">Novorossiysk</a> alitumia tovuti yake binafsi kuwasiliana na Waziri Mkuu Vladimir Putin na kuzungumzia matatizo lukuki yanayowakabili maafisa wa polisi nchini Urusi. </p>
<p>Kwenye ujumbe wake wa video unaopotakina katika anwani hii ya mtandaoni <a href="http://www.dymovskiy.ru/">www.dymovskiy.ru</a> na YouTube (<a href="http://www.youtube.com/watch?v=2G3KbBfpg24&#038;feature=related">sehemu ya I</a> na <a href="http://www.youtube.com/watch?v=2dJkMLxvulw">sehemu ya II</a> [RUS]), Aleksey Dymovskiy anaonekana kuwa mtulivu na anayejieleza kwa usahihi mkubwa. Anazungumzia juu ya kushuka kwa hadhi ya polisi, rushwa, ufisadi na jinsi gani malipo duni yanavyokuwa kama sumu inayowala maafisa wengi wa polisi nchini Urusi.</p>
<blockquote><p>Nafikiri watu wengi watanielewa. Nataka kuchapa kazi, lakini nimechoshwa na mipango ya kingano ambapo tunalazimishwa kupeleleza jinai ambazo hazipo.  Nimechoshwa na mipango ya kutunga ambapo tunaambiwa tuwafunge watu fulani. Nimechoshwa na jinai za kutunga zinazoandaliwa ili kuwatupa watu fulani gerezani. </p></blockquote>
<p>Akiendelea kuweka wazi mambo mbalimbali, Dymovskiy anakiri kumtupa mtu asiye na hatia gerezani kwa sababu ya kulazimishwa na mkubwa wake kazini:</p>
<blockquote><p>Mkurugenzi wa Idara ya mambo ya Ndani alinitunukia cheo cha Meja, ambacho nilikipata mwezi Mei, kwa sababu tu nilimwahidi kutumpa mtu asiye na hatia gerezani. Siogopi kueleza jambo hili. Naelewa kuwa naweza kuadhibiwa kwa sababu hii. Lakini ni ukweli nami ninaukiri.</p></blockquote>
<p>Dymovsky pia anamwomba Waziri Mkuu Vladimir Putin kupeleleza matatizo hayo na kumalizia mbali tatizo la ufisadi katika jeshi la polisi.<br />
Video yake hiyo ilipata watembeleaji wengi sana muda mfupi tu tangu ichapishwe na vilevile maelfu waliibofya kwenye YouTube. Ilichukuliwa pia sana na kuchapishwa na vyombo vikuu vya habari za Urusi na kujadiliwa sana katika blogu nyingi. Ni mfano mmoja kati ya kadhaa ya kwanza ambapo raia wa Urusi wanafaulu vema kabisa kutumia miundo mipya ya majukwa ya habari ili kuwasiliana na serikali hasa kuhusu masuala nyeti yanayoikabili nchi. </p>
<p>Upekee wa &#8220;hotuba za kiraia kwa njia ya video&#8221; nchini Urusi inaelezwa vema zaidi kwa maoni yenye tahadhari kutoka katika moja ya blogu maarufu zaidi nchini inayoitwa <a href="http://dolboeb.livejournal.com/1696532.html">dolboeb</a>:</p>
<blockquote><p>Risala yenye nguvu ya pekee. Sitashangaa kama itageuka kuwa mbinu ambukizi ya utafutaji masoko. Mhusika mkuu anaonekana kama mtu wa kutoka sayari nyingine.</p></blockquote>
<p>Mwanablogu mwingine <a href="http://marchenk.livejournal.com/191686.html">marchenk</a> anaandika:</p>
<blockquote><p>Hakuna hata mmoja wetu aliye malaika&#8230; simhusudu [Dymovskiy] kama askari mwaminifu na mpenda ukweli (mwenyewe amekiri kwamba alitunukiwa cheo cha Meja kwa kumfunga mtu asiye na hatia gerezani).  […] Hata hivyo, nampa heshima kwa ajili ya ujasiri wake wa kuwa mkweli. Kwa hiyo, kumbe kuna maafisa wengine wa polisi walio waaminifu. Kwa sababu yao, ni muhimu kuhakikisha kunakuwepo na mabadiliko katika jeshi la polisi. </p>
<p>Ninamwombea Mungu ili kwamba uwekaji wake wazi huu wa mambo umpe kinga na atendewe haki katika hali yake. </p></blockquote>
<p>Siku ya Jumapili, tarehe 8 Novemba, Rashid Nurgaliev, Waziri wa Urusi wa Mambo ya Ndani, alitangaza ukaguzi wa jeshi la polisi huko Novorossiysk. Wakati huohuo, Dymovskiy amefukuzwa kazi kwa sababu ya “uzushi na vitendo ambavyo vinaharibu sifa” ya polisi.</p>
<p>Katika mahojiano yake na kituo cha redio cha Urusi, “<a href="http://www.echo.msk.ru/">Ekho Moskvy</a>,” Dymovskiy alisema kwamba amekuwa akifuatiliwa na kwa hiyo alikuwa akifikiria kuhamishia familia yake jijini Moscow kwa sababu za kiusalama. </p>
]]></content:encoded>
			<wfw:commentRss>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/11/ofisa-aweka-wazi-ufisadi-wa-polisi-kupitia-mtandao/feed/</wfw:commentRss>
		<slash:comments>0</slash:comments>
		</item>
		<item>
		<title>Tunisia: Mwanablogu Fatma Arabicca Awekwa Kizuizini</title>
		<link>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/11/tunisia-mwanablogu-fatma-arabicca-awekwa-kizuizini/</link>
		<comments>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/11/tunisia-mwanablogu-fatma-arabicca-awekwa-kizuizini/#comments</comments>
		<pubDate>Sat, 07 Nov 2009 12:12:30 +0000</pubDate>
		<dc:creator>j nambiza tungaraza</dc:creator>
				<category><![CDATA[Cyber-Activism]]></category>
		<category><![CDATA[English]]></category>
		<category><![CDATA[Freedom of Speech]]></category>
		<category><![CDATA[Internet & Telecoms]]></category>
		<category><![CDATA[Law]]></category>
		<category><![CDATA[Middle East & North Africa]]></category>
		<category><![CDATA[Roundups]]></category>
		<category><![CDATA[Tunisia]]></category>

		<guid isPermaLink="false">http://sw.globalvoicesonline.org/?p=567</guid>
		<description><![CDATA[Ilichapwa kwanza naAmira Al Hussaini  &#183; Imetafsiriwa na j nambiza tungaraza &#183;  Angalia ujumbe mama 
Mwanablogu wa Kitunisia Fatma Riahi ambaye hublogu kama Fatma Arabicca, ameshtakiwa kwa udhalilishaji katika blogu yake na hivi sasa amewekwa kizuizini.Kundi limeundwa kwenye Facebook kumuunga mkono mwanablogu huyu mwenye umri wa miaka 34, ambaye pia anatuhumiwa kublogu kwenye [...]]]></description>
			<content:encoded><![CDATA[<em>Ilichapwa kwanza na<a href="http://globalvoicesonline.org/author/amira-al-hussaini/">Amira Al Hussaini</a>  &middot; Imetafsiriwa na <a href='http://sw.globalvoicesonline.org/author/j-nambiza-tungaraza/'>j nambiza tungaraza</a> &middot;  <a href='http://globalvoicesonline.org/2009/11/07/tunisia-blogger-fatma-arabicca-detained/'>Angalia ujumbe mama</a></em> 
<br /><p>Mwanablogu wa Kitunisia Fatma Riahi ambaye <a href="http://fatma-arabicca.blogspot.com/">hublogu</a> kama Fatma Arabicca, ameshtakiwa kwa udhalilishaji katika blogu yake na hivi sasa amewekwa kizuizini.Kundi limeundwa kwenye <em><a href="http://www.facebook.com/home.php?ref=home#/group.php?gid=171535170769&#038;ref=nf">Facebook</a></em> kumuunga mkono mwanablogu huyu mwenye umri wa miaka 34, ambaye pia anatuhumiwa kublogu kwenye <em>Debat Tunise</em> (Mdahalo wa Tunisia). </p>
]]></content:encoded>
			<wfw:commentRss>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/11/tunisia-mwanablogu-fatma-arabicca-awekwa-kizuizini/feed/</wfw:commentRss>
		<slash:comments>0</slash:comments>
		</item>
		<item>
		<title>Tamasha la Blogu Indonesia</title>
		<link>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/11/tamasha-la-blogu-indonesia/</link>
		<comments>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/11/tamasha-la-blogu-indonesia/#comments</comments>
		<pubDate>Fri, 06 Nov 2009 10:39:42 +0000</pubDate>
		<dc:creator>j nambiza tungaraza</dc:creator>
				<category><![CDATA[East Asia]]></category>
		<category><![CDATA[English]]></category>
		<category><![CDATA[Indonesia]]></category>
		<category><![CDATA[Internet & Telecoms]]></category>
		<category><![CDATA[Photos]]></category>
		<category><![CDATA[Technology]]></category>
		<category><![CDATA[Video]]></category>
		<category><![CDATA[Weblog]]></category>

		<guid isPermaLink="false">http://sw.globalvoicesonline.org/?p=547</guid>
		<description><![CDATA[Tulitembelea tamasha la blogu la Indonesia au PestaBlogger 2009. Hii nim ara ya tatu kwa tukio hili la mwaka kufanyika. Tukio hili lilishuhudia wanablogu kutoka kila sehemu ya Kisiwa hiki ambacho pia ni Taifa wakimiminika mjini Jakarta ili kusherehekea, kujadili na kujumuika.]]></description>
			<content:encoded><![CDATA[<em>Ilichapwa kwanza na<a href="http://globalvoicesonline.org/author/preetam/">Preetam Rai</a>  &middot; Imetafsiriwa na <a href='http://sw.globalvoicesonline.org/author/j-nambiza-tungaraza/'>j nambiza tungaraza</a> &middot;  <a href='http://globalvoicesonline.org/2009/10/27/at-the-indonesian-blogger-festival/'>Angalia ujumbe mama</a></em> 
<br /><p>Indonesia ina uwanja wa blogu uliosisimka na wenye msisitizo mkubwa kwa jamii. Tamasha la mwaka la wanablogu (Pestablogger) la Indonesia liliwavutia wanablogu na wapenzi wa teknolojia kutoka sehemu zote za taifa.  </p>
<p><img alt="" src="http://globalvoicesonline.org/wp-content/uploads/2009/10/pbblogger011.jpg" title="pestablogger09" class="aligncenter" width="480" height="271" /></p>
<p>Ukumbi uliojaa wa tamasha la blogu la Indonesia</p>
<p><object width="425" height="344"><param name="movie" value="http://www.youtube.com/v/cZwFCS2aO4U&#038;rel=0&#038;color1=0xb1b1b1&#038;color2=0xcfcfcf&#038;hl=en&#038;feature=player_embedded&#038;fs=1"></param><param name="allowFullScreen" value="true"></param><param name="allowScriptAccess" value="always"></param><embed src="http://www.youtube.com/v/cZwFCS2aO4U&#038;rel=0&#038;color1=0xb1b1b1&#038;color2=0xcfcfcf&#038;hl=en&#038;feature=player_embedded&#038;fs=1" type="application/x-shockwave-flash" allowfullscreen="true" allowScriptAccess="always" width="425" height="344"></embed></object><br />
Taswira kutoka kwenye tamasha la blogu.</p>
<p><img alt="" src="http://globalvoicesonline.org/wp-content/uploads/2009/10/pbblogger02.jpg" title="pestablogger09" class="aligncenter" width="480" height="271" /><br />
Hii ilikuwa ni mara ya tatu kwa tukio hili la mwaka kufanyika na ni vizuri kuona idadi ya washiriki inaongezeka kila mwaka.<br />
<div class="wp-caption aligncenter" style="width: 490px"><img alt="pestablogger09" src="http://globalvoicesonline.org/wp-content/uploads/2009/10/pbblogger03.jpg" width="480" height="271" /><p class="wp-caption-text">pestablogger09</p></div><br />
Kipindi cha majadiliano juu ya maadili ya kublogu<br />
<img alt="" src="http://globalvoicesonline.org/wp-content/uploads/2009/10/pbblogger06.jpg" title="pestablogger09" class="aligncenter" width="480" height="360" /><br />
Kipindi cha majadiliano juu ya uanahabari wa kiraia<br />
<img alt="" src="http://globalvoicesonline.org/wp-content/uploads/2009/10/pbblogger07.jpg" title="pestablogger09" class="aligncenter" width="480" height="360" /><br />
Mwanahabari wa kiraia akielezea uzoefu wake kwa wanablogu<br />
<img alt="" src="http://globalvoicesonline.org/wp-content/uploads/2009/10/pbblogger08.jpg" title="pestablogger09" class="aligncenter" width="480" height="360" /><br />
Kipindi cha majadiliano juu ya kuunganisha kwenye utengano ndani ya Indonesia kwa kutumia blogu. Washiriki pia walijadili njia ambazo Indonesia inaweza kutumia kuiunganisha na dunia ya nje.<br />
<img alt="" src="http://globalvoicesonline.org/wp-content/uploads/2009/10/pbblogger101.jpg" title="pestablogger09" class="aligncenter" width="480" height="271" /><br />
Tristam (aliyewakilisha shirika la wadhamini), Chip, (mkereketwa wa teknolojia kutoka Vietnam) na Retty (Mwanablogu wa Indonesia) wakiwa katika majadiliano. Tukio hili la Indonesia halikushuhudia viwango vya ushiriki kutoka nje ambavyo Kampuchea au Thailand huvishuhudia. Hata hivyo, watu waliojaa udadisi wanatiririka na tunatumaini kupata watu zaidi kutoka maeneo ya Kusini Mashariki ya Asia wakati ujao.<br />
<img alt="" src="http://globalvoicesonline.org/wp-content/uploads/2009/10/pbblogger12.jpg" title="pestablogger09" class="aligncenter" width="480" height="270" /><br />
Msanii wa Batik akitengeneza shati la tamasha la blogu<br />
<img alt="" src="http://globalvoicesonline.org/wp-content/uploads/2009/10/pbblogger11.jpg" title="pestablogger09" class="aligncenter" width="480" height="271" /><br />
Wanablogu wanachukua mapumziko kutoka kwenye majadiliano na kuburudika na muziki.</p>
]]></content:encoded>
			<wfw:commentRss>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/11/tamasha-la-blogu-indonesia/feed/</wfw:commentRss>
		<slash:comments>0</slash:comments>
		</item>
		<item>
		<title>Saudia Arabia: Ambako Kuiga Kazi Kinyume cha Haki Miliki ni Kosa la Jinai</title>
		<link>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/11/saudia-arabia-ambako-kuiga-kazi-kinyume-cha-haki-miliki-ni-kosa-la-jinai/</link>
		<comments>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/11/saudia-arabia-ambako-kuiga-kazi-kinyume-cha-haki-miliki-ni-kosa-la-jinai/#comments</comments>
		<pubDate>Tue, 03 Nov 2009 12:06:46 +0000</pubDate>
		<dc:creator>Christian Bwaya</dc:creator>
				<category><![CDATA[English]]></category>
		<category><![CDATA[General]]></category>
		<category><![CDATA[Internet & Telecoms]]></category>
		<category><![CDATA[Law]]></category>
		<category><![CDATA[Media]]></category>
		<category><![CDATA[Middle East & North Africa]]></category>
		<category><![CDATA[Protest]]></category>
		<category><![CDATA[Saudi Arabia]]></category>
		<category><![CDATA[Weblog]]></category>

		<guid isPermaLink="false">http://sw.globalvoicesonline.org/?p=458</guid>
		<description><![CDATA[Wanablogu wa Kisaudia wanaungana ili kumuunga mkono mwanablogu mwenzao anayelituhumu gazeti moja kuwa limetumia picha na kuzinakili kutoka mwenye blogu yake bila ruhusa. ]]></description>
			<content:encoded><![CDATA[<em>Ilichapwa kwanza na<a href="http://globalvoicesonline.org/author/amira-al-hussaini/">Amira Al Hussaini</a>  &middot; Imetafsiriwa na <a href='http://sw.globalvoicesonline.org/author/bwaya/'>Christian Bwaya</a> &middot;  <a href='http://globalvoicesonline.org/2009/10/20/saudi-arabia-where-plagiarism-is-a-crime/'>Angalia ujumbe mama</a></em> 
<br /><p>Wanablogu wa Kisaudia wanaungana ili kumuunga mkono mwanablogu mwenzao anayelituhumu gazeti moja kuwa limetumia picha na kuzinakili kutoka mwenye blogu yake bila ruhusa. </p>
<p><em><a href="http://saudijeans.org/2009/10/14/alyaum-steals-kaust-blogger/">Saudi Jeans</a></em>‘ Ahmed Al Omran anazo sifa kiduchu mno kwa gazeti hilo linalotuhumiwa kwa kitendo cha kutumia kazi za wengine kinyume cha haki miliki: </p>
<blockquote><p>Ingawa gazeti la al – Yaum, kwa muda mrefu limefurahia nafasi kubwa katika Jimbo la Mashariki, (EP) linabaki kuwa kati ya machapicho duni zaidi nchini. Nilizaliwa na kukuzwa katika Jimbo la Mashariki, na nilizoea kusoma magazeti ya Ashraq al-Awsat, al-Hayat na al-Watan lakini sio al-Yaum. </p></blockquote>
<p>Kutofurahishwa kwa Al Omran kulichochewa zaidi baada ya <em><a href="http://saudiaggie.blogspot.com/2009/10/i-should-be-getting-paid-for-this.html">Saudi Aggie</a></em>, mwanafunzi mwenye jina la Nathan wa <em>Chuo Kikuu cha Sayansi na Teknolojia cha Mfalme Abdulla</em> (KAUST) <a href="http://globalvoicesonline.org/2009/09/26/saudi-arabia-kaust-to-inspire-scientific-achievement-and-more/">kilichofunguliwa hivi karibuni</a> alipoleta malalamiko kwamba gazeti hilo limetumia picha zake pamoja na uchambuzi wake kuhusu uchaguzi wa wanafunzi hivi majuzi. Ameweka nakala ya habari hizo kutoka gazetini na kuwauliza wasomaji wake:</p>
<blockquote><p>Siwezi kuamini hili! Angalia makala hii iliyochapishwa hivi majuzi kwenye gazeti maarufu la Saudi Arabia, Al Yaum. Je, picha hizi zinaonekana kana kwamba zinafahamika? Vipi kuhusu maneno? Kama huwezi kusoma Kiarabu, hii ilichukuliwa karibu neno kwa neno kutoka kwenye makala ya blogu yangu niliyoipa jina la ‘<a href="http://saudiaggie.blogspot.com/2009/10/elections.html">uchaguzi</a>’ na kuichapa Oktoba 5, 2009. Hii haiwezi kuwa sahihi kisheria, hata hapa Saudi Arabia!</p></blockquote>
<p>Mwanafuzi huyo wa Kimarekani anaongeza: </p>
<blockquote><p>
Kama ningekuwa Marekani ningefungua kesi ya haki miliki ya utaaluma dhidi ya Al Yaum. Kama lingekuwa ni Gazeti la New York Times limetumia kazi yangu bila ruhusa, ningekuwa tajiri sasa hivi. Hivi haki miliki za utaaluma kwa mawazo na picha zilizochapishwa zina thamani yoyote hapa?</p></blockquote>
<p>Al Omran anazingatia: </p>
<blockquote><p>Nathan anafikiria kuwashitaki, jambo ambalo nadhani litakuwa zuri sana, lakini labda wameshajitia aibu vilivyo wao wenyewe.  </p></blockquote>
<p>Watoa maoni kwenye blogu ya Nathan wanaguswa na yaliyompata mwanablogu: </p>
<p><em>Mazoo</em> anaandika: </p>
<blockquote><p>Ninasikitika kuona hili linatokea kwako&#8230;<br />
Lakini, hili ni jambo lililozoeleka hapa Saudi Arabia&#8230;</p>
<p>Nimesikia kesi nyingi ambazo kazi za marafiki zangu (maandiko ya blogu, picha na mawazo) yameibwa na waandishi habari wavivu. Walilalamikia hali hii na wengine waliaandikia wahariri wakuu –wengine wao huandika taarifa za kuomba msamaha na wengine wao humfukuza kazi mtu aliyeiba maudhui</p></blockquote>
<p><em>Al Hanouf</em>, anayejielezea mwenyewe kuwa ni mwanafunzi wa sheria, anataka haki itendeke: </p>
<blockquote><p>Kama kitendo hiki kikiangaliwa chini ya makosa ya jinai yanayohusiana na kompyuta, basi huyu – mwana habari – inatakiwa awe jela kwa zaidi ya miezi sita na kukulipa si chini ya fedha ya Riyali za Saudia 250,000.<br />
Unapaswa uende kwa mwanasheria, na tafadhali usilimalize hili kwa kuliandikia gazeti barua pepe! Kuna sheria, na (gazeti) halitaweza kurekebisha makosa yake kama tutalimaliza suala hili kwa njia zatu za kizembe!</p></blockquote>
<p>Na Chiara anashauri: </p>
<blockquote><p>Nami ninashiriki katika kuchefuka na uvunjifu huu wa sheria ya haki miliki, na njia iliyozoeleka ya kutafsiri na ‘kuiba’ kazi za wengine si nafuu. Unaweza kuweka blogu yako nzima chini ya haki miliki kama ambavyo wanablogu wengine wamefanya, na kufanya namna ambayo jina lako litaonekana kwenye picha. </p></blockquote>
<p>Kwenye makala fuatilizi, Nathan anaandika:  </p>
<blockquote><p>Nchini Saudi Arabia, umbea huenea kama vile ugonjwa wa mlipuko. Blogu hii imepokea makumi elfu ya watembeleaji wapya katika juma moja tu </p>
<p>[…] </p>
<p>Nilikuja Saudia kujenga madaraja (ushirikiano), sio kutengeneza maadui. Nilikuja kusoma na kutafiti katika Chuo kikuu ambacho kinajitahidi kwa nguvu zote kuwa moja wapo ya vyuo vikuu bora vya utafiti duniani, na sio kupata fedha kutoka kwa watu ama mashirika. </p>
<p>Ninataka uwajibikaji. Ilichokifanya <em>Al Yaum</em> kilikuwa ni makosa, lakini mwenendo wa mjadala pia una makosa. </p></blockquote>
<p>Na maneno yake ya mwisho kwa wasomaji wake ni: </p>
<blockquote><p>Kama unataka kuazima kitu kutoka kwenye blogu yangu, tafadhali omba kwanza. Hakuna mtu, nikijijumuisha na mimi, anayependa kutokuelewana. </p></blockquote>
<p>Kwa kutumia kifaa cha kutafsiri, <a href="http://saudiaggie.blogspot.com/2009/10/i-should-be-getting-paid-for-this.html?showComment=1255467311093#c5285446355482995533">mwandishi husika</a> anamwandikia Nathan akilielezea vyema suala lake.</p>
]]></content:encoded>
			<wfw:commentRss>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/11/saudia-arabia-ambako-kuiga-kazi-kinyume-cha-haki-miliki-ni-kosa-la-jinai/feed/</wfw:commentRss>
		<slash:comments>0</slash:comments>
		</item>
		<item>
		<title>Trinidad &amp; Tobago: Kampeni ya 350</title>
		<link>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/10/trinidad-tobago-kampeni-ya-350/</link>
		<comments>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/10/trinidad-tobago-kampeni-ya-350/#comments</comments>
		<pubDate>Mon, 26 Oct 2009 12:24:39 +0000</pubDate>
		<dc:creator>j nambiza tungaraza</dc:creator>
				<category><![CDATA[Americas]]></category>
		<category><![CDATA[Cyber-Activism]]></category>
		<category><![CDATA[English]]></category>
		<category><![CDATA[Environment]]></category>
		<category><![CDATA[Gender]]></category>
		<category><![CDATA[Health]]></category>
		<category><![CDATA[Human Rights]]></category>
		<category><![CDATA[Ideas]]></category>
		<category><![CDATA[Indigenous]]></category>
		<category><![CDATA[Industry]]></category>
		<category><![CDATA[Internet & Telecoms]]></category>
		<category><![CDATA[Politics]]></category>
		<category><![CDATA[Protest]]></category>
		<category><![CDATA[Roundups]]></category>
		<category><![CDATA[Trinidad & Tobago]]></category>

		<guid isPermaLink="false">http://sw.globalvoicesonline.org/?p=473</guid>
		<description><![CDATA[Ilichapwa kwanza naJanine Mendes-Franco  &#183; Imetafsiriwa na j nambiza tungaraza &#183;  Angalia ujumbe mama 
“Trinidad na Tobago ni kisiwa tajiri na nchi inayoendelea tajiri kwa mafuta na gesi asilia. Lakini pia tunashuhudia madhara mabaya ya maendeleo ya haraka kwenye  nyanja za viwanda katika visiwa vyetu. Hii ni fursa ya sauti za wanawake [...]]]></description>
			<content:encoded><![CDATA[<em>Ilichapwa kwanza na<a href="http://globalvoicesonline.org/author/janine-mendes-franco/">Janine Mendes-Franco</a>  &middot; Imetafsiriwa na <a href='http://sw.globalvoicesonline.org/author/j-nambiza-tungaraza/'>j nambiza tungaraza</a> &middot;  <a href='http://globalvoicesonline.org/2009/10/23/trinidad-tobago-350-action/'>Angalia ujumbe mama</a></em> 
<br /><p>“Trinidad na Tobago ni kisiwa tajiri na nchi inayoendelea tajiri kwa mafuta na gesi asilia. Lakini pia tunashuhudia madhara mabaya ya maendeleo ya haraka kwenye  nyanja za viwanda katika visiwa vyetu. Hii ni fursa ya sauti za wanawake kusikika”: <a href="http://tillahwillah.wordpress.com/2009/10/23/women-350-climate-action-in-trinidad/">Attillah Springer </a>anajihusisha na kampeni ya hali ya hewa 350.</p>
]]></content:encoded>
			<wfw:commentRss>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/10/trinidad-tobago-kampeni-ya-350/feed/</wfw:commentRss>
		<slash:comments>0</slash:comments>
		</item>
		<item>
		<title></title>
		<link>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/10/344/</link>
		<comments>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/10/344/#comments</comments>
		<pubDate>Sun, 04 Oct 2009 05:00:10 +0000</pubDate>
		<dc:creator>j nambiza tungaraza</dc:creator>
				<category><![CDATA[Bahrain]]></category>
		<category><![CDATA[Cyber-Activism]]></category>
		<category><![CDATA[English]]></category>
		<category><![CDATA[Internet & Telecoms]]></category>
		<category><![CDATA[Middle East & North Africa]]></category>
		<category><![CDATA[Roundups]]></category>
		<category><![CDATA[Software & Tools]]></category>
		<category><![CDATA[TYPE]]></category>
		<category><![CDATA[Technology]]></category>
		<category><![CDATA[WORLD]]></category>

		<guid isPermaLink="false">http://sw.globalvoicesonline.org/?p=344</guid>
		<description><![CDATA[ &#183; Imetafsiriwa na j nambiza tungaraza &#183;  Angalia ujumbe mama 
Kutoka Bahrain, Redbelt, anatabiri mwisho wa kublogu.. kama tunavyojua.
]]></description>
			<content:encoded><![CDATA[<em> &middot; Imetafsiriwa na <a href='http://sw.globalvoicesonline.org/author/j-nambiza-tungaraza/'>j nambiza tungaraza</a> &middot;  <a href='http://globalvoicesonline.org/2009/10/03/bahrain-the-end-of-blogging/'>Angalia ujumbe mama</a></em> 
<br /><p>Kutoka Bahrain, <em><a href="http://theredbelt.com/2009/09/end-of-blogging.html">Redbelt</a></em>, anatabiri mwisho wa kublogu.. kama tunavyojua.</p>
]]></content:encoded>
			<wfw:commentRss>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/10/344/feed/</wfw:commentRss>
		<slash:comments>0</slash:comments>
		</item>
		<item>
		<title>Palestina: Maoni Juu ya Kuzinduliwa Kwa Huduma ya Google.ps</title>
		<link>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/08/palestina-maoni-juu-ya-kuzinduliwa-kwa-huduma-ya-google-ps/</link>
		<comments>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/08/palestina-maoni-juu-ya-kuzinduliwa-kwa-huduma-ya-google-ps/#comments</comments>
		<pubDate>Sun, 16 Aug 2009 09:08:31 +0000</pubDate>
		<dc:creator>j nambiza tungaraza</dc:creator>
				<category><![CDATA[Breaking News]]></category>
		<category><![CDATA[English]]></category>
		<category><![CDATA[Feature]]></category>
		<category><![CDATA[General]]></category>
		<category><![CDATA[Governance]]></category>
		<category><![CDATA[Internet & Telecoms]]></category>
		<category><![CDATA[Middle East & North Africa]]></category>
		<category><![CDATA[Palestine]]></category>
		<category><![CDATA[Qatar]]></category>
		<category><![CDATA[Technology]]></category>
		<category><![CDATA[Weblog]]></category>

		<guid isPermaLink="false">http://sw.globalvoicesonline.org/?p=298</guid>
		<description><![CDATA[Google imeongeza anwani ya google.ps (google palestina) kwenye orodha yake zana inayotoa huduma za utafutaji zinazolenga sehemu mbali mbali. Anwani hiyo mpya inakusudiwa kufanya kazi katika ukanda wea Magharibi na Gaza, ambako watoaji huduma za intaneti hufanyia kazi zao. ]]></description>
			<content:encoded><![CDATA[<em>Ilichapwa kwanza na<a href="http://globalvoicesonline.org/author/jillian-york/">Jillian C. York</a>  &middot; Imetafsiriwa na <a href='http://sw.globalvoicesonline.org/author/j-nambiza-tungaraza/'>j nambiza tungaraza</a> &middot;  <a href='http://globalvoicesonline.org/2009/08/13/palestine-reactions-to-launch-of-google-ps/'>Angalia ujumbe mama</a></em> 
<br /><p>“Kwa miaka kadhaa google imekuwa ikiongeza anwani za sehemu maalum kama vile google.co.uk na google.jo ambazo zinatoa huduma za utafutaji maalum kwa sehemu hizo,” anasema mwanablogu <em>ArabCrunch</em>, alipokuwa <a href="http://arabcrunch.com/2009/08/breaking-google-launches-a-palestinian-domain.html">akitangaza </a>uamuzi wa Google wa kuongeza anwani maalum ya <a href="http://google.ps/">google.ps</a> katika orodha. Anwani hiyo mpya ya sehemu maalum inakusudia kufanya kazi katika Ukanda wa Magharibi na Gaza, ambako ndiko watoaji uduma za intaneti wanapofanyia kazi.</p>
<p>Wiki iliyopita blogu ya <em>Google Arabia</em> <a href="http://google-arabia.blogspot.com/">ilitangaza</a> ongezo hilo na sababu zilizopelekea uamuzi huo:</p>
<blockquote><p>Leo tunaongeza anwani nyingine katika orodha yetu, google.ps. Anwani hii mpya itawapa watumiaji wanaoongea Kiarabu waliopo katika majimbo ya Kipalestina, ambao wanatumia huduma zinazotolewa na watoa huduma za intaneti wa Kipalestina, uwezo wa kutumia Google kwa Kiarabu – na hatimaye, kuzifikia habari zinazolenga zaidi sehemu hiyo. Ukijumuishwa uzinduzi wa google.ps, tutatimiza jumla ya anwani zaidi ya 160 za google duniani. </p></blockquote>
<p>Katika <a href="http://arabcrunch.com/2009/08/breaking-google-launches-a-palestinian-domain.html">tamko</a> kwa <em>ArabCrunch</em>, Google pia ilifafanua kwa jinsi gani mabadiliko hayo yataathiri huduma ya maneno ya kutangazia biashara - AdWords: </p>
<blockquote><p>Kwa kutumia AdWords unaweza kulenga matangazo yako kwa nchi au majimbo, au kwa maeneo maalum pamoja na miji. Mfumo wa AdWords unatumia vigezo kadhaa ili kuamua kulionyesha tangazo lako pamoja na kujumuisha anwani ya Google inayotumiwa (.fr, .de, .kr, na kadhalika.), neno halisi analulitumia mtafutaji wakati wa kutafuta na ikiwezekana, tanweza kufahamu sehemu alipo mtumiaji kutegemeana na anwani ya kiitikadi ya intaneti ( au anwani ya IP).  “. Mfumo wa AdWords unatumia vigezo kadhaa ili kuamua kulionyesha tangazo lako pamoja na kujumuisha anwani ya Google inayotumiwa (.Com, .De, .Kr, na kadhalika.), neno halisi analulitumia mtafutaji wakati wa kutafuta na ikiwezekana, tanweza kufahamu sehemu alipo mtumiaji kutegemeana na anwani ya kiitikadi ya intaneti ( au anwani ya IP).</p></blockquote>
<p>Blogu ya <em>Window into Palestine</em> <a href="http://windowintopalestine.blogspot.com/2009/08/google-launches-palestine-specific-web.html">inaelezea</a> kwamba wapalestina walioko Yerusalem Mashariki hawatakuwa na uwezo wa moja kwa moja kuifikia huduma ya google.ps <em>(zingatia: Mtu yeyote anaweza kuipata anwani ya google.ps kwa kuchapa anwani hiyo moja kwa moja):</em></p>
<blockquote><p>Ukiitoa Yerusalem Mashariki, ambayo inaangukiwa kwenye utawala wa Kiisraeli, Wapalestina walioko Ukanda wa Magharibi na Gaza wamekuwa wakiitegemea anwani ya google.jo, anwani ya Jordan, na ile ya Misri www.google.com.eg.</p></blockquote>
<p>Mtumiaji wa Twita <em>migueldeicaza</em> <a href="http://twitter.com/migueldeicaza/statuses/3287959889">alionyesha msisimko</a> wake wa ongezo hilo kwenye familia ya Google:<br />
<img alt="" src="http://globalvoicesonline.org/wp-content/uploads/2009/08/miguel.JPG" title="miguel" class="aligncenter" width="636" height="247" /><br />
<em>daiski</em>, mtumiaji mwingine wa Twita mwenye makazi huko Qatar, <a href="http://twitter.com/daiski/status/3284342629">aliishukuru</a> google kwa kufanya hilo:<br />
<img alt="" src="http://globalvoicesonline.org/wp-content/uploads/2009/08/daiski.bmp" title="daiski" class="aligncenter" width="631" height="238" /></p>
<p><a href="http://google.ps/">Google.ps</a> inapatikana kwa Kiingereza na kwa Kiarabu.</p>
]]></content:encoded>
			<wfw:commentRss>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/08/palestina-maoni-juu-ya-kuzinduliwa-kwa-huduma-ya-google-ps/feed/</wfw:commentRss>
		<slash:comments>0</slash:comments>
		</item>
		<item>
		<title>Afrika: Ujio wa Mkonga wa Seacom Wazua Mjadala</title>
		<link>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/07/afrika-ujio-wa-mkonga-wa-seacom-wazua-mjadala/</link>
		<comments>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/07/afrika-ujio-wa-mkonga-wa-seacom-wazua-mjadala/#comments</comments>
		<pubDate>Mon, 27 Jul 2009 14:18:29 +0000</pubDate>
		<dc:creator>j nambiza tungaraza</dc:creator>
				<category><![CDATA[English]]></category>
		<category><![CDATA[Feature]]></category>
		<category><![CDATA[Internet & Telecoms]]></category>
		<category><![CDATA[Kenya]]></category>
		<category><![CDATA[Mozambique]]></category>
		<category><![CDATA[Nigeria]]></category>
		<category><![CDATA[South Africa]]></category>
		<category><![CDATA[Sub-Saharan Africa]]></category>
		<category><![CDATA[Swahili]]></category>
		<category><![CDATA[Tanzania]]></category>
		<category><![CDATA[Uganda]]></category>
		<category><![CDATA[Weblog]]></category>

		<guid isPermaLink="false">http://sw.globalvoicesonline.org/?p=276</guid>
		<description><![CDATA[Ujio wa mkonga unaopita chini ya bahari utakao ongeza uwezo na kupunguza gharama za intaneti barani Afrika umewasha majadiliano na mvuto katika ulimwengu wa blogu wa Afrika. Seacom, ambayo inaunganisha Afrika Kusini, Tanzania, Kenya, Uganda na Msumbiji na Ulaya pamoja na Asia, ilianza kutumika moja kwa moja Alhamisi, kwa kuziunganisha nchi za Afrika ya mashariki na Afrika ya kusini kwenye mtandao wa dunia wenye wigo mpana. ]]></description>
			<content:encoded><![CDATA[<em>Ilichapwa kwanza na<a href="http://globalvoicesonline.org/author/rebekah-heacock/">Rebekah Heacock</a>  &middot; Imetafsiriwa na <a href='http://sw.globalvoicesonline.org/author/j-nambiza-tungaraza/'>j nambiza tungaraza</a> &middot;  <a href='http://globalvoicesonline.org/2009/07/24/africa-the-arrival-of-seacom-cable-sparks-debate/'>Angalia ujumbe mama</a></em> 
<br /><p>Ujio wa mkonga unaopita chini ya bahari utakao ongeza uwezo na kupunguza gharama za intaneti barani Afrika umewasha majadiliano na mvuto katika ulimwengu wa blogu wa Afrika. <a href="http://www.seacom.mu/index2.asp">Seacom</a>, ambayo inaunganisha Afrika Kusini, Tanzania, Kenya, Uganda na Msumbiji na Ulaya pamoja na Asia, <a href="http://www.guardian.co.uk/technology/2009/jul/23/east-africa-broadband-revolution">ilianza kutumika moja kwa moja</a> Alhamisi, kwa kuziunganisha nchi za Afrika ya mashariki na Afrika ya kusini kwenye mtandao wa dunia wenye wigo mpana.<br />
<div class="wp-caption aligncenter" style="width: 310px"><img alt="Seacom inaunganisha mwambao wa Afrika ya mashariki na Ulaya pamoja na Asia" src="http://globalvoicesonline.org/wp-content/uploads/2009/07/picture-1-300x271.png" title="Seacom" width="300" height="271" /><p class="wp-caption-text">Seacom inaunganisha mwambao wa Afrika ya mashariki na Ulaya pamoja na Asia</p></div></p>
<p>Miji ya Johannesburg, Nairobi na Kampala <a href="http://www.google.com/hostednews/afp/article/ALeqM5iHrESmY6eTaALo3tbsjwGSPkPP1Q">iliunganishwa </a>Alhamisi, na Addis Ababa pamoja na Kigali inatarijia kufuata. Ujio wa mkonga huo ulipangwa kufikav mnamo mwanzoni mwa mwezi wa saba, lakini <a href="http://allafrica.com/stories/200906290065.html">mashumbulizi ya maharamia</a> nje kidogo ya pwani ya Somalia yalichelewesha utekelezaji.</p>
<p>Kiunganishi hiki cha chini ya bahari kinatarajiwa kupunguza gharama za upana wa masafa kwa asilimia 90 na kuongeza uwezo wa makongamano yanayotumia video, urushaji wa matangazo ya televisheni yenye picha za hali juu pamoja na huduma za intaneti zenye mwendo wa kasi kwenye mwambao wa Afrika ya mashariki.</p>
<p>“Mmmh… nasuburi kwa hamu kuanza upakuzi,” anaandika <a href="http://itblogkenya.blogspot.com/2009/07/seacom_22.html">IT blog Kenya</a>.</p>
<p>Huko Uganda, Josh kutoka blogu ya <a href="http://inanafricanminute.blogspot.com/2009/07/kung-fu-baby-and-seacom-cable-launch.html">In African Minute</a> ameshaanza kubaini tofauti:</p>
<blockquote><p>Mbinu inayojulikana ili kuangalia video za YouTube barani Afrika ni kwa kubonyeza alama ya kugandisha video wakati inapoanza, subiri kwa dakika 20 (au zaidi) mpaka hapo video itakapopakuliwa yote, halafu angalia. Leo nipo kwenye sherehe ya kuzindua SEACOM… kwenye kona ya chumba cha kongamano, Peter Mereton Meneja wa ununuzi wa SEACOM, alinipa ishara niionyeshe tarakilishi yenye ukurasa wa YouTube uliokuwa tayari. Tuliizindua <a href="http://www.youtube.com/watch?v=bxAirY-5QCQ">Kung Fu Baby</a> na kwa mara ya kwanza katika Afrika, niliona video ya YouTube ikipakuliwa yote na kuchezwa katika sekunde 6.</p></blockquote>
<p>Munashe wa <a href="http://www.techmasai.com/2009/07/24/seacom-the-under-sea-cable-has-arrived/">TechMasai</a> naye anafurahia:</p>
<blockquote><p>Mkonga wa chini ya bahari wa Seacom tuliouandika <a href="http://www.techmasai.com/2008/04/02/eassy-east-african-submarine-cable/">kitambo kidogo nyuma</a> umetimia na umeanza kufanya kazi leo. Ni mchakato wa kimapinduzi kutokana na ukweli kwamba nchi ambazo zitautumia hivi sasa, ambazo zinajumuisha kenye, Uganda, Msumbiji, Afrika Kusini na Uganda.</p>
<p>… Ni wakati mzuri kwa Afrika, Ninaweza kudhibitisha hilo kwa Kenya ambayo mpaka hivi sasa ilitegemea setilaiti kwa ajili ya mahitaji yake ya intaneti.</p></blockquote>
<p>Jeremy, mwanablogu wa Kinaijeria anayeandika katika <a href="http://naijablog.blogspot.com/2009/07/east-africa-goes-broadband.html">NaijaBlog</a>, analinganisha Seacom na mikongo mbalimbali ya Afrika magharibi. Afrika Magharibi bado ipo chini:</p>
<blockquote><p>Afrika ya Mashariki imekwenda na huduma ya masafa mapana ya intaneti… wakati Afrika ya Magharibi bado ipo kwenye sehemu ya kuanzia mbio (kwa kweli, bado ipo kwenye vyumba vya kubadilishia nguo ikijiuliza ni nini cha kuvaa) wakiwa na SAT3 isiyo na manufaa ambayo hukatika-katika, pamoja na Glo1 9je wakandarasi wa Alcatel wamekwama chini ya mabiwi ya mchanga?) na wakandarasi wengine wawili wapya, WACS na Main1 bado wakiwa mbali zaidi ya upeo (mwaka kesho kama tukiwa na bahati). Afrika ya mashariki imekumbatia huduma ya masafa mapana ya intaneti na kushika mbio wakati Afrika ya Magharibi  inasuasua na kukodoa macho.</p></blockquote>
<p>Twita nayo inanguruma na habari za Seacom. Baadhi ya watumniaji wana shauku, wakati wengine wana mashaka:</p>
<p>“Bado sijaweza kuamini kuwa unaweza kupakua mtandao wote wa Intaneti kupitia mkongo mmoja mdogo wa manjano <a href="http://twitter.com/search?q=%23seacom">#seacom</a>&#8220;<br />
— <a href="http://twitter.com/ncallegari/statuses/2815733071">ncallegari</a></p>
<blockquote><p>“Seacom ilizinduliwa_kwa hakika_leo. Na tuangalie itachukua muda gani kwa mawakala wa intaneti kuongeza kasi na kupunguza gharama…”<br />
— <a href="http://twitter.com/dnyaga/status/2808617797">dnyaga</a></p>
<p>‘je ni mimi au ni huduma za intaneti katika Nairobi ambazo zimezorota leo tangu <a href="http://twitter.com/search?q=%23seacom">#seacom</a> ilipozinduliwa? Pengine uwezo wa mkubwa wa inteneti unaburudika na mandhari ya bahari kabla ya kutufikia”<br />
— <a href="http://twitter.com/mentalacrobatic/statuses/2804058608">mentalacrobatic</a>
</p></blockquote>
<p>Mengi ya mashaka juu ya Seacom yapo kwenye suala la bei: japokuwa baadhi ya wataalamu wa mambo wanadai kuwa gharama za upana wa masafa zitashuka kwa asilimia 90, wengine wanaamini kwamba makato ya gharama yanaweza yakawa madogo zaidi. <a href="http://www.kachwanya.com/?p=428">Kachwanya</a> anaandika:</p>
<blockquote><p>Katika dunia sawa gharama zinapaswa zishuke kwa zaidi ya asilimia 90, hivi sasa inawagharimu mawakala wa kutoa intaneti dola 6500  za Kimarekani (takriban Shilingi 487500 za Kenya) kwa kila kipimo cha Megabiti za upana wa masafa, lakini shika pumzi yako, usitarajie miujiza katika hili. Hivi karibuni Mkurugenzi Mtendaji Mkuu wa UUnet Tom Omariba alidai kuwa mikonga itashusha gharama kwa asilimia 20-30.</p></blockquote>
<p>Mwanablogu <a href="http://www.truekenyan.com/2009/07/23/oh-kenyans-we-have-been-duped-again/">TrueKenyan</a> guswa na suala la uwazi:</p>
<blockquote><p>
Seacom wamekataa katu kutuwekea wazi, sisi walaji wa intaneti, ni mawakala gani wa kusambaza intaneti walionunua upana wa masafa kutoka kwao. Hivyo bado tupo kizani na hatufahamu ni wapi tunapoweza kununua huduma ya intaneti yenye uhakika na kwa bei nafuu… kwa hiyo jambo pekee ninaloweza kufanya ni kuendelea na wakala wangu wa intaneti huku nikiitazama mashine wakati ikipakua kurasa kwa kasi inayoamua yenyewe huku nikiwaza kuwa siku moja ndoto yetu itatimia. </p></blockquote>
<p>Akitoa maoni katika blogu ya Mtanania <a href="http://issamichuzi.blogspot.com/2009/07/jk-azindua-kituo-cha-mkongo-wa-fibre.html">Issa Michuzi </a>[SW}, mdau pia anahofu juu ya gharama, japokuwa ana matumaini makubwa ya baadaye: </p>
<blockquote><p>Asanteni sana kwa huo mkonga. Sasa kutandaza fibre-optic cables kwenye miji mbalimbali tunaanza lini? Manake kuwa na inter-country connection wakati within the country hatuna connection nzuri bado gharama zitakuwa juu na kwa maoni yangu tutakuwa tuna-under utilise capacity ya hiyo under sea cable. For the moment, well done! For the future, we have to work had!</p></blockquote>
<p>Kwa <a href="http://jellyfishcoolman.wordpress.com/2009/07/24/seacom-goes-live/">Jellyfish</a>, ambaye anayatupilia mbali masuala ya gharama kwa kusema kuwa ongezeko la kasi la kiasi hicho na kiwango cha huduma mkwa kawaida huenda sambamba na ongezeko la bei, ujio wa Seacom ni jambo zuri:</p>
<blockquote><p>
Katika tukio lililoratibiwa na kutangzwa sana SEACOM iliwasha funguo ambayo mara moja ilieneza Terabiti za upana wa masafa katika kasi ya mwanga kupitia nyuzi za vioo zilizotengenezwa na kupigwa msasa katika kiwango cha hali juu. </p></blockquote>
<p>Na kwa mwanablogu wa Afrika Kusini <a href="http://twitter.com/akianastasiou/status/2797795511">Aki Anastasiou</a>, “Hii ni MB ndogo kwa talakilishi yangu ya mapajani, TB moja kubwa kwa Afrika.”</p>
]]></content:encoded>
			<wfw:commentRss>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/07/afrika-ujio-wa-mkonga-wa-seacom-wazua-mjadala/feed/</wfw:commentRss>
		<slash:comments>0</slash:comments>
		</item>
	</channel>
</rss>
