GlobalVoices katika

Humanitarian Response

Hifadhi ya mada · 38 jumbe


Habari mpya Kuhusu Humanitarian Response

12 Februari 2013

Udhaifu wa Watawala wa Afrika unajionesha Mali?

Ousmane Gueye katika tovuti ya Mondoblog anaandika [fr] kuhusu kuchelewa kupeleka vikosi vya kijeshi kasikazini mwa Mali:

Kama tungekuwa tunasaiili matokeo ya watu wenye amani na huru kuingilia kati hali ya mambo nchini Mali, basi ni wazi kuwa kwa kuchelewa kupeleka vikosi vya ulinzi, nchi za Afrika zimewakosea wananchi wa Mali kwa mara nyingi…kelele zote za wakuu wa nchi lakini bado hawajaweza kutimiza lengo lolote waliloliweka wao kama hatua ya kupunguza nguvu ya Waslamu wenye msimamo mkali nchini Mali.

2 Januari 2013

Watu 60 Wauawa kwa Msongamano nchini Abidjan

Magogo ya miti yaliyokuwa yameanguka barabarani yanaonekana kusababisha msongamano mkubwa na ulioua watu 60 na kujeruhi wengine 49 wakati wa sherehe za kuukaribisha mwaka mpya mjini Abidjan, Côte d'Ivoire. Kutokana na ukweli kuwa eneo hilo halikuwa na mwanga wa kutosha inawezekana ndio sababu iliyochangia tukio hilo la msongamano ulisababisha mkanyagano wa watu.

Israel Yoroba jijini Abidjan anaripoti kuhusu msongamano huo wa kutisha [fr] wakati watu wengi wakiwa wamekusanyika kusubiri kushuhudia milipuko ya fataki kuashirika mwaka mpya katika wilaya ya Plateau. Alama habari #drameplateau ilianzishwa kutoa nafasi ya kupatikana kwa habari za wakati huo huo kuhusu tukio hilo la kusikitisha na namna ya kuwasaidia waathirika. Hili nijanga la tatu la namna hii tangu mwaka 2009 [fr] nchini Côte d'Ivoire.

10 Oktoba 2012

Je, Una Swali Lolote kwa Jimmy Carter?

Rais wa zamani wa Marekani Jimmy Carter anapokea maswali kupitia mitandao ya kijamii ya Facebook na Twita (#CarterQA) kama sehemu ya kuadhimisha miaka 30 ya Kituo cha Carter (Carter Center) kinachojishughulisha na “kupigania masuala ya amani na kupambana na magonjwa duniani kote”. Rais Carter atakuwa anayajibu maswali hayo kwa njia ya video tarehe 19 Oktoba, 2012.

27 Agosti 2012

Photos jumbe
Ufilipino: Mafuriko Yaathiri Vitongoji vya Jiji la Manila na Mikoa ya Karibu

Soma makala hii.

Mvua kubwa ilisababisha mafuriko katika vitongoji vingi ya jiji la Manila pamoja na majimbo ya jirani katika Kisiwa cha Luzon nchini Ufilipino. Mhariri wa Global Voices aliye huko Manila, Mong Palatino, anakusanya picha kutoka katika majukwaa mbalimbali ya habari za kiraia yanayoonyesha athari kubwa ya mafuriko hayo katika mji huo mkuu wa nchi.

10 Aprili 2011

Video jumbe
Japani: Tsunami yaathiri eneo la pwani, yaacha kila kitu kimeharibiwa

Soma makala hii.

Kufuatia tetemeko kubwa kuwahi kutokea nchini, Japani imekumbwa na tsumani mbaya zaidi iliyowahi kutokea. Watu wengi nchini kote wameganda kwenye luninga zao wakati vipande vya habari vinavyoonesha tsunami lenye urefu wa zaidi ya mita 7 kwenda juu likisomba magari na majengo.

20 Novemba 2010

Haiti: Kuokoa Maisha

“Idadi ya wagonjwa waliotibiwa katika siku 10 zilizopita ni 227″: matumaini ya kweli kwa haiti wanaeleza uzoefu wao wakati wanasaidia kupambana na ugonjwa wa kipindupindu.

9 Novemba 2010

Haiti: Video Inayookoa Maisha

Soma makala hii.

Mganga nayeishi jijini Fransisco ambaye pia ni mwanablogu Dkt. Jan Gurley amezuru Haiti mara mbili tangu lilipotokea tememeko la ardhi la Januari 12 ili kuwahudumia watu kwa kujitolea. Ziara yake...

18 Julai 2010

Video jumbe
Afrika ya Kusini: Dakika 67 za Mabadikio – Siku ya Mandela

Soma makala hii.

Nelson Mandela alitumikia kifungo cha miaka 27 jela kule katika Kisiwa cha Robben, Afrika Kusini. Kitu ambacho watu wengi hawajui ni kwamba Madiba (kama ambavyo wengi wanapenda kumwita huko Afrika ya Kusini) alitumia miaka 67 ya maisha yake katika kupiga vita ubaguzi wa rangi na umaskini. Jumapili hii Julai 18 2010, kutakuwa na maadhimisho ya miaka yake 92 - na pia Siku ya Mandela - siku ambayo watu duniani kote watajitolea dakika 67 ili kuifanya dunia iwe sehemu nzuri ya kuishi kwa wote.

3 Aprili 2010

Chile: Mchakato wa Ujenzi Mpya Baada ya Tetemeko la Ardhi

Soma makala hii.

Mwezi mmoja baada ya tetemeko baya kabisa nchini Chile, Rais Sebastián Piñera ametangaza mpango wa ujenzi mpya wa miundombingu ya nchi na majengo, akiwataka raia wa Chile kutoa mapendekezo jinsi gani mchakato huo utekelezwe na kusimamiwa.

14 Machi 2010

Moroko: Wafanyakazi wa Shirika la Misaada La Kikristu Wafukuzwa

Soma makala hii.

Wiki iliyopita, wafanyakazi 20 wa Kijiji cha Matumaini, makazi madogo ya yatima katika mji mdogo wa Moroko vijijini, waliondolewa (walifukuzwa) nchini bila onyo, kwa madai ya kuhubiri dini.

Sehemu za Dunia

Nchi

Lugha