<?xml version="1.0" encoding="UTF-8"?>
<rss version="2.0"
	xmlns:content="http://purl.org/rss/1.0/modules/content/"
	xmlns:wfw="http://wellformedweb.org/CommentAPI/"
	xmlns:dc="http://purl.org/dc/elements/1.1/"
	xmlns:atom="http://www.w3.org/2005/Atom"
	xmlns:sy="http://purl.org/rss/1.0/modules/syndication/"
	xmlns:slash="http://purl.org/rss/1.0/modules/slash/"
	>

<channel>
	<title>Global Voices in Swahili &#187; Health</title>
	<atom:link href="http://sw.globalvoicesonline.org/category/topics/health/feed/" rel="self" type="application/rss+xml" />
	<link>http://sw.globalvoicesonline.org</link>
	<description>Dunia inaongea, je unasikiliza?</description>
	<lastBuildDate>Wed, 02 Dec 2009 12:35:07 +0000</lastBuildDate>
	<generator>http://wordpress.org/?v=2.8.4</generator>
	<language>en</language>
	<sy:updatePeriod>hourly</sy:updatePeriod>
	<sy:updateFrequency>1</sy:updateFrequency>
			<item>
		<title>Afya Duniani: Siku ya Vyoo Duniani Yatoa Harufu</title>
		<link>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/11/afya-duniani-siku-ya-vyoo-duniani-yatoa-harufu/</link>
		<comments>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/11/afya-duniani-siku-ya-vyoo-duniani-yatoa-harufu/#comments</comments>
		<pubDate>Wed, 25 Nov 2009 10:46:39 +0000</pubDate>
		<dc:creator>j nambiza tungaraza</dc:creator>
				<category><![CDATA[Brunei]]></category>
		<category><![CDATA[Development]]></category>
		<category><![CDATA[English]]></category>
		<category><![CDATA[Environment]]></category>
		<category><![CDATA[Ethiopia]]></category>
		<category><![CDATA[Feature]]></category>
		<category><![CDATA[Gender]]></category>
		<category><![CDATA[Health]]></category>
		<category><![CDATA[India]]></category>
		<category><![CDATA[Oman]]></category>
		<category><![CDATA[Science]]></category>
		<category><![CDATA[Singapore]]></category>
		<category><![CDATA[Thailand]]></category>
		<category><![CDATA[United Kingdom]]></category>
		<category><![CDATA[Weblog]]></category>

		<guid isPermaLink="false">http://sw.globalvoicesonline.org/?p=731</guid>
		<description><![CDATA[Ingawa inaweza kusikika kama masihara, Siku ya Vyoo Duniani inatilia maanani kwenye suala ambalo si la mzaha linalowakwaza karibu nusu ya watu wote duniani – ukosefu wa vyoo na mfumo wa usafi.]]></description>
			<content:encoded><![CDATA[<em>Ilichapwa kwanza na<a href="http://globalvoicesonline.org/author/juhie-bhatia/">Juhie Bhatia</a>  &middot; Imetafsiriwa na <a href='http://sw.globalvoicesonline.org/author/j-nambiza-tungaraza/'>j nambiza tungaraza</a> &middot;  <a href='http://globalvoicesonline.org/2009/11/19/global-health-world-toilet-day-raises-a-stink/'>Angalia ujumbe mama</a></em> 
<br /><p><img alt="" src="http://globalvoicesonline.org/wp-content/uploads/2009/11/1019110937_99be0d6df3_m.jpg" title="Tiled Toilet" class="alignright" width="180" height="240" /><br />
Ingawa inaweza kusikika kama vile masihara, <a href="http://www.worldtoiletday.com/">Siku ya Vyoo Duniani</a> inatilia maanani kwenye suala ambalo si la mzaha linalowakwanza karibu nusu ya watu wote duniani – ukosefu wa vyoo na mfumo wa usafi.</p>
<p>Watu wanaweza kuwa wanaona aibu kuongea wazi kuhusu hili suala, lakini kila mmoja hujisaidia, kwenye choo au la. Siku ya Vyoo Duniani inasaidia watu kusherehekea umuhimu wa usafi na kuwaelimisha watu bilioni 2.5 ambao hawana vyoo na mfumo wa usafi wenye uhakika. Video hii iliyotengenezwa na asasi isiyo ya kibiashara WaterAid <a href="http://www.youtube.com/watch?v=-T2eH7zrDJg">inaonyesha</a> starehe ya kuwa na choo.</p>
<p>Kusherehekea kopo lako kunaweza kuonekana kama ujinga, lakini kutokuwa na kopo siyo tu kunaweza kukusababishia aibu, kukosa heshima na masuala mengine ya kiusalama, bali pia kunaweza kukusababishia magonjwa yanayoweza kuzuilika na hata kifo. Pale watu wanapokosa vyoo, wanalazimika kujisaidia mitaani kweupe, kwenye viwanja au vichochoroni. Matokeo? Uchafuzi wa maji ya kunywa na vyanzo vya chakula, jambo ambalo linapelekea hatari nyingi za kiafya. Ukosefu wa mfumo wa usafi ndiyo sababu kubwa ya maambukizi na huua <a href="http://worldtoiletday.com/about.html">watu milioni 1.8</a>, hasa watoto, kila mwaka. Hata nchi zenye vyoo vya kutosha huwa zinakabiliana na matatizo yanayotokana na vyoo vichafu vya umma mpaka utupaji majitaka unaoharibu njia za maji.</p>
<p>Vanilla, anayeblogu kwenye <em>Let&#39;s Look At It This Way</em> kutokea Singapore, <a href="http://whatsayyouvanilla.blogspot.com/2009/11/world-toilet-day.html">anasema</a> kuwa watu wanapaswa kutilia maanani vyoo:</p>
<blockquote><p> “ Ninajua kwamba hii ni mada chafu kwa watu wengi. Ni bahati mbaya kwamba hii mada bado ni ‘mwiko’ kuiongelea wazi na watu wengi hawana uelewa kuhusu ukubwa wa tatizo. Ninashindwa kuelewa ni kwa jinsi gain hii inaweza kuwa mada isiyo na maana wakati, kwa wastani, huwa tunakwenda chooni mara 2500 kwa mwaka, au mara 6-8 kwa siku. Wakati wa maisha yetu, hutumia muda wa miaka 3 vyooni.&#8221; </p></blockquote>
<p>Chini ya maandalizi ya asasi isiyo ya kibiashara <a href="http://worldtoiletday.com/wto.html">The World Toilet Organisation</a>, Siku ya Vyoo Duniani inasherehekewa dunia nzima kwa matukio mbalimbali. Ili kuuelimisha umma zaidi, wiki hii WaterAid <a href="http://wateraidnews.blogspot.com/2009/11/launch-of-new-iphone-application-brings.html">ilitangaza</a> uzinduzi wa zana mpya ya Kutafutia Vyoo nchini Uingereza ya simu za mkononi za iPhone. Zana hiyo ya bure inawasaidia Waingereza kutafuta choo cha umma kilicho karibu zaidi  wakati pia inawakumbusha jinsi walivyo na bahati ya kuwa na vyoo safi na salama. Tukio kubwa zaidi leo, linaloitwa <a href="http://worldtoiletday.com/squat/">Mchuchumao Mkubwa</a>, linawataka watu wasimame na wachuchumae kwa dakika moja katika sehemu za umma ili kuongeza utambuzi. <a href="http://www.flickr.com/groups/1216217@N24/">Picha</a> hizi zinaonyesha watu waliochuchumaa dunia nzima, pamoja <a href="http://www.flickr.com/photos/25532596@N04/4116769214/in/pool-1216217@N24">na hii ya</a> watoto wa chekechea huko Singapore:</p>
<p><img alt="" src="http://globalvoicesonline.org/wp-content/uploads/2009/11/4116769214_1b876f8640.jpg" title="Singapore Squat" class="aligncenter" width="500" height="273" /></p>
<p>Blogu inayotokea Brunei, <em>the world according to panyaluru </em>…, pia <a href="http://panyaluru.blogspot.com/2009/11/cut-paste-toilets.html">inaonyesha kuridhika</a> na vyoo kwa kuliweka suala hili kwenye muktadha sawia:</p>
<blockquote><p> “Fikiria ikiwa tunatembea mbele ya mlolongo wa maduka kule Kiulap au Gadong. Mara tu tumbo linaunguruma kama vile ambavyo haujawahi kusikia. Halisimami kukupa mapumziko. Linaunguruma na kuunguruma. Ngurumo. Taa ni ya manjano tayari kubadilika kuwa ya kijani. Lakini hakuna vyoo unavyoviona. Hakuna hata choo kimoja cha umma kwenye mlolongo wa maduka… ongezea pia kuwa hakuna maji, karatasi ya chooni, hakuna chochote! Hiyo inaweza kuwa siku mbaya zaidi katika maisha yako, jinamizi baya, au jinamizi baya zaidi ya yale yaliyowakuta watoto kwenye filamu za Elm Street. Katika siku hii, hebu na tuvienzi vyoo.”</p></blockquote>
<p>Ukiachilia mbali upande makini wa suala hili, watu wengi wametumia mzaha kuadhimisha siku ya Vyoo Duniani. Huko Uingereza blogu ya <em>London City Drains</em> imeweka chemsha bongo ya vyoo yenye maswali 10, wakati katika <a href="http://www.youtube.com/watch?v=zx2oVPjnUXs">video</a> hii mwalimu wa sekondari Matt Cheplic anaimba kuhusu siku hii.</p>
<p>Baadhi ya wanablogu wanasema kuwa vyoo pekee vinaweza visiwe jibu. Sandhya, anayeblogu kwenye <em>Maradhi Manni </em>nchini India, <a href="http://maradhimanni.blogspot.com/2009/11/big-squat-to-take-stand-on-sanitation.html">anasema</a> wanaume wengi hawatumii vyoo vilivyopo:</p>
<blockquote><p>Kwenye mji kama Chennai, ambako hali ya hewa ni ya joto kwa karibu miezi 10 ya mwaka, huwaona wanaume wanakojoakando ya barabara kila wakati. Wkati wanawake wanaweza kujidhibiti  na kwenda nyumbani kujisaidia, kwa nini wanaume hawawezi kufanya hivyo, sijui kwa nini. Kwa hiyo, kwanza watu wote wanabidi wapigwe faini kali kwa kufanya kosa hili (naam, ni kosa) pale pale wanapokamatwa. Nimewahi kuwaona wakifanya hivyo kwenye ukuta wa vyoo vya umma! Kule Srinagam, nimewahi kuwaona wakikojoa kwenye ukutra wa boma la hekalu pamoja na kuwa kila mtaa unaolizunguka hekalu una vyoo, ambavyo vilikuwa visafi, lakini vya kulipia!”</p></blockquote>
<p>Wakati ukosefu wa mfumo wa usafi unaathiri kila mtu, miiko inayozunguka suala la vyoo inawaathiri vikubwa wanawake zaidi ya  wengine. <a href="http://worldtoiletday.com/squat">Katika baadhi ya nchi</a>, staha huwalazimisha wanawake kufanya shughuli zao kwenye makonde kabla ya jua kuchomoza au kujizuia mpaka mpaka baada ya jua kuzama, jambo ambalo linasababisha madhara ya kiusalama na kiafya. Joanne Sprague, anayeblogu kwenye <em>Overturning Boulders</em> nchini India, <a href="http://overturningboulders.blogspot.com/2009/11/but-where-do-women-do-their-business.html">anabaini</a> kuwa wanawake hawapo kwenye mzunguko wa kwenda haja asubuhi mijini Chennai, wakati huko Ethiopia blogu ya <em>AN ADVENTURE IN ADDIS</em> <a href="http://anadventureinaddis.com/2009/11/17/world-toilet-day/">inabaini </a>hali kama hiyo pia:</p>
<blockquote><p>“Nimekuwa nikisikia mara nyingi juu ya ukosefu wa vyoo kwa wanawake au ukosefu wa vyoo kwa ujumla; kwamba wasichana wa rika la kuwa wali huko mashambani huamka saa 10 za alfajiri kwenda nje kwenye giza kufanya shughuli zao ili wasitaniwe na wavulana shuleni au huacha kwenda shule kabisa. Wanaume hukojoa kila mahali, sigara mkononi na kuna kuna dhana kuwa wanawake hawapaswi kufanya hivyo, kama wanafikiriwa hata kidogo… ninataka kuona bango kubwa kwa lugha ya Ki-Amhara linalosema “wasichana nendeni pia’ lenye picha ya mwanasesere anayevutia wa kike aliyeketi chooni.” </p></blockquote>
<p>Kusherehekea Siku ya Vyoo Duniani, mwanablogu Jonathan Stray, anawachukua wasomaji kwenda <a href="http://jonathanstray.com/world-toilet-day">ziara ya kimataifa ya vyoo </a>ambavyo ameshawahi kuvizuru, kuanzia Thailand na Uingereza mpaka Afrika Magharibi na Oman, na anahitimisha:</p>
<blockquote><p> “Sisi watu wa Magharibi na vyoo vyetu vya kuvuta na karatasi za chooni na chemchemi zinazong’ara ni tofauti na wengine wengi; wengine wote waliobaki hufikiri kuwa bafu ni sehemu iliyolowana, inayonuka, ikiwa wanayo hayo mabafu. Choo kizuri kinamaanisha kuwa pengine una kiwango kizuri cha maisha, kwa hiyo burudika na choo chako. Siku njema ya Vyoo Duniani!  </p></blockquote>
<p><em>Picha ya <a href="http://www.flickr.com/photos/nedrichards/1019110937/">choo cha vigae</a> imepigwa na <a href="http://www.flickr.com/photos/nedrichards/">nedrichards</a> kwenye Flickr, Haki Miliki Huru.</em></p>
]]></content:encoded>
			<wfw:commentRss>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/11/afya-duniani-siku-ya-vyoo-duniani-yatoa-harufu/feed/</wfw:commentRss>
		<slash:comments>0</slash:comments>
		</item>
		<item>
		<title>Afrika Kusini: Kikaragosi Kiliochoathirika na VVU Kwenye Kipindi cha Sesame Chaelimisha Kuhusu Ukimwi</title>
		<link>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/11/afrika-kusini-kikaragosi-kiliochoathirika-na-vvu-kwenye-kipindi-cha-sesame-chaelimisha-kuhusu-ukimwi/</link>
		<comments>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/11/afrika-kusini-kikaragosi-kiliochoathirika-na-vvu-kwenye-kipindi-cha-sesame-chaelimisha-kuhusu-ukimwi/#comments</comments>
		<pubDate>Mon, 23 Nov 2009 10:38:13 +0000</pubDate>
		<dc:creator>Christian Bwaya</dc:creator>
				<category><![CDATA[Arts & Culture]]></category>
		<category><![CDATA[Children]]></category>
		<category><![CDATA[Education]]></category>
		<category><![CDATA[English]]></category>
		<category><![CDATA[Feature]]></category>
		<category><![CDATA[General]]></category>
		<category><![CDATA[Health]]></category>
		<category><![CDATA[South Africa]]></category>
		<category><![CDATA[U.S.A.]]></category>
		<category><![CDATA[Weblog]]></category>
		<category><![CDATA[Youth]]></category>

		<guid isPermaLink="false">http://sw.globalvoicesonline.org/?p=696</guid>
		<description><![CDATA[Wakati kipindi cha watoto cha Mtaa wa Sesame (Sesame Street) kikisherehekea maadhimisho ya miaka 40 mwezi huu, kwa kizindua msimu wake  mpya leo, kikaragosi kizuri kinachovutia cha Muppet katika toleo la Afrika Kusini kinaendelea kusaidia kupambana na kuelimisha kuhusu VVU/UKIMWI. ]]></description>
			<content:encoded><![CDATA[<em>Ilichapwa kwanza na<a href="http://globalvoicesonline.org/author/juhie-bhatia/">Juhie Bhatia</a>  &middot; Imetafsiriwa na <a href='http://sw.globalvoicesonline.org/author/bwaya/'>Christian Bwaya</a> &middot;  <a href='http://globalvoicesonline.org/2009/11/11/south-africa-sesame-streets-hiv-positive-muppet-raises-awareness/'>Angalia ujumbe mama</a></em> 
<br /><p><img alt="" src="http://globalvoicesonline.org/wp-content/uploads/2009/11/Kami22.jpg" title="Kami" class="alignright" width="200" height="260" /><br />
Wakati kipindi cha watoto cha <a href="http://www.sesamestreet.org/home/">Mtaa wa Sesame</a> (Sesame Street) kikisherehekea maadhimisho ya miaka 40 mwezi huu, kwa kizindua msimu wake  mpya leo, kikaragosi kizuri kinachovutia cha Muppet katika toleo la Afrika Kusini kinaendelea kusaidia kupambana na kuelimisha kuhusu VVU/UKIMWI. </p>
<p>Wakati kipindi cha Sesame Street kinatazamwa katika zaidi ya <a href="http://www.sesameworkshop.org/newsandevents/sesameupdates/sesame_40thbirthday">nchi 140</a>, kila toleo huzungumzia masuala yanayotokea kwenye jamii husika na kwa kumtumia vikaragosi tofauti. <a href="http://muppet.wikia.com/wiki/Kami">Kami</a> mwenye rangi ya Njano-dhahabu alionekana kwa mara ya kwanza kwenye kipindi mwenza cha Sisame Street cha Afrika Kusini kinachoitwa <a href="http://www.schooltv.co.za/TakHome.htm">Takalani Sesame</a>, mwaka 2002 kujibu matatizo ya nchi yanayohusiana na UKIMWI. Kama kikaragosi cha kwanza duniani chenye VVU, kinasaidia kuwaelimisha watoto kuhusu ugonjwa na kushughulikia masuala yanayohusiana na kuwa mwathirika wa UKIMWI. Jina la Kami <a href="http://www.sesameworkshop.org/aroundtheworld/southafrica">linatoka</a> kwenye neno la kiSetswana “Kamogelo”, lenye maana ya “kukubalika.” Sunshinestar110, anayeblogu kwenye <em>U dont Like My Opinion&#8230;That’s Fine!</em> <a href="http://thatsfine2009.blogspot.com/2009/11/happy-birthday-to-you.html">anazungumzia zaidi</a> kuhusu Kami:</p>
<blockquote><p>“Kami ni mwathirika wa VVU mwenye afya, yatima wa miaka mitano mwenye bashasha ambaye ana aibu kidogo lakini huchangamka akijongelewa kwa njia ya kirafiki, pia anajua mengi kuhusu Virusi vya UKIMWI, alimpoteza mama yake kwa ugonjwa huo. Kami alipozinduliwa, akiwa na nywele zake za kahawia na pia alivaa fulana, na kutembea kwenye mtaa wa Susame na kujiuliza huku akihofu kama wenyeji watataka kucheza nae. Hakuwa na haja ya kuogopa kwa sababu vikaragosi vingine vilimpokea kwa bashasha”</p></blockquote>
<p>Kami aliletwa kuwasaidia watoto wengi wa Afrika Kusini wanaotaabika na janga la VVU/UKIMWI. Inaaminika kuwa Afrika Kusini ina idadi kubwa zaidi ya watu walio na VVU duniani – inakadiriwa kuwa watu <a href="http://www.unaids.org/en/CountryResponses/Countries/south_africa.asp">milioni 5.7</a> Kwa makadirio, kati ya walioathirikia, 280,000 ni watoto wa umri wa miaka chini ya 14 na kuna yatima milioni 1.4 nchini kutokana na UKIMWI. Zaidi ya madhara ya kimwili ya kuwa na VVU, vilevile kuna unyanyapaa na miiko inayotokana na kuwa na ugonjwa, ambayo husababisha ugumu kwa watu kupata matibabu stahiki na msaada. Takalani Sesame, ambayo inajumuisha lugha zote rasmi 11 za Afrika Kusini, inajaribu kuwasaidia watoto kuyatazama masuala haya kwa ujasiri kupitia Kami.</p>
<p>Hata hivyo, kulikuwa na mkanganyiko wakati Kami alipoanza kuonyeshwa, hasa hasa nchini Marekani, ambapo wengi walikasirishwa na kuwa kipindi cha watoto kinanamchezesha mhusika mwenye VVU. <em>Haven on Earth</em> <a href="http://haven-on-earth.spaces.live.com/blog/cns!C13DE188EF218F14!382.entry?sa=500695506">anafafanua</a> mjadala huo:</p>
<blockquote><p>“Ingawa ilitaarifiwa kuwa ujio wa Kami kwenye kipindi cha Sesame Street nchini Afrika Kusini ulikuwa unakaribishwa.(Nina wakati mgumu kukubaliana na ukweli huu kwa sababu kiwango kikubwa cha kukataa bado kipo), kulikuwa na mkanganyiko ulio wazi hapa Marekani. Ninakumbuka kusoma kuhusu suala hili (hii ni sababu ya mimi kufurahia kukutana na kipindi kikirushwa kutokea Afrika Kusini – nisingelifikiria kukitafuta). Iliondokea kuwa kundi la wabunge wa Congress wa chama cha Republican walituma barua kwa Rais wa Shirika la Utangazaji la Umma (PBS) linalorusha kipindi cha Sesame Street. Barua ilidai kwamba mipango ya kuleta mhusika kama huyo ambaye ni mwathirika wa UKIMWI nchini Marekani haikuwa sahihi, kwa kuzingatia umri wa watazamaji. Walipendekeza kwamba hatua hiyo ingeathiri ufadhili wa umma kwa Shirika hilo (PBS).”</p></blockquote>
<p>Kami hajawahi kuonekana kwenye kipindi cha Sesame Stree cha Marekani, ingawa amedhihirisha kuwa mhusika aliyefanikiwa sana kwenye kipindi cha Takalani Sesame na zaidi. Mwaka 2003, UNICEF <a href="http://www.unicef.org/media/media_16631.html">ilimteua</a> kuwa “Shujaa wa Watoto” duniani. Katika <a href="http://www.youtube.com/watch?v=9eXlNn-C8BY">video</a> hii, anaungana na Rais wa zamani wa Marekani Bill Clinton kutoa ujumbe kuhusu VVU/UKIMWI. Jamie, anayeblogu kwenye <em>No day but Today</em>&#8230;, <a href="http://phaino.blogspot.com/2006/12/world-according-to-sesame-street.html">anajadili</a> mafanikio mengine ya Kami:</p>
<blockquote><p> “Kwa sababu watoto wengi wa Afrika Kusini wanamfahamu mtu fulani mwenye UKIMWI, mhusika huyo amekuwa shujaa wa taifa, anayependwa na watu wa nchi hiyo. Kami ameonekana kwenye Umoja wa Mataifa na Benki ya Dunia na alihojiwa na Katie Couric. Ameteuliwa kuwa balozi wa UNICEF wa watoto na ameonekana kwenye vipande vya onyesho la Takalami pembeni mwa Desmond Tutu na Nelson Mandela.”</p></blockquote>
<p>Pamoja na mafanikio ya Kami, wanablogu wengine bado wanaamini kuwa si mhusika sahihi kwa toleo la Kimarekani la Sesame Street. Emily Meyer, anayeblogu kwa ajili ya darasa lake la heshima, <a href="http://hons101fall09eem.blogspot.com/2009/10/kami-hiv-muppet.html">anasema</a>:</p>
<blockquote><p>“Ingawa ni muhimu kwa Wamerekani kufahamu kuhusu VVU/UKIMWI na hatari ya ugonjwa wenyewe, nadhani kuwafundisha watoto katika umri wa miaka miwili na mitatu ni kwenda mbali sana. Watoto wadogo kiasi hiki hawataweza kuelewa kuhusu VVU na hawataelewa madhara yake. Kama Kami alitakiwa aletwe Marekani kama njia kueneza elimu na kudhibiti UKIMWI, sidhani kama matokeo yaliyokusudiwa yangetokea&#8230;Watoto nchini Marekani hawalazimishwi kuhusika na masuala ya UKIMWI katika umri huo mdogo. Nadhani wakati sahihi kwa watoto nchini Marekani kujifunza kuhusu hatari ya virusi vya UKIMWI ni wanapokuwa wakubwa, kadri ya miaka kumi ama kumi na moja au wakati mwanafunzi anapoanza kujihusisha na vitendo vya mapenzi kimwili”</p></blockquote>
<p>Bado, wanablogu wengi, kama huyu hapa <a href="http://beckyluz.wordpress.com/2008/12/16/kami-the-hiv-positive-muppet/">anayeandika kwenye</a> <em>Muppets and History</em>, anamwona Kami kama mfano mwingine wa namna Sesame Street inavyosukuma mipaka. Wengine <a href="http://joburgjoblog.blogspot.com/2006/03/celebrating-aids-research.html">wanaonyesha upendo</a> wao kwa kikaragosi huyo na ujumbe anaowaletea watoto. Na wengine wanadhani anatakiwa atumike kwenye matoleo mengine ya Sesame Street. Katika blogu yake binafsi, Steisha Pintado <a href="http://steishapintado.wordpress.com/2008/12/18/final-grades-kami/">anasema</a>:</p>
<blockquote><p>“Anawaonyesha watoto kwamba ni sawa kumkumbatia mtu mwenye virusi vya UKIMWI, na anaeleza nini cha kufanya anapokuwa na kidonda kwenye kidole chake au kama umejikata mwenyewe. Anaifundisha hadhira ya watoto wadogo kuhusu kukabiliana na kuumwa na kupotelewa&#8230;.Ingawa ngono huwa haitajwi kamwe katika kuzungumzia hali ya Kami, watu wengine wamesema kuwa kuwepo kwa mhusika mwenye virusi vya UKIMWI lisingekuwa jambo sahihi kwa hadhira ya watazamaji wadogo. Mbunge mmoja hata alidai kuwa Warsha ya Sesame ingepoteza msaada wa kifedha kutoka serikalini kama ingerusha kipindi chenye mhusika huyo kwenye nchi yetu. Inashangaza kusikia maneno haya. Wazazi wanatumia muda mfupi (na unaopungua kila siku) na watoto wao, na wanaruhusu runinga kuwaelimisha zaidi na zaidi. Ni wazi wazazi wengi hawawafundishi watoto wao namna ya kuyakabili masuala nyeti  ya uelewa na kukubalika. Wazazi tayari wamewaruhusu Warsha ya Sesame kuingiza suala la kukubalika kwa wale wenye ulemavu na kuugua, na pia kwa wale wenye rangi na dini tofauti. Je, hii ina tofauti gani? </p></blockquote>
]]></content:encoded>
			<wfw:commentRss>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/11/afrika-kusini-kikaragosi-kiliochoathirika-na-vvu-kwenye-kipindi-cha-sesame-chaelimisha-kuhusu-ukimwi/feed/</wfw:commentRss>
		<slash:comments>0</slash:comments>
		</item>
		<item>
		<title>Ujauzito na Magereza: Afya na Haki za Wanawake Magerezani</title>
		<link>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/11/ujauzito-na-magereza-afya-na-haki-za-wanawake-magerezani/</link>
		<comments>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/11/ujauzito-na-magereza-afya-na-haki-za-wanawake-magerezani/#comments</comments>
		<pubDate>Thu, 05 Nov 2009 13:24:11 +0000</pubDate>
		<dc:creator>Christian Bwaya</dc:creator>
				<category><![CDATA[Americas]]></category>
		<category><![CDATA[Argentina]]></category>
		<category><![CDATA[Brazil]]></category>
		<category><![CDATA[Conversations for a Better World]]></category>
		<category><![CDATA[East Asia]]></category>
		<category><![CDATA[Eastern & Central Europe]]></category>
		<category><![CDATA[Ecuador]]></category>
		<category><![CDATA[English]]></category>
		<category><![CDATA[Feature]]></category>
		<category><![CDATA[General]]></category>
		<category><![CDATA[Health]]></category>
		<category><![CDATA[Human Rights]]></category>
		<category><![CDATA[Humanitarian]]></category>
		<category><![CDATA[Laos]]></category>
		<category><![CDATA[Peru]]></category>
		<category><![CDATA[Photography]]></category>
		<category><![CDATA[Russia]]></category>
		<category><![CDATA[Spain]]></category>
		<category><![CDATA[Spanish]]></category>
		<category><![CDATA[U.S.A.]]></category>
		<category><![CDATA[Video]]></category>
		<category><![CDATA[Weblog]]></category>
		<category><![CDATA[Western Europe]]></category>

		<guid isPermaLink="false">http://sw.globalvoicesonline.org/?p=493</guid>
		<description><![CDATA[Mapambano bado yanaendelea kuhakikisha haki za binadamu kwa wanawake wajawazito duniani pote, ni inaelekea kwamba katika mchakato huo, wanawake waliopo magerezani wanasahauliwa. Je ni hatua zipi zilizochukuliwa kuhakikisha kuwa nao wanaangaliwa kwa utu, kwa kuzingatia uhai wanaoubeba.]]></description>
			<content:encoded><![CDATA[<em>Ilichapwa kwanza na<a href="http://globalvoicesonline.org/author/juliana-rincon-parra/">Juliana Rincón Parra</a>  &middot; Imetafsiriwa na <a href='http://sw.globalvoicesonline.org/author/bwaya/'>Christian Bwaya</a> &middot;  <a href='http://globalvoicesonline.org/2009/10/24/pregnancy-and-prisons-womens-health-and-rights-behind-bars/'>Angalia ujumbe mama</a></em> 
<br /><p><img alt="" src="http://globalvoicesonline.org/wp-content/uploads/2009/10/2044749780_4ade9e2e3f-300x225.jpg" title="2044749780_4ade9e2e3f" class="aligncenter" width="300" height="225" /></p>
<p><strong>Je, wanawake wote wajawazito wanastahili haki sawa za binadamu, au wanawake wajawazito walio jela huziacha haki hizo? </strong></p>
<p>Kuna maswali machache yanayokuja akilini kuhusu haki ya mwanamke mjamzito kuishi na kumlea mwanae anapokuwa kapatikana na hatia kwa kosa la jinai la namna fulani:<br />
•	Inakuwaje kwao wanapokuwa wajawazito na kupata mtoto wakiwa gerezani?<br />
•	Je, wanapaswa kuwa kipaumbele wakati kuna wanawake wengine nje ya vyuo vya mafunzo bila msaada wa kitabibu?<br />
•	Je, ujauzito unapaswa kuwa juu ya hali nyinginezo za kisheria kumhakikishia mwanamke mjamzito haki zake za kibinadamu? </p>
<p><strong>Marekani: wanawake walio kwenye uchungu wa kuzaa hawatafungwa tena minyororo.  </strong></p>
<p>Je unaweza kufikira mwanamke akijifungua huku mikono yake ikiwa kwenye pingu na miguu yake ikiwa imefungwa na minyororo kwenye kitanda? <a href="http://www.rhrealitycheck.org/user/malika-sadaa-saar">Malika Saada Saar</a>, mwanzilishi na Mkurugenzi Mtendaji wa <a href="http://www.rebeccaproject.org/">Mradi wa Rabecca kwa Haki za Binadamu</a>, <a href="http://www.rhrealitycheck.org/blog/2009/10/06/in-labor-and-in-chains">anatuelezea</a> kuhusu kitendo hiki ambacho bado kinatokea nchini Marekani, ambapo wanawake wajazito wanaotumikia kifungo wamekuwa wakifungwa minyororo wakati wa uchungu na kujifungua na kuwa hiki ni kitendo kilichozoeleka katika baadhi ya magereza (ya kurekebishia tabia), ingawa ni hatari kwa afya ya mama na mtoto. Ifuatayo ni video ya mahojiano yaliyoambatanishwa kwenye makala iliyoandikwa kwa ajili ya mradi wa <em>RH Reality Check</em>, jamii ya mtandaoni kuhusu afya na haki ya uzazi na jinsia inatupa taarifa na uchambuzi kwa afya ya uzazi:</p>
<p><object width="425" height="344"><param name="movie" value="http://www.youtube.com/v/CWj1uHdxnt8&#038;color1=0x234900&#038;color2=0x4e9e00&#038;hl=es&#038;feature=player_embedded&#038;fs=1"></param><param name="allowFullScreen" value="true"></param><param name="allowScriptAccess" value="always"></param><embed src="http://www.youtube.com/v/CWj1uHdxnt8&#038;color1=0x234900&#038;color2=0x4e9e00&#038;hl=es&#038;feature=player_embedded&#038;fs=1" type="application/x-shockwave-flash" allowfullscreen="true" allowScriptAccess="always" width="425" height="344"></embed></object><br />
<strong><br />
Kitu gani hutokea kwa mtoto mchanga wa wa mfungwa baada ya kuzaliwa?</strong></p>
<p>Nchi mbalimbali zina kanuni tofauti kuhusiana na watoto magerezani. Kwa mfano, nchini Argentina, kwa mujibu wa <em>Ajintem</em>, chombo cha mawasiliano cha taarifa za uhamamiaji,  <a href="http://portal.ajintem.com/archivo/80-argentina-prision-domiciliaria-para-embarazadas-y-madres.html">sheria ilipitishwa</a> mwaka uliopita ikifafanua kwamba wanawake wajawazito, wanawake wenye watoto wadogo chini ya miaka mitano na wale wenye watoto walemavu wangenufaika na mpango wa kutumikia kifungo chao makwao chini ya ulinzi wa nyumbani. Sheria hii ingewanufaisha si tu akina mama, ambao kwa kuwa gerezani wasingepata huduma za afya wakati wa ujauzito, lakini pia (ingemnufaisha) mtoto, ambaye angelelewa ama katika mazingira yasiyo salama yanayokosa uhuru na upungufu wa udhibiti wa afya na chakula, au wangelelewa mbali na mama, na hivyo kusababisha mlolongo wa matatizo mengine. Hata hivyo, ujumbe ni kwa ajili ya mahakimu kufuatilia kiini cha sheria na kutoa ruhusa hii kwa wanawake wale ambao hawahusishwi na mashitaka ya jinai ya matumizi ya nguvu, kuhakikisha kwamba idadi kubwa ya raia iliyobaki haiuchukulii ujauzito kama kadi ya kumtoa mtu jela bure.</p>
<p>Katika visiwa vya Canary, kwa mujibu wa blogu ya <em>Prisiones y penas</em>, ambayo huandika kuhusu habari zinazohusu jela na magereza, wanawake wanaruhusiwa <a href="http://prisionesypenas.blogspot.com/2009/09/detenidas-con-hijos-en-carceles.html">kuishi na watoto wao hadi umri wa miaka mitatu</a> ndani ya selo zao, lakini wakiwa pamoja na wafungwa wenzao, kitu ambacho sio mazingira mazuri sana kwako. Kwa hiyo, wanawake wajawazito au wanawake wenye watoto wenye umri wa chini ya miaka 3 huambiwa kuhusiana na kuingia kwenye magereza kuwa si vizuri kwa mtoto kukualia gerezani, na hupewa uchaguzi wa kumpeleka mtoto kwa wanafamilia wengine. Hali ni hii hii huko <a href="http://www.reuters.com/article/worldNews/idUSTRE5085ZV20090109">Peru</a> na <a href="http://russiatoday.com/Top_News/2009-07-27/russia-s-prison-born-children-marked-for-life.html">Urusi</a>. Nchini Marekani, kuna magereza mawili tu yenye kuruhusu jambo hili, huko New York na Nebraska, <a href="http://www.amnestyusa.org/women/custody/toomuchtime/pt_02/e_moms.html">kama ilivyoonyeshwa na mpiga picha maarufu Jane Evelyn Atwood</a> kwenye insha ya picha zake tatu kwa ajili ya <a href="http://www.amnestyusa.org/women/custody/toomuchtime/"><em>Shirika la kimataifa la Amnesty International</em>, inayoitwa <em>Too Much Time</em></a>, ambapo alitembelea dazani nyingi za magereza kote duniani kurekodi na kuweka kumbukumbu za maisha ya wafungwa.</p>
<p>Kwa nini mfumo wa magereza nchini Marekani hauruhusu, kwa ujumla, wanawake wenye watoto kubaki nao? Atwood anaeleza kwamba kwa sababu ya mazingira ufungwa, hairuhusiwi. Kwenye <a href="http://prisonphotography.wordpress.com/2009/10/07/women-behind-bars-jane-evelyn-atwoods-too-much-time/"><em>blogu ya Prison Photography</em> wanaelezea madai haya</a>: </p>
<blockquote><p>Watoto hawahusishwi kwenye magereza yote isipokuwa mawili tu nchini Marekani. Tishio la usalama linatajwa kama sababu: mtoto ndani ya gereza ni dhaifu na atakuwa shabaha ya malengo maovu siku zote. Madai yanaonekana kuwa hayana maana kwa kiasi fulani kwa unapofananisha na mifumo ya adhabu kwa nchi nyinginezo.</p></blockquote>
<p>Insha ya Atwood kwenye wavuti ya <em>Amnesty International</em> inaonyesha mambo mawili, sehemu inayohusu taratibu za kujifungua huku umefungwa minyororo kama yalivyoelezwa kwenye <a href="http://www.amnestyusa.org/women/custody/toomuchtime/pt_02/f_vanbab.html">Mtoto wa Vanessa</a> na pia inaonyesha jambo jingine kuhusu mfumo wa magereza na umama, kwa kutumia picha za wanawake wakati mpigapicha akisoma insha kuhusu uzoefu wake wa kutembelea magereza huku akipiga picha. </p>
<p><strong>Ujauzito kama zana ya mapatano? </strong></p>
<p>Kwa nini haki za wanawake wajawazito gerezani zinatatanisha? Katika  <em>Russia Today</em>, idhaa ya matangazo ya Kirusi, <a href="http://russiatoday.com/Top_News/2009-07-27/russia-s-prison-born-children-marked-for-life.html">mada hii inatajwa</a> panapojadiliwa suala la watoto kuzaliwa na kulelewa katika mfumo wa magereza wa Kirusi:</p>
<blockquote><p>Wenye kutilia mashaka (suala hili) wanadhani akina mama wengine hupata ujauzito kwa makusudi ili tu kurahisisha maisha huko gerezani. Ruhusa ya kwenda hospitali, halafu kuwa na ratiba iliyojaa muda mwingi na mwanao –ni afadhali kuliko kukaa kwenye seli ya magereza, wanadai. </p></blockquote>
<p>Na kuna wanawake ambao wanaona kwamba kuwa na mimba ni njia pekee ya kukwepa hukumu, kama ilivyotokea mwezi Juni, pale mwanamama wa Kiingereza aliwekwa ndani na kuhukumiwa kifo huko Laos kwa sababu ya kusafirisha madawa ya kulevya akapata ujauzito gerezani na akanusurika kunyongwa, kwa sababu serikali ya Laos isingemnyonga mwanamama mjamzito. <a href="http://www.dailyexpress.co.uk/posts/view/105278/No-firing-squad-for-girl-who-fell-pregnant-in-jail">Madai yaliyotolewa </a>kwa mujibu wa jarida la Kiingereza la <em>Daily Express</em>, ni kwamba alipata ujauzito kwa kupandikiziwa mbegu za kiume ‘ili kupata hukumu nyepesi zaidi” </p>
<p><strong>Kwa maneno yao: Wanawake wanaeleza kuhusu watoto wao na maisha ya gerezani</strong></p>
<p>Geraldin Rodríguez, Mwajentina aliye kwenye jela za Ecuador kwa sababu ya biashara ya madawa ya kulevya anamueleza <a href="http://marcosbrugiati.blogspot.com/2009/07/carcel-de-mujeres.html">Marcos Brugiati</a>, mwandishi mshiriki katika chapisho la mtandaoni linalohusiana na masuala ya sanaa liitwalo <em><a href="http://www.indexarte.com.ar/noticias/562/las-rejas-de-la-carcel-el-arte-de-la-espera.htm">Plastica-Argentina</a></em>, masimulizi kuhusu kuigiza na kufanya maonyesho ndani ya jela, kupata ujauzito gerezani na kumpata mwanae. Aliruhusiwa kuwa na mwanae, lakini akaamua kwamba mwanae anahitaji kukua akiwa mtu huru:</p>
<blockquote><p> “Decidí que salga para vivir, tenía miedo que sufra de grande los traumas que hoy tengo. Se lo llevó al año mi hermano quien se hice cargo con su esposa”.</p></blockquote>
<div class="translation">Niliamua aondoke ili aishi, nilikuwa na wasiwasi angeteswa na msongo wa mawazo nilionao leo. Baada ya mwaka kaka yangu alimchukua na anamtunza kwa kushirikiana wa mke wake. </div>
<p>Juvinete yuko kwenye <a href="http://www.nortecastilla.es/20080908/vida/quedarse-embarazada-prision-irresponsable-20080908.html">gereza la Kihispania</a>, na alikuwa mjamzito wakati alipofungwa kwa kusafirisha madawa ya kulevya. Anasimulia habari zake kwenye gazeti la kanda huko Uhispania linaloitwa <em><a href="http://www.nortecastilla.es/20080908/vida/quedarse-embarazada-prision-irresponsable-20080908.html">NorteCastilla</a></em>. Miaka mitatu baada ya kujifungua mwanae akiwa gerezani, mwanae ilibidi aondoke, na alipelekwa kwa familia ya kufikia. Juvinete humuona mwanae huyo wa kike kila baada ya siku 15 na kila miezi miwili hupata ruhusa ya wiki mbili kukaa na mwanae. Hata hivyo, mambo hayaonekani kuwa mazuri sana: kuna uwezekano kwamba Juvinete atapelekwa Brazil alikozaliwa, na anahofia matokeo ya mabadiliko haya kwa mwanae. Anao ushauri kwa mwanamke yeyote anayeamua kupata ujauzito akiwa jela:</p>
<blockquote><p>-Intento convencerlas para que no se queden en estado dentro porque ver a un niño privado de libertad es muy duro, es irresponsable. Ellos no tienen que pagar nuestros errores.</p></blockquote>
<div class="translation">
Ninajaribu kuwashawishi wasipate ujauzito wakiwa bado ndani kwa sababu kumuona mtoto akikosa uhuru wake ni vigumu sana, ni kutokuwajibika. (Watoto wanaozaliwa jela) wasilipie gharama ya makosa yetu</div>
<p>.  </p>
<p>Kwenye wavuti ya <em><a href="http://www.womenandprison.org/motherhood/kebby-warner.html">Woman and Prison</a></em>, iliyojikita katika kuyatazama maisha ya wanawake wakiwa kwenye mifumo ya magereza , <a href="http://www.womenandprison.org/motherhood/kebby-warner.html">mfungwa Kebby Warner anaongelea ujauzito wake</a> mwenyewe alipokuwa akitumikia kifungo kwenye gereza la Kimarekani, na jinsi alivyotendewa wakati wa ujauzito wake, utungu na baadae, wakati alipokuja kunyang’anywa mwanae. Hapa ni muhtasari anapoandika kuhusu hatua za kujifungua: </p>
<blockquote><p>Wakati wa utungu, hakuna mtu anaruhusiwa kuwa kwenye chumba cha kujifungulia. Familia yangu wala haikujua kwamba nilikuwa ninajifungua au nimempata (mwanagu) mpaka nilipokuwa nimetoka hospitali. Wakati huo wa siku tatu baadhi ya walinzi walikuwa ndani ya chumba, lakini muda mwingi, wakati wauguzi walipowaomba kukaa nje ya mlango, walitii. Nimesikia simulizi za kutisha za wanawake wakifungwa kwa mnyororo kwenye kitanda cha uzazi. Ninashukuru kwa kutokukumbana na hali hiyo. Wauguzi wengi walinitendea kama binadamu badala ya mfungwa.</p></blockquote>
<p>Unaweza kusoma shuhuda zaidi kuhusu kukua na mzazi gerezani na madhara mbalimbali ambayo kufunga wanawake kunaweza kuyawasababisha kwa watoto wao <a href="http://www.womenandprison.org/motherhood/index.html">kwenye Wanawake na Magereza</a>.</p>
<p>Kwa hiyo unafikiriaje? Kwa wanawake wajawazito duniani kote kutokupata huduma za afya za namna yoyote, je jitihada zaidi zinahitajika kuwanufaisha wanawake walio gerezani? Je, kuna tofauti kati ya wanawake wanaotumikia kifungo kwenye magereza (ya mafunzo) na wale wanaoishi nje? Je, ni lazima kuwatendea tofauti?<br />
<em><br />
Picha iliyotumika kwenye makala hii ni “17 de noviembre” ya <a href="http://www.flickr.com/photos/daquellamanera/2044749780/">daquella manera</a>.</em></p>
]]></content:encoded>
			<wfw:commentRss>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/11/ujauzito-na-magereza-afya-na-haki-za-wanawake-magerezani/feed/</wfw:commentRss>
		<slash:comments>0</slash:comments>
		</item>
		<item>
		<title>Trinidad &amp; Tobago: Kampeni ya 350</title>
		<link>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/10/trinidad-tobago-kampeni-ya-350/</link>
		<comments>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/10/trinidad-tobago-kampeni-ya-350/#comments</comments>
		<pubDate>Mon, 26 Oct 2009 12:24:39 +0000</pubDate>
		<dc:creator>j nambiza tungaraza</dc:creator>
				<category><![CDATA[Americas]]></category>
		<category><![CDATA[Cyber-Activism]]></category>
		<category><![CDATA[English]]></category>
		<category><![CDATA[Environment]]></category>
		<category><![CDATA[Gender]]></category>
		<category><![CDATA[Health]]></category>
		<category><![CDATA[Human Rights]]></category>
		<category><![CDATA[Ideas]]></category>
		<category><![CDATA[Indigenous]]></category>
		<category><![CDATA[Industry]]></category>
		<category><![CDATA[Internet & Telecoms]]></category>
		<category><![CDATA[Politics]]></category>
		<category><![CDATA[Protest]]></category>
		<category><![CDATA[Roundups]]></category>
		<category><![CDATA[Trinidad & Tobago]]></category>

		<guid isPermaLink="false">http://sw.globalvoicesonline.org/?p=473</guid>
		<description><![CDATA[Ilichapwa kwanza naJanine Mendes-Franco  &#183; Imetafsiriwa na j nambiza tungaraza &#183;  Angalia ujumbe mama 
“Trinidad na Tobago ni kisiwa tajiri na nchi inayoendelea tajiri kwa mafuta na gesi asilia. Lakini pia tunashuhudia madhara mabaya ya maendeleo ya haraka kwenye  nyanja za viwanda katika visiwa vyetu. Hii ni fursa ya sauti za wanawake [...]]]></description>
			<content:encoded><![CDATA[<em>Ilichapwa kwanza na<a href="http://globalvoicesonline.org/author/janine-mendes-franco/">Janine Mendes-Franco</a>  &middot; Imetafsiriwa na <a href='http://sw.globalvoicesonline.org/author/j-nambiza-tungaraza/'>j nambiza tungaraza</a> &middot;  <a href='http://globalvoicesonline.org/2009/10/23/trinidad-tobago-350-action/'>Angalia ujumbe mama</a></em> 
<br /><p>“Trinidad na Tobago ni kisiwa tajiri na nchi inayoendelea tajiri kwa mafuta na gesi asilia. Lakini pia tunashuhudia madhara mabaya ya maendeleo ya haraka kwenye  nyanja za viwanda katika visiwa vyetu. Hii ni fursa ya sauti za wanawake kusikika”: <a href="http://tillahwillah.wordpress.com/2009/10/23/women-350-climate-action-in-trinidad/">Attillah Springer </a>anajihusisha na kampeni ya hali ya hewa 350.</p>
]]></content:encoded>
			<wfw:commentRss>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/10/trinidad-tobago-kampeni-ya-350/feed/</wfw:commentRss>
		<slash:comments>0</slash:comments>
		</item>
		<item>
		<title>Trinidad &amp; Tobago: Mtrini Mpaka Kwenye Mifupa?</title>
		<link>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/10/trinidad-tobago-mtrini-mpaka-kwenye-mifupa/</link>
		<comments>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/10/trinidad-tobago-mtrini-mpaka-kwenye-mifupa/#comments</comments>
		<pubDate>Sat, 24 Oct 2009 07:45:46 +0000</pubDate>
		<dc:creator>j nambiza tungaraza</dc:creator>
				<category><![CDATA[Americas]]></category>
		<category><![CDATA[Cyber-Activism]]></category>
		<category><![CDATA[English]]></category>
		<category><![CDATA[Governance]]></category>
		<category><![CDATA[Health]]></category>
		<category><![CDATA[Ideas]]></category>
		<category><![CDATA[Law]]></category>
		<category><![CDATA[Politics]]></category>
		<category><![CDATA[Roundups]]></category>
		<category><![CDATA[Trinidad & Tobago]]></category>

		<guid isPermaLink="false">http://sw.globalvoicesonline.org/?p=447</guid>
		<description><![CDATA[Ilichapwa kwanza naJanine Mendes-Franco  &#183; Imetafsiriwa na j nambiza tungaraza &#183;  Angalia ujumbe mama 
“Kila siku ambayo ninapitia habari ninazidi kushawishika kuwa ninataka kuachana na klabu ya ‘Mimi ni Mtrini’ na kwenda sehemu nyingine”: Coffeewallah ameshachoka na kila kitu kuanzia uhalifu mpaka kodi.
]]></description>
			<content:encoded><![CDATA[<em>Ilichapwa kwanza na<a href="http://globalvoicesonline.org/author/janine-mendes-franco/">Janine Mendes-Franco</a>  &middot; Imetafsiriwa na <a href='http://sw.globalvoicesonline.org/author/j-nambiza-tungaraza/'>j nambiza tungaraza</a> &middot;  <a href='http://globalvoicesonline.org/2009/10/23/trinidad-tobago-trini-to-the-bone-2/'>Angalia ujumbe mama</a></em> 
<br /><p>“Kila siku ambayo ninapitia habari ninazidi kushawishika kuwa ninataka kuachana na klabu ya ‘Mimi ni Mtrini’ na kwenda sehemu nyingine”: <a href="http://coffeewallah.blogspot.com/2009/10/in-news-today.html">Coffeewallah</a> ameshachoka na kila kitu kuanzia uhalifu mpaka kodi.</p>
]]></content:encoded>
			<wfw:commentRss>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/10/trinidad-tobago-mtrini-mpaka-kwenye-mifupa/feed/</wfw:commentRss>
		<slash:comments>0</slash:comments>
		</item>
		<item>
		<title>Namibia: Kampeni ya Kukomesha Chanjo za Lazima</title>
		<link>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/10/namibia-kampeni-ya-kukomesha-chanjo-za-lazima/</link>
		<comments>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/10/namibia-kampeni-ya-kukomesha-chanjo-za-lazima/#comments</comments>
		<pubDate>Mon, 19 Oct 2009 12:13:43 +0000</pubDate>
		<dc:creator>j nambiza tungaraza</dc:creator>
				<category><![CDATA[English]]></category>
		<category><![CDATA[Governance]]></category>
		<category><![CDATA[Health]]></category>
		<category><![CDATA[Human Rights]]></category>
		<category><![CDATA[Law]]></category>
		<category><![CDATA[Namibia]]></category>
		<category><![CDATA[Roundups]]></category>
		<category><![CDATA[Sub-Saharan Africa]]></category>

		<guid isPermaLink="false">http://sw.globalvoicesonline.org/?p=386</guid>
		<description><![CDATA[Ilichapwa kwanza naNdesanjo Macha  &#183; Imetafsiriwa na j nambiza tungaraza &#183;  Angalia ujumbe mama 
Kampeni ya kukomesha Chanjo kwa kulazimishwa nchini Namibia imezinduliwa: “ umoja wa Asasi za kijamii umetoa wito kwa Wanamibia wote kujiunga na kampeni ya kulaani chanjo kwa wanawake waishio na VVU bila ya ridhaa yao. 
]]></description>
			<content:encoded><![CDATA[<em>Ilichapwa kwanza na<a href="http://globalvoicesonline.org/author/ndesanjo-macha/">Ndesanjo Macha</a>  &middot; Imetafsiriwa na <a href='http://sw.globalvoicesonline.org/author/j-nambiza-tungaraza/'>j nambiza tungaraza</a> &middot;  <a href='http://globalvoicesonline.org/2009/10/16/namibia-petition-to-end-forced-sterilisation/'>Angalia ujumbe mama</a></em> 
<br /><p><a href="http://endforcedsterilisation.wordpress.com/2009/10/16/petition-launched-to-end-forced-sterilisation/">Kampeni ya kukomesha Chanjo kwa kulazimishwa nchini Namibia imezinduliwa</a>: “ umoja wa Asasi za kijamii umetoa wito kwa Wanamibia wote kujiunga na kampeni ya kulaani chanjo kwa wanawake waishio na VVU bila ya ridhaa yao. </p>
]]></content:encoded>
			<wfw:commentRss>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/10/namibia-kampeni-ya-kukomesha-chanjo-za-lazima/feed/</wfw:commentRss>
		<slash:comments>0</slash:comments>
		</item>
		<item>
		<title>Nchi za Kiarabu: Homa ya Mafua ya Nguruwe Yaendelea</title>
		<link>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/07/nchi-za-kiarabu-homa-ya-mafua-ya-nguruwe-yaendelea/</link>
		<comments>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/07/nchi-za-kiarabu-homa-ya-mafua-ya-nguruwe-yaendelea/#comments</comments>
		<pubDate>Fri, 24 Jul 2009 14:17:11 +0000</pubDate>
		<dc:creator>Christian Bwaya</dc:creator>
				<category><![CDATA[Bahrain]]></category>
		<category><![CDATA[Egypt]]></category>
		<category><![CDATA[English]]></category>
		<category><![CDATA[General]]></category>
		<category><![CDATA[Health]]></category>
		<category><![CDATA[Media]]></category>
		<category><![CDATA[Middle East & North Africa]]></category>
		<category><![CDATA[Religion]]></category>
		<category><![CDATA[Saudi Arabia]]></category>
		<category><![CDATA[Syria]]></category>
		<category><![CDATA[Travel]]></category>
		<category><![CDATA[Weblog]]></category>

		<guid isPermaLink="false">http://sw.globalvoicesonline.org/?p=241</guid>
		<description><![CDATA[Homa ya mafua ya nguruwe au H1N1 bado inatawala vichwa vya habari vya magazeti katika nchi za Kiarabu kwani wagonjwa wapya wanaendelea kugunduliwa na mamlaka za afya na kutangazwa katika vyombo vya habari kila siku. Huu ni muhtasari wa yale wanayoongea wanablogu huko Bahrain, Jordan, Misri na Syria.]]></description>
			<content:encoded><![CDATA[<em>Ilichapwa kwanza na<a href="http://globalvoicesonline.org/author/amira-al-hussaini/">Amira Al Hussaini</a>  &middot; Imetafsiriwa na <a href='http://sw.globalvoicesonline.org/author/bwaya/'>Christian Bwaya</a> &middot;  <a href='http://globalvoicesonline.org/2009/07/09/arab-world-swine-flu-fever-continues/'>Angalia ujumbe mama</a></em> 
<br /><p>Homa ya mafua ya nguruwe au H1N1 bado inatawala vichwa vya habari vya magazeti katika nchi za Kiarabu kwani wagonjwa wapya wanaendelea kugunduliwa na mamlaka za afya na kutangazwa katika vyombo vya habari kila siku.</p>
<p>Huko Bahraini, <em><a href="http://sillybahrainigirl.blogspot.com/2009/07/coming-home-to-sick-place.html">Silly Bahraini Girl </a></em>(ambaye ni mimi) amerudi nyumbani na kushangazwa na kile alichokiona katika kiwanja cha ndege cha nchini mwake:</p>
<blockquote><p>Ukweli wa jinsi sehemu hii ilivyogeuka na kuwa ya kiwendawazimu unakupiga usoni sekunde ile unapotua kwenye kiwanja cha ndege cha kimataifa na kuona wafanyakazi wa ardhini wamevaa vitambaa vya kitabibu kufunika pua, kuanzia wahudumu mpaka maofisa wa uhamiaji.<br />
“Mna tatizo gani?” Ninawauliza. “Kuna maambukizi Bahraini?” Niliendelea kuuliza […] hali ilionekana kuwa ngumu na kiwango cha wendawazimu wa mafua haya ya nguruwe kilikuwa juu kuliko niliyokutana nao kokote nilikosafiri tangu matatizo haya ya nguruwe yalipoikamata dunia. Kwanini hapakuwepo hata mtu mmoja aliyevaa matambara haya kwenye viwanja vya San Fransisco, Chicago, Toronto na Heathrow ambako nilisafiri<br />
katika majuma machache yaliyopita?</p></blockquote>
<p>Bado tukiwa Bahraini, <em><a href="http://suhailalgosaibi.com/2009/07/09/the-shocking-truth-about-swine-flue/">Sohail Al Gosaibi</a></em> ananusa njama kwenye hewa, anaona kwamba kukuza sana madhara ya mafua ya nguruwe kunayanufaisha mashirika ya habari, watangaza biashara na viwanda vya madawa. Mwanablogu wa Kisaudia anaandika:</p>
<blockquote><p>Vyombo vya habari siku zote hukuza hali ya mambo, kumbuka kwamba hofu huuza. Na magazeti na idhaa za habari ni lazima viuze nafasi za matangazo na muda wa kurusha matangazo hewani ili kutengeneza fedha, na kwa kadiri habari inavyokuwa inatishia na kuogopesha ndivyo wanavyopata watazamaji na wasomaji wengi zaidi, ambavyo huongeza watangaza biashara, na faida zaidi.</p></blockquote>
<p><em>Al Gosaibi </em>ananukuu makala aliyoisoma na kuhitimisha:</p>
<blockquote><p>Kwa mujibu wa makala, Serikali za Marekani na Uingereza zina hifadhi ya madawa ya Tamifluiflu yenye thamani ya mabilioni ya dola ambazo lazima wazitumie ndani ya miezi michache ijayo, vinginevyo yatapita muda wake. Inafurahisha, eeh?</p></blockquote>
<p>Na akizungumzia nadharia, mwanablogu wa <em><a href="http://jordanreformwatch.wordpress.com/2009/06/30/stupid-watch/">Jordan Reform Watch</a> </em>pia anacho cha kusema na kuandika:</p>
<blockquote><p>Ahhh..mafua ya nguruwe pamoja na nadharia zote za njama zinazoambatana nayo… “mwanasayansi” wa Kijordani bingwa wa magonjwa anadai kuwa Maka na Madina ziko mbali na ugonjwa huo, kwa hiyo hakuna haja ya kuzungumzia uwezekano wa mlipuko ambao unaweza kutokea kutokana na mamilioni ya mahujaji kuwa karibu karibu wakati wa hija…</p>
<p>Uweni nguruwe…Nendeni kwenye Hija…na mtakuwa mbali na ugonjwa…</p></blockquote>
<p>Mwanablogu wa Kimisri <em><a href="http://egyptianchronicles.blogspot.com/2009/07/h1n1-follow-up-5-more-cases.html">Zeinobia</a></em>, anayeblogu kupitia blogu ya<em> Egyptian Chronicles</em>, kadhalika anaguswa na jinsi ugonjwa utakavyosambaa wakati wa Haji [Msimu wa Hija ya Waislamu Maka kila mwaka], ambapo mamilioni ya mahujaji kutoka sehemu mbalimbali duniani hukusanyika Maka ili kutimiza nguzo hiyo. Anaandika:</p>
<blockquote><p>majadiliano kuhusu mustakabali wa Hija na Omra [hija ndogo] mwaka huu bado ni suala linaloendelea. Waziri wa Afya anataka kuifuta Omra wakati Waziri wa Utalii anapinga kufutwa huko, sihitaji kuzungumzia kuhiji.<br />
Ni kweli majadiliano ni makali miongoni mwa mashehe wa dini wenyewe. Saudia Arabia inaelewa changamoto iliyonayo tayari na imeamua kushughulikia hali hiyo kwa kadiri inavyoweza katika Omra na hija, inashauri kuwa mahujaji wajawazito, wazee na watoto waepuke kuhiji mwaka huu, Ninauheshimu uamuzi huu.<br />
Pia ninalo pendekezo zuri zaidi. Katika mnazingira kama haya<br />
kwa nini tusiwaruhusu tu wale mahujaji wa kwanza wake kwa waume kuhudhuria Omra na Hija.</p></blockquote>
<p>Kituo chetu cha mwisho ni Syria, ambapo mwanablogu <em><a href="http://yaser1978.wordpress.com/2009/07/04/%D8%A5%D8%B9%D9%84%D8%A7%D9%86-%D8%A3%D9%88%D9%84-%D8%AD%D8%A7%D9%84%D8%A9-%D8%A7%D8%B5%D8%A7%D8%A8%D8%A9-%D8%A8%D8%A5%D9%86%D9%81%D9%84%D9%88%D9%86%D8%B2%D8%A7-%D8%A7%D9%84%D8%AE%D9%86%D8%A7%D8%B2/">Yaser Arwani</a></em> [ar] anatuunganisha na habari inayosema kwamba mgonjwa wa kwanza wa mafua wa nguruwe kuripotiwa Syria ilitaarifiwa na daktari wa Ki-Syria, anayefanya kazi Australia na alikuwa akiitembelea nchi yake. Daktari huyu wa kike alisafiri kwenda Syria kupitia Uwanja wa Kimataifa wa Dubai na ugonjwa haukuwa umegunduliwa mpaka siku chache baada ya kuwasili kwake.</p>
]]></content:encoded>
			<wfw:commentRss>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/07/nchi-za-kiarabu-homa-ya-mafua-ya-nguruwe-yaendelea/feed/</wfw:commentRss>
		<slash:comments>1</slash:comments>
		</item>
		<item>
		<title>Saudi Arabia: Je, mafua ya nguruwe yatatishia Hija?</title>
		<link>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/05/saudi-arabia-je-mafua-ya-nguruwe-yatatishia-hija/</link>
		<comments>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/05/saudi-arabia-je-mafua-ya-nguruwe-yatatishia-hija/#comments</comments>
		<pubDate>Mon, 25 May 2009 02:39:34 +0000</pubDate>
		<dc:creator>Christian Bwaya</dc:creator>
				<category><![CDATA[English]]></category>
		<category><![CDATA[General]]></category>
		<category><![CDATA[Health]]></category>
		<category><![CDATA[Middle East & North Africa]]></category>
		<category><![CDATA[Religion]]></category>
		<category><![CDATA[Saudi Arabia]]></category>
		<category><![CDATA[Weblog]]></category>

		<guid isPermaLink="false">http://sw.globalvoicesonline.org/?p=158</guid>
		<description><![CDATA[Kila mwaka mamilioni ya Waislamu hukusanyikia Maka kuhiji, moja ya nguzo tano za Uislamu. Je, msimu wa hija ya mwaka huu utatishiwa na homa ya mafua ya nguruwe? Wanablogu wanayo maoni ya kusema.]]></description>
			<content:encoded><![CDATA[<em>Ilichapwa kwanza na<a href="http://globalvoicesonline.org/author/amira-al-hussaini/">Amira Al Hussaini</a>  &middot; Imetafsiriwa na <a href='http://sw.globalvoicesonline.org/author/bwaya/'>Christian Bwaya</a> &middot;  <a href='http://globalvoicesonline.org/2009/05/15/saudi-arabia-will-swine-flu-threaten-hajj/'>Angalia ujumbe mama</a></em> 
<br /><p>Kila mwaka mamilioni ya Waislamu husafiri kwenda  Maka kuhiji, moja ya nguzo tano za Uislamu. Je, msimu wa hija ya mwaka huu utatishiwa na homa ya mafua ya nguruwe? Wanablogu wanayo maoni ya kusema.</p>
<p>Kwenye blogu ya <em><a href="http://xrdarabia.org/2009/05/08/swine-flu-and-umrah/">CrossRoads Arabia</a></em>, <em>John Burgess</em> anaeleza:</p>
<blockquote><p>Mtafiti wa Kisaudi katika sheria za Kiislamu (Sharia) amegundua kuwa kuna uwezekano wa kuwazuia baadhi ya mahujaji (wale ambao walishahiji kabla yaani, mahujaji wa ‘kurudia’) hasa wanaotoka maeneo ambayo kwa sasa yanatishiwa na mlipuko wa mafua ya nguruwe. Nina hisi kwamba wazo hili linakuja sasa kwa sababu ya Haji ambayo itafanyika mwishoni mwa mwezi Novemba. Hija ni wajibu wa msingi, ambao kila Mwislamu hutakiwa kuutimiza angalau mara moja katika maisha yake, inapowezekana.</p>
<p>Hali kama hii ilijitokeza miaka michache iliyopita, ambapo homa ya mafua ya ndege (H5N1) ilikuwa tishio. Msomi mmoja wa Kisaudi alitoa wito wa kuifuta Hija ikiwa mlipuko ungekuwa mkubwa zaidi, lakini <a href="http://www.islamonline.net/English/News/2005-11/22/article07.shtml">pendekezo hilo lilizimwa na wenzake</a>. Hoja ilikuwa kwamba Hija haijawahi kufutwa kwa minajili tu ya kiafya na kwamba kufanya hivyo kungekuwa kuukiuka Uislamu. Badala yake, wale walio wagonjwa, kimaadili <em>hutakiwa</em> kutokuitimiza hija yao.</p>
<p>Magonjwa yaambukizwayo yana historia ndefu na Hija. Zipo kumbukumbu nyingi za milipuko ya magonjwa kama kipindupindu na maafa ya maelfu huko Maka, Madina na Jedah kwa miaka mingi sasa. Ni kuelekea karne ya 19 ndipo ambapo <a href="http://etd.gsu.edu/theses/available/etd-07082007-174715/unrestricted/low_michael_c_200708_ma.pdf">sheria za kutenga wagonjwa</a> zilianza kutumika ili kukomesha ueneaji wa magonjwa katika eneo hilo takatifu, hadi manyumbani mwa mahujaji. Sheria hizo pamoja na kutiliwa mkazo kwa mchujo wa kiafya kwa mahujaji unaelezwa kuweza kusaidia kuwalinda mahujaji. Muda utahitajika kuona ikiwa hili linawezekana. Mafua ya nguruwe, kama ilivyokuwa kwa mafua ya ndege hapo awali, yanaweza kuja kuwa jambo lisilo na uzito unaoonekana hivi sasa. Isipokuwa hivyo, hata hivyo, ni vyema watu wakaanza kulitafakari kuanzia sasa.</p></blockquote>
<p>Blogu ya <em><a href="http://mideasti.blogspot.com/2009/05/postpone-hajj-due-to-swine-flu.html">Middle East Institute&#39;s Editor&#39;s Blog </a></em>inaongeza:</p>
<blockquote><p>Jambo hili linazidi kuwa jipya kila uchao. Mufti mkuu wa Misri anapendeza wanazuoni wa Kiislamu kutangaza fatwa [tamko la kidini] <a href="http://www.almasry-alyoum.com/article2.aspx?ArticleID=210861">kuahirisha Hija kwa sababu ya mafua ya nguruwe</a>. Fatwa yenyewe inapatikana <a href="http://www.almasry-alyoum.com/article2.aspx?ArticleID=210851">hapa</a> kwa Kiarabu. Tilia maanani –ninajua na naendelea kurudia hili –hapajawahi kuwapo suala kama hili katika Misri. Kusema kweli, <a href="http://www.who.int/csr/don/2009_05_13/en/index.html">kwa mujibu wa Shirika la Afya Duniani (WHO)</a>, maambukizo yaliyothibitishwa katika Mashariki ya Kati yote ni Israel (wagonjwa saba). Na Shirika hilo la Afya Duniani (WHO) linasema “ Shirika halijashauri kusitishwa kwa safari kwa sababu ya mlipuko wa virusi vya mafua ya nguruwe.” Ndio, na suala jingine: Hija haijafika, ni mpaka mwezi wa Novemba. Hivi kuna kitu nitakuwa nakosea hapa? Je, katika historia ya Uislamu, hivi imewahi kutokea Hija ikaahirishwa kwa sababu tu za kiafya? Sijui, lakini ninatarajia kuwa tungehitaji walau mgonjwa mmoja ili kuhalalisha uamuzi huu. (Si tu kwamba hakuna taarifa za ugonjwa Mashariki ya Kati, isipokuwa Israel, lakini pia hakuna mgonjwa yoyote Indonesia, Malayasia, Pakistani – ndio hata kokote waliko Waislamu)</p></blockquote>
]]></content:encoded>
			<wfw:commentRss>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/05/saudi-arabia-je-mafua-ya-nguruwe-yatatishia-hija/feed/</wfw:commentRss>
		<slash:comments>1</slash:comments>
		</item>
		<item>
		<title>Gumzo la moja kwa moja kuhusu Virusi vya ukimwi na Ukimwi mtandaoni Tarehe 6 machi</title>
		<link>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/03/gumzo-la-moja-kwa-moja-kuhusu-virusi-vya-ukimwi-na-ukimwi-mtandaoni-tarehe-6-machi/</link>
		<comments>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/03/gumzo-la-moja-kwa-moja-kuhusu-virusi-vya-ukimwi-na-ukimwi-mtandaoni-tarehe-6-machi/#comments</comments>
		<pubDate>Fri, 06 Mar 2009 12:49:45 +0000</pubDate>
		<dc:creator>Egidio Ndabagoye</dc:creator>
				<category><![CDATA[Announcements]]></category>
		<category><![CDATA[Cyber-Activism]]></category>
		<category><![CDATA[Development]]></category>
		<category><![CDATA[English]]></category>
		<category><![CDATA[Feature]]></category>
		<category><![CDATA[Health]]></category>
		<category><![CDATA[Rising Voices]]></category>
		<category><![CDATA[Weblog]]></category>

		<guid isPermaLink="false">http://sw.globalvoicesonline.org/?p=95</guid>
		<description><![CDATA[Mradi wa <a href="http://rising.globalvoicesonline.org/">Rising Voices</a> na <a href="http://globalvoicesonline.org/">Global Voices</a> wanaandaa gumzo la moja kwa moja mtandaoni kwa wanablogu na wanaharakati siku ya Ijumaa mwezi wa tatu mwaka huu(saa 11 jioni kwa saa za Nairobi) mada kuu ikiwa jinsi ya kublogu na kuongeza uelewa na habari kuhusu virusi vya ukimwi na Ukimwi.]]></description>
			<content:encoded><![CDATA[<em>Ilichapwa kwanza na<a href="http://globalvoicesonline.org/author/juhie-bhatia/">Juhie Bhatia</a>  &middot; Imetafsiriwa na <a href='http://sw.globalvoicesonline.org/author/egidio-ndabagoye/'>Egidio Ndabagoye</a> &middot;  <a href='http://globalvoicesonline.org/2009/03/04/blogging-positively-live-chat-about-hivaids-on-march-6/'>Angalia ujumbe mama</a></em> 
<br /><p><img alt="" src="http://globalvoicesonline.org/wp-content/uploads/2009/02/blogging-positively-banner-800.gif" class="aligncenter" width="800" height="196" /><br />
Mradi wa <a href="http://rising.globalvoicesonline.org/">Rising Voices</a> na <a href="http://globalvoicesonline.org/">Global Voices</a> wanaandaa gumzo la moja kwa moja mtandaoni kwa wanablogu na wanaharakati siku ya Ijumaa mwezi wa tatu mwaka huu(saa 11 jioni kwa saa za Nairobi) mada kuu ikiwa jinsi ya kublogu na kuongeza uelewa na habari kuhusu virusi vya ukimwi na Ukimwi.</p>
<p>Kila mmoja anakaribishwa</p>
<p><strong>Muda</strong>:New York 3 asubuhi | Buenos Aires 6mchana | London 8mchana | Johannesburg,Beirut 10jioni | Nairobi, Moscow 11 jioni | New Delhi 1:30 usiku | Hong Kong 4usiku | Tokyo 5 usiku</p>
<p><strong>Chumba cha gumzo</strong>:http://www.worknets.org/chat/</p>
<blockquote><p><strong>Jinsi ya kujiunga</strong>:Bonyeza kingo hapo juu tumia jina lako.Kisha chagua chumba utakacho kujiunga kwa kubonyeza ingia.Baada ya kuingia chagua ukubwa wa maandishi upande  wa kushoto wa kiwambo cha tarakishi yako, jiunge katika gumzo</p></blockquote>
<p>Gumzo la tarehe 6 mwezi wa 3 litajenga mada iliyoletwa  katika majadiliano yaliofanikiwa wiki iliyopita. Gumzo la tarehe 27 mwezi wa  pili lilitoa tamko kama vile umuhimu wa kublogu kwa watu walioathirika na virusi vya ukimwi na jukumu  katika upelekaji na ushawishi wa maarifa,lakini kikubwa lililenga kwenye <strong>muongozo wa  kublogu vyema </strong>,muongozo ulitengenezwa na Global Voices kutoa ushauri tunu jinsi ya kublogu kuhusu masuala ya Virusi vya Ukimwi na Ukimwi. Muongozo huo bado ni kazi inayooendelea, kwa hiyo tunatafuta msaada kutengeneza na kutoa matokeo. Kwa wale waliokuwa na nia au waliokwisha blogu kuhusu maafa wanahimizwa kushiriki katika  gumzo wiki hii, hasa wale wanaoishi au walioathirika na virusi vya ukimwi.  Gumzo la Ijumaa litalenga masuala kama vile uanzishwaji makundi maalum ya kazi au vitengo kwa ajili ya mchakato wa kutengeneza muongozo wa kublogu vyema kadhalika gumzo hilo litajadili kuhusu aya na  na mada zipi zijumuishwe kwenye muongozo. </p>
<p>Pia kuna mada nyingine ambazo utataka kujadili wakati wa gumzo,tafadhali weka maoni chini.Natumaini mtashirikiana nasi tarehe 6 mwezi wa tatu</p>
]]></content:encoded>
			<wfw:commentRss>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/03/gumzo-la-moja-kwa-moja-kuhusu-virusi-vya-ukimwi-na-ukimwi-mtandaoni-tarehe-6-machi/feed/</wfw:commentRss>
		<slash:comments>1</slash:comments>
		</item>
		<item>
		<title>Angola: Ebola Inapokaribia, Mipaka yafungwa</title>
		<link>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/01/angola-ebola-inapokaribia-mipaka-yafungwa/</link>
		<comments>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/01/angola-ebola-inapokaribia-mipaka-yafungwa/#comments</comments>
		<pubDate>Sun, 18 Jan 2009 08:52:09 +0000</pubDate>
		<dc:creator>j nambiza tungaraza</dc:creator>
				<category><![CDATA[Angola]]></category>
		<category><![CDATA[D.R. of Congo]]></category>
		<category><![CDATA[Feature]]></category>
		<category><![CDATA[General]]></category>
		<category><![CDATA[Health]]></category>
		<category><![CDATA[Portuguese]]></category>
		<category><![CDATA[Sub-Saharan Africa]]></category>
		<category><![CDATA[Weblog]]></category>

		<guid isPermaLink="false">http://sw.globalvoicesonline.org/?p=46</guid>
		<description><![CDATA[Baada ya kuzuka kwa ugonjwa wa ebola kwenye Jamburi ya Kidemokrasi ya Kongo, maambukizi ya ugonjwa huo bado hayajafika nchini Angola. Ili kuuzuia kusambaa kwa virusi hatari vya  ugonjwa huo, nchi hiyo jirani imefunga mpaka wake na Jamhuri ya Kidemorasi ya Kongo, kadhalika imezuia uhamiaji wa watu kati ya nchi hizo mbili. Anaandika Clara Onofre.]]></description>
			<content:encoded><![CDATA[<em>Ilichapwa kwanza na<a href="http://globalvoicesonline.org/author/clara-onofre/">Clara Onofre</a>  &middot; Imetafsiriwa na <a href='http://sw.globalvoicesonline.org/author/j-nambiza-tungaraza/'>j nambiza tungaraza</a> &middot;  <a href='http://globalvoicesonline.org/2009/01/14/angola-with-ebola-around-the-corner-borders-are-closed/'>Angalia ujumbe mama</a></em> 
<br /><p>Kutokana na <a href="http://globalvoicesonline.org/2009/01/11/dr-congo-containing-the-ebola-outbreak/">kuzuka tena kwa virusi vya Ebola katika Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo</a>, serikali ya Angola imeamua <a href="http://www.iol.co.za/index.php?set_id=1&#038;click_id=68&#038;art_id=nw20090106140149695C625689">kufunga mpaka kati ya nchi hizo mbili</a>, katika jaribio la kuzuia kuingia kwa virusi hivyo hatari katika himaya ya taifa hilo., Hivyo kusitisha mara moja uhamiaji wa kawaida unaoendelea kati ya Lunda Norte (jimbo lililoko kaskazini mashariki ya nchi) na Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo. Lazima izingatiwe kwamba jimbo la Lunda Norte ni sehemu ya migodi ya dhahabu, anyowavuta wafanyakazi wengi wahamiaji. <a href="http://www.blog.comunidades.net/nelo/index.php?op=arquivo&#038;idtopico=481918">Nelo de Carvalho </a>[pt] anaandika katika <em>blog do Nelo Ativado </em>kuhusu vizingiti vilivyoko kwenye mpaka huo na changamoto ambazo serikali inazikabili:</p>
<blockquote><p>&#8220;Kusema kwamba mpaka lazima ufungwe na kwamba mtu yeyote asiingie au kutoka nchini, kwa kutumia mpaka huo. Hakuna hata mbu anayeambukiza ugonjwa wa dengue atakayeweza kupenya, na kama akiweza kupenya, ni lazima aandamwe. Ni mkakati ambao hata mtoto inabidi autekeleze wakati akicheza mchezo wa polisi au mwanajeshi au hata jenerali. Kwa hiyo hatuna mamlaka au mamlaka ya kisheria kufikiria mara mbili juu ya hili. Tunaweza kuomba na kutumaini kwamba kila kitu kitakwenda kama tunavyotarajia. Wakati huu wa kuuanza mwaka, tunawaombea bahati nzuri Waangola wote, kuwe au kusiwe na ebola.&#8221;</p></blockquote>
<p>Kwa mujibu wa Katibu wa Afya wa Angola, serikali inajitayarisha kuwafahamisha wananchi juu ya mpango uliowekwa ili kuzuia maambukizi ya virusi hivi vyenye nguvu. Pamoja na jimbo la Lunda Norte, hatua hizo pia zitatekelezwa katika majimbo ya Moxico, Malanje, Uige na Lunda Sul. Inaaminika kwamba kumekuwepo na kesi zipatazo 40 za ebola, na zaidi ya vifo 10 vilivyoripotiwa katika Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo katika miezi miwili iliyopita.</p>
<p>Miaka miwili iliyopita, virusi hivyo, pia vikitokea kutokea Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo, hasa kutokea kwenye jimbo la Kasai Magharibi,  vilisababisha vifo vya watu wapatao 180. Blogu ya <a href="http://lampeirota.blogs.sapo.pt/44070.html">Lampeirota</a> inalalamika kuhusu hali hii:</p>
<blockquote><p>&#8220;Mara kwa mara, huongelea kuhusu ugonjwa huu. Sina tabia ya kufikiria kuhusu jambo hili, najikinga nyuma ya dhana  kwamba siyo rahisi kwa ugonjwa kunikuta nikiwa sijajiandaa.</p>
<p>Namna hii [ya kufikiria] ni potofu. Hatuwezi kuwa na uhakika juu ya mambo kama haya. Husambaa kila mahali kwa haraka sana.</p>
<p>Nawasikitikia wanaoukabili huu ugonjwa.</p>
<p>Siyo kifo kinachonitisha. Ni njia ya kukielekea&#8221;. </p></blockquote>
<p>Pia kwa mujibu wa mwakilishi wa Shirika la Afya Duniani (WHO) nchini Angola, Diosdado Nsue-Micawg, inahisiwa kwamba ushikaji wa miili ya nyani waliokufa kwenye misitu  ya Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo ndiyo chanzo cha kuibuka tena kwa ugonjwa huu. Japokuwa kwa bahati nzuri <a href="http://www.iol.co.za/index.php?set_id=1&#038;click_id=68&#038;art_id=nw20090112152927801C175821">hapajakuwa na kesi za ugonjwa wa ebola nchini Angola</a>, Katibu wa Afya  anasema kwamba nchi hiyo imejiandaa kupambana na hali yoyote itakayojitokeza kutokana na uzoefu wake na <a href="http://en.wikipedia.org/wiki/Marburg_virus">ugonjwa wa homa na kuvuja damu wa Marbug</a>, ugonjwa wenye hatari pungufu zaidi ya ebola. </p>
<p>Hii ni mara ya nne kwa virusi vya ebola kuzuka ndani ya Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo tangu ulipoibuka kwa mara ya kwanza mwaka 1976. Ugonjwa unaoambukiza haraka huzua homa, kutapika, kuharisha pamoja na kutokwa damu ndani na nje ya mwili. Mnamo mwaka 2005 <a href="http://www.reuters.com/article/africaCrisis/idUSL8586536">watu 329 walifariki kutokana na ugojwa wa Marbug kwenye jimbo la kaskazini la Uige</a> nchini Angola, Karibu kabisa na mpaka wa Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo.</p>
<p><img src='http://globalvoicesonline.org/wp-content/uploads/2009/01/2536860585_e4689c3966.jpg' alt='' class='aligncenter' /><br />
<strong>Picha ya kitaalamu ya vijidudu vinavyosababisha ugonjwa wa Ebola. Picha kwa hisani ya CDC/Cynthia Goldsmith. Kupitia mtumiaji wa Flickr <a href="http://www.flickr.com/photos/hukuzatuna/">hukuzatuna</a>.</strong></p>
]]></content:encoded>
			<wfw:commentRss>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/01/angola-ebola-inapokaribia-mipaka-yafungwa/feed/</wfw:commentRss>
		<slash:comments>0</slash:comments>
		</item>
	</channel>
</rss>
