GlobalVoices katika

Human Rights

Hifadhi ya mada · 124 jumbe


Habari mpya Kuhusu Human Rights

4 Mei 2013

Ethiopia: Mwanablogu Ahukumiwa Miaka 18 Jela kwa “Kuvunja Katiba”

Soma makala hii. GV Advocacy

Mnamo Mei 1, Mahakama Kuu ya Ethiopia ilitoa hukumu kali kwa mwandishi aliyeshinda tuzo Eskinder Nega, ambaye sasa atatumikia kifungo cha miaka 18 jela. Mohamed Keita wa Kamati ya Kuwalinda Waandishi anasema, “Kushitakiwa na hatimaye kutiwa hatiani kwa Eskinder na waandishi wengine ni dalili za utawala unaoogopa maoni ya raia wake.”

Wabunge wa Ukraine Wataka Utoaji Mimba Upigwe Marufuku Kisheria

Soma makala hii.

Mapema mwezi Aprili, Wabunge watatu kutoka kambi ya Upinzani iitwayo“Svoboda” walipeleka mswada bungeni wenye lengo la kupiga marufuku utoaji mimba nchini Ukraine. Tetyana Bohdanova anataarifu mwitikio wa watumiaji wa mtandao kufuatia hatua hii ya Bunge la Ukraine.

16 Aprili 2013

Uturuki: Polisi Watumia Mabomu ya Machozi Kuwatawanya AkinaMama Waandamanaji

Soma makala hii.

Wafungwa wa kisiasa wa Kikurdi wamefikia siku yao ya 55 ya mgomo wa kula. Kuna mamia ya wafungwa wa kisiasa walio kwenye mgomo wa kula nchini Uturuki, na hii imesababisha maandamano mshikamano katika bara la Ulaya, na hususani ndani ya Uturuki. Mapema jana [4 Novemba 2012], wanawake ambao ni mama wa baadhi ya wafungwa wa kisiasa walifanya maandamano ya kukaa, na walijikuta wakipambana na mabomu ya machozi, pamoja na kunyunyuziwa maji ya kuwasha. Wa- Kurdi duniani kote wanapinga kimya kinachotumika kushughulikia adha yao.

15 Aprili 2013

Asasi za Kiraia za Urusi “Zakaguliwa” na Mwendesha Mashitaka

Soma makala hii. RuNet Echo

Wanaharakati wa DemVybor katika jiji kuu la eneo la Voronezh waliripoti kwenye blogu ya DemVybor[ru] kwamba Asasi Zisizo ki-Serikali zinakaguliwa na ofisi ya mwendesha mashitaka wa umma wa jiji hilo. Mashirika...

2 Machi 2013

Wa-Mauritania Wapinga Udhalilishaji wa Viwanja vya Tahrir Square

صورة من الوقفة نشرها حساب موريتانيا اليوم على فيسبوك

Mwandamanaji akisema “Tunapinga Udhalilishaji” picha ya Jarida la “Mauritania Today” kwenye mtandao wa Facebook.


Siku ya Jumanne Februari 12, 2013, kikundi cha wanaharakati wa ki-Mauritania kiliandaa [ar] maandamano mbele ya Ubalozi wa Misri jijini Nouakchott, mji mkuu wa Mauritania, kupinga udhalilishaji wa kijinsia na ubakaji ambao wanawake wa ki-Misri wamekuwa wakikumbana nao kwenye viwanja vya Tahrir jijini Cairo.

Tukio hilo la maandamano liliratibiwa na “Etkelmi” (Sema kwa kiarabu) [ar - fr], Asasi Isiyo ya Kiserikali inayopambana na ubakaji nchini Mauritania. Mekfoula Brahim anawapa heshima wale wote walioshiriki maandamano hayo [ar]:

شكرا لكم يا مواطنو ا العالم على وقفتكم امام السفارة المصرية فى انواكشوط لدعم نساء مصر اللائى يمارسن حقهن فى التظاهر السلمى فى مصر وعلينا جميعا القيام بوقفة اخرى احتجاجا على دعم الارهاب علنا من طرف الكثيرين والتأصيل له فى ثقافتنا المنفتحة

Asante sana wananchi wote duniani kote kwa kuandamana mbele ya Ubalozi wa Misri jijini Nouakchott kuwaunga mkono wanawake wa Misri wanaotumia haki yao ya kuandamana kwa amani nchini Misri. Tuanze kuandaa mandamano mengine kuwapinga wale (wengi) wanaounga mkono ugaidi na wale wanaojaribu kuuchukua utamaduni wentu wa uwazi.

18 Februari 2013

Vurugu Zinazofadhiliwa na Serikali Nchini Angola

Mwanablogu Claudio Silva anaandika kwenye makala yake Africa Ni Nchi kwamba mtazamo wa kina juu ya vurugu zinazofadhiliwa na serikali (kufukuzwa watu mijini na kupigwa kwa waandamanaji) unahitajika ili kuelewa video mbili zilizosambaa sana mtandaoni na kuleta sintofahamu kubwa nchini (tazama habari maalumu za Global Voices). Anaandika “vurugu za Angola zimetoka ngazi za juu: Serikali”.

12 Februari 2013

Udhaifu wa Watawala wa Afrika unajionesha Mali?

Ousmane Gueye katika tovuti ya Mondoblog anaandika [fr] kuhusu kuchelewa kupeleka vikosi vya kijeshi kasikazini mwa Mali:

Kama tungekuwa tunasaiili matokeo ya watu wenye amani na huru kuingilia kati hali ya mambo nchini Mali, basi ni wazi kuwa kwa kuchelewa kupeleka vikosi vya ulinzi, nchi za Afrika zimewakosea wananchi wa Mali kwa mara nyingi…kelele zote za wakuu wa nchi lakini bado hawajaweza kutimiza lengo lolote waliloliweka wao kama hatua ya kupunguza nguvu ya Waslamu wenye msimamo mkali nchini Mali.

14 Januari 2013

Mwanaharakati wa Pakistani Khudi Ali Auawa Katika Mlipuko wa Bomu

Soma makala hii.

Mnamo Januari 10, 2013 katika jiji la Quetta lililopo Kaskazini Mashariki mwa nchi ya Pakistani, watu 82 walipoteza maisha kwenye milipuko ya mabomu yaliyolenga eneo ambalo kimsingi lenye idadi kubwa ya Waislamu wa Shia jamii ya Hazara. Irfan Khudi Ali, mwanaharakati mashuhuri wa haki za binadamu ambaye bila kuchoka aliweka wazi uonevu wa kikabila unaofanywa kwa waShia wa Hazara nchini Pakistan, alifariki katika shambulio lililofuata. Kifo chake kimechochea watu kumpa heshima kwa juhudi zake kwa kuanzisha tena maandamano kupinga mauaji ya watu wa Shia nchini Pakistani.

11 Januari 2013

Mashoga Washambuliwa Kaskazini mwa Kameruni

Oscarine Mbozo’a anaripoti [fr] katika blogu ya L'Actu kuwa shoga mmoja akiwa ameambatana na mwenzi wake walizomewa karibu na soko mnamo tarehe 6, Januari 2013, mjini Maroua, Kaskazini mwa Kameruni:

Goche Lamine, mfanyabiashara wa madawa, alikamatwa na mwanafunzi wa shule ya sekondari aitwaye Sanda, mwenye umri wa miaka 17. Umati wa watu uliokuwepo sehemu hiyo baada ya kugutushwa na mtoto aliyekuwa akipiga kelele “samaroka! Samaroka (yaani mashoga katika lugha ya ki-Fulfulde), uliwakimbilia watu hao na kuanza kuwarushia mawe.

8 Januari 2013

Video jumbe
Mwaka Mpya na Mienendo ya Zamani Nchini Bahrain

Soma makala hii.

Wakati nchi mbalimbali ulimwenguni kote zikiukaribisha mwaka mpya kwa fataki na shamrashamra, serikali ya Bahraini iliandaa utaratibu wa aina yake kwa waandamanaji nchini humo. kwa bahati, watumiaji wa mtandao wa intaneti walikuwa tayari, kuonesha na kuweka kumbukumbu ya baadhi ya matukio kwa ajili ya kushuhudiwa na sehemu nyingine yote ya ulimwengu.

Sehemu za Dunia

Nchi

Lugha