Habari kuhusu Haki za Binadamu kutoka Aprili, 2014
Hadhi ya Wanawake Katika Jamii ya Kihindi Leo
Transhuman Collective (THC), mwanafunzi aliyepikwa na Soham Sarcar & Snehali Shah, ni mradi wa taaluma shirikishi unaongozwa na falsafa yaTranshumanism. Katika video hii iliyotengenezwa na kupandishwa kwenye mtandao wa YouTube na Transhumanism inaonyesha kuwa kunakosekana heshima ya msingi kwa wanawake katika jamii ya Kihindi iliyokithiri mfumo dume. Video hii inachangia...
Win Tin: Mfungwa wa Kisiasa wa Myanmar Aliyefungwa kwa Muda Mrefu Zaidi Afariki Dunia
Mwandishi wa habari na mwanaharakati Win Tin ni mmoja wa viongozi wa harakati za kutetea demokrasia.
VIDEO: Wanafunzi wa Iran Wavuruga Hotuba ya Mgombea Urais wa Chama Tawala
Wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Amirkabir kilichopo mjini Tehran, nchini Iran waliimba nyimbo zenye vibwagizo vinavyomwuunga mkono Mir Hussein Mousavi na Mehdi Karroubi, ambao ni viongozi wa vyama vya Upinzani nchini humo waliowahi kuongoza maandamano ya Green Movement.
Asilimia 20-40% ya Fedha Katika Sekta ya Maji Barani Afrika Hupotelea kwa Utoaji Rushwa
Mustapha Sesay, Balozi wa Uadilifu wa Afrika Magharibi aliandika kuhusu ufisadi katika sekta ya maji kwenye mtandao wa Waandishi wa Habari wa WASH wa Afrika Magharibi : Suala la upatikanaji wa maji safi na kwa bei nafuu ni haki ya kibinadamu lakini hii haijapewa kipaumbele inavyohitajika sana. Utoaji rushwa katika...
Mwanablogu wa Iran Aliyefungwa Aandika Barua Kuelezea Anavyoteswa
Mwanablogu anayefahamika kama Siamak Mehr ameandika barua ya wazi kutoka jela anakoishi kwenye chumba kidogo na wafungwa 40. Anatumikia kifungo cha miaka minne kwa kosa la kublogu
“Ni wa Kike!”: Kampeni ya Kukomesha Utoaji wa “Mimba za Kike” Nchini India na China
Tovuti ya MujeresMundi, inayoongozwa na mtaalamu wa mawasiliano anayeishi Peru na Ubelgiji Xaviera Medina, inahusika na kampeni ya kuelemisha watu kuhusu “Ni mtoto wa Kike” inakosudiwa kukomesha utoaji wa mimba za kike nchini India na China: Wasichana wanauawa mithili ya mauaji ya kimbari ya jinsia katika muongo mmoja kuliko watu...
Kwa nini Rwanda Inaituhumu Ufaransa Kusaidia Mauaji ya Kimbari ya 1994
Wakati Rwanda ikiwakumbuka waathirika wa mauaji ya kimbari yalitokea miaka 20 iliyopita, Rais Kagame anasema tena kuwa Ufaransa lazima “ikabiliane na ukweli mgumu” wa kukiri kushiriki kwenye mauaji hayo ya mwaka 1994 [fr]. Kama matokeo ya matamshi hayo, serikali ya Ufaransa imesusia matukio yote ya kukumbuka mauaji hayo na waziri...
Mazungumzo ya GV: “Mtandao wa Twita” wa Siri wa Kimarekani Nchini Cuba
Mpango wa siri wa Marekani wa kubadili utawala nchini Cuba wenye huduma ya ujumbe inayofanana na Twita iitwayo ZunZuneo sasa unaangaliwa kwa mashaka baada ya kuwepo kwa taarifa kuwa maelfu ya wa-Cuba walidanganyika kujisajili kupata huduma hizo. Je, kutakuwa na madhara kwa wanaharakati wa kidijitali duniani kote? Wengine wana mashaka...
Urabuni: Hijab na Ubaguzi wa Kimagharibi
Mwanablogu wa Mirsi Nadia El Awady anaandika posti ya blogu yake ambapo anahoji kama wanawake wanaovaa Hijabu wanabaduliwa kwenye nchi za magharibi ama la. Nadia, kama Mmisri alikulia Marekani na ameishi kwa kipindi kirefu Ulaya, anaelezea uzoefu wake kuhusu mwitikio alioupata kwenye nchi za Mashariki na Magharibi linapokuja suala la...
Amnesty International: ‘Mfululizo wa Ghasia ni Tishio la Utawala wa Sheria Nchini Venezuela’
Shirika la kutetea haki za binadamu, Amnesty International limetoa taarifa inayo weka kumbukumbu sawa “kuhusu madai ya uvunjifu wa haki za bindamu na unyanyasaji uliofanywa katika mukhtadha wa maadamano makubwa ya umma tangu mwezi Februari.” “Nchi hiyo iko kwenye hatari ya kuwa na mfululizo wa matukio ya ghasia kama hatua...