GlobalVoices katika

Ideas

Hifadhi ya mada · 26 jumbe


Habari mpya Kuhusu Ideas

6 Mei 2013

TEDXSão Tomé: Mkutano Wanukia São Tomé na Príncipe

TEDXSão Tomé

TEDXSão Tomé

Uandikishaji wa awali kwa ajili ya mkutano wa TEDXSão Tomé umezinduliwa rasmi. Mkutano huo una kaulimbiu inayosema “Visiwa Vimeunganishwa : São Tomé + Príncipe = Áfrika Vimeunganishwa na Ulimwengu” na utafanyika tarehe 20 Juni. Wasemaji katika mkutano huo waliothibitishwa ni pamoja: Dynka Amorim, Ismael Sequeira, Profesa Robert Drewes na Aoaní d'Alva. Tiketi linapatikana kwa Euro 20. Zaidi kuhusu mkutano huo tembelea ukurasa wa Facebook na tovuti [viungo vyote katika lugha ya Kireno].

23 Disemba 2012

Utambulisho wa Jamii ndogo ya Balkan

Face the Balkans subjects of stories

Picha ya mwonekano wa tovuti ya Balkans.

Waandishi vijana kumi na watano kutoka katika nchi zipatazo sita tofauti wametengeneza mfululizo wa masimulizi binafsi kuhusu masuala ya namna jamii zenye watu wachache (kwa mapana yake) zinavyoweza kuwakilishwa kutoka Bosnia na Herzegovina, Kosovo, Serbia, na Macedonia. Habari zinapatikana katika lugha za Kiingereza, Kijerumani, na Kifaransa katika mwonekano wa tovuti ya Balkans.

20 Novemba 2012

Mradi wa Tafsiri: Kauli ya Linda Uhuru wa Intaneti Ulimwenguni

GV Advocacy

Katika siku saba zijazo, Wafasiri wa Kujitolea wa Mradi wa Lingua wa taasisi ya Global Voices watakuwa wakitafsiri makala maalumu ambayo ni harakati ya utetezi unaofanywa na umma mtandaoni na...

10 Oktoba 2012

Je, Una Swali Lolote kwa Jimmy Carter?

Rais wa zamani wa Marekani Jimmy Carter anapokea maswali kupitia mitandao ya kijamii ya Facebook na Twita (#CarterQA) kama sehemu ya kuadhimisha miaka 30 ya Kituo cha Carter (Carter Center) kinachojishughulisha na “kupigania masuala ya amani na kupambana na magonjwa duniani kote”. Rais Carter atakuwa anayajibu maswali hayo kwa njia ya video tarehe 19 Oktoba, 2012.

30 Agosti 2012

Brazil: Mtoto wa Miaka 13 Aonyesha Matatizo ya Shule Kupitia Facebook

Diário de Classe [pt], ukurasa wa Facebook uliofunguliwa na Isadora Faber, aliye na miaka 13 na anayetokea Santa Catarina, Brazil, tayari umeonyesha kupendwa zaidi ya mara 176,000. Huku lengo lake likiwa ni “kuonyesha ukweli kuhusu shule za umma”, Isadora anaweka picha zinazoonyesha maeneo yanayohitaji kufanyiwa ukarabati katika shule yake pamoja na kutoa taarifa kuhusu matatizo mengine mengi ya jumla.

23 Juni 2012

Video jumbe
Kenya: Kilimo cha Bustani Mijini Chashika Kasi

Soma makala hii.

Nchini Kenya, wakazi wa mjijini wanajifunza mbinu mbalimbali za kulima mazao ya chakula kwa ajili ya matumizi binafzi na kwa ajili ya kuuza katika maeneo madogo. kwa watu wenye kipato kidogo au wasio na kipato, ukulima wa mijini unaweza kuwa ndiyo ufumbuzi wa kujihakikishia uwepo wa chakula. Video hizi zinaonyesha jinsi ambavyo chakula kinaweza kuzalishwa katika makasha na vifaa vingine vya kubebea kwa kutumia maeneo na rasilimali kidogo.

2 Februari 2011

Video jumbe
Misri: Wanawake Wanaoandamana Waenziwa Kwenye Mtandao

Soma makala hii.

Nafasi ya wanawake katika upinzani dhidi ya serikali unaoendelea nchini Misri imenasa macho ya wanablogu na raia wanaoeneza habari kwenye tovuti za mitandao ya kijamii.

17 Agosti 2010

China: Pato la Taifa Linaongezeka, Matumizi Katika Huduma za Jamii je?

Soma makala hii.

Tunaendelea kusikia kuwa uchumi wa China unaendelea kukua; je matumizi ya huduma za jamii yameongezeka? Akiba binafsi zinabaki kwenye benki, anaandika mwanablogu mmoja: kutokea hospitali mpaka shuleni mpaka malipo ya uzeeni, China haiwezi kujilinganisha.

13 Agosti 2010

Ufilipino: Maoni ya Wanablog Juu ya Elimu ya Ya afya ya Uzazi

Soma makala hii.

Mwaka huu wa masomo serikali ya Philippines inatekeleza mpango wa elimu ya uzazi kwenye shule za umma unaofadhiliwa na Umoja wa Mataifa kwa ajili ya watoto na vijana. Na wanablogu wametoa maoni juu ya suala hilo.

27 Machi 2010

Global Pulse 2010: Mwaliko wa kuzungumza na watoa uamuzi mtandaoni

Soma makala hii.

Kuanzia tarehe 29 hadi 31 Machi, vuguvugu linalojulikana kama Global Pulse 2010, yaani Mapigo ya Moyo ya Ulimwengu 2010, linakusudia kuwakusanya jumla ya watu 20,000 kupitia mtandao ili wafanya mazungumzo kuhusu mada mbalimbali kuanzia zinazohusu maendeleo ya binadamu hadi sayansi na teknolojia.

Sehemu za Dunia

Nchi

Lugha