Kutokuwepo uwazi na weledi katika mchakato wa kumchagua mgombea, mbali na kufahamika nani hasa watachukua nafasi zinazogombewa kabla hata ya uchaguzi katika taasisi hiyo. Hizo zilikuwa baadhi ya sababu zilizotolewa na mwanaharakati wa haki za binadamu, Benilde Nhalivilo, wakati akijitoa rasmi kugombea nafasi kwenye Tume ya Taifa ya Uchaguzi ya Msumbiji[pt], chombo kinachohusika na kuandaa na kusimamia chaguzi nchini humo. Taarifa zaidi zinapatikana kwenye gazeti la A Verdade [pt].
Habari Maalum Kuhusu Governance
-
Kitabu-pepe Kipya cha GV: Sauti ya Kiafrika ya Matumaini na Mabadiliko
30 Disemba 2012
-
Mkanganyiko wa Makubaliano ya OIC Kuanzisha Ofisi Nchini Myanmar
30 Novemba 2012
-
Mradi wa Tafsiri: Kauli ya Linda Uhuru wa Intaneti Ulimwenguni 20 Novemba 2012
-
Kuwait: Ni Maandamano Makubwa Kabisa Kuwahi Kutokea?
27 Oktoba 2012
-
Pakistani: Msichana wa Kikristo wa Miaka 11 Awekwa Kizuizini kwa Kukashifu Dini.
16 Septemba 2012
Habari mpya Kuhusu Governance
5 Mei 2013

Wagombea wa Urais katika Uchaguzi wa Madagaska
Habari Mpya: Hapa ni orodha kamili ya wagombea 49 [fr] wanaowania nafasi ya Urais katika uchauzi ujao. Orodha hiyo haina jina la rais wa sasa wa mpito.
Siku ya mwisho ya kurudisha fomu kwa ajili ya kugombea Urais katika uchaguzi ujao ilikuwa tarehe 28 Aprili, na inavyoonekana ni wagombea wachache sana wasiotarajiwa wamejitokea kuwania kiti hicho. Wakati wagombea wa awali walikuwa wapya kabisa wasiofahamika sana, wanasiasa wachache machachari wanaofahamika wanatarajiwa kugombea akiwemo rais wa zamani Didier Ratsiraka, rais wa sasa wa mpito Andry Rajoelina [fr] na mke wa rais wa zamani Ravalomanana, anayeitwa Lalao Ravalomanana.
4 Mei 2013
Wabunge wa Ukraine Wataka Utoaji Mimba Upigwe Marufuku Kisheria
Mapema mwezi Aprili, Wabunge watatu kutoka kambi ya Upinzani iitwayo“Svoboda” walipeleka mswada bungeni wenye lengo la kupiga marufuku utoaji mimba nchini Ukraine. Tetyana Bohdanova anataarifu mwitikio wa watumiaji wa mtandao kufuatia hatua hii ya Bunge la Ukraine.
24 Aprili 2013

Jaribio la Mapinduzi katika Visiwa vya Comoro
Jeshi la Pilisi nchini Comoro limesema linawashikilia watu wanaosemekana kuwa wahaini raia wa Kongo na Chadi kwa tuhuma za jaribio la kuiangusha serikali lililofanyika mwisho wa wiki. Linfo.re anaongeza kwamba [fr]:
Makamanda wa Jeshi hawakutaka kupambana waziwazi na wahaini hao. Waliamini kwamba ” Kujeruhi raia wa Comoro kwa lengo la kuwalinda wakubwa inaleta picha ya usaliti kwa nchi hiyo ya Comoro”.
15 Aprili 2013
Asasi za Kiraia za Urusi “Zakaguliwa” na Mwendesha Mashitaka

Wanaharakati wa DemVybor katika jiji kuu la eneo la Voronezh waliripoti kwenye blogu ya DemVybor[ru] kwamba Asasi Zisizo ki-Serikali zinakaguliwa na ofisi ya mwendesha mashitaka wa umma wa jiji hilo. Mashirika...
27 Februari 2013
Bulgaria: Gharama Kubwa za Nishati Zasababisha Maandamano
Ruslan Trad anataarifu kuwa, siku ya Jumapili tarehe 17 Februari, makumi ya maelfu ya watu katika mji mkuu wa Bulgaria, Sofia pamoja na majiji mengine waliendelea na maandamano kupinga bei kubwa za nishati ya umeme pamoja na gharama za kupasha joto.
12 Februari 2013

Udhaifu wa Watawala wa Afrika unajionesha Mali?
Ousmane Gueye katika tovuti ya Mondoblog anaandika [fr] kuhusu kuchelewa kupeleka vikosi vya kijeshi kasikazini mwa Mali:
Kama tungekuwa tunasaiili matokeo ya watu wenye amani na huru kuingilia kati hali ya mambo nchini Mali, basi ni wazi kuwa kwa kuchelewa kupeleka vikosi vya ulinzi, nchi za Afrika zimewakosea wananchi wa Mali kwa mara nyingi…kelele zote za wakuu wa nchi lakini bado hawajaweza kutimiza lengo lolote waliloliweka wao kama hatua ya kupunguza nguvu ya Waslamu wenye msimamo mkali nchini Mali.
28 Januari 2013

Mauritania:Ghadhabu Dhidi ya Kauli ya Balozi wa Marekani

Picha ya maandamano dhidi ya Ubalozi wa Marekani mjini Nouakchott – Iliwekwa kwenye ukurasa wa Facebook ya Vijana wa Kukusanya Nguvu ya Kidemokrasia
11 Januari 2013

Rais wa Chadi Awateua Wanawe Kushika Nafasi Nyeti
Djamil Ahmat anaripoti kuwa rais Déby wa Chadi amemteua mwanae wa kiume Mahamat Idriss Déby, 24, kuwa brigedia jenerali [fr] pamoja na maafisa wengine wanne. Tchadanthopus anaongeza kuwa mwanae mwingine Zackaria Idriss Deby alisemekana kukabidhiwa umakamu wa rais [fr] nafasi ambayo inampa madaraka yote wakati baba yake anapokuwa nje ya nchi.
30 Disemba 2012

Video ya Kuomba Ujenzi wa Vyoo vya Umma huko Jharkhand, India
Amit Topno, mwakilishi wa jumuiya ya hiari “inayopiga picha za video” aliripoti kwamba wakati wa kijiji cha Nichitpur katika Jimbo la Jharkhand hawana choo chochote cha umma kinachotumika. Wanavijiji wanaziomba mamlaka za serikali za mitaa kupitia video hii kuhakikisha kuwa vyoo vinavyostahili matumizi ya binadamu vinajengwa.




























Kiungo cha RSS kwa Governance 











mambo vipi wanablog muko powa wote.kama mumenisoma nijibuni.
Asante. Nimepita hapa natafuta japan na china wamemalizaje ugomvi wao kuhusu visiwa,pia chanzo cha ugomvi...