· Novemba, 2009

Habari kuhusu Mahusiano ya Kimataifa kutoka Novemba, 2009

Azerbaijan: Baada ya Hukumu ya Wanablogu wa Video

  23 Novemba 2009

Siku chache baada ya hukumu ya vijana wanaharakati wawili wa blogu za video huko Azerbaijan, wanablogu wengine wanaanza kuongea kwa sauti juu ya kifungo cha Adnan Hajizade na Emin Milli. Wanaharakati hawa wa mtandaoni watatumikia vifungo vya miaka miwili na mwingine miaka miwili na nusu gerezani baada ya mashitaka ambayo...

Misri na Aljeria: Pambano la Twita

Katika sehemu nyingi duniani, hakuna linalounganisha zaidi – au wakati mwingine kutenganisha – zaidi ya pambano la mpira wa miguu. Washabiki wa Misri na Aljeria, katika ulimwengu wote wa Waarabu na zaidi, walilidhihirisha hilo Jumamosi hii wakati timu zao zilipokwenda sambamba wakati wa kuwania kuingia fainali za Kombe la Dunia huko Afrika Kusini.

Misri: Haki ya Kijerumani kwa Marwa El Sherbini

Muuaji wa Marwa El-Sherbini, mwanamke wa Kimisri ambaye alichomwa visu mpaka kufa na muhamiaji mwenye asili ya Urusi na Ujerumani, Alex Wiens, ndani ya mahakama huko Ujerumani, amehukumiwa kifungo cha maisha, bila uwezekano wa kuachiwa mapema. Haki hatimaye imetolewa na muuaji anaadhibiwa, wanasema wanablogu wa Misri.